Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 27
    1. #1
      Kieleweke's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd June 2009
      Posts : 79
      Rep Power : 520
      Likes Received
      8
      Likes Given
      12

      Default Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Kwanza combination yake unapoingia form five ni Physics, Chemistry na Biolology (PCB), au Chemistry, Biolology, Geography (CBG).

      Anyway siku hizi University zimekuwa kibao hivyo maadam una Biology na Chemistry basi kuna kila linalowezekana ufike form six na baada ya hapo usomee udaktari.

      Zamani Chuo kilikuwa nikimoja tu hapa nchini yaani Muhimbili. Sasa vimeenea kila kona. Kuna Kairuki, Kuna Bugando nasikia Ifakara nako kumefunguliwa. Du viko tele.

      Turudi kwenye yale masomo yaani Biology, Chemistry, Physics. Hakuna aliyepita sekondari asisimulie kuhusu masomo haya. Na ndiyo yanayoongoza kwa wanafunzi kufeli. Hivyo ni masomo magumu kuliko maelezo.

      Najua kuna watu wanayatandika A au B lakini inabidi uwe kichwa kwelikweli.

      Serikali inajua ugumu wa msomo hayo, inajua wanafunzi wanayachukia. Inafanya kampeni nyingi kusisitiza wanafaunzi wasichukie masomo ya sayansi.

      Lakini wakati serikali inasisitiza tukimbilie masomo haya, tunaona madaktari ni moja ya fani chache za sayansi zinazoongoza kwa migomo. Kuanzia mwaka 2000 hadi leo si chini ya migomo sita.

      Lakini sijawahi kusikia meneja wa kamouni akigoma. Sijawahi kusikia Waziri akigoma. Sijawahi kusikia mahakimu au majaji wakigoma. Tena wale wasiogoma masomo waliyosoma utaona wengi ni yale kama history, geography, Kiswahili, English, French kwa kifupi yanaitwa arts.

      Sasa kwa nini kama ninasoma nijihangaishe na masomo maguumu ya kuumiza kichwa wakati najua nikianza kazi nitaumiza kichwa tena kugoma na kuamziwa nichague kuendelea na kazi au nifukuzwe kazi.

      Hivyo, nimeamua sitaki udaktari kwa sababu ambazo sasa hata mtanzania wa umri wa miaka sita najua. Udaktari na migomo ni pete na kidole.

      Nataka kazi zile ambazo zitanifanya niwe na nyumba Mbezi_Beach (Dar), Capri_Point (Mwanza) na sehemu ya mji wowote ambako tunapaita "Uzunguni".

      Nitakuwa wa ajabu kumshawishi mwanafunzi asomee udaktari. Asomee wa nini? Umsaidie nini?

      Niseme nisiseme> Ninataka mwanafunzi asome awe mbunge au Waziri. Na ndiyo maana na wao siku hizi wanafunga safari nyingi kwenda kutembelea Bunge ili siku moja waje wawe wabunge waachane na njaa ya kugomagoma ya udaktari.

      Cheers

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      mtanzania1989's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2010
      Posts : 383
      Rep Power : 533
      Likes Received
      80
      Likes Given
      347

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      message imefika
      Kenneth Mwazemb likes this.

    4. #3
      Kenneth Mwazemb's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd January 2010
      Location : Mbozi
      Posts : 11
      Rep Power : 479
      Likes Received
      3
      Likes Given
      12

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      We kijana umesema kweli kabisa, tatizo lililopo ni kwamba udaktari ni fani ya kale mno na ina watu wake. Sayansi kawaida wasomi wake wanakuwa na vichwa moko kidogo kwasababu ya kubundia. Mtoto mmoja aliulizwa swali akimaliza shule angependa afanye kazi gani au awe nani alidai anataka awe fisadi akijua kuwa kuitwa fisadi Tanzania ni heshima kwani mafisadi ndiyo wenye fedha nchi hii, wanatembelea ma-VX, wanaheshimika na wanaitwa waheshimiwa.

