Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

    Report Post
    Page 1 of 13 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 260
    1. #1
      Tumaini Makene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2012
      Posts : 1,059
      Rep Power : 8906
      Likes Received
      2228
      Likes Given
      768

      Default MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi



      MFANYABIASHARA maarufu na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mustafa Jaffer Sabodo amekichangia tena Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), sh. milioni 10, huku akitoa ahadi nyingine mpya ya kukipatia chama hicho mradi wa kukiingizia mapato na kuchimba visima kwa majimbo ya chama hicho kwa miaka 10.


      Amesema kuwa kazi inayofanywa na chama hicho kutoa elimu ya uraia hadi vijijini, huku kikizidi kuimarisha mtandao wake kwenye ngazi za vitongoji na mitaa kikidhamiria kuendelea kupigania na kutetea haki za wananchi, inapaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania mpenda maendeleo.

      Mfanyabiashara huyo ambaye amekuwa akijitokeza waziwazi bila uoga kukichangia chama hicho cha upinzani, akisema anafurahishwa na kazi ambayo kinafanya ya kutetea maslahi na rasilimali za Watanzania kutengeneza fursa za maendeleo, ameongeza kuwa amefurahishwa na Operesheni Okoa Kusini, ambayo chama hicho kilifanya karibuni mikoa ya Lindi na Mtwara.

      Akizungumza jana nyumbani kwake ambako alikutana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa kwa ajili ya kuzungumzia mchakato wa utekelezaji wa ahadi alizotoa kwa chama hicho, Mzee Sabodo aliahidi kuwa baada ya kukamilika kwa jengo la kuegesha magari linalojengwa katikati ya Jiji la Dar es Salaam, sehemu ya mapato yatatumika kuchimba visima kwa miaka 10.

      Mbali ya sehemu ya mapato kutoka katika jengo hilo la kuegesha magari ambalo linajengwa na Taasisi ya Khoja Shia Ithnasheri Jamaat (KSIJAMAAT), pia Mzee Sabodo alisema kuwa sehemu ya chini ya jengo hilo ambayo itakuwa na maduka, CHADEMA itapatiwa duka moja kama mmoja wa miradi ya kukipatia mapato.

      “Mtapata sehemu ya mapato ili kuchimba visima kwenye majimbo yenu kwa miaka kumi…pia mtapata duka pale ili mpate mradi wa mapato. Ili kuharakisha utekelezaji wa ahadi ya visima vile vingine fanyeni survey ninyi wenyewe na mpate mkandarasi, itakuwa sehemu ya gharama ya uchimbaji…hizi milioni 10 mtapata hundi hapa mkafanye kazi za wananchi,” alisema Mzee Sabodo.

      Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Slaa, mbali ya kumshukuru na kumpongeza Mzee Sabodo kwa ujasiri wake wa kuendelea kujitoa kusaidia harakati za kupigania haki za wananchi, mabadiliko ya kiutawala na kimfumo nchini, aliahidi kuwa chama hicho kitaendelea kutimiza wajibu wake kwa maslahi ya Watanzania.

      “Umekuwa mtu wa msaada mkubwa kwetu, umeendelea kuwatia moyo Watanzania wote wa kila namna kuacha uoga wa kuchangia harakati hizi, kwani lengo letu ni kuwatumikia Watanzania katika kila fursa tunayoipata, ambapo kwa sasa tutaendelea kuisimamia na kuiwajibisha serikali ya CCM ambayo ni dhahiri ielekea mwisho na wananchi wameichoka.

      “Nasi tunawaahidi Watanzania wote kuwa tutaendelea kuwatumikia na hatutawaangusha, tunatambua kuwa katika mparanganyiko huu mkubwa, kama ugumu wa maisha, hali mbaya ya uchumi, siasa zinazoyumba, ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma na migogoro katika makundi mbalimbali ya kijamii kwa sababu ya uongozi mbovu, CHADEMA linabaki kuwa ndiyo tumaini pekee kwa Watanzania,” alisema Dkt. Slaa.

