Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

    Report Post
    Page 2 of 2 FirstFirst 12
    Results 21 to 37 of 37
    1. #1
      Mikael P Aweda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 1,844
      Rep Power : 6549
      Likes Received
      2455
      Likes Given
      2232

      Default Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      WanaJF,
      Jumamosi, Mungu akinijalia nitahudhuria mkutano wa kwanza wa Tume ya Katiba watakapokuwa Kisarawe,pwani. Jambo hilo tunalifanya makusudi ili tupanguze yale tuliyo nayo kabla hatujapata fursa nyingine Dsm.

      Kwa kuwa zoezi hili linaenda kwa kasi sana, na kwa kuwa hatuna uhakika kama tunaweza kusema kila kitu wakija hapa Dsm, na kwa kuwa hawaendi kila mahali (nina maanisha kila kata au mtaa wako) na
      kwa kuwa baadhi yetu wanajf ni waajiriwa na tuko busy na hamtapata nafasi hii adimu sana na,
      kwa kuwa tayari kuna malalamiko ya wakuu wa wilaya kuwaandaa watu na kuwafundisha kitu cha kusema, na kwa kuwa baadhi ya wana Jf wako nje ya nchi na wanaitakia mema nchi yetu (mf mwanakijiji etc)
      Hivyo basi, kwa heshima na unyenyekevu tunaomba tukakuwakilishie hoja yako unayoona ni muhimu sana kupitia jukwaa letu murua na ambayo unahisi ni muhimu ikajumuishwa katika katiba mpya.

      Tumejipanga kuhakikisha kuwa kila hoja muhimu inayoboresha muskabali wa watanzania wote bila kujali mipaka vyama, dini, kabila inawasilishwa kwenye tume husika bila upendeleo.

      1) IKUMBUKWE; Vyama vinazaliwa na kufa lakini Taifa letu lipo hadi mwisho wa Dunia, hivyo ni matarajio yangu kuwa ushabiki wa kidini na kisiasa hautakuwepo ktk mjadala huu.

      2) Fafanua vizuri hoja yako ili ieleweke vizuri, kiasi kwamba mwana JF ye yote ambaye atapata fursa ya kuhudhuria mikutano hii ya Katiba aweze kuelezea vizuri kwa niaba yako (siyo lazima sisi).
      Sisi (kama watanzania kwanza kabla ya kuwa wanachadema) tunajitahidi kuratibu vizuri kila mahali lakini siyo garantii kuwa tutawasilisha kila jambo.

      Kwa hiyo, napendekezo uzi huu hapa JF uwe kisima cha kuchukua mawazo mapya kwa kila mwana jf kutoa hoja hapa ama kuchota mawazo mapya na kuyawasilisha ktk tume husika kwa kuwa tunatofautiana uwezo wa kuibua mambo yenye maslahi kwa nchi yetu, Pili,inawezekana hoja yako mimi sikubaliani nayo, hivyo yule mwenye mawazo kama yako atayawasilisha kwa niaba yako.

      NB; Paw,Silencer, PainKiller, Roulette, Fang, Buchanan, Cookie ni matarajio yangu kuwa uzi huu mtaupa muda kidogo ili tupate mawazo mengi kwa maslahi ya nchi yetu.

      Regards
      Aweda, Mikael
      FJM and jouneGwalu like this.
      Mikael P Aweda 0784 583 330
      Elimu kwanza

    2. RukaaJuu Final

    3. #21
      Mikael P Aweda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 1,844
      Rep Power : 6549
      Likes Received
      2455
      Likes Given
      2232

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Nimegundua mawazo mengi yapo kwenye utawala bora badala ya uongozo bora ( refer Prof Shivji na mijadala yake ITV) Tunahitaji pia kujadili Autonomy ya uongozi ktk ngazi ya Msingi/shina, kijiji/mitaa na wilaya.

      Uwezo wao wa kujichagulia viongozi, kumiliki ardhi na kuamua hatma ya maisha yao kwa ujumla. mjadala huu ni mwelekeo wa uongozi bora vs utawala bora.

