Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tanzania na Misaada: Tujadili hili...

    Report Post
    Page 4 of 7 FirstFirst ... 23456 ... LastLast
    Results 61 to 80 of 139
    1. #1
      kula kwa tindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 416
      Rep Power : 467
      Likes Received
      70
      Likes Given
      43

      Default Tanzania na Misaada: Tujadili hili...

      Kuna maswali mengi yamekua yanasumbua Akili,hasa akili za wenye ufahamu wa juu..
      Je!! Kwa Nchi ya Tanzania inaweza kuendesha shughuli zake bila kutegemea misaada na mikopo toka Nchi za nje?

      Na endapo unadhani inawezekana Tanzania ikaendesha bila huo utegemezi, au haiwezi kuachana na utegemezi..
      TOA SABABU ZAKO HAPA!

      Kwanini haiwezi kutegema Mikopo na misaada?

      Kwanini inaweza kuendesha shughuli zake bila misaada na mikopo?


    2. #61
      kitero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2012
      Location : Kaskazini
      Posts : 516
      Rep Power : 473
      Likes Received
      98
      Likes Given
      48

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Mtoa mada natumaini wengi hawajamuelewa,hapa kunawengine tumesha anza siasa.Mikopo ni muhimu sana katika kuleta maendeleo,tena nchi jajiri na kubwa ndiyo zinaongoza kwa mipoko,ila hazipewi misaada.Nijinsi gani tutakavyo weza kutumia miko na misaada ili tusiwe tegemezi wa misaada? Na si tegemezi wa mikopo

    3. #62
      webondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2012
      Location : Chini ya mwembe
      Posts : 1,167
      Rep Power : 593
      Likes Received
      178
      Likes Given
      381

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Quote By kula kwa tindo View Post
      Hahahahaaaaaa.... Mkuu wewe una akili Timamu ndio maana umejitambua... Mchango wako ni muhimu hapa CHUONI JF
      Hahahaha! Haya bhana, labda nichangie kiduchu!
      Umezungumzia mambo mawili hapo; MIKOPO NA MSAADA. Kwa issue ya mkopo kama nchi nadhani hilo halina shaka, nchi nyingi duniani maskini na tajiri (Uchina, Marekani na zingine) zina mikopo, hii ina maana kuwa nchi kukopa au kudaiwa mkopo ni kawaida na wala sio dhambi.

      But; kuendesha nchi kwa msaada ni mbaya, hasa kwa nchi yenye rasilimali za kutosha kama Tanzania na zingine. Kwahiyo mtazamo wangu ni kuwa haileti maana sana kwa nchi kujiendesha kwa msaada.

    4. #63
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,985
      Rep Power : 16312
      Likes Received
      3401
      Likes Given
      4342

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      [QUOTE=kula kwa tindo;4223942]Vipi kwenye Jimbo lako,Ulishawahi kuhoji kuhusu maendeleo yenu kwa MP wako?
      Na ulishahudhuria japo kikao kimoja cha kiongoji?
      [/QUOTE
      KWA BAHATI MBAYA KWETU KUNA GAMBA NDUNGULILE HATA TULIPOPANDISHIWA NAULI YA KIVUKO KWA 200%ALIKAA KIMYA JE UTAHOJI NINI TENA .KESI YA NGEDERE USIMPELEKEE NYANI NI WALEWALE
      Kosea njia utaelekezwa,lakini usikosee mtu wakuoa /kuolewa naye,vinginevyo majuto yatakuwa sehemu ya maisha yako.tuliza kichwa unapochagua mwenzi wa maisha.

    5. #64
      kula kwa tindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 416
      Rep Power : 467
      Likes Received
      70
      Likes Given
      43

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Quote By Alexism View Post
      Nichangia lakini sijui kama nikotimamu,maana thead hii imetusi watu,badirisha heading mkuu. WENYE AKILI TIMAM TU!
      Mkuu Pole kama nimekukwaza..
      Hivi jiulize, MP anasimama Bungeni anaisifu Serikali kua imepiga hatua kwa kuongeza Misaada na Mikopo, alafu mwananchi anamsifia huyo MP,unadhani HUYU ANA AKILI TIMAMU?

