Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: M'kiti wa kijiji Kilolo (CHADEMA) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

    Report Post
    Page 2 of 3 FirstFirst 123 LastLast
    Results 21 to 40 of 50
    1. #1
      Sabung'ori's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th July 2011
      Posts : 822
      Rep Power : 561
      Likes Received
      233
      Likes Given
      16

      Default M'kiti wa kijiji Kilolo (CHADEMA) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Mkuu wa Wilaya ya Kilolo mkoani
      Iringa, Gerald Guninita
      amemkamata na kumweka chini
      ya ulinzi, Mwenyekiti wa Serikali
      ya Kijiji cha Udekwa kilichopo
      Tarafa ya Mahenge, Obadiah
      Lubugo, kwa kutochangia Sh.
      70,000 za Mbio za Mwenge.
      Lubugo, ambaye ni Mwenyekiti
      wa Serikali ya Kijiji kupitia Chama
      cha Demokrasia na Maendeleo
      (Chadema), alionja kadhia hiyo
      juzi baada ya kuelekeza fedha
      hizo katika manunuzi ya chaki
      kwenye Shule ya Msingi Udekwa.
      Rekodi ya kijiji hicho inaonyesha
      kuwa tangu Tanzania ilipopata
      uhuru mwaka 1961, Mwenge
      huo haujawahi kupita hapo hadi
      hivi sasa, tukio ambalo linatoa
      tafsiri tofauti na michango halisia
      ya wananchi.
      Akilalamikia hatua hiyo mbele ya
      mkutano wake na waandishi wa
      habari, Lubugo alisema
      amehuzunishwa na hatua hiyo
      ya Mkuu wa Wilaya kumkamata
      na kumlazimisha kulipa fedha
      hizo wakati Mwenge huo
      ulishapita Juni 22, mwaka huu.
      “Amenikamata na kunilazimisha
      kulipa huo mchango wakati
      shuleni (Udekwa) kulikuwa
      hamna hata chaki na tulipeleka
      kwa Mkuu wa Shule Sh. 274,000
      na akasaini kwa ajili ya manunuzi
      ya chaki na mambo mengine.
      Lakini cha ajabu alipofika kijijini
      kwetu, DC akasema kama sina
      fedha hizo nikae Polisi kuanzia
      tarehe 29 mwezi Juni hadi Julai
      2, mwaka huu ndipo nipelekwe
      ofisini kwake," alilalamika.
      Lubugo alisema Sh. 274,000
      zilizoelekezwa na serikali ya kijiji
      kwenda kwenye manunuzi ya
      chaki na masuala mengine ya
      kitaaluma, zilipitishwa na
      wajumbe wa serikali yake
      kutokana na shule hiyo kutopata
      mgawo wa fedha serikalini kwa
      matumizi hayo.
      Hata hivyo, kwa mujibu wa barua
      iliyoandikwa na Halmashauri ya
      Wilaya hiyo, yenye kumbukumbu
      namba KDC/A4/1/30 ya Aprili 12,
      mwaka huu, kwenda kwa
      maofisa watendaji wa kata,
      ikielekeza maandalizi na
      michango ya Mbio za Mwenge
      wa Uhuru, inaagiza kila kijiji
      kuchangia Sh.70,000.
      “Sehemu ya barua hiyo inaeleza
      hivi: "Mwisho wa kuwasilisha
      michango hiyo ni tarehe 10 Mei,
      2012 na kila Mtendaji wa Kijiji
      anapaswa kupatiwa risiti.
      Ningependa mhimize suala la
      uchangiaji wa Mbio za Mwenge
      kwa vijiji vilivyo kwenye kata
      zenu ambapo kila kijiji
      kinatakiwa kuchangia
      Sh.70,000.”
      NIPASHE ilipomtafuta Mkuu wa
      Wilaya hiyo kwa njia ya simu ya
      mkononi pamoja na kumtumia
      ujumbe mfupi wa maandishi
      (SMS), kwa ajili ya kumtaka
      kuthibitisha au kukanusha madai
      hayo, lakini hakujibu.
      Afisa Habari wa wilaya hiyo
      aliyejulikana kwa jina moja la
      Christopher, aliwajibu waandishi
      wa habari kwamba hawezi
      kupokea simu na ameagiza
      afuatwe kijiji cha Lundamatwe.
      SOURCE: NIPASHE

    2. Miaka 50

    3. #21
      Angel Msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Posts : 6,266
      Rep Power : 1826
      Likes Received
      1397
      Likes Given
      0

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Mwenge una faida gani kwa huyo mwenyekiti?