    5. #4
      Advicer's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st November 2010
      Posts : 242
      Rep Power : 861
      Likes Received
      34
      Likes Given
      4

      Default

      Usitukane fani kama uliopt physics and chemistry.ingawa co magumu kama muwazavyo.

    6. #5
      mtanzania1989's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2010
      Posts : 383
      Rep Power : 533
      Likes Received
      80
      Likes Given
      347

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Wapo ambao watatoa kejeli , ila ukweli utabaki ni wachache ambao si madaktari ila vichwa vyao
      vinaruhusu kusomea udaktari au fani kadhaa za sayansi ,yafaa nini kuonekana mzuri darasani tangu
      utotoni hadi kidato cha nne mnapoanza kuachana , lakini , mwisho wa siku uliyekuwa unampita ndo
      anakuja kuthaminiwa zaidi

    7. Miaka 50

    8. #6
      mdizi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th January 2011
      Posts : 1,106
      Rep Power : 798
      Likes Received
      309
      Likes Given
      66

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      hujui tofauti ya profession na cheo au nafasi ya uongozi .... Udaktari ni profession na ubunge/uwaziri ni vyeo tu au uongozi ambavyo huingii darasani kusomea.... anyway go back and review your IQ

    9. #7
      mtanzania1989's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2010
      Posts : 383
      Rep Power : 533
      Likes Received
      80
      Likes Given
      347

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Wapo ambao watatoa kejeli , ila ukweli utabaki ni wachache ambao si madaktari ila vichwa vyao
      vinaruhusu kusomea udaktari au fani kadhaa za sayansi ,yafaa nini kuonekana mzuri darasani tangu
      utotoni hadi kidato cha nne mnapoanza kuachana , lakini , mwisho wa siku uliyekuwa unampita ndo
      anakuja kuthaminiwa zaidi

    10. #8
      Dijovisonjn's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Posts : 146
      Rep Power : 409
      Likes Received
      19
      Likes Given
      4

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Kwanza ubunge au uwaziri sio professional hvyo duniani kote hakuna chuo kinachofundsha non professional!
      Pili sio kosa kuwashauri wanafunzi ila hujawashauri vizuri na kwa uwazi! Kwanza, binafsi nimesoma arts tokea form three hadi form six na chuo kikuu nasoma kozi za social science. Nautambua ugumu wa science na nautambua ulaini wa arts! Lakin mwisho wa siku wanafunzi wa science vyuoni wanapewa motivation kubwa zaidi kuliko wa kozi nyingne, mfano, wakati wanafunzi wa social science wakiwa hawana mkopo kabisa (kuanzia mwaka huu), wanafunz wa education wakipewa 50% wao wa science wana 100% plus pesa za field na kununulia vifaa vya kujifunzia pamoja na pesa za books and stationary!
      Pili, vijana weng unaowaona wanazunguka na bahasha town wakitafuta ajira karibia wote hawajasoma kozi za science, wanafunzi karibia wote wa kozi za science wana uhakika wa ajira baada ya masomo yao!

      Kuhusu wanascience wengi kutokuwa na maisha mazuri kama wanaarts wengi jibu nadhan ni rahisi, wanascience hawana hayo maisha kwa sababu hawana elimu ya social science! Sidhan kama wanascience wanafundshwa namna ya kuishi na watu (social interaction), sidhan kama wanascience pamoja na kupata mshahara mkubwa zaidi ya watumishi wengine wengi tu wanajua how to run their social life!
      MBALI NA HAYO MACHACHE KOZI ZA SCIENCE NI NZURI SANA NA BINAFSI NAWASHAURI WANAOZISOMA KUZISOMA KWA MOYO ILI NCHI IWE NA WANASCIENCE WENGI!

      Kuhusu mgomo wa madaktari mi nadhani hayo ni mapambano ya kuiboresha sekta ya afya ili iwe bora na yenye manufaa kwao wenyewe na kwa jamii kwa ujumla na sio busara kuutumia kuwadiscourage wanaosoma masomo ya science!

