Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

    Report Post
    Page 4 of 13 FirstFirst ... 23456 ... LastLast
    Results 61 to 80 of 260
    1. #1
      Tumaini Makene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2012
      Posts : 1,062
      Rep Power : 8907
      Likes Received
      2231
      Likes Given
      768

      Default MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi



      MFANYABIASHARA maarufu na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mustafa Jaffer Sabodo amekichangia tena Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), sh. milioni 10, huku akitoa ahadi nyingine mpya ya kukipatia chama hicho mradi wa kukiingizia mapato na kuchimba visima kwa majimbo ya chama hicho kwa miaka 10.


      Amesema kuwa kazi inayofanywa na chama hicho kutoa elimu ya uraia hadi vijijini, huku kikizidi kuimarisha mtandao wake kwenye ngazi za vitongoji na mitaa kikidhamiria kuendelea kupigania na kutetea haki za wananchi, inapaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania mpenda maendeleo.

      Mfanyabiashara huyo ambaye amekuwa akijitokeza waziwazi bila uoga kukichangia chama hicho cha upinzani, akisema anafurahishwa na kazi ambayo kinafanya ya kutetea maslahi na rasilimali za Watanzania kutengeneza fursa za maendeleo, ameongeza kuwa amefurahishwa na Operesheni Okoa Kusini, ambayo chama hicho kilifanya karibuni mikoa ya Lindi na Mtwara.

      Akizungumza jana nyumbani kwake ambako alikutana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa kwa ajili ya kuzungumzia mchakato wa utekelezaji wa ahadi alizotoa kwa chama hicho, Mzee Sabodo aliahidi kuwa baada ya kukamilika kwa jengo la kuegesha magari linalojengwa katikati ya Jiji la Dar es Salaam, sehemu ya mapato yatatumika kuchimba visima kwa miaka 10.

      Mbali ya sehemu ya mapato kutoka katika jengo hilo la kuegesha magari ambalo linajengwa na Taasisi ya Khoja Shia Ithnasheri Jamaat (KSIJAMAAT), pia Mzee Sabodo alisema kuwa sehemu ya chini ya jengo hilo ambayo itakuwa na maduka, CHADEMA itapatiwa duka moja kama mmoja wa miradi ya kukipatia mapato.

      “Mtapata sehemu ya mapato ili kuchimba visima kwenye majimbo yenu kwa miaka kumi…pia mtapata duka pale ili mpate mradi wa mapato. Ili kuharakisha utekelezaji wa ahadi ya visima vile vingine fanyeni survey ninyi wenyewe na mpate mkandarasi, itakuwa sehemu ya gharama ya uchimbaji…hizi milioni 10 mtapata hundi hapa mkafanye kazi za wananchi,” alisema Mzee Sabodo.

      Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Slaa, mbali ya kumshukuru na kumpongeza Mzee Sabodo kwa ujasiri wake wa kuendelea kujitoa kusaidia harakati za kupigania haki za wananchi, mabadiliko ya kiutawala na kimfumo nchini, aliahidi kuwa chama hicho kitaendelea kutimiza wajibu wake kwa maslahi ya Watanzania.

      “Umekuwa mtu wa msaada mkubwa kwetu, umeendelea kuwatia moyo Watanzania wote wa kila namna kuacha uoga wa kuchangia harakati hizi, kwani lengo letu ni kuwatumikia Watanzania katika kila fursa tunayoipata, ambapo kwa sasa tutaendelea kuisimamia na kuiwajibisha serikali ya CCM ambayo ni dhahiri ielekea mwisho na wananchi wameichoka.

      “Nasi tunawaahidi Watanzania wote kuwa tutaendelea kuwatumikia na hatutawaangusha, tunatambua kuwa katika mparanganyiko huu mkubwa, kama ugumu wa maisha, hali mbaya ya uchumi, siasa zinazoyumba, ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma na migogoro katika makundi mbalimbali ya kijamii kwa sababu ya uongozi mbovu, CHADEMA linabaki kuwa ndiyo tumaini pekee kwa Watanzania,” alisema Dkt. Slaa.