      Kwa maoni yangu lazima tuachane na utawala bora ktk katiba mpya, badala yake tukazanie uongozi bora ambao umejikita kwenye dhana ya nguvu ya umma. Najua hili linahitaji maelezo marefu sana kueleweka kwa mtu ambaye hana background hii na hajamsikiliza prof Shivji.
      Mikael P Aweda 0784 583 330
      Elimu kwanza

    4. FJM
      #22
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,175
      Rep Power : 2569
      Likes Received
      5327
      Likes Given
      4587

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Quote By Mikael P Aweda
      Kwenye Red,
      FJM Hivi ni lazima Rais apendekeze halafu wabunge wapitishe JINA mmoja? Kwanini tusiseme kuwa Wataomba kazi kwa utaratibu tofauti kabisa wa kuchaguliwa bungeni ili wawe huru. Hapa namaanisha wakuu wa Polisi, mkiti wa tume ya Uchaguzi, Mkurugenzi wa Takukuru, DCI nk. Ni swali la ufahamu tu.
      Kwangu mimi sioni kabisa sababu ya kuwa na TAKUKURU, hii idara ifutwe, it is waste of public funds. Ukiwa na DPP, police zinazofanya kazi vizuri huna haja ya TAKUKURU.

      IGP, DCI, DPP, and most definately mwenyekiti wa tume ya uchaguzi wanaweza ku-apply hapo sina tatizo. Lakini kwa mkuu wa TISS lazima ufanyike utararibu mwingine tofauti na wa ku-apply na pendinge nilifiki internal organs zinasaidiana na ofisi ya rais ili kupata nominee, then bunge lipewe nafasi ya kuthibitisha au kukataa. (hapa ni kwa TISS), Lakini hata hivyo TISS yenyewe inabidi kuundwa upya including sheria zinasimamia hiyo taasisi.
      Mikael P Aweda and ng'wandu like this.

    5. #23
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2266
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      1. Tunataka Tanganyika Yetu

      2. Wakuu wa wilaya waondolewe, nafasi zao zishikwe na wabunge

      3. Majimbo yawe wilaya, na ya punguzwe

      4. Ili kinamama wagangamale viti maalumu vifutwe

      5. Wakuu wa mikoa wapigiwe kura (Uchaguzi mkuu)

      6. RAS na DAD wawe makatibu wa mikoa wakisaidiwa na wakurugenzi wanatosha kuwakilisha serikali

      7. Mawaziri na manaibu wao wasizidi 25.

      8. Wakuu wote wa taasisi nyeti waombe kazi, kamati ya bunge iwainterview, na wapitishwe na bunge (TISSS Nk)

      9. TISS iboreshwe kimfumo, na FIU, TAKAkuru na vingine viwe chini ya TISS) na policy zoa zipitiwe na kamati ya bunge. Kwanza nahisi hawana hata policies za operation (Hizi za mabwepande a-a)

      10 Mfumo wa kiutawala uwe unganifu, Kijiji, kata, Wilaya, Mkoa, Taifa. Miundo bado iko hovyo ngazi za chini.

      11. Tume isimamishe mara moja kazi za wajumbe wa nyumba kumi, maana ni wa CCM. Wasitambilike katika serikali ya mtaa

      12. Wajue kabisa kwamba wanatakiwa kuandika rasimu ya katiba ya Tanganyika kama standby.

      13. Jesh JWTZ lipunguzwe, hawana kazi, tuweke idadi ndogo na vifaa vya kisasa. Tupo sisi reserve army.

      14. Tuwe na viwango, vya chini katika shule zetu zote, bila hivyo isifunguliwe, afya NK.

      15. Viwanja vyetu vya michezo na vingine vilivyoporwa na CCM virudishwe serikalini

      16. Raisi awajibiswe na bunge na asiwe na mamlaka ya kuwajibisha bunge

      17. mawaziri wote wawajibishwe na bunge

      18. Wabunge, Madiwani, Maviti wote wawajibike kwa mabaraza yao.

      19. wajumbe wa mabaraza ngazi za chini wajulikane na wachaguliwe.

