Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

    Report Post
    Results 1 to 19 of 19
    1. #1
      Return Of Undertaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Posts : 666
      Rep Power : 543
      Likes Received
      466
      Likes Given
      0

      Default Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      *Ni kwa viongozi kukataa kuhojiwa

      *Yasisitiza kuchunguza tuhuma zao

      *Yaonya haitakubali kuyumbishwa


      JESHI la Polisi limesema licha ya viongozi wa Chadema kukataa kuhojiwa, litaendelea kuchunguza tuhuma za chama hicho dhidi ya baadhi ya maofisa wa serikali na kuchukua hatua zaidi.
      Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso alisema jeshi hilo haliwezi kuyumbishwa na mtu au kikundi cha watu katika kutekeleza majukumu yake na litafanya kazi kwa kufuata sheria na maadili.

      Kauli hiyo imetolewa siku moja baada ya Kamati Kuu ya Chadema kukataa baadhi ya viongozi wake kuhojiwa ikisema haioni sababu ya kutii agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi.

      Dk. Nchimbi alitoa agizo hilo baada ya viongozi watatu wa Chadema, Katibu Mkuu, Dk. Wilbrod Slaa, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kudai baadhi ya maofisa usalama wa taifa wamekuwa wakiwafuatilia wakiwatishia kuwaua.

      “Jeshi la polisi ni chombo cha umma kinachowajibika kulinda watu na mali zao, pia tunatekeleza kazi zetu kwa haki, usawa na bila ubaguzi wowote. Hili la viongozi wa Chadema kukataa kuhojiwa haliingii akilini hata kidogo.

      “Kwa akili ya kawaida, chukulia mtu amevamiwa nyumbani kwake na majambazi akapiga kelele kuomba msaada na askari au watu wengine wakafika kumpatia msaada, kweli atashindwa kuwaelezea kilichompata?

      “Hawa Chadema kukataa kwao hakutuzuii sisi kufanya kazi na hatuwezi kuyumbishwa na kikundi au mtu yeyote bali tunafanya kazi kwa mujibu wa sheria na maadili.

      “…sitowaeleza sasa tunachokifanya ndani ya jeshi la polisi lakini baada ya uchunguzi wetu kukamilika tutafanya uamuzi… isitoshe katika malalamiko yao waliwataja watu kwa majina,”alisema Senso.

      Taarifa zilizopatikana ndani ya jeshi hilo zilidai kuwa hatua ya viongozi wa Chadema kukaidi kuhojiwa kunaweza kusababisha wakamatwe.

      Juzi Dk. Slaa alitangaza kwamba hakubaliani na agizo la Dk Nchimbi kutaka kuwahoji kwa kuwa akisema kuwa yeye na wenzake hawana tena imani na vyombo vya serikali ikiwamo polisi.

      Dk. Slaa alilitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wake lenyewe kuhusiana na madai yao na kutoa tamko na sio kuwahoji wao ambao ndio walalamikaji.

      Alisisitiza kwamba Chadema hakina imani na polisi kwa kuwa wamekuwa wakipuuza malalamiko wanayopelekwa na chama hicho.

      Chadema imekuwa ikiwasilisha madai yake mengi polisi yakiwamo ya wabunge wake kupigwa mkoani Mwanza lakini hakuna hatua zilizochukuliwa, alisema.

      Dk. Slaa alisema kama Serikali isipokaa vizuri katika usalama wa raia wake na kutimiza wajibu na ahadi zake kwa Watanzania, taifa litakwenda pabaya.

      Naye Msaidizi wa Usalama wa Taifa, Jack Zoka ambaye ni mmoja wa maofisa usalama aliyetajwa kuhusika kuwatisha viongozi hao wa Chadema amekwisha kutoa kauli akidai kuwa malalamiko ya viongozi wa CHADEMA ni propaganda za siasa na zinapaswa kupuuzwa.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Naytsory's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 725
      Rep Power : 761
      Likes Received
      127
      Likes Given
      2

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Polisi wajiangalie vizuri, kwani Watanzania wengi kwa sasa hawana imani na vyombo vya dola kutokana matukio yaliyowahi kutokea na yanayotokea sasa ni lazima wananchi wengi watakosa imani. Inaonekana vyombo vya dola na usalama wa Taifa viko kwa maslahi ya Chama tawala kitu ambacho ni hatari kwa amani ya Taifa letu. Tunamwomba Mwenyezi Mungu awaondoe Watawala wenye nia kama hii.

