Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: M'kiti wa kijiji Kilolo (CHADEMA) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 50
    1. #1
      Sabung'ori's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th July 2011
      Posts : 859
      Rep Power : 572
      Likes Received
      247
      Likes Given
      16

      Default M'kiti wa kijiji Kilolo (CHADEMA) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Mkuu wa Wilaya ya Kilolo mkoani
      Iringa, Gerald Guninita
      amemkamata na kumweka chini
      ya ulinzi, Mwenyekiti wa Serikali
      ya Kijiji cha Udekwa kilichopo
      Tarafa ya Mahenge, Obadiah
      Lubugo, kwa kutochangia Sh.
      70,000 za Mbio za Mwenge.
      Lubugo, ambaye ni Mwenyekiti
      wa Serikali ya Kijiji kupitia Chama
      cha Demokrasia na Maendeleo
      (Chadema), alionja kadhia hiyo
      juzi baada ya kuelekeza fedha
      hizo katika manunuzi ya chaki
      kwenye Shule ya Msingi Udekwa.
      Rekodi ya kijiji hicho inaonyesha
      kuwa tangu Tanzania ilipopata
      uhuru mwaka 1961, Mwenge
      huo haujawahi kupita hapo hadi
      hivi sasa, tukio ambalo linatoa
      tafsiri tofauti na michango halisia
      ya wananchi.
      Akilalamikia hatua hiyo mbele ya
      mkutano wake na waandishi wa
      habari, Lubugo alisema
      amehuzunishwa na hatua hiyo
      ya Mkuu wa Wilaya kumkamata
      na kumlazimisha kulipa fedha
      hizo wakati Mwenge huo
      ulishapita Juni 22, mwaka huu.
      “Amenikamata na kunilazimisha
      kulipa huo mchango wakati
      shuleni (Udekwa) kulikuwa
      hamna hata chaki na tulipeleka
      kwa Mkuu wa Shule Sh. 274,000
      na akasaini kwa ajili ya manunuzi
      ya chaki na mambo mengine.
      Lakini cha ajabu alipofika kijijini
      kwetu, DC akasema kama sina
      fedha hizo nikae Polisi kuanzia
      tarehe 29 mwezi Juni hadi Julai
      2, mwaka huu ndipo nipelekwe
      ofisini kwake," alilalamika.
      Lubugo alisema Sh. 274,000
      zilizoelekezwa na serikali ya kijiji
      kwenda kwenye manunuzi ya
      chaki na masuala mengine ya
      kitaaluma, zilipitishwa na
      wajumbe wa serikali yake
      kutokana na shule hiyo kutopata
      mgawo wa fedha serikalini kwa
      matumizi hayo.
      Hata hivyo, kwa mujibu wa barua
      iliyoandikwa na Halmashauri ya
      Wilaya hiyo, yenye kumbukumbu
      namba KDC/A4/1/30 ya Aprili 12,
      mwaka huu, kwenda kwa
      maofisa watendaji wa kata,
      ikielekeza maandalizi na
      michango ya Mbio za Mwenge
      wa Uhuru, inaagiza kila kijiji
      kuchangia Sh.70,000.
      “Sehemu ya barua hiyo inaeleza
      hivi: "Mwisho wa kuwasilisha
      michango hiyo ni tarehe 10 Mei,
      2012 na kila Mtendaji wa Kijiji
      anapaswa kupatiwa risiti.
      Ningependa mhimize suala la
      uchangiaji wa Mbio za Mwenge
      kwa vijiji vilivyo kwenye kata
      zenu ambapo kila kijiji
      kinatakiwa kuchangia
      Sh.70,000.”
      NIPASHE ilipomtafuta Mkuu wa
      Wilaya hiyo kwa njia ya simu ya
      mkononi pamoja na kumtumia
      ujumbe mfupi wa maandishi
      (SMS), kwa ajili ya kumtaka
      kuthibitisha au kukanusha madai
      hayo, lakini hakujibu.
      Afisa Habari wa wilaya hiyo
      aliyejulikana kwa jina moja la
      Christopher, aliwajibu waandishi
      wa habari kwamba hawezi
      kupokea simu na ameagiza
      afuatwe kijiji cha Lundamatwe.
      SOURCE: NIPASHE