    4. #22
      Mtoto Wa Mbale's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th May 2011
      Posts : 420
      Rep Power : 494
      Likes Received
      143
      Likes Given
      1

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Huyu Guninita ni mtoto wa mzee Guninita?

    5. #23
      Chepii's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th March 2011
      Posts : 62
      Rep Power : 428
      Likes Received
      3
      Likes Given
      3

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Mi naona Mwenge uwe una waswa siku ya Uhuru tu. Badala ya kuuzungusha nchi nzima kwakisingizio cha kuzindua miradi ya maendeleo ifunguliwe na wakuu wa wilaya/mikoa nk.

    6. #24
      SHEMGUNGA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2012
      Posts : 332
      Rep Power : 437
      Likes Received
      21
      Likes Given
      0

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      sasa mabadiliko yanaonekana kamata mwiz men hawa tunao mpaka kieleweke!

    7. #25
      Marire's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st May 2012
      Posts : 2,224
      Rep Power : 958
      Likes Received
      604
      Likes Given
      0

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      T 2015 cdm

    8. FemaTV & Radio

    9. #26
      mgt software's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 1,750
      Rep Power : 784
      Likes Received
      140
      Likes Given
      201

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      dc kichaa kweli kweli anathamini koroboi, mwenge kwa kawaida unahamasisha ngono zembe kila unapolala, uacha virus watu 10
      "Mtoto wa Maskini Hachagui Malezi, Tanganyika siyo Masikini Masikini ni wewe Unayehonga Haki yako Kwa Mafisadi" Bamugileki

    10. #27
      Remmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2009
      Location : home
      Posts : 4,342
      Rep Power : 7768
      Likes Received
      1545
      Likes Given
      1793

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      We ni kweli Mwenge umepita huko Juni 22? Mbona Kama unadanganya vile?

    11. #28
      Malova's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st April 2011
      Posts : 534
      Rep Power : 515
      Likes Received
      82
      Likes Given
      9

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Hawa wehu sana kwa kukimbisa moto unaoeneza ukimwi nchin kila mwaka

    12. RC.
      #29
      RC.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th May 2012
      Posts : 348
      Rep Power : 421
      Likes Received
      30
      Likes Given
      16

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      jambo hili linasikitisha sana kama hali ndiyo hii ya kuchanga pesa kwaajili ya mwenge kila kijiji Tshs.70,000 mara vijiji vyote TANZANIA bara na visiwani, ni shilingi ngapi? halafu kila mwaka serikali inatenga mamillioni ya pesa kwaajili ya mwenge! hamuoni kwamba huu ni mradi wa mafisadi? tunaomba mdhibiti na mkaguzi wa mahesabu ya serikali akague pesa hizi zinatumikaje halafu ripoti iwekwe wazi kisha uwekwe mjadala wa kitaifa kama tuendelee kukimbiza mwenge au uwekwe makumbusho ya taifa!?na pia tujue mnufaika ninani? wakijulikana hawa mashetani tuwatangaze kama MAADUI WA TAIFA LA TANZANIA! NA TUWATENGE TUSISHIRIKIANE NAO.

    13. #30
      Return Of Undertaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Posts : 658
      Rep Power : 541
      Likes Received
      462
      Likes Given
      0

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Dah inatia maumivu ya kichwa unaweza kujitoa muhanga hivi hivi

    14. #31
      TUKUTUKU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Location : KIPALAPALA TU
      Posts : 8,366
      Rep Power : 2114
      Likes Received
      1728
      Likes Given
      676

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Hongera sana mpiganaji,ipo siku magamba watanyooka!!
      "A friend in need,is a friend indeed"

    15. #32
      giiti junior's Avatar
      Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Posts : 31
      Rep Power : 353
      Likes Received
      4
      Likes Given
      1

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Moto dhidi ya chaki!