      Dkt. Slaa aliyeambatana na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA, Antony Komu, aliongeza kuwa visima vya ahadi hii mpya kutokana na mapato ya jengo la maegesho ambayo ni tofauti na ahadi za visima vingine alizowahi kutoa mwaka jana na mapema mwaka huu, vitachimbwa katika maeneo mbalimbali ya Tanzania yenye kero kubwa za maji.



      Mbali ya ahadi hizo mpya za jana, Mzee Sabodo na Dkt. Slaa walizungumzia juu ya mchakato wa utekelezaji wa ahadi mbalimbali zingine za mfanyabiashara huyo na kada wa CCM, ambazo amekuwa akitoa kwa CHADEMA mara kadhaa tangu mwaka 2010, zikiwemo za ujenzi wa chuo, uchimbaji wa visima, ofisi za makao makuu ya chama hicho na baiskeli 100 za walemavu.
      Last edited by Tumaini Makene; 5th July 2012 at 22:51.
      "Nothing in the world is more dangerous than sincere ignorance and conscientious stupidity." Martin Luther King

    2. Miaka 50

    3. #61
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,306
      Rep Power : 1198
      Likes Received
      1182
      Likes Given
      1557

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Something is very wrong; there is something I don't LIKE about it. Can't point it out yet but it is there...
      Just say it. So many past promises have not been honored and He keeps making new promises. right?

    4. #62
      POMPO's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 12th March 2011
      Posts : 2,955
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1090
      Likes Given
      625

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      sidhani kama kinachonitatiza ni Sabodo kuchangia; la hasha. Kuna vitu ambavyo sidhani kama vimekaa sahihi... ngoja nirudi nyuma kidogo..
      Mkuu, hebu nenda mbele maana ukirudi nyuma, utapoteza muelekeo juu ya hili...FUNGUKA

    5. #63
      KIGOMA KWETU's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Posts : 77
      Rep Power : 372
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Tumaini Makene ..mfano mzuri ni jirani zetu wa kenya, waangalieni vyama vya upinzani wanavyouana wenyewe kwa wenywe wakati mzee moi katulia kwake...shame siasa za tz hakika sitopiga kula kamwe maisha..huyu sabodo halipi kodi sasa ameona ahamie upande wa pili wa shilingi hasije sumbuliwa 2015, chadema fikirila hii kitu itawacost

    6. #64
      Mtumishi Wetu's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 12th October 2010
      Location : Arusha
      Posts : 2,840
      Rep Power : 3544
      Likes Received
      536
      Likes Given
      5147

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Tumaini Makene Mkuu ukisikia uzalendo wa kweli kwa Mtanzania ndio huo, bila kujali dini kabila wala chama anafanya kile kinachotakiwa kufanywa na Watanzania wote!!!VIVA MZEE SABODO VIVA MAKAMANDA WA CDM, DAIMA MBELE NYUMA NI MWIKO!!!

      Tumaini Makene likes this.

    7. #65
      Mwikimbi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th March 2008
      Posts : 1,543
      Rep Power : 948
      Likes Received
      346
      Likes Given
      128

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By mpayukaji
      Naona kama Sabodo anawadhalilisha Chadema kwa faida zake binafsi na chama chake cha mafisadi. Huwa siamini wafanya biashara ambao ukiwauliza walivyochuma huo utajiri utakuta ni mafisadi wa kunuka. Hakika penye udhia penye rupia. Chadema wanazidi kuingia kwenye tope la ufisadi.
      usafi wa sabodo unajulikana tangu enzi za nyerere, huyu si mwizi ni kama wafanyibiashara waliopata pesa kihalali kama ndesamburo, aikaeli mbowe nk, siyo kila tajiri ni mwizi

    8. FemaTV & Radio

    9. #66
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,306
      Rep Power : 1198
      Likes Received
      1182
      Likes Given
      1557

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Tumaini Makene
      Bila shaka watakuwa wanajiandaa kukaa kikao cha kumwita ni mdini, mkanda na mkabila. Viongozi wa kikao ni wale wanaoongoza kwa kuugua CHADEMA-phobia, Wassira, Mwigulu, Yule mpayukaji wao mkuu, Martha Mlata, Stella Manyanya, Lusinde na wengine kibao kama mnavyowajua wale ambao akili zao zimejaa ubaguzi muda wote. Mchawi huwa wa kwanza kuwaita wenzake wachawi ili kupoteza lengo la mashambulizi.
      Makini, umesema sehemu ya mazungumzo ilihusu utekelezaji wa ahadi zake za nyuma, please tupe maelezo ya ziada.utekelezaji wa ahadi zake za nyuma umefikia wapi?