    2. #2
      DALLAI LAMA's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st February 2012
      Posts : 3,122
      Rep Power : 0
      Likes Received
      741
      Likes Given
      0

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Lema alisema kuwa angewasilisha hoja binafsi bungeni iyo koroboi izimwe milele. Arusha 2nasubiri akitoka honeymoon kwani alituahidi toka kampeni zake
      Dawa kuchanana tu likes this.

    3. #3
      kanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 790
      Rep Power : 585
      Likes Received
      316
      Likes Given
      416

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      poor governance at all.tutaona vibwanga vingi sana kabla ya 2015.tuzidi kuomba uzima.

    4. #4
      Edson's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2009
      Posts : 7,310
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1806
      Likes Given
      433

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      uonevu wa hali a juu kabisa!!
      I'm Naturaly Evasive..

    5. #5
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,988
      Rep Power : 2594
      Likes Received
      641
      Likes Given
      777

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Wenyeviti wa vijiji igeni mfano huu, kuliko kukimbiza masanamu (Hii koroboi ina nini hasa). Mwenzenu kanunua chaki watoto wanasoma. Huyu anaingia kwenye mashujaa gruop of Tanganyika.
      Crashwise and RC. like this.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.


    6. #6
      kiraia's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2007
      Location : Kowamrasa
      Posts : 647
      Rep Power : 721
      Likes Received
      83
      Likes Given
      487

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Huyu mwenyekiti awe mfano kwa wenyeviti wote wa chadema wanaaongoza vijiji.
      Crashwise and RC. like this.
      The most dangareous position in which to sleep is with your feet on your office desk.

    7. #7
      Third Eye's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th January 2012
      Posts : 217
      Rep Power : 475
      Likes Received
      42
      Likes Given
      16

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Binafsi ata mi mwenge una faida gan had utumie garama zote izo sijui, anaejua anijuze tafadhari

    8. #8
      dudus's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2011
      Posts : 2,339
      Rep Power : 1018
      Likes Received
      1323
      Likes Given
      531

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Hivi mwenge ni suala la kiserikali? Mimi miaka yote huwa naona wahusika wakuu wa shughuli hiyo ni makada wa CCM na hasa UVCCM which means ni suala la kichama zaidi. Kama ndivyo, ni muhimu sasa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani vinavyoongoza Halmashauri, kata, au vijiji mbali mbali kuwaandikia wenyeviti husika kutowachangisha wananchi wa maeneo yao kwa ajili ya mwenge.

      Tungependa pia kuona CHADEMA wakitoa msimamo wao hadharani na matangazo kwenye vyombo vya habari juu ya msimamo wao rasmi juu ya suala hili na hatua zipi zichukuliwe kwa watendaji wa serikali watakao wanyanyasa wananchi kuhusiana na hili kama alivyofanya huyu Mkuu wa Wilaya.

      Hii nchi ni huru na kila mtu ana haki ya kufuata itikadi au kuabudu chochote anachoona kinafaa. Wanaotaka kuabudu/kukimbiza mioto waachwe wafanye hivyo kwa utashi na gharama zao wenyewe na sio kulamizisha wananchi.

    9. #9
      KIDUNDULIMA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th August 2010
      Posts : 560
      Rep Power : 560
      Likes Received
      74
      Likes Given
      245

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      asante sana mwenyekiti chadema kwa kuwanyima hela hao kunguni wanyonya damu. Fedha za elimu za wilaya wale wao pasipo kuleta hata kiduchu kijijiji na michango nayo wapelekewe ili wakale kwenye mwenge wapi na wapi?