    11. #9
      meningitis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2010
      Location : sewahaji
      Posts : 2,918
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      1014
      Likes Given
      149

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      hata walimu wa science wanalalamika kukosa 'semina' kulinganisha na wenzao wa arts.

    12. #10
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,170
      Rep Power : 24271
      Likes Received
      4677
      Likes Given
      2296

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Iko wapi chuo cha ubunge?
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    13. #11
      Nyakageni's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,248
      Rep Power : 0
      Likes Received
      769
      Likes Given
      52

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      ukweli ni kuwa serikali ni legelege!

    14. #12
      Cape city's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th October 2011
      Location : CAPE TOWN
      Posts : 96
      Rep Power : 404
      Likes Received
      23
      Likes Given
      1

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      U are talking nonsense...

    15. #13
      Lorah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd August 2008
      Posts : 667
      Rep Power : 681
      Likes Received
      91
      Likes Given
      127

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      wasisome udaktari serikali ya CCM itaagiza madaktari nje hahahaha hivi mbona hawafiki jamamani kweli Serikali ya CCM ni DHAIFU NA RAIS NI DHAIFU...

    16. #14
      Deofm's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 27th February 2012
      Posts : 225
      Rep Power : 410
      Likes Received
      31
      Likes Given
      26

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Quote By mtanzania1989
      Wapo ambao watatoa kejeli , ila ukweli utabaki ni wachache ambao si madaktari ila vichwa vyao
      vinaruhusu kusomea udaktari au fani kadhaa za sayansi ,yafaa nini kuonekana mzuri darasani tangu
      utotoni hadi kidato cha nne mnapoanza kuachana , lakini , mwisho wa siku uliyekuwa unampita ndo
      anakuja kuthaminiwa zaidi

      Profesa Shaba aliwahi kumweliza Nyerere hili, alipojifananisa maisha ya shuleni na mh Daudi mwakawago na baadae kulinganisha maisha yao ya ajira. Nyerere alimpeleka shaba ulaya akachunguzwe kwa nini analewa hivyo. wazungu wakamwambia hawajawahi kuona kifaa kama hicho, wakaomba wabaki nae lakini Nyerere alikataa akamrudisha hapa bongo ambapo alikuwa hapate pesa ya kutosha hata bia hivyo aliendelea na gongo hadi maisha yake yakaharibika.

      hatari kwa taifa, watoto wetu wanataka maisha mazuri kwa jasho kidogo, haya yanapatikana kwenye usanii, uongozi na sheria, kwa hiyo serikali inapobishana na madaktari hadharani inawafanya watoto waogope kuwa wanasayansi.

      Vipi kuhusu ile posho ya sh, 200,000/= kwa siku, wahesimiwa si wanalipwa nje ya mishahara yao?

      Tupunguze hizi tuongeze motisha kwa wanasayansi vingineyo nchi yetu kila kitu tutaomba India. Maendeleo ya kisanii hayalisaidii taifa. Rais Museveni alizungumza hivi majuzi alipoona kuwa sekta ya sanaa imekuwa kwa 8% na ile ya kilimo kwa 1%.

      chonde chonde rais wetu, ingawa wewe ni MSANII, lakini usiwabugudhi wanasayansi hivi, kwani ukiendelea hivi utakumbukwa kwa karne nyingi zijazo kama MSANII MAARUFU DUNIANI.

    17. #15
      CHUAKACHARA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd June 2011
      Posts : 3,022
      Rep Power : 7642
      Likes Received
      990
      Likes Given
      752

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Quote By Kieleweke
      Kwanza combination yake unapoingia form five ni Physics, Chemistry na Biolology (PCB), au Chemistry, Biolology, Geography (CBG).

      Anyway siku hizi University zimekuwa kibao hivyo maadam una Biology na Chemistry basi kuna kila linalowezekana ufike form six na baada ya hapo usomee udaktari.

      Zamani Chuo kilikuwa nikimoja tu hapa nchini yaani Muhimbili. Sasa vimeenea kila kona. Kuna Kairuki, Kuna Bugando nasikia Ifakara nako kumefunguliwa. Du viko tele.