    10. #67
      jogi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 3,983
      Rep Power : 1212
      Likes Received
      970
      Likes Given
      247

      Default

      Quote By Rejao
      CDM inabidi warudi shule wakasome Portfolio Theory. Naona somo la diversification limewakalia kushoto kabisa. Why always wanategemea source moja ya finance? Tena mbaya zaidi kutoka kwa individual!! Hawawezi kubuni njia nyingine za kuraise fund?
      CHEMBA ya iramba magharibi imewahi kusema cdm inafadhiliwa kwa siri na cdu cha ujerumani,cdm kinawaonyesha wafadhili wake hadharani CHEMBA imeumbuka, mnyama kutoka gombe alisema cdm ni wadini (wakristo) jamii ya washia (sabodo) waislam (prof. Safari) inajitokeza hadharani kuthibitisha cdm si wadini, mnyama anatamani kurudi msituni nape akawadanganya watanzania eti cdm ni chama cha kikanda m4c imewachakaza kusini (lindi na mtwara) sasa wanalaumiana, mbeya, iringa, mwanza n.k zinamfanya nape kuwa kijana wa mipasho na kutoa tafsiri mpya ya gamba kila kukicha Picha itakuwa tamu pale INJINI YA MANYANYA itakapo kuwa salo serikali itakapoumbuliwa kwa habari za utekaji nyara wa dr. ULIMBOKA
      Njilembera likes this.

    11. #68
      Rejao's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 4th May 2010
      Location : Long Street
      Posts : 8,756
      Rep Power : 0
      Likes Received
      3343
      Likes Given
      2878

      Default

      Quote By Kimbunga
      Duh Rejao kumbe wewe mzee wa finance na mambo ya investment? Umenikumbusha mbali
      Hahahah...niligusa gusa huko miaka ya nyuma mkuu.

    12. #69
      Mnyakatari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th October 2010
      Posts : 697
      Rep Power : 674
      Likes Received
      250
      Likes Given
      180

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Sidhani jama ni jambo la kufurahia bila kutafakari.

    13. #70
      majebere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 2,206
      Rep Power : 0
      Likes Received
      322
      Likes Given
      111

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Cheza na hela wewe, jamaa wametoa meno kama matangazo ya whitedent. Mnawapaka mavi wadosi halafu mnafurahia vihela vyao. Zitawatokea puani hizo.

    14. #71
      KIJOME's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 7th June 2012
      Posts : 1,323
      Rep Power : 0
      Likes Received
      244
      Likes Given
      220

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      .....JAH akujalie baba sabodo kwa moyo wako wa kuwakumbuka wanyonge wa nchi hii ili kusaidia mapambano haya kuelekea uhuru wa kweli...

    15. #72
      Rejao's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 4th May 2010
      Location : Long Street
      Posts : 8,756
      Rep Power : 0
      Likes Received
      3343
      Likes Given
      2878

      Default

      Quote By lodrick
      Hivi unataka kutuambia kwamba Sabodo ndio source pekee ya finance kwa CHADEMA tangia kianzishwe? Kaa ukijua hakuna ubaya wowote kwa chama kupata ufadhili kutoka kwa individuals, vinginevyo ungeanza kuwalaumu magamba kwa tabia yao ya kupokea misaada kutoka kwa wafanyabiashara kwa ajili ya kufinance kampeni zao.
      Quote By Duble Chris
      Rejeo huwezi kukataa pesa zinazo ingia kumbuka kuwa CDM hawaombi msaada kwake bali huyu mzee anaguswa utendaji mzuri wa CDM na anamua kuwasupport
      Naona mnatumia nguvu nyingi sana kukitetea CDM...tafuteni kufahamu vizuri matumizi ya hizo pesa kwanza ndio mje kufanya utetezi wenu hapa. Mimi nimejaribu tu kuwapa changamoto CDM watafute njia mbadala za kujiongezea kipato badala ya kumtegemea mtu mmoja tu.

