Naamka asubuhi nasikia kelele za walioishiwa na uwezo wa kufikiria...oh serikali inahusika...baada ya kusikiliza kwa makini nikajua yule mhusika na kifo cha ndugu yangu amepigwa na watu wasiojulikana....Nikasema na moyo wangu kweli ubaya unalipwa hapa hapa duniani...nina bahati ya kuwa na marafiki madaktari lakini nimepunguza mapenzi na hawa jamaa hata simu huwa siwapigii tena....
Kitu kimoja watu wasiochokijua ni jinsi gani watu fulani wanatumia mbinu chafu kuivuruga serikali yenye nia ya kuongeza maendeleo.
huyu dk. kwake Kiskulu ana duka kubwa sana la dawa na akaunti yake ina pesa nyingi sana kuliko kawaida na pia madai yake ya kutetea madaktari wa serikali ili masikini tufe haikuwa na mahesabu mazuri........
Maadili ya utaalamu wao hayapaswi kuvunjwa kwa kisingizio cha migomo nafikiri ingekuwa vyema wangetumia chombo mbadala kufikisha malalamiko yao..kwanza sio media iliyovurunda ....kuna wakati Mkapa alisema waandishi wa Tanzania hawajui kazi yao nakubaliana nae kabisa....
Madaktari wangeongea na mabosi wao kwanza ambao ni Wananchi wa jamhuri ya Tanzania na kuomba ushirikiano wa wananchi katika kulizungumzia hili na sio kuleta zengwe, ila wao wakaona wamchukue mwehu mmoja awaongoze kutuua ....haswa wakitaka waongezewe pesa wananunue magari zaidi na kushinda leaders baada ya kazi.....
Nasema hivi mkirudia mgomo hamgomei serikali mnatugomea sisi na hiko chama kinachowapotosha kinashangaza sana kilipaswa kikae na wananchi wazungumze namna nzuri ya kutatua matatizo huku madaktari wakiendelea na kazi zao, sasa kimekosa kauli, kimeonekana kabisa ni chama cha majimbo ukabila, udini na mbaya ni cha kutuua sisi sisi watanzania.....
poleni hamtopata kura na pia hamtaongoza ........

Reply With Quote




Follow Us Here