Charles Tylor hakuhukumiwa kwa makosa aliyoyatenda yeye binafsi, bali yalitendwa chini ya mamlaka yake wakati alikuwa na uwezo kuyazuia kutendeka. Waliyoyatenda wapo mtaani wanakula bata kwa fedha dhalimu walizozipata baada ya kumwaga damu za ndugu zao.
Inawezekana Tylor alikuwa na nia njema ya kuzuia uhalifu usiingie na kuenea Liberia lakini kanuni za kibinadamu zilikiukwa vikubwa. Hivyo kupelekea historia mbaya kwa Afrika na huzuni kubwa kwa nasaba yake...
JK, inawezekana kabisa kwamba nyuma ya hizi brutal zinazofanywa na dola dhidi ya raia wako hakuna NIA wala MAAMUZI yako, lakini inawezekana walio chini yako wanaamua wakiamini wanafanya kwa niaba. Inawezekana kabisa kwamba inakuuma na kukusumbua sana haya matukio mfululizo yanayodhalilisha nafasi yako na utu wako lakini huna la kufanya.
Inawezekana kabisa kupitia nafasi yako uliyo nayo sasa unadhibiti vyombo vya kutoa haki (mahakama) kutenda haki isiyo haki. Hivyo kutumika kukandamiza na kubamiza matumaini ya raia wako wengi.
Take my words...
- Chukua hatua za kinidhamu dhidi ya wanaoharibu kwa kutumia jina na nafasi yako..
- Kukaa kwako kimya ni jibu tosha kwamba you are behind na uhalifu dhidi ya binadamu unaofanywa na wasaidizi wako...
- Siku hazigandi, hivyo usiporekebisha sasa tegemea uwezekano wa wewe kushtakiwa kwenye mahakama ya uhalifu wa kivita muda wowote ule.

Reply With Quote


Follow Us Here