    4. #3
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,731
      Rep Power : 2268
      Likes Received
      602
      Likes Given
      783

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Hata wao wanaweza kuwa ni kundi la watu tu. Issue ni Tabia.
      Ndibalema likes this.
      Simple life is healthier than egoism.

    5. #4
      cheichei2010's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th September 2010
      Posts : 544
      Rep Power : 549
      Likes Received
      182
      Likes Given
      42

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Niambie ni Mtanzania gani mwenye imani na jeshi la polisi?Ukiwa na tatizo umeenda kuto taarifa,unapigwa mzinga kwanza halafu ndio unaeleza tatizo.wanaweza wakampata mhalifu,wakala hela yake halafu wanakuja kukushauri uachane na hiyo kesi kwani haitafanikiwa.Huku ukiwaacha wamekula hela yako na ya mhalifu.
      dbwogi likes this.

    6. #5
      Udaa's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th June 2012
      Posts : 230
      Rep Power : 397
      Likes Received
      17
      Likes Given
      0

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Police thithiem sina imani nao.hata wao wanajijua jinsi wtz tusivyo na imani nao.


    7. #6
      Nyakageni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,259
      Rep Power : 1543
      Likes Received
      770
      Likes Given
      52

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Polisi yenyewe ni kakikundi kadogo ka watu!

    8. #7
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,460
      Rep Power : 1190
      Likes Received
      1436
      Likes Given
      939

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Quote By Return Of Undertaker
      *Ni kwa viongozi kukataa kuhojiwa

      *Yasisitiza kuchunguza tuhuma zao

      *Yaonya haitakubali kuyumbishwa


      JESHI la Polisi limesema licha ya viongozi wa Chadema kukataa kuhojiwa, litaendelea kuchunguza tuhuma za chama hicho dhidi ya baadhi ya maofisa wa serikali na kuchukua hatua zaidi.
      Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso alisema jeshi hilo haliwezi kuyumbishwa na mtu au kikundi cha watu katika kutekeleza majukumu yake na litafanya kazi kwa kufuata sheria na maadili.....
      Kama suala la kuwataja watu kwa majina ni ishu mbona Regnald Mengi aliwataja mpaka kwa majina Polisi waandamizi kuhusika katika mchezo mchafu wa kula hongo ili wambambikize kesi ya madawa ya kulevya mwanaye mbona kimyaaa!!

      Watanzania tuamke Tanzania hamna Polisi huru hiki chombo nahisi kinafanya kazi kwa maelekezo ya kikundi fulani cha wahuni, nitasimamia huu mfano wangu wa aliyoyasema Regnald Mengi mpaka naenda kaburini.
      Ndibalema likes this.
      Mnang'oa meno ya Tembo ili mukayauze, mnang'oa meno na Kucha za Watanzania wasio na hatia ili iweje?

    9. #8
      KOMBAJR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th November 2011
      Posts : 3,917
      Rep Power : 5962
      Likes Received
      809
      Likes Given
      229

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Hivi yule Polisi ayeita rai Panya kule Arusha aliishia wapi?halichukuliwa hatua gani?Je yule askari inayesadikiwa kuwa ndiyo alikuwa muhusika mkuu katika ile kesi ya wafanyabiashara na Jaji akaagiza akamatwe mbona mpaka leo hatujasikia kitu?
      Face Reality As it Is, Not As it Was or As You Wish It To Be.

    10. #9
      Ndet's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 29th June 2012
      Posts : 5
      Rep Power : 349
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Quote By Naytsory
      Polisi wajiangalie vizuri, kwani Watanzania wengi kwa sasa hawana imani na vyombo vya dola kutokana matukio yaliyowahi kutokea na yanayotokea sasa ni lazima wananchi wengi watakosa imani. Inaonekana vyombo vya dola na usalama wa Taifa viko kwa maslahi ya Chama tawala kitu ambacho ni hatari kwa amani ya Taifa letu. Tunamwomba Mwenyezi Mungu awaondoe Watawala wenye nia kama hii.
      Nawaunga mkono viongozi wa cdm kwa msimamo wao, kwasababu wabunge wao wa mwanza walijeruhiwa, lakini mpaka leo polisisiemu hawajasema kitu. kesi ya ngedele kumpelekea nyani utakuwa unachekesha.