      Dkt. Slaa aliyeambatana na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA, Antony Komu, aliongeza kuwa visima vya ahadi hii mpya kutokana na mapato ya jengo la maegesho ambayo ni tofauti na ahadi za visima vingine alizowahi kutoa mwaka jana na mapema mwaka huu, vitachimbwa katika maeneo mbalimbali ya Tanzania yenye kero kubwa za maji.



      Mbali ya ahadi hizo mpya za jana, Mzee Sabodo na Dkt. Slaa walizungumzia juu ya mchakato wa utekelezaji wa ahadi mbalimbali zingine za mfanyabiashara huyo na kada wa CCM, ambazo amekuwa akitoa kwa CHADEMA mara kadhaa tangu mwaka 2010, zikiwemo za ujenzi wa chuo, uchimbaji wa visima, ofisi za makao makuu ya chama hicho na baiskeli 100 za walemavu.
      Attached Thumbnails    
      Last edited by Tumaini Makene; 5th July 2012 at 22:51.
      "Nothing in the world is more dangerous than sincere ignorance and conscientious stupidity." Martin Luther King

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,591
      Rep Power : 22053
      Likes Received
      991
      Likes Given
      769

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      CCM apo ingekuwa hamu yao wangemlimboka au ata kumuwangwe!
      Twakutakia maisha marefu mzee wetu!
      WEnye wivu wajinyonge
      Tumaini Makene likes this.
      WB Tanzania lead economist Jacques Morisset said the GDP doubled in 10 years, but it has failed to produce any significant decline in poverty levels.

    4. FJM
      #3
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,167
      Rep Power : 2566
      Likes Received
      5317
      Likes Given
      4585

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Mara ya mwisho CCM walimtuma Sophia Simba kwenda kumwangukia Mzee Sabodo, safari hii sijui watamtuma nani? Labda yule msoma nukta - Nchemba!
      Tumaini Makene likes this.

    5. #4
      Manyanza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Location : Look Behind You......
      Posts : 4,419
      Rep Power : 25469
      Likes Received
      1143
      Likes Given
      908

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      sijui CCM wanajisikiaje wakione mzee Sabodo akikisaidia Chama cha CDM kiasi hiki
      Tumaini Makene likes this.

    6. #5
      Sunshow's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th November 2011
      Posts : 689
      Rep Power : 517
      Likes Received
      95
      Likes Given
      2

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Safi sana mzee Sabodo kwa pamoja tutaikomboa Tanzania.
      Tumaini Makene likes this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      varavara's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th May 2012
      Posts : 25
      Rep Power : 356
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      yah! tunahitaji watu kama sabodo ambao wanachangia harakati bila mabadiliko bila woga, iwe kwa kutoa fedha au kujitoa binafsi mbele ya umma kutetea na kusimamia harakati za mabadiliko...

    9. #7
      Tumaini Makene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2012
      Posts : 1,059
      Rep Power : 8906
      Likes Received
      2228
      Likes Given
      768

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Manyanza
      sijui CCM wanajisikiaje wakione mzee Sabodo akikisaidia Chama cha CDM kiasi hiki
      Bila shaka watakuwa wanajiandaa kukaa kikao cha kumwita ni mdini, mkanda na mkabila. Viongozi wa kikao ni wale wanaoongoza kwa kuugua CHADEMA-phobia, Wassira, Mwigulu, Yule mpayukaji wao mkuu, Martha Mlata, Stella Manyanya, Lusinde na wengine kibao kama mnavyowajua wale ambao akili zao zimejaa ubaguzi muda wote. Mchawi huwa wa kwanza kuwaita wenzake wachawi ili kupoteza lengo la mashambulizi.
      MKALIKENYA likes this.
      "Nothing in the world is more dangerous than sincere ignorance and conscientious stupidity." Martin Luther King

    10. #8
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,394
      Rep Power : 10868
      Likes Received
      3773
      Likes Given
      426

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Asante baba,asante sana.
      Tumaini Makene likes this.