      20. Mikataba yote ya taifa ipitishwe bungeni, either katika kamati na ile mikubwa bungeni.

      21. TISS itoe taarifa zake kwenye magazeti, bungeni, na kadhalika. Ila tu zile za ulinzi ziende kwa kamati ya bunge. Eti hata ununuzi wa rada ni siri.

      Kwa kifupi tuna taka Dola Umma

      Aweda, Good work, unaelekea unapotakiwa.
      Last edited by Communist; 11th July 2012 at 17:00.
      Simple life is healthier than egoism.

    6. #24
      jouneGwalu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Location : Studio
      Posts : 2,341
      Rep Power : 969
      Likes Received
      1314
      Likes Given
      1755

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Safi sana Aweda!

      Binafsi sipo kwenye nafasi ya kutulia hapa ila ningependa kutoa mawazo ya mjumuisho, hvyo labda baadae nikipata mda nitafafanua au mtanisaidia kufafanua!

      Kwanza ni suala la structure ya Executive yetu, hvi ni lazima tuwe na Rais, Makamu na Waziri Mkuu?
      Nadhani ni mda sasa tuamue moja, kama tunamtaka waziri mkuu basi nafasi ya rais ni either ifutwe kwa maana ya kwamba tuwe na rais ambaye ni alama tu ya utaifa wetu ila hana mamlaka sana,
      au kama vipi tuondoe cheo cha Waziri Mkuu asiye na mamlaka kamili ya kuliwajibisha baraza ambalo hajaliteua wala kuiwajibisha serikali ambayo yeye ni mtendaji mkuu....
      Huu umekuwa ni mvurugo wa mda mrefu sana na umetuachia mgogoro wa maingiliano ya kimamlaka.
      Ni bora tuwe na Waziri Mkuu mwenye mamlaka kamili na Rais atakayekuwa kama ni nembo tu ya utaifa wetu ila asiwe mtendaji wala mfanya maamuzi, au tuwe na rais mwenye mamlaka kamili akisaidiwa na makamu wake ila hcho cheo cha waziri mkuu garasa tukifutilie mbali.

      Pia kuna masuala ya rasilimali za TAIFA, kama Watu, Madini, Gas, Mafuta, Ardhi, Mifugo, Misitu na rasilimali zingine zote za thamani za nchi tuangalie tunaweza kusema nini juu ya hivi vitu pia
      Mikael P Aweda likes this.

    7. #25
      kalendi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th March 2012
      Posts : 94
      Rep Power : 380
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Default

      1. Huduma zote za jamii zisimamiwe na serikali yaani( elimu, afya, maji na barabara)
      2. Viongozi wote tunaowachagua(kama walivyopendekeza wenzangu) ndio wasimamizi wa huduma zote
      3. Viongozi kwa kuwa ndio wasimamizi wa huduma hizo ni marufuku na ni mwiko kwa viongozi kwenda kupata huduma hizo kwenye taasisi binafsi au ngambo. Ni lazima wao na hata famila zao kupata huduma hizo kwenye taasisi za umma.

    8. Miaka 50

    9. #26
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,632
      Rep Power : 1110
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      756