    6. #65
      kula kwa tindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 416
      Rep Power : 467
      Likes Received
      70
      Likes Given
      43

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      [QUOTE=nivea;4223989]
      Quote By kula kwa tindo View Post
      Vipi kwenye Jimbo lako,Ulishawahi kuhoji kuhusu maendeleo yenu kwa MP wako?
      Na ulishahudhuria japo kikao kimoja cha kiongoji?
      [/QUOTE
      KWA BAHATI MBAYA KWETU KUNA GAMBA NDUNGULILE HATA TULIPOPANDISHIWA NAULI YA KIVUKO KWA 200%ALIKAA KIMYA JE UTAHOJI NINI TENA .KESI YA NGEDERE USIMPELEKEE NYANI NI WALEWALE
      Duh.. Pole sana, lakini bado hujachelewa Elimu ya utambuzi iko open.... Waalike hapa Jamvini Jamaa na Marafiki ili tupeane maneno ya Busara ili kwa pamoja Tuinusuru Tanzania yetu inayonyonywa na Mabeberu.. Pamoja Daima usikate tamaa....
      Nivea likes this.


    7. #66
      christine ibrahim's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2012
      Posts : 2,887
      Rep Power : 946
      Likes Received
      471
      Likes Given
      440

      Default

      Quote By Maundumula View Post
      KIla nchi duniani ina mikopo. Kwa kifupi hatuwezi kujiendesha bila mikopo kwakuwa hata Marekani na China wana mikopo.
      Toa sababu!.....sisi tuna kila kitu hatuna sababu ya kukopa km rasilimali zitasimamiwa vzr,bt c o kwa system iliyopo!

    8. #67
      kula kwa tindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 416
      Rep Power : 467
      Likes Received
      70
      Likes Given
      43

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Uko Sahihi kwa 100%,
      Je! Ulisha wahi mhoji MP wako (kama ulipiga kura) Juu ya usimamizi wa Raslimali zenu? Na yeye anasimamia vp maendeleo yenu? Uliwahi hudhuria vikao vya selikali ya mtaa wenu?
      Quote By webondo View Post
      Hahahaha! Haya bhana, labda nichangie kiduchu!
      Umezungumzia mambo mawili hapo; MIKOPO NA MSAADA. Kwa issue ya mkopo kama nchi nadhani hilo halina shaka, nchi nyingi duniani maskini na tajiri (Uchina, Marekani na zingine) zina mikopo, hii ina maana kuwa nchi kukopa au kudaiwa mkopo ni kawaida na wala sio dhambi.

      But; kuendesha nchi kwa msaada ni mbaya, hasa kwa nchi yenye rasilimali za kutosha kama Tanzania na zingine. Kwahiyo mtazamo wangu ni kuwa haileti maana sana kwa nchi kujiendesha kwa msaada.

    9. #68
      kula kwa tindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 416
      Rep Power : 467
      Likes Received
      70
      Likes Given
      43

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Thanks Mkuu.. Ndio maana nilisema WACHANGIE WALIO NA AKILI TIMAMU.. Nilimaanisha Sihitaji USIASA HAPA.. Kwani Siasa ndizo zimetufikisha HAPA.. UTAJIRI TUNAO LAKINI TUKO FRONT KWA KUOMBAOMBA ..

      Quote By kitero View Post
      Mtoa mada natumaini wengi hawajamuelewa,hapa kunawengine tumesha anza siasa.Mikopo ni muhimu sana katika kuleta maendeleo,tena nchi jajiri na kubwa ndiyo zinaongoza kwa mipoko,ila hazipewi misaada.Nijinsi gani tutakavyo weza kutumia miko na misaada ili tusiwe tegemezi wa misaada? Na si tegemezi wa mikopo

    10. #69
      Hayajamani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2012
      Location : Utopia
      Posts : 625
      Rep Power : 476
      Likes Received
      174
      Likes Given
      404

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Inawezekana tukaendelea kwa kutegemea misaada na makusanyo ya nchi pia. Kikubwa ni uadilifu na uwajibikaji. Kuhakikisha kuwa mapato ya nchi kwa vyanzo vya ndani yanakusanywa kama ipasavyo kwa uadilifu, pia kuongeza nguvu katika uzalishaji wa viwanda, kilimo na elimu ili huduma za kijamii ziwe bora kwa maisha bora pia.

      Budget isiwe inategemea zaidi misaasa (pledges), walau asilimia kama 60 - 70% iwe ni mapata ya nchi ambapo zaidi ya nusu ya budget ya maendeleo itokane na mapato ya nchi na asilimia fulani ndogo itegemee wafadhili. Tatizo ni kwamba kuna vyanzo vingi na vya kutegemeka vya mapato ya nchi vinakuwa na maslahi ya kifisadi kwa kunufaisha wachache hivyo mapato yakusanywayo hapa nchini kuwa madogo sana.