      Turudi kwenye yale masomo yaani Biology, Chemistry, Physics. Hakuna aliyepita sekondari asisimulie kuhusu masomo haya. Na ndiyo yanayoongoza kwa wanafunzi kufeli. Hivyo ni masomo magumu kuliko maelezo.

      Najua kuna watu wanayatandika A au B lakini inabidi uwe kichwa kwelikweli.

      Serikali inajua ugumu wa msomo hayo, inajua wanafunzi wanayachukia. Inafanya kampeni nyingi kusisitiza wanafaunzi wasichukie masomo ya sayansi.

      Lakini wakati serikali inasisitiza tukimbilie masomo haya, tunaona madaktari ni moja ya fani chache za sayansi zinazoongoza kwa migomo. Kuanzia mwaka 2000 hadi leo si chini ya migomo sita.

      Lakini sijawahi kusikia meneja wa kamouni akigoma. Sijawahi kusikia Waziri akigoma. Sijawahi kusikia mahakimu au majaji wakigoma. Tena wale wasiogoma masomo waliyosoma utaona wengi ni yale kama history, geography, Kiswahili, English, French kwa kifupi yanaitwa arts.

      Sasa kwa nini kama ninasoma nijihangaishe na masomo maguumu ya kuumiza kichwa wakati najua nikianza kazi nitaumiza kichwa tena kugoma na kuamziwa nichague kuendelea na kazi au nifukuzwe kazi.

      Hivyo, nimeamua sitaki udaktari kwa sababu ambazo sasa hata mtanzania wa umri wa miaka sita najua. Udaktari na migomo ni pete na kidole.

      Nataka kazi zile ambazo zitanifanya niwe na nyumba Mbezi_Beach (Dar), Capri_Point (Mwanza) na sehemu ya mji wowote ambako tunapaita "Uzunguni".

      Nitakuwa wa ajabu kumshawishi mwanafunzi asomee udaktari. Asomee wa nini? Umsaidie nini?

      Niseme nisiseme> Ninataka mwanafunzi asome awe mbunge au Waziri. Na ndiyo maana na wao siku hizi wanafunga safari nyingi kwenda kutembelea Bunge ili siku moja waje wawe wabunge waachane na njaa ya kugomagoma ya udaktari.

      Cheers
      Mimi baba yenu nina ushauri tofauti na wewe mtoto! Soma Science halafu achana nayo tafuta nafasi za kisiasa. Si mnaona wabunge maprofesa wa science wamo bungeni. Bilal ni nuclear scientist/physicist and I can dare say that he has never and will never practice nuclear physics!!!

    18. #16
      ZeMarcopolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th May 2008
      Posts : 7,191
      Rep Power : 5038
      Likes Received
      2426
      Likes Given
      2224

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Hujawahi kusikia meneja wa kampuni amegoma, sawa. Je, umeshawahi kusikia mganga mkuu wa hospitali amegoma? waganga wakuu ndio wanaofukuza madaktari waliogoma. Meneja ni sawa na mganga mkuu.
      Kama udaktari umekushinda ni udhaifu wako mwenyewe na sio kosa la taaluma ya udaktari. Huna skills za kuuza ndio maana, wenye skills wanaenjoy profession yao fresh tu...
      "To greed, all nature is insufficient"

    19. #17
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,646
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      haya matatizo ya sasa si ya kudumu yanapita. Tunahitaji madaktari tena sana. Tusiache mbachao kwa msala upitao. Naungana kabisa na Albert Einstein aliyewahi kusema " In the middle of a crisis, lies the opportunity". Hii ni fursa kwetu kama nchi kukabili changamoto zilizopo for better!
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    20. #18
      Tutor B's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th June 2011
      Location : Bukoba Municipal
      Posts : 1,974
      Rep Power : 1188
      Likes Received
      598
      Likes Given
      45