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      1.tume ya uchaguzi iundwe kwa kushirikisha wajumbe wa vyama vyote na isiteuliwe na rais, iwe chini ya jaji mkuu.
      2.Wabunge wawe madarakani kwa vipindi viwili ya miaka mitano mitani basi
      3.Wananchi wawe na uwezo/ modality ya kumuondoa madarakani mbunge wao endapo atakuwa hatekelezi ahadi zake na kuwahudumia ipasavo
      4. Madaraka ya rais ni makubwa mno hasa ya uteuzi, pia sheria ikishatungwa na bunge hakuna haja rais kuisani iwe sheria, ikishapitishwa na bunge automatically iwe sheria
      5. Kinga ya rais ya kutoshitakiwa akiwa madarakani au baada ya madaraka iondolewe
      6.Matokeo ya uchaguzi wa urais yahojiwe mahakamani, na pia yakishatangazwa kuwe na kipindi cha mwezi mmoja kabla ya kuapishwa rais ili kama kuna mtu mwenye shaka na matokeo afungue kesi
      7.Idadi ya wizara na mawaziri itamkwe kwenye katiba mpya na kila rais ateue kufuatana na katiba sio ilivo sasa hivi anateua kwa kushauriana na mke na watoto wake
      8.Mawaziri wasiwe wabunge ila waombe kazi ya uwaziri wajiriwe na hakuna haja ya manaibu waziri na katibu mkuu wa wizara na wakurugenzi wanatosha kuongoza wizara, na mawaziri washiriki ushabiki wa vyama.
      9.Speaker wa bunge akitoka chama tawala naibu wake atoke kwenye chama rasmi cha upinzani bungeni yaani kinafuatia kwa wingi wa wabunge
      10.Jaji mkuu asiteuliwe bali aajiriwe na ajira idhibitishwe na bunge hivo hivo kwa mkurugenzi wa TAKUKURU, tume ya haki za binadamu, mkaguzi na mdhibiti mkuu wa serikali.
      11.Muundo wa muungano uwe na wa serikali tatu ya Tanganyika na Zanzibar zitakazoongozwa na mawaziri wakuu watakaoteuliwa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
      12.Adhabu ya kifo ifutwe kwenye sheria za nchi
      13. vyeo vya wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya vifutwe na badala ya wawepo wakurugenzi wa wilaya na mikoa watakaomba kazi hizo na ajira zao kuidhinishwa na bunge.

      14 .Chama cha siasa amabacho hakitapata hata mbunge mmoja wakati wa uchaguzi mkuu kifutwe mara moja

      kwa leo inatosha nitaendelea kuchangia mengine
      Mikael P Aweda and ng'wandu like this.
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    10. #27
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,632
      Rep Power : 1110
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      756

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Quote By jouneGwalu
      Safi sana Aweda!

      Binafsi sipo kwenye nafasi ya kutulia hapa ila ningependa kutoa mawazo ya mjumuisho, hvyo labda baadae nikipata mda nitafafanua au mtanisaidia kufafanua!

      Kwanza ni suala la structure ya Executive yetu, hvi ni lazima tuwe na Rais, Makamu na Waziri Mkuu?
      Nadhani ni mda sasa tuamue moja, kama tunamtaka waziri mkuu basi nafasi ya rais ni either ifutwe kwa maana ya kwamba tuwe na rais ambaye ni alama tu ya utaifa wetu ila hana mamlaka sana,
      au kama vipi tuondoe cheo cha Waziri Mkuu asiye na mamlaka kamili ya kuliwajibisha baraza ambalo hajaliteua wala kuiwajibisha serikali ambayo yeye ni mtendaji mkuu....
      Huu umekuwa ni mvurugo wa mda mrefu sana na umetuachia mgogoro wa maingiliano ya kimamlaka.
      Ni bora tuwe na Waziri Mkuu mwenye mamlaka kamili na Rais atakayekuwa kama ni nembo tu ya utaifa wetu ila asiwe mtendaji wala mfanya maamuzi, au tuwe na rais mwenye mamlaka kamili akisaidiwa na makamu wake ila hcho cheo cha waziri mkuu garasa tukifutilie mbali.

      Pia kuna masuala ya rasilimali za TAIFA, kama Watu, Madini, Gas, Mafuta, Ardhi, Mifugo, Misitu na rasilimali zingine zote za thamani za nchi tuangalie tunaweza kusema nini juu ya hivi vitu pia
      Nakuunga mkono hakuna haja ya makamu wa rais na waziri mkuu! mmojawapo anatosha,.pia hakuna haja ya manaibu waziri au manaibu katibu mkuu! wizara ikiwa na waziri, katibu mkuu na mkurugenzi mkuu imekamilika!!
      ng'wandu likes this.
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    11. #28
      FIDIVIN's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th August 2010
      Posts : 186
      Rep Power : 484
      Likes Received
      39
      Likes Given
      20

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Acheni mambo ya kikoloni, katiba mpya kila mtu anatakiwa ajisemee, nyie mnaenda kila mkutano kuziba nafasi za wengine, udhulieni mkutano mmoja toa maona yako basi, mnataka kumsemea nani?
      Hii ni kinyume na haki za wananchi na ni udhalilishaji mkubwa.