    11. #10
      Baba Hellen's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2012
      Location : TANGA
      Posts : 388
      Rep Power : 424
      Likes Received
      28
      Likes Given
      13

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      hawa polisi wenyewe ni sehemu ya tatizo alafu niaibu chombo kikubwa kamahiki kujidhalilisha mbele ya umma JAMANI UUUUUWI!!!! Nchi hii kila kitu kime EXPIRE

    12. #11
      Ndibalema's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th April 2008
      Location : Mbagala
      Posts : 6,641
      Rep Power : 2010
      Likes Received
      1656
      Likes Given
      1635

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Ni vizuri Mwema na maafande wake wakajua kwamba Chama chochote kinaweza kukaa madarakani hivyo wasije wakamtukana mamba kabla hawajavuka mto.
      "Makalio ya sufuria hayaogopi moto"

    13. #12
      Bobuk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 2,069
      Rep Power : 923
      Likes Received
      837
      Likes Given
      0

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Hawa Polisi vipi? au ndiyo wanazidi kutuaminisha kwamba JESHI la POLISI huwa wanajiunga VILAZA Dr. Ulimboka aliwataja kwa majina watu waliohusika kumteka na kumtesa tunaomba basi kwanza wakawahoji
      1. ACP Msangi
      2. Abeid Afisa wa Ikulu
      3. Pinda aliyesema Liwalo na liwe

    14. #13
      Ringo Edmund's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2010
      Location : MDAWI
      Posts : 3,671
      Rep Power : 1361
      Likes Received
      885
      Likes Given
      586

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      tuongeze vifaa gani ili intelejensia iweze kugundua mambo ya uhalifu na wahalifu badala ya maandamano na mikutano?
      au tochi ya intelejensia imeisha betri?
      au tuvunje intelejejsia na tuunde intelejensia nyingine?
      mbona imefanya kazi kwenye faru na mtalii?
      ​kusema ni fedha na kusikilizwa ni zahabu.

    15. #14
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,188
      Rep Power : 24275
      Likes Received
      4683
      Likes Given
      2300

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Polisi wetu ni wanasiasa tulishawazoea
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    16. #15
      jmushi1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2007
      Posts : 14,376
      Rep Power : 16493
      Likes Received
      4301
      Likes Given
      5491

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Wanatoa ahadi eti uchunguzi ukikamilika watatoa taarifa, at the same time, wamewatisha kina Slaa kuwa wanaweza kuwakamata.Sasa ina maana wakiwakamata ndo watasema?Ama wana mpango wa kung'oa watu meno na kucha?
      "One of the penalties for refusing to participate in politics is that you end up being governed by your inferiors"-Plato

    17. #16
      babujii's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th April 2012
      Posts : 64
      Rep Power : 372
      Likes Received
      5
      Likes Given
      31

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Quote By Return Of Undertaker
      *Ni kwa viongozi kukataa kuhojiwa

      *Yasisitiza kuchunguza tuhuma zao

      *Yaonya haitakubali kuyumbishwa


      JESHI la Polisi limesema licha ya viongozi wa Chadema kukataa kuhojiwa, litaendelea kuchunguza tuhuma za chama hicho dhidi ya baadhi ya maofisa wa serikali na kuchukua hatua zaidi.
      Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso alisema jeshi hilo haliwezi kuyumbishwa na mtu au kikundi cha watu katika kutekeleza majukumu yake na litafanya kazi kwa kufuata sheria na maadili.

      Kauli hiyo imetolewa siku moja baada ya Kamati Kuu ya Chadema kukataa baadhi ya viongozi wake kuhojiwa ikisema haioni sababu ya kutii agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi.

      Dk. Nchimbi alitoa agizo hilo baada ya viongozi watatu wa Chadema, Katibu Mkuu, Dk. Wilbrod Slaa, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kudai baadhi ya maofisa usalama wa taifa wamekuwa wakiwafuatilia wakiwatishia kuwaua.

      “Jeshi la polisi ni chombo cha umma kinachowajibika kulinda watu na mali zao, pia tunatekeleza kazi zetu kwa haki, usawa na bila ubaguzi wowote. Hili la viongozi wa Chadema kukataa kuhojiwa haliingii akilini hata kidogo.

      “Kwa akili ya kawaida, chukulia mtu amevamiwa nyumbani kwake na majambazi akapiga kelele kuomba msaada na askari au watu wengine wakafika kumpatia msaada, kweli atashindwa kuwaelezea kilichompata?

