Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CHADEMA haiwapiganii Wananchi masikini

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. #1
      William Mshumbusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th March 2012
      Posts : 325
      Rep Power : 510
      Likes Received
      184
      Likes Given
      0

      Default CHADEMA haiwapiganii Wananchi masikini

      Kufanya siasa ni kitu kigumu sana. Na sisi tuko pembeni tu tukiwasukuma wenzetu wajitoe muhanga bila kuogopa kuwapigania wanyonge.

      Ni nani atakaebisha kuwa CHADEMA ni chama cha kufata upepo tu. Na matukio makubwa ya ajabu na yakutisha ni upepo tu na hayaachi madhara yoyote kwa viongozi.


      Mifano.EPA, RICHIMOND, ishu ya katibu wizara ya madini kuhonga wabunge JAIRO, MGAO wa umeme USIO NA KIKOMO, IPTL, SONGASI, MIRAHABA YA 3% KWENYE MADINI, MIGOMO YA WAFANYAKAZI na vifo vingi vyenye utata kama CHACHA WANGWE, prf Chachage, Amina, katibu wa chadema arumeru, Wakili aliyekuwa akiistaki selikali swala la mgombea binafsi. Aliyekuwa katibu mkuu wa wafanyakazi wa shirika la reli na aliongoza migomo mingi tu.

      Mashambulizi kwa Kubenea, Kiwia na mbunge wa ukerewe na sasa Ulimboka
      Yote haya ni upepo tu.


      Mi naamini nchi inaongozwa na wendawazimu na wakatimwingine tunahitaji kuacti uwendawazimu kidogo ndipo kieleweke. Kwa mtazamo wa sasa wa CHADEMA ambao ni wa wastani sana 2015 ata wakishinda hawatapewa nchi kama Arusha.

      Tusipende sana kukaa nyuma ya mawazo ya viongozi wetu wa vyama bila hata ya kuyahoji. Kwa mtazamo nilionao Mishahara ya wanasiasa na posho ni hongo tosha na zinafanikiwa sana kuwaziba midomo na kuwafanya wasaau kabisa matatizo ya wananchi wao na jinsi ya kuyatatua.

      Mwaka huu kanda ya ziwa shinyanga,MWANZA, tabora wanaupungufu mkubwa wa vyakula na wanategemea kuuza pamba ili wanunue vyakula. Bei ndio hiyo 650. Toka 1360 ilipoishia mwaka jana Wabunge tunaowategemea wanakula posho tu bungeni.

      Kwanini wasitoke warudi wafanye M4C KANDA YA ZIWA tuone uzalendo wao.

      Kumbuka watu wanaotegemea Pamba ni mil 16 Tz na kati yao mil 8 wanauwezo wa kupiga kura na nizaidi ya waliopiga kura wote tanzania uchaguzi ulioisha.

      Uchaguzi unaofata wakipiga kura asilimia 20 ya waliojiandikisha mtasema watanzania wajinga? Tunatumia akili nyingi mno kuadresi vitu vidogo.

      Naomba Lema apewe uwenyekiti ata kwa miezi sita tu. Au ata nyerere au Tundulisu. Naamini viongozi watashika adabu

      Mi ustaarabu wa Mbowe unanichosha mdahalo unapokuwa wa moto mjengoni utasikia. Jamani nanihii mwachie kiongozi wako wa upinzani azungumze na akiongea ni kupoza tu.

      Mi narudia tena na tena Kwa chadema safi hatuna haja ya kuwa na wanaharakati na vyama vya wafanyakazi vitakosa kazi kabisa

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      MTAZAMO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 4,230
      Rep Power : 2203
      Likes Received
      1813
      Likes Given
      2449

      Default Re: CHADEMA haiwapiganii Wananchi masikini

      CDM are not aggressive enough! huwezi ku compromise na CCM lazima washinikizwe kila sekunde,kila dakika hadi wajisalimishe!

    4. #3
      SHEMGUNGA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2012
      Posts : 332
      Rep Power : 437
      Likes Received
      21
      Likes Given
      0

      Default Re: CHADEMA haiwapiganii Wananchi masikini

      usiogope cdm inaenda step by step haikurupuki!

    5. #4
      mfarisayo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd November 2010
      Location : tanganyika
      Posts : 3,135
      Rep Power : 1063
      Likes Received
      463
      Likes Given
      1104

      Default Re: CHADEMA haiwapiganii Wananchi masikini

      Aaah! Shemejiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii iii, wewe tena?
      “Mwaka jana tulikutana na ‘single’ yaani waliandika mashairi kwa uchache, lakini mwaka huu tumepata albamu nzima…” :- Dk Ndalichako

    6. #5
      NewOrder's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 274
      Rep Power : 888
      Likes Received
      109
      Likes Given
      93

      Default Re: CHADEMA haiwapiganii Wananchi masikini

      Frustrations zako ni halali kabisa lakini umezitua kwa wrong person!! CCM ndio imeshindwa kuchukua hatua kukomesha mambo yote hayo. Unasikia jinsi mjengoni wanavounga mkono kwa asilimia wengine 200% matumizi ya bajeti zinazojadiliwa. Unasikia jinsi CHADEMA unaowalaumu wakipinga bajeti hizo na wakitoa maoni mbadala!!

      Nikukumbushe yafuatayo:
      a) Ni ninyi mnaobeza CHADEMA kufanya maandamano. Mnataka subira ifike 2015 Uchaguzi Mkuu.
      b) Ni ninyi mnaobeza miongozo na taarifa zinapoombwa na vyama vya upinzani.
      c) Ni ninyi mnaoaminishwa kuwa CHADEMA ni wanaharakati na mkaamini.
      d) Ni ninyi mlioukodolea wizi wa kura 2010 na kutoipigia kura UPINZANI. Hamkuwapa meno ya kurekebisha uliyoyataja.
      e) Ni ninyi mliodanganywa kwa wali, vilemba, khanga na t-shirts, fedha na lifti za maroli. Mkasahau picha kubwa!!!

      Ni udhaifu kudai CHADEMA atoke Bungeni aje kufanya M4C sehemu ulizozitaja na akiwaacha watu (wabunge wa CCM) waliosema "Kama sio elfu moja, pamba haitauzwa". Una haki gani ya kudai CHADEMA isimamie hilo wakati haiundi serikali iliyofanya maamuzi ya sh. 650??

      Tulia unyolewe, umeweka matumaini kwa CHADEMA wakati mbaya. Fanya marekebisho mwaka 2015 Ucahguzi Mkuu!
      KOMBESANA likes this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      William Mshumbusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th March 2012
      Posts : 325
      Rep Power : 510
      Likes Received
      184
      Likes Given
      0

      Default Re: CHADEMA haiwapiganii Wananchi masikini

      Neworder tuko pamoja mkuu nachoangalia chadema wanafanya nini na si wanasema nini?

      Na hapa naangalia Chadema kama Chama na si mtu kama mtu.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...