      Mfano ushuru wa biashara kubwa kubwa, migodi, uingizaji wa bidhaa, utalii utaona mambo mengi yanakwepa kodi au kukusanywa kidogo ukilinganisha na uhalisia wa biashara. Hivyo hunufaisha mafisadi (wahuni) wachache. Pia siasa iwe nzuri bila kukumbatia mafisadi wachache wanaotaka vyote viwe vyao.

      Pia wananchi wajikite zaidi kwenye kilimo, biashara na shughuli nyingine za kiuchumi. Tuache kuendekeza malumbano ya kijingakijinga ya haya madini tulioletewa na wageni wahuni (hasa Wazungu na Waarabu). Tuache uvivu na kujishughulisha kiakili na kimwili.

      Uwekezaji uwepo ila kuhakikisha nchi inafaidi sio kupunjika, Mfano wawekezaji wa madini wanaweza kukaa miaka kadhaa eti wanachukua udongo ukapimwe nje (tonnages) na hata wakianza exploitation nchi haifaidiki sana.

      Serikali kuongoza/kushauri vyanzo vya kiuchumi ili wananchi wake wapate ajira na kuwa na masha bora. Ugawanaji wa pato la nchi pia, mfano nchi yetu karibu maendeo yote yana vyanzo vizuri vya kiuchumi. Lakini sababu ya kuwa na akili ya kushikiwa hatujui au tukigundua inakuwa ni kuchelea.

      Mfano Mikoa ya kusini kuna madini, pia kilimo, biashara, Uvuvi lakini no exploitation of hizo resouces. Tatizo lingine distribution of economy, ni aibu kusikia eti 70% ya pato la nchi lipo Dar Es Salaam! What is Dar es Salaam? Hivi tsunami ikija kutokea bahari na kufunika Dar ina maana TZ imekwisha!

      Tuhamasishe maendeleo ya nchi nzima, ingawa ni lazima maeneo fulani yawe mbele kwa mengine, lakini sio 70% ya pato la nchi eneo moja kama inavyoonekana Dar. Badala yake kuna foleni zisizokuwa na sababu na kupoteza muda mwingi wa kufanya kazi, tatizo la high population density isiyokuwa na sababu kwa ajili ya serikali kushindwa kushughulikia na kuratibu huduma muhimu za kimaendeo sehemu nyingine za nchi.

      Mkakati wa kupeleka makao makuu ya nchi Dodoma ulikuwa ni mpango mzuri sana, lakini viongozi wa serikali wameshindwa kutekeleza hilo. Ina maana kama Raisi akihama rasmi na kuacha pale ikulu karibu na soko la samaki kuwa meseum, vitu vingi vitahamia Dom na maeneo mengine na kusaidia kupunguza misongamano isiyo ya lazima Dar na pia maendeleo kusambaa maeneo mengine.

      Hivyo tukijipanga na kubadili tabia tunaweza kusonga mbele kwa kwa kutegemea mapato yetu kwa kiasi kikubwa na wafadhili kwa kiasi fulani pia.

    11. #70
      SJUMAA26's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Posts : 343
      Rep Power : 629
      Likes Received
      69
      Likes Given
      2

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Quote By Maundumula View Post
      KIla nchi duniani ina mikopo. Kwa kifupi hatuwezi kujiendesha bila mikopo kwakuwa hata Marekani na China wana mikopo.
      Una uhakika kuwa kila nchi duniani inakopa, au umejazwa ujinga na kuaminishwa upumbavu na Magamba? Halafu, kama Uingereza wanaruhusu ushoga, na sisi Tz lazima tuwe hivyo?

    12. #71
      Ng'wanangwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th August 2010
      Posts : 6,016
      Rep Power : 1656
      Likes Received
      1138
      Likes Given
      419

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      ina maana 2siojadili huu mnakasha ha2na akili? duh!
      CCM HAIKUBALIKI ...TUSHIRIKIANE KUITOKOMEZA...