      “Hawa Chadema kukataa kwao hakutuzuii sisi kufanya kazi na hatuwezi kuyumbishwa na kikundi au mtu yeyote bali tunafanya kazi kwa mujibu wa sheria na maadili.

      “…sitowaeleza sasa tunachokifanya ndani ya jeshi la polisi lakini baada ya uchunguzi wetu kukamilika tutafanya uamuzi… isitoshe katika malalamiko yao waliwataja watu kwa majina,”alisema Senso.

      Taarifa zilizopatikana ndani ya jeshi hilo zilidai kuwa hatua ya viongozi wa Chadema kukaidi kuhojiwa kunaweza kusababisha wakamatwe.

      Juzi Dk. Slaa alitangaza kwamba hakubaliani na agizo la Dk Nchimbi kutaka kuwahoji kwa kuwa akisema kuwa yeye na wenzake hawana tena imani na vyombo vya serikali ikiwamo polisi.

      Dk. Slaa alilitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wake lenyewe kuhusiana na madai yao na kutoa tamko na sio kuwahoji wao ambao ndio walalamikaji.

      Alisisitiza kwamba Chadema hakina imani na polisi kwa kuwa wamekuwa wakipuuza malalamiko wanayopelekwa na chama hicho.

      Chadema imekuwa ikiwasilisha madai yake mengi polisi yakiwamo ya wabunge wake kupigwa mkoani Mwanza lakini hakuna hatua zilizochukuliwa, alisema.

      Dk. Slaa alisema kama Serikali isipokaa vizuri katika usalama wa raia wake na kutimiza wajibu na ahadi zake kwa Watanzania, taifa litakwenda pabaya.

      Naye Msaidizi wa Usalama wa Taifa, Jack Zoka ambaye ni mmoja wa maofisa usalama aliyetajwa kuhusika kuwatisha viongozi hao wa Chadema amekwisha kutoa kauli akidai kuwa malalamiko ya viongozi wa CHADEMA ni propaganda za siasa na zinapaswa kupuuzwa.
      ni kweli haiingiii akilini mtu kuvamiwa na majambazi na kukataa kuhojiwa na mamlaka zinazokubalika lakini ikiwa jambazi amekutegua kiuno halafu anakuja kukuchukua akupeleke hospitali,je! hii pia inaingia akilini una hakika gani kama ndo anataka akakuangamize ili kupoteza ushahidi? hapa panahitajika mtu tofauti na haya majambazi ili kutafuta undani wa tatizo lililopo. jamani tusiwe wanasiasa hata katika mambo ya kitaaluma. POLISI acheni hizo.

    18. #17
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,533
      Rep Power : 1263
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      28

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Quote By Return Of Undertaker
      *
      Jeshi la polisi ni chombo cha umma kinachowajibika kulinda watu na mali zao, pia tunatekeleza kazi zetu kwa haki, usawa na bila ubaguzi wowote. Hili la viongozi wa Chadema kukataa kuhojiwa haliingii akilini hata kidogo.

      .
      kama kuna kitu jeshi la polisi halifanyi ni hilo hapo juu, mara ngapi tunaona mapolisi wanahusishwa na ujambazi..embu watutokee hapa
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune


    19. #18
      Lyceum's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2009
      Posts : 547
      Rep Power : 600
      Likes Received
      100
      Likes Given
      128

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      Mi nadhani polisi wanapaswa kutueleza/ kutupa matokeo ya vipaza sauti chumbani kwa Slaa na tuhuma nyingine. Huu sio wakati wa kutoa majibu mepesi kwa lengo la kuuaminisha umma mambo yasiyokuwepo.

      POLISI YANYENI KAZI YENU ACHENI SIASA ZA KIBABAISHAJI. Msifikiri umahiri wa kazi unatokana na mavazi yenu, la hasha. Tuanataka umahiri.

      After all wananchi wa leo wana uelewa mkubwa sana.

      We need intelligible explanations to such serious issues.

    20. #19
      Malova's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st April 2011
      Posts : 534
      Rep Power : 516
      Likes Received
      82
      Likes Given
      9

      Default Re: Polisi wawatisha viongozi wa CHADEMA

      POLI NYINYIEMU, mnaacha kutafuta ukweli wa tuhuma kwa kufanya uchungu mnataka kuwahoji walalamikaji. UPUUZI mtupu

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...