      Mmelewa support ya jf mnaanza kudhani nyie ndo wasemaji wa wananchi?

    12. #29
      kalendi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th March 2012
      Posts : 94
      Rep Power : 380
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      1. Tuwe na mikoa isiyozidi 12
      2. Kila wilaya iwe na; mkurugenzi na wataalamu mbalimbali watakaoshughulika na kazi mbalimbali ya kitaalum yanayohusiana na majukumu ya kila siku ya kiwilaya.
      3. Kila wilaya mbuge mmoja.
      4. Wizara zisizozidi 12.
      5. Hakuna meya
      6. Hakuna mkuu wa wilaya
      7. Hakuna katibu tarafa
      Mikael P Aweda likes this.

    13. #30
      Mikael P Aweda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 1,844
      Rep Power : 6549
      Likes Received
      2455
      Likes Given
      2232

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Quote By FIDIVIN
      Acheni mambo ya kikoloni, katiba mpya kila mtu anatakiwa ajisemee, nyie mnaenda kila mkutano kuziba nafasi za wengine, udhulieni mkutano mmoja toa maona yako basi, mnataka kumsemea nani?
      Hii ni kinyume na haki za wananchi na ni udhalilishaji mkubwa.

      Mmelewa support ya jf mnaanza kudhani nyie ndo wasemaji wa wananchi?
      Hatuendi kila mkutano mkuu, ila tunawawezesha wanaJF na watz kuchota mawazo mazuri hapa. Ila nini maoni yako kuhusu Ma DC wanaowakusanya watu wanaowataka na kuwapa cha kusema?
      ng'wandu likes this.
      Mikael P Aweda 0784 583 330
      Elimu kwanza

    14. #31
      Mikael P Aweda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 1,844
      Rep Power : 6549
      Likes Received
      2455
      Likes Given
      2232

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Vipi kuhusu uraia wa nchi mbili?
      Uongozi wa ngazi ya chini kabisa uanzie wapi? Misingi/mashina au vijiji/mitaa? Kwa kwanini?
      Vipi kuhusu nafasi ya mabalozi wa nyumba kumi? Turasimishe hiyo nafasi au ifutwe? If yes, why? If no, Why? Tusijikite mijini tu.
      Mikael P Aweda 0784 583 330
      Elimu kwanza

    15. #32
      Mikael P Aweda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 1,844
      Rep Power : 6549
      Likes Received
      2455
      Likes Given
      2232

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Quote By kalendi
      1. Huduma zote za jamii zisimamiwe na serikali yaani( elimu, afya, maji na barabara)
      2. Viongozi wote tunaowachagua(kama walivyopendekeza wenzangu) ndio wasimamizi wa huduma zote
      3. Viongozi kwa kuwa ndio wasimamizi wa huduma hizo ni marufuku na ni mwiko kwa viongozi kwenda kupata huduma hizo kwenye taasisi binafsi au ngambo. Ni lazima wao na hata famila zao kupata huduma hizo kwenye taasisi za umma.
      Mkuu no 1 na 2 nina swali,
      Nijuavyo, hata sasa huduma zote za umma zinasimamiwa na serikali au? Fafanua kidogo.
      Mikael P Aweda 0784 583 330
      Elimu kwanza

    16. #33
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2266
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Quote By Mikael P Aweda
      Hatuendi kila mkutano mkuu, ila tunawawezesha wanaJF na watz kuchota mawazo mazuri hapa. Ila nini maoni yako kuhusu Ma DC wanaowakusanya watu wanaowataka na kuwapa cha kusema?
      Kuna wengine hawapendi wengine waelewe, wanapenda waelewe wenyewe. Usishangae kamanda.
      Simple life is healthier than egoism.