    11. #9
      makusanya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2011
      Posts : 329
      Rep Power : 467
      Likes Received
      42
      Likes Given
      154

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Watamtuma mabuba,jionista na lile chemba wao kujibu mapigo ngoja uone
      Tumaini Makene likes this.

    12. #10
      kula kwa tindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 416
      Rep Power : 462
      Likes Received
      70
      Likes Given
      40

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Saaaafi Sabodo..
      Hawa ndio wazalendo tunao wahitaji.. Sio VILAZA wanaochukua MIFWEZA yetu na kwenda kunenepesha wakoloni huku Serikali ikibebeshwa mzigo wa madeni na wao wakiendelea kuponda raha bila aibu.. Mungu atakupa zaidi yale wanao jinadu kwa HARAMBEE Makanisani
      Tumaini Makene likes this.

    13. #11
      kula kwa tindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 416
      Rep Power : 462
      Likes Received
      70
      Likes Given
      40

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Saaaafi Sabodo..
      Hawa ndio wazalendo tunao wahitaji.. Sio VILAZA wanaochukua MIFWEZA yetu na kwenda kunenepesha wakoloni huku Serikali ikibebeshwa mzigo wa madeni na wao wakiendelea kuponda raha bila aibu.. Mungu atakupa zaidi yale wanao jinadi kwa HARAMBEE Makanisani

    14. #12
      MwanaFalsafa1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Posts : 5,443
      Rep Power : 9877
      Likes Received
      609
      Likes Given
      444

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Politics aside namadmire sana mzee huyu kwani hata kama tuna tofautiana kisera vitendo kama hivi vinaonyesha kweli uzalendo.
      Tumaini Makene likes this.

    15. #13
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,602
      Rep Power : 15259
      Likes Received
      3727
      Likes Given
      2862

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Manyanza
      sijui CCM wanajisikiaje wakione mzee Sabodo akikisaidia Chama cha CDM kiasi hiki
      Hukumbuki jibu la Nape kwa wanaojiondoa CCM ndilo linalomhusu Sabodo

    16. #14
      RUCCI's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th October 2011
      Posts : 33
      Rep Power : 391
      Likes Received
      9
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By MwanaFalsafa1
      Politics aside namadmire sana mzee huyu kwani hata kama tuna tofautiana kisera vitendo kama hivi vinaonyesha kweli uzalendo.
      Sera zako ni zipi?

    17. #15
      mzee wa njaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th June 2011
      Posts : 1,340
      Rep Power : 669
      Likes Received
      194
      Likes Given
      107

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Ninachodhani ni kwamba Mr. Sabodo anafanya biashara zake kihalali sana. Kama ingekuwa vinginevyo wangemtupia kashfa na kumchafua Magazetini kama kawaida yao. Lakini kwenye hili wanaona aibu sana na tunajua wana hasira za kufa mtu huku wakishuhudia Chadema wakila bingo kila kukicha kutoka kwa mzee Sabodo.
      Tumaini Makene likes this.

    18. #16
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,488
      Rep Power : 46707
      Likes Received
      16316
      Likes Given
      8395

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Something is very wrong; there is something I don't LIKE about it. Can't point it out yet but it is there...
      Kaa la Moto and ndyoko like this.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    19. #17
      Nyani Ngabu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 15th May 2006
      Location : Ikungulyabashashi
      Posts : 39,162
      Rep Power : 31372
      Likes Received
      9571
      Likes Given
      683

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Huyu mzee asije akaishia Mabwepande...
      ndyoko likes this.
      Miafrika Ndivyo Tulivyo.

    20. #18
      mpayukaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2010
      Posts : 950
      Rep Power : 920
      Likes Received
      337
      Likes Given
      1498

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Naona kama Sabodo anawadhalilisha Chadema kwa faida zake binafsi na chama chake cha mafisadi. Huwa siamini wafanya biashara ambao ukiwauliza walivyochuma huo utajiri utakuta ni mafisadi wa kunuka. Hakika penye udhia penye rupia. Chadema wanazidi kuingia kwenye tope la ufisadi.
      ndyoko likes this.