    16. #73
      EMMANUEL NSAMBI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th October 2011
      Posts : 357
      Rep Power : 454
      Likes Received
      78
      Likes Given
      17

      Default Re: Nani atawatoa CHADEMA kwenye mtego wa Sabodo?

      Quote By mpayukaji










      Sina ugomvi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wala mpenzi wake mpya Mustafa Jafary Sabodo. Nina ugomvi na staili ya Sabodo ya 'kukisaidia' Chadema. Kila akijisikia kupata publicity, huwaita viongozi wa Chadema na kuwapa milioni kadhaa za shilingi. Sijajua ni kwanini Chadema hawataki kujua historia ya 'utajiri' wa Sabodo anayejinasibu kama mjamaa aliyekuwa karibu na baba wa taifa Mwl Julius Nyerere. Kwa wanaojua ushupavu na uwazi wa Mwalimu wanashangaa ni kwanini uhusiano wao na Sabodo umekuwa maarufu baada ya kifo cha Mwalimu kama hakuna namna? Pia kuna utata zaidi ya nia ya Sabodo kusimama na kulala CCM lakini bado akajifanya ana mapenzi na Chadema. Je Sabodo ametumwa na CCM kuwahujumu Chadema kwa njia ya kuwadhalilisha ili wakati ukifika CCM watumia udhaifu huu kuwaumbua na kuwamaliza kisiasa?Je Sabodo anasukumwa na uzalendo na mapenzi wa demokrasia na Chadema au anatumwa na genge la wahindi linaloanza kuhofia maslahi yao kama CCM itapoteza dola? Je kwa namna hii si kuiweka Chadema kishawishini ili hatimaye iingie mfukoni mwa Sabodo na genge lake? Tunahofia hili kutokana na mazoea ya kuona karibu kila utawala kuanzia awamu ya pili unakuwa na mhindi nyuma yake akiwakilisha maslahi ya genge lake na watawala mafisi na mafisadi. Nani mara hii kasahau Gulamali aliyefikia hadi kumwita first lady Sitti Mwinyi Shemeji? Huyu alifika chini ya Ali Hassan Mwinyi sawa na Mohamed Raza alivyosifika chini ya Salmin Amour . Nani mara hii kasahau yule Mhindi, Sailesh Vithlani wa rada wa wakati wa Benjamin Mkapa? Nani haoni ujio wa Mohamed Dewji aka Mo anavyozidi kuwa maarufu chini ya serikali ya Jakaya Kikwete? Je Sabodo anacheza karata mbili yaani Chadema na CCM ili atayepita naye apete? Maana ni mwanachama wa CCM na 'mfadhili' wa Chadema. Wenye kujua siasa vizuri hawafurahishwi kuona viongozi tena wa juu wa Chadema wakipanga kama vitoto vya shule mbele ya mkuu wa shule kupokea cheki toka kwa Sabodo. Je Chadema emiridhika na kujishusha hadhi hadi kuwa chama kinachoweza kufadhiliwa na mtu binafsi tena mwenye madoa badala ya umma wa watanzania ambao wamekuwa wakikiunga mkono? Kwa wanaojua thamani ya imani ya umma wanashangaa kuona Chadema inavyozidi kujivua nguo kwa zawadi na ahadi ya vishilingi milioni kadhaa bila kujua kuwa hapo baadaye hili laweza kuigharimu madaraka. Nani atawasaidia na wakamsikiliza? Naomba nitoe hoja.
      Chadema hata wewe na mimi tukiwaita wanaitikia wito.Siyo kwa Sabodo tu hebu waite wewe kama hawatakuja.Kile
      ni chama cha wote haijalishi una uwezo gani.Ndio maana wana kesi nyingi walizosingiziwa kufanya mikutano isiyo halali,
      wao wakipita na wananchi wakitaka kywasalimia wanasimama na sio kama magamba wanafunga vioo utafikiri wameona mbun'go.