      REST IN PEACE, DR.D.D. HAULE...Wema hawana Maisha

    13. #72
      stroke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2012
      Posts : 1,563
      Rep Power : 682
      Likes Received
      170
      Likes Given
      5

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      bado muda wa kufanya hivyo haujafika, lakini nchi ni kama kampuni, no matter how rich you may be..lazima itafikia mahali utahitaji kukopa ili kufanya baadhi ya mambo..tuseme..labda kupunguza utegemezi ikwa 80% hiyo 20% sio mbaya tukiwa tunakopa..lakini tukiwa na uwezo mzuri wa kulipa kwa wakati..ili kujikwamua..

    14. #73
      Najijua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2010
      Location : Morogoro - Tanzania
      Posts : 905
      Rep Power : 595
      Likes Received
      124
      Likes Given
      39

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Nyerere alifanya mengi hii NCHI pasipo kuchimba madini wala utalii haukuwa chanzo kikubwa cha pato la taifa.

      Nyerere aliweza yote hayo kwa KILIMO ambakop LEO mnaowaita VIGOGO na washirika wao wa kibiashara wameji binafsishia mashamba hayo na sasa wameyatelekeza kuwa MAPORI.

      Tunaweza kabisa tukiwa serious na KILIMO, tunaweza tukikusanya KODI ipasavyo na toka kwa wote bila kuweka ujanja ujanja, tunaweza tukiacha MATUMIZI YASIYO YA LAZIMA, tunaweza tukirekebisha mikataba ya MADINI na kupata gawio stahiki, tunaweza mbuga zetu zikisimamiwa ipasavyo


      Quote By kula kwa tindo View Post
      Kuna maswali mengi yamekua yanasumbua Akili,hasa akili za wenye ufahamu wa juu..
      Je!! Kwa Nchi ya Tanzania inaweza kuendesha shughuli zake bila kutegemea misaada na mikopo toka Nchi za nje?

      Na endapo unadhani inawezekana Tanzania ikaendesha bila huo utegemezi, au haiwezi kuachana na utegemezi..
      TOA SABABU ZAKO HAPA!

      Kwanini haiwezi kutegema Mikopo na misaada?

      Kwanini inaweza kuendesha shughuli zake bila misaada na mikopo?
      "Be the Window through which many young will see their future"

    15. #74
      sir.JAPHET's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Posts : 611
      Rep Power : 479
      Likes Received
      90
      Likes Given
      45

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      ^tumefika hapa tulipo kwa UDHAIFU WA RAIS,
      UPUUZI WA CCM,
      UZEMBE WA BUNGE NA WABUNGE...wa ccm^

    16. #75
      Ernesto Che's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 606
      Rep Power : 549
      Likes Received
      99
      Likes Given
      24

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Quote By kula kwa tindo View Post
      Kuna maswali mengi yamekua yanasumbua Akili,hasa akili za wenye ufahamu wa juu..
      Je!! Kwa Nchi ya Tanzania inaweza kuendesha shughuli zake bila kutegemea misaada na mikopo toka Nchi za nje?

      Na endapo unadhani inawezekana Tanzania ikaendesha bila huo utegemezi, au haiwezi kuachana na utegemezi..
      TOA SABABU ZAKO HAPA!

      Kwanini haiwezi kutegema Mikopo na misaada?

      Kwanini inaweza kuendesha shughuli zake bila misaada na mikopo?
      Tutaachana na utegemezi iwapo serikali itakuwa na ubunifu wa vyanzo vya mapato zaidi ya sigara na pombe. Kuna watu wengi wana uwezo wa kubuni vyanzo vya mapato ila serikali imedumaa akili kwa kutegemea kuiba maliasili ya nchi. Watupe nafasi chadema tubadilishe hali ya uchumi wetu kwa kutumia utajiri aliotupatia Mungu
      "If there is no struggle, there is no progress.”

    17. #76
      Ernesto Che's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 606
      Rep Power : 549
      Likes Received
      99
      Likes Given
      24

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Quote By SJUMAA26 View Post
      Una uhakika kuwa kila nchi duniani inakopa, au umejazwa ujinga na kuaminishwa upumbavu na Magamba? Halafu, kama Uingereza wanaruhusu ushoga, na sisi Tz lazima tuwe hivyo?
      Ni kweli mkuu kuna nchi hususan za Middle East hazina madeni, pia Vatican, na Scandinavain
      "If there is no struggle, there is no progress.”