    21. #19
      mpayukaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2010
      Posts : 950
      Rep Power : 920
      Likes Received
      337
      Likes Given
      1498

      Default Nani atawatoa CHADEMA kwenye mtego wa Sabodo?











      Sina ugomvi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wala mpenzi wake mpya Mustafa Jafary Sabodo. Nina ugomvi na staili ya Sabodo ya 'kukisaidia' Chadema. Kila akijisikia kupata publicity, huwaita viongozi wa Chadema na kuwapa milioni kadhaa za shilingi. Sijajua ni kwanini Chadema hawataki kujua historia ya 'utajiri' wa Sabodo anayejinasibu kama mjamaa aliyekuwa karibu na baba wa taifa Mwl Julius Nyerere. Kwa wanaojua ushupavu na uwazi wa Mwalimu wanashangaa ni kwanini uhusiano wao na Sabodo umekuwa maarufu baada ya kifo cha Mwalimu kama hakuna namna? Pia kuna utata zaidi ya nia ya Sabodo kusimama na kulala CCM lakini bado akajifanya ana mapenzi na Chadema. Je Sabodo ametumwa na CCM kuwahujumu Chadema kwa njia ya kuwadhalilisha ili wakati ukifika CCM watumia udhaifu huu kuwaumbua na kuwamaliza kisiasa?Je Sabodo anasukumwa na uzalendo na mapenzi wa demokrasia na Chadema au anatumwa na genge la wahindi linaloanza kuhofia maslahi yao kama CCM itapoteza dola? Je kwa namna hii si kuiweka Chadema kishawishini ili hatimaye iingie mfukoni mwa Sabodo na genge lake? Tunahofia hili kutokana na mazoea ya kuona karibu kila utawala kuanzia awamu ya pili unakuwa na mhindi nyuma yake akiwakilisha maslahi ya genge lake na watawala mafisi na mafisadi. Nani mara hii kasahau Gulamali aliyefikia hadi kumwita first lady Sitti Mwinyi Shemeji? Huyu alifika chini ya Ali Hassan Mwinyi sawa na Mohamed Raza alivyosifika chini ya Salmin Amour . Nani mara hii kasahau yule Mhindi, Sailesh Vithlani wa rada wa wakati wa Benjamin Mkapa? Nani haoni ujio wa Mohamed Dewji aka Mo anavyozidi kuwa maarufu chini ya serikali ya Jakaya Kikwete? Je Sabodo anacheza karata mbili yaani Chadema na CCM ili atayepita naye apete? Maana ni mwanachama wa CCM na 'mfadhili' wa Chadema. Wenye kujua siasa vizuri hawafurahishwi kuona viongozi tena wa juu wa Chadema wakipanga kama vitoto vya shule mbele ya mkuu wa shule kupokea cheki toka kwa Sabodo. Je Chadema emiridhika na kujishusha hadhi hadi kuwa chama kinachoweza kufadhiliwa na mtu binafsi tena mwenye madoa badala ya umma wa watanzania ambao wamekuwa wakikiunga mkono? Kwa wanaojua thamani ya imani ya umma wanashangaa kuona Chadema inavyozidi kujivua nguo kwa zawadi na ahadi ya vishilingi milioni kadhaa bila kujua kuwa hapo baadaye hili laweza kuigharimu madaraka. Nani atawasaidia na wakamsikiliza? Naomba nitoe hoja.
      seniorgeek and mayenga like this.

    22. #20
      MNYISANZU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,298
      Rep Power : 2016
      Likes Received
      584
      Likes Given
      76

      Default Re: Nani atawatoa CHADEMA kwenye mtego wa Sabodo?

      CDM ni chama makini chenye viongozi makini. Usifananishe na CCM

    23. Study Abroad
    Page 1 of 13 12311 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...