    17. #74
      ndyoko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 4,505
      Rep Power : 1706
      Likes Received
      1199
      Likes Given
      1916

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Something is very wrong; there is something I don't LIKE about it. Can't point it out yet but it is there...
      funguka kaka, your ideas and wisdom is out there to be admired and shared!
      “If you can not get what you love, then love what you have”

    18. #75
      Kiganyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2012
      Posts : 1,162
      Rep Power : 983
      Likes Received
      708
      Likes Given
      400

      Default Sabodo Achangia M4C - CHADEMA


      Mfanyabiashara maarufu na Kada wa CCM, Mzee Mustafa Jaffer Sabodo akikabidhi hundi ya Sh10m kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod Slaa nyumbani kwa Upanga, Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA, Antony Komu. Fedha hizo ilikuwa sehemu ya mchango mwingine wa Mzee Sabodo pamoja na ahadi kwa ajili ya kusaidia shughuli za chama hicho kuendelea kufanya kazi zake za kuimarisha na kueneza mtandao wake, ngazi za mitaa na vitongoji nchi nzima.




      Dkt. Slaa akipeana mkono na Sabodo.

    19. #76
      ndyoko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 4,505
      Rep Power : 1706
      Likes Received
      1199
      Likes Given
      1916

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By mpayukaji
      Naona kama Sabodo anawadhalilisha Chadema kwa faida zake binafsi na chama chake cha mafisadi. Huwa siamini wafanya biashara ambao ukiwauliza walivyochuma huo utajiri utakuta ni mafisadi wa kunuka. Hakika penye udhia penye rupia. Chadema wanazidi kuingia kwenye tope la ufisadi.
      Na kweli huu ni mpayuko haswaaaa!
      “If you can not get what you love, then love what you have”

    20. #77
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,982
      Rep Power : 2589
      Likes Received
      637
      Likes Given
      776

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By makusanya
      Watamtuma mabuba,jionista na lile chemba wao kujibu mapigo ngoja uone
      Tatizo la CCM ni kuchumia tumbo, hata mimi ningikuwa na pesa nisingewachangia ng'oooo. Kuna mmoja alikimbia na mchango wangu siku za nyuma. Sirudii tena.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    21. #78
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,982
      Rep Power : 2589
      Likes Received
      637
      Likes Given
      776

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Rejao
      Naona mnatumia nguvu nyingi sana kukitetea CDM...tafuteni kufahamu vizuri matumizi ya hizo pesa kwanza ndio mje kufanya utetezi wenu hapa. Mimi nimejaribu tu kuwapa changamoto CDM watafute njia mbadala za kujiongezea kipato badala ya kumtegemea mtu mmoja tu.
      Unatamani ungepewa wewe, Tatizo lenu si tunalijua?
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    22. #79
      Third Eye's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th January 2012
      Posts : 167
      Rep Power : 461
      Likes Received
      26
      Likes Given
      13

      Default

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Something is very wrong; there is something I don't LIKE about it. Can't point it out yet but it is there...

      nilijua ni mimi tu mwenye mashaka na hizi charity, what if huyu mzee anajitengenezea mazingira mazuri na whoever comes to power? I mean ikitokea Chadema imeingia madarakan hawawezi kumtosa mfadhiri wao, na Ccm ikibaki hawewezi kumtosa kada wao, i think he is playing safe

    23. #80
      Tutor B's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th June 2011
      Location : Bukoba Municipal
      Posts : 1,966
      Rep Power : 1187
      Likes Received
      595
      Likes Given
      41

      Default Re: Sabodo Achangia M4C - CHADEMA

      Nimeona! CDM tunachukua nchi kiulaini kwani chama chetu kinapendwa na wengi.
      "Ukipendwa - penda, ipo siku utapenda - usipendwe"

    Page 4 of 13 FirstFirst ... 23456 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...