    17. #34
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2266
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Quote By Mikael P Aweda
      Vipi kuhusu uraia wa nchi mbili?
      Uongozi wa ngazi ya chini kabisa uanzie wapi? Misingi/mashina au vijiji/mitaa? Kwa kwanini?
      Vipi kuhusu nafasi ya mabalozi wa nyumba kumi? Turasimishe hiyo nafasi au ifutwe? If yes, why? If no, Why? Tusijikite mijini tu.
      Hapana, tutatengeneza wahaini. Kama mtakubali basi na mwanamke mmoja aruhusiwe kuolewa na wanaume wawili.
      Mikael P Aweda likes this.
      Simple life is healthier than egoism.

    18. #35
      CHESEA INGINE's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th November 2010
      Posts : 170
      Rep Power : 467
      Likes Received
      14
      Likes Given
      164

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Hodi hodi wana jf. Nipo!. Hii mada nimeipenda.
      Ningetaka katika katiba yaingizwe haya.
      1.kwamba sera kuu za nchi ziingizwe kwenye katiba kusudi anayetaka uongozi atuambie atakavyotekeleza sera zetu. Isiwe kama sasa kila chama kinakuja na zake.
      2.wakuu wa mikoa wagombee kama wanavyofanya wabunge.
      3.elimu itamkwe ya kuwa ni bure kuanzia msingi mpaka chuo kikuu. Wakimaliza, jkt kwa kipindi cha miaka miwili.
      4.ardhi kamwe isimilikishwe kwa wageni kwa namna yeyote ile. Iwe kwa wazawa tu.mapori yaliyoko yaachwe yalivyo. Watanzania wanaongezeka lakini ardhi haiongezeki. Kwa vizazi vijavyo.
      Ahsante sana!

    19. #36
      Mikael P Aweda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 1,844
      Rep Power : 6549
      Likes Received
      2455
      Likes Given
      2232

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      Quote By CHESEA INGINE
      Hodi hodi wana jf. Nipo!. Hii mada nimeipenda.
      Ningetaka katika katiba yaingizwe haya.
      1.kwamba sera kuu za nchi ziingizwe kwenye katiba kusudi anayetaka uongozi atuambie atakavyotekeleza sera zetu. Isiwe kama sasa kila chama kinakuja na zake.
      2.wakuu wa mikoa wagombee kama wanavyofanya wabunge.
      3.elimu itamkwe ya kuwa ni bure kuanzia msingi mpaka chuo kikuu. Wakimaliza, jkt kwa kipindi cha miaka miwili.
      4.ardhi kamwe isimilikishwe kwa wageni kwa namna yeyote ile. Iwe kwa wazawa tu.mapori yaliyoko yaachwe yalivyo. Watanzania wanaongezeka lakini ardhi haiongezeki. Kwa vizazi vijavyo.
      Ahsante sana!

      Wakuu wa mikoa wakigombea, vipi kuhusu wakuu wa wilaya? Je, kama mkuu wa wilaya akichaguliwa kwa kura atakuwa anawajibika kwa mkuu wa Mkoa au kwa wapiga kura wake? Ufafanuzi.
      Mikael P Aweda 0784 583 330
      Elimu kwanza

    20. #37
      Bobuk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 2,065
      Rep Power : 922
      Likes Received
      835
      Likes Given
      0

      Default Re: Tume ya Katiba mpya, ni jambo gani ungetaka tukakusemee kwenye mikutano inayoendelea?

      1. Mshahara na mapato ya viongozi wa wakuu wa kitaifa yajulikane kwa walipa kodi/Watanzania (How? I don't know)
      2. Viongozi wote wa kitaifa wastaafu wanaoendelea kuhudumiwa na kodi zetu wasijihusishe na siasa za vyama. (A Case Study Mkapa huko Arumeru Mashariki)
      3. Wakuu wa Majeshi ya ULINZI na USALAMA eg CDF, IGP, yule wa Magereza, FFU wasijihusishe na SIASA za vyama hata baada ya kustaafu (A case Study Mboma (CDF) alitaka kugombea ubunge)

    Page 2 of 2 FirstFirst 12

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...