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Ubunge na uwaziri hausomewe wewe! Wengi wa wabunge namawaziri wana professionals zao.
      Madaktari wapo, waandisi wapo, wanasheria wapo, n.k.
      Mkitambua hilo, mtajadiliana vyema.
      Turudi tulikotoka - zamani siasa / uongozi ilikuwa kazi ya watu wenye busara, wazee, na wasioweza kuzalisha. Watu wenye nguvu zao walishughulika na kazi za uzalishaji mali, katika kuzalisha waligundua vitu vingi ambavyo ndo sasa hivi vinatusaidia kama vitendea kazi.
      Mambo yalipoharibuka - hata watu wenye nguvu, professionals zao waanza kuonja kazi za kiuongozi / kisiasa - wakawa wanakimbia professionals zao.
      Nakumbuka wakati wa ujana wangu nilikuwa napenda kumtembelea Daktari mmoja mzee, alikuwa na hospitali yake. Kwa kweli alikuwa akinieleza mambo mengi kuhusu serikali yetu enzi zile. Moja na kubwa alonieleza na siwezi kulisaau alisema hivi ....
      "Rais wetu ndo aliiharibu nchi, wasomi wengi alikuwa anawateua kuwa mabalozi, aliingiza siasa sehemu za kazi lakini kwa uficho mkubwa"
      Wasomi hawa walipoonja raha ya kukaa bila kufanya kazi ndo waambukiza watoto wao kupendelea kazi raisi raisi kama za kusimama majukwaani na kubwabwata maneno ya kukopi na kupest. Wanashinda na vitabu vya wana-falsafa wakikariri vimisemo mbalimbali ili wakisimama kwenye mikusanyiko waweze kushangiliwa - WIZI MTUPU
      Someni masomo ya sayansi muwe watenda kazi kama mtakavyokuwa mmeteuliwa na Mungu.

      Kieleweke likes this.
      "Ukipendwa - penda, ipo siku utapenda - usipendwe"

    21. #19
      Tutor B's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th June 2011
      Location : Bukoba Municipal
      Posts : 1,974
      Rep Power : 1188
      Likes Received
      598
      Likes Given
      45

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Quote By ZeMarcopolo
      Hujawahi kusikia meneja wa kampuni amegoma, sawa. Je, umeshawahi kusikia mganga mkuu wa hospitali amegoma? waganga wakuu ndio wanaofukuza madaktari waliogoma. Meneja ni sawa na mganga mkuu.
      Kama udaktari umekushinda ni udhaifu wako mwenyewe na sio kosa la taaluma ya udaktari. Huna skills za kuuza ndio maana, wenye skills wanaenjoy profession yao fresh tu...
      Kumbe tuko wachache tunaotambua hilo.
      ZeMarcopolo likes this.
      "Ukipendwa - penda, ipo siku utapenda - usipendwe"

    22. #20
      Kieleweke's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd June 2009
      Posts : 79
      Rep Power : 520
      Likes Received
      8
      Likes Given
      12

      Default Re: Nauchukia udaktari. Wanafunzi msiusomee. Hauvutii kama Ubunge, Uwaziri

      Quote By mdizi
      hujui tofauti ya profession na cheo au nafasi ya uongozi .... Udaktari ni profession na ubunge/uwaziri ni vyeo tu au uongozi ambavyo huingii darasani kusomea.... anyway go back and review your IQ
      Hebu sema kwa mujibu wa IQ yako ni mahala gani kwenye post yangu nimesema Ubunge, Uwaziri ni profession?

      Quote By Mungi
      Iko wapi chuo cha ubunge?
      Unadhani wakati ninapost sikujua kwamba ubunge si proffession ya kupata chuoni? Nimeandikapost kistaa nikijua mpo mtakaokurupuka kana kwamba nimesema hivyo ni profession.


      Quote By Dijovisonjn
      Kwanza ubunge au uwaziri sio professional hvyo duniani kote hakuna chuo kinachofundsha non professional!
      Wewe, unatakiwa kujibiwa majibu mengi, lakini jibu lako la kwanza ni kama la hao wawili, ila kwa sababu hujagusa neo IQ basi hayo ya IQ yanamgusa yule mwenzenu na si wewe.

