re: Dr. Namala Mkopi (kiongozi wa MAT) afikishwa mahakama ya Kisutu

By
Electron
Kiongozi wa madaktari nchini Dr. Namala Mkopi (daktari bingwa wa watoto),amefikishwa katika mahakama ya Kisutu asubuhi hii kujibu shutuma za uchochezi na kupuuza amri ya mahakama ya kusitisha mgomo wa madaktari unaoendelea nchini.
N.B. Mgomo huo haukunzishwa na MAT, ulianzishwa na inayoitwa Jumuiya ya Madaktari chini ya kamati inayoongozwa na Dr. Ulimboka, na kuungwa mkono na madaktari nchini.
Tusubiri kuona hili saga litakavyoendelea....
Keep your friend close and your enemies closer. Don Coleorne
Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi au kuanza kutoa majibu ya anachotakiwa kukijibu yeye mahakamani .......ana akili timamu na atajibu hivyo ila ninachojiuliza na nimeuliza wenzangu humu bila kupata majibu ni kwamba.....je alipopata court order aliitekeleza?? Mtasema hakuwa ameitisha mgomo yeye lakini wanachama wake (MAT- Chama kinachotambuliwa kisheria) walikuwa katika mgomo na amri ya mahakama ilimtaka awatangazie kuwa mgomo ni batili hadi mahakama itakapofanya uamuzi wa shauri lililopo mbele yake.....na je katika kutekeleza amri hiyo ..yeye binafsi alikwenda kazini??
The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!
Follow Us Here