    10. #10
      Mbunge wa ilula's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd June 2012
      Posts : 128
      Rep Power : 5238
      Likes Received
      8
      Likes Given
      5

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Manunuzi ya chaki ni jambo jema kuliko hilo analolishikilia DC ambalo halina tija kwa taifa,watoto wasisome mwengeupte?

    11. #11
      Adrian Stepp's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2011
      Posts : 1,583
      Rep Power : 719
      Likes Received
      441
      Likes Given
      2679

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      pumbav kabisa guninita!!
      Precise pangolin likes this.
      Watu wakimya wamejaliwa busara, ufahamu na midomo inayonuka!

    12. #12
      BHULULU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2012
      Posts : 3,167
      Rep Power : 8414
      Likes Received
      902
      Likes Given
      740

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Mwenyekiti juuuuuuuuuuuuuuu!"Dizii "ziiiiiiiiiiiiiiiiii

    13. #13
      Ndyali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Posts : 549
      Rep Power : 491
      Likes Received
      140
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By kiraia View Post
      Huyu mwenyekiti awe mfano kwa wenyeviti wote wa chadema wanaaongoza vijiji.
      Mkuu, huyu mkuu wa wilaya ametutengenezea penati mhimu kupitia mwenyekiti wetu, hivyo CHADEMA wilaya watume timu kuifuta ccm katika kijiji hicho bila kusahau kupeleka msaada katika shule ya kijiji watoto waelimike. Badala ya kuchangia mwenge uliowapelekea ukimwi.
      Last edited by Ndyali; 6th July 2012 at 11:23.
      james chapacha likes this.

    14. #14
      james chapacha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2012
      Posts : 508
      Rep Power : 465
      Likes Received
      104
      Likes Given
      25

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      DC elimu yake kama ya luc na prof Maji,anajsikia wivu kuona watoto wadogo wanaelekea kumzidi elimu

    15. #15
      DALLAI LAMA's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st February 2012
      Posts : 3,122
      Rep Power : 0
      Likes Received
      741
      Likes Given
      0

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Ivi huyu si mtoto wa gamba john guninita?

    16. #16
      ibange's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 1,372
      Rep Power : 1114
      Likes Received
      407
      Likes Given
      23

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Tumshali kwa false imprisonment plz. Wasiliana nami privately nikusaidie

    17. #17
      Lubaluka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2009
      Posts : 473
      Rep Power : 608
      Likes Received
      22
      Likes Given
      19

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Mwenge ni Kiini Macho kwa sasa!! Mi sitaki hata kuuona ..........
      Always The Silence of Our Friends Hurts more than the Noise of Our Enemy.

    18. #18
      Marire's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st May 2012
      Posts : 2,360
      Rep Power : 990
      Likes Received
      634
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Third Eye View Post
      Binafsi ata mi mwenge una faida gan had utumie garama zote izo sijui, anaejua anijuze tafadhari
      nilivyokuwa mdogo wakubwa zangu walikuwa wanatuambia mwenge unaleta njaa hadi leo huwa naogopa kuangalia huo mwenge.
      Third Eye likes this.

    19. #19
      popobawa2012's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th July 2012
      Posts : 86
      Rep Power : 367
      Likes Received
      4
      Likes Given
      16

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Quote By Mbunge wa ilula View Post
      Manunuzi ya chaki ni jambo jema kuliko hilo analolishikilia DC ambalo halina tija kwa taifa,watoto wasisome mwengeupte?
      hao ndo wametoka semina elekzi! apa dawa ni 1 tu CDM 2015 ata kwa ngumi tupo tayar ama cvo tutaishia kulialia kama mazuzu

    20. #20
      Makyomwango's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 234
      Rep Power : 461
      Likes Received
      42
      Likes Given
      14

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Quote By kiraia View Post
      Huyu mwenyekiti awe mfano kwa wenyeviti wote wa chadema wanaaongoza vijiji.
      Mimi sijawahi na sitakuja changia hiyo koroboi. Kiiukweli wananchi wa vijijini wananyanyasika sana.

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...