    18. #77
      Kevin.A's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd April 2012
      Posts : 12
      Rep Power : 366
      Likes Received
      4
      Likes Given
      61

      Angry re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Wewe mtoa mada (kula kwa mtindo)...Kuwa mwerevu na acha zarau na kebehi...Kwani Title ingekuwa "Naomba Tujadili hili" bila kuweka " KWA WENYE AKILI TIMAMU TU!!" ujumbe wako usingefika?Je ni kweli baadhi ya wanachama wa JF hawana akili timamu?Sijaipenda kabisa..

    19. #78
      nyanzalapy's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th April 2012
      Posts : 35
      Rep Power : 370
      Likes Received
      11
      Likes Given
      18

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Quote By christine ibrahim View Post
      Toa sababu!.....sisi tuna kila kitu hatuna sababu ya kukopa km rasilimali zitasimamiwa vzr,bt c o kwa system iliyopo!
      Nionavyo mimi ni kweli tuna rasilimali kemkem zinazoweza kututoa hapa tulipo ila tatizo kubwa linaloikumba nchi yetu ni technology yetu, hatuwezi ku utilize hizi resources kwa kiwango kitakacho tusababisha kuepukana/kupunguza kiwango cha mikopo.

      Nionavyo ni kwamba ushauri kwa serikali izidishe nguvu kwenye kuhakikisha technolojia yetu inakuwa, Pia ipunguze kuwapatia wawekezaji wageni maeneo ambayo yana rasilimali zisizojizalisha mpaka ambapo tutakuwa na uwezo wa kuzivuna kama taifa tuzivune wenyewe na sio wageni (ikiwezekana serikali ndio iwe inasimamia uvunaji wa rasilimali hizo pale tutakapokawa tayari kitaaluma na technolojia), Pamoja na michango mengi ambayo imetolewa na wachangiaji wengine huko mwanzo.

      Pia nashauri ifikie wakati Siasa na Taaluma vitenganishwe Tanzania ili kuleta maendeleo ya Nchi, nasema hivi nikimaanisha kwamba kuna tabia ya wanasiasa wetu (sio wote) kuwaingilia wataalam wetu kwa madai kuwa wapigakura wangu wanataka iwe hivi bila kuangalia ushauri wa kitaalam ambao umezingatia faida na hasara za utekelezaji wa hilo jambo kwa namna hiyo, (tumeshuhudia hata watumishi wamekuwa wakishushwa vyeo sababu za kisiasa),

      Sambamba na hilo pia watumishi tuache ushabiki wa kisiasa katika kutekeleza majukumu yetu bali tufanye kazi kulingana na taratibu na sheria za kazi husika hapa namaanisha kuwa sio sababu Serikali inayotawala ni CCM basi mimi kwa namna moja au nyingine nakwamisha utekelezaji wa jambo fulani ili tu lawama ziende kwa utawala chama husika kuwa wameshindwa kulifanikisha jambo husika,

      Au sababu halmashauri fulani inaongozwa na chama tofauti na CCM basi wafanyakazi wenye mlengo tofauti wakwamishe mambo kwa makusudi ili ionekane kuwa hicho chama kimeshindwa kutekeleza majukumu yake, Nafikiri kwa staili hii nchi yetu milele itakuwa ni tegemezi,

      Kwenye swala la kuleta Maendeleo au kujenga Taifa, tofauti za kisiasa zisichukue nafasi ikiwezekana Tanzania tuwe na sera inayohamasisha Utaifa kwanza, siasa baadae.
      "Never Make Someone your priority ,While they make you just an option"

    20. #79
      Acha Uvivu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th April 2011
      Posts : 418
      Rep Power : 495
      Likes Received
      103
      Likes Given
      13

      Default

      Quote By Maundumula View Post
      KIla nchi duniani ina mikopo. Kwa kifupi hatuwezi kujiendesha bila mikopo kwakuwa hata Marekani na China wana mikopo.
      Wewe hapa hapajakufaa, mkopo na msaada unashindwaje kutofautisha? Na mleta mada katahadharisha, kasema kwa wenye uwezo wa kufikiri tu. Wewe hujafudhu.

    21. #80
      Katavi's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 31st August 2009
      Location : Lyamba Lya Mfipa
      Posts : 19,929
      Rep Power : 16838
      Likes Received
      2640
      Likes Given
      2033

      Default re: THINKERS: Naomba Tujadili hili

      Tunaweza kujiendesha wenyewe endapo tutarudiwa na fahamu.

    Page 4 of 7 FirstFirst ... 23456 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...