      Quote By Dijovisonjn
      Pili sio kosa kuwashauri wanafunzi ila hujawashauri vizuri na kwa uwazi! Kwanza, binafsi nimesoma arts tokea form three hadi form six na chuo kikuu nasoma kozi za social science. Nautambua ugumu wa science na nautambua ulaini wa arts!
      Napenda watu wasiomungunya maneno. Hapa nakupa 100%


      Quote By Dijovisonjn
      Lakini mwisho wa siku wanafunzi wa science vyuoni wanapewa motivation kubwa zaidi kuliko wa kozi nyingne, mfano, wakati wanafunzi wa social science wakiwa hawana mkopo kabisa (kuanzia mwaka huu), wanafunzi wa education wakipewa 50% wao wa science wana 100% plus pesa za field na kununulia vifaa vya kujifunzia pamoja na pesa za books and stationary!
      Mkuu, hayo hayana tofauti na wakati ule wa JKT ambapo mtu aliyetoka kozi kama ualimu alikuwa hakai kambini bali anapata kitengo cha kufundisha shule za jeshi. Hebu muulize mwalimu yeyote kama anapenda ualimu kwa kuwa jeshini kuna unafuu au kama kulikuwa na unafuu.

      Quote By Dijovisonjn
      Pili, vijana wengi unaowaona wanazunguka na bahasha town wakitafuta ajira karibia wote hawajasoma kozi za science, wanafunzi karibia wote wa kozi za science wana uhakika wa ajira baada ya masomo yao!
      Lakini ndiyo ajira hizihizi wanazogoma ambazo napenda mnipe majibu kwa nini tusikimbie

      Quote By Dijovisonjn
      Kuhusu wanascience wengi kutokuwa na maisha mazuri kama wanaarts wengi jibu nadhani ni rahisi, wanascience hawana hayo maisha kwa sababu hawana elimu ya social science! Sidhani kama wanascience wanafundishwa namna ya kuishi na watu (social interaction), sidhani kama wanascience pamoja na kupata mshahara mkubwa zaidi ya watumishi wengine wengi tu wanajua how to run their social life!

      Mkuu,
      Kuwa muangalifu unapojibu hoja hii. Madaktari wanafundishwa aina fulani ya phsychology ili kuweza kumkabili mgonjwa na hata ndugu za mgonjwa.

      Kuna jamaa humu kasema kuna kijana aliambiwa unataka ukiua ufanye kazi gani, kijana akasema nataka niwe FISADI. Na kama unavyosema ili uwe fisadi ni lazima uwe na SocialNetwork kubwa.


      Quote By Dijovisonjn
      Kuhusu mgomo wa madaktari mi nadhani hayo ni mapambano ya kuiboresha sekta ya afya ili iwe bora na yenye manufaa kwao wenyewe na kwa jamii kwa ujumla na sio busara kuutumia kuwadiscourage wanaosoma masomo ya science!
      Mkuu,

      Mwenye macho haambiwi ona na mwenye masikio haambiwi sikia. Mizozo ya madaktari unweza hata kuandika kitabu na kikanunuliwa na hakitakuwa chini ya page 150.


      Quote By CHUAKACHARA
      Mimi baba yenu nina ushauri tofauti na wewe mtoto! Soma Science halafu achana nayo tafuta nafasi za kisiasa. Si mnaona wabunge maprofesa wa science wamo bungeni.Bilal ni nuclear scientist/physicist and I can dare say that he has never and will never practice nuclear physics!!!
      Nakubaliana na wewe kuhusu future ya maisha yangu. Lakini mimi nimeongea ni terms of majority. Zaidi ya nusu ya wabunge ni wanasheria na ukiongezea fani zingine za arts zikiwemo practical arts kama zile za akina John Komba, Sugu, MajiMarefu nk. Bado hujawataja watangazaji kama Marehemu Amina Chifupa, Jenister Mhagama nk ndipo utapata picha ya ninachokisema.

      na hao ndiyo waliojaza majumba kule Mbezi_Beach ambapo la bei ya chini si chini ya milioni 700.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...