    16. #33
      piper's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th January 2012
      Posts : 1,593
      Rep Power : 765
      Likes Received
      244
      Likes Given
      39

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Tanzania ni nchi ya kipekee, bora koroboi itembezwe elimu baadaye

    17. #34
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,466
      Rep Power : 19781
      Likes Received
      4295
      Likes Given
      1229

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Hii ndio serikali ya dhaifu!

    18. #35
      Froida's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Posts : 3,744
      Rep Power : 1317
      Likes Received
      720
      Likes Given
      147

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      mwenge hata wana CCM wenyewe hawautaki leo unaambiwa Tanga hakukuwa na CCM mkoa wala CCM wailaya pangani kuupokea mwenge walipoulizwa wamesema akaulizwe mkuu wa mkoa Chiku Gallawa ,huyu mwenyekiti wa kijiji kichwa kafata taratibu yeye na kamati yake wameona watoto kwanza safiiiiiiiiiii

    19. #36
      ismathew's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2011
      Posts : 252
      Rep Power : 455
      Likes Received
      37
      Likes Given
      76

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Mkuu wa wilaya, alichokifanya ni kitu kisichoeleweka, hapo tuseme ni chuki binafsi ya kisiasa.
      Mwenge umefika wakati wa kwenda makumbusho ya Taifa. Kwa sababu tokea miaka
      hamsini iliyopita, umeshachangia mambo ambayo hayana faida. Kwanza umaskini na
      kuharibu kwa kiasi kikubwa cha mazingira nchini, yaani (out door air pollution).
      Kwa sababu kuchoma mafuta ya taa kwa kuzunguka Tanzania nzima kila mwaka,
      huo ni uzalishaji wa (Carbon Dioxide). Ambayo inawaathiri wagonjwa wa Pumu,
      kuathiri miche mashambani na misitu kukauka, na kibaya zaidi kuleta (Acid Rain).
      Ambayo uharibu mazao, maji na ardhi, sasa kuna faida gani ya kuendelea na mwenge
      wakati hauna hata asilimia moja ya maendeleo kwa Watanzania.

    20. #37
      Kamakabuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2007
      Posts : 1,065
      Rep Power : 799
      Likes Received
      142
      Likes Given
      257

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      hivi michango ya mwenge kwa kulazimishwa bado ipo? Mlichelewa wapi? Huku hata wafanyabiashara wanaombwa mchango hawalazimishwi. Mwenge unapopita hakuna ulazima wa kufunga duka lako; ni takabuli tu!

    21. #38
      MALUNGU's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd June 2011
      Posts : 216
      Rep Power : 446
      Likes Received
      66
      Likes Given
      219

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Hongera mh. mwenyekiti kwa ujasiri wako.

    22. #39
      only83's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Dodoma-Mjengoni
      Posts : 4,157
      Rep Power : 1846
      Likes Received
      1431
      Likes Given
      1539

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Hii ndio serikali ya Tanzania bwana, mwenge wa uhuru ni muhimu kuliko chaki za watoto mashuleni. Kweli tuna kazi watanzania.
      "Problems can not be solved by the same level of thinking that created them"
      "Matatizo hayawezi kutatuliwa na uwezo ule ule mdogo wa watawala wa CCM walioyasababisha"




    23. #40
      Wild fauna's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd April 2012
      Posts : 313
      Rep Power : 419
      Likes Received
      96
      Likes Given
      0

      Default Re: M'kiti wa kijiji kilolo(chadema) aswekwa lupango kwa kutochangia mwenge

      Nakumbuka when i was form 3 pale darajan sec marangu,hii koroboi ili lala pale chuo cha walimu marang ili upandishwe mt k'njaro.the next day 2lifanya usafi pale uwanjani tukaokota USED CONDOM malboro moja! Since dat day i dont want to hear a thng call mwenge

    Page 2 of 3 FirstFirst 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...