Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

    Report Post
    Page 3 of 13 FirstFirst 12345 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 260
    1. #1
      Tumaini Makene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2012
      Posts : 1,061
      Rep Power : 8907
      Likes Received
      2231
      Likes Given
      768

      Default MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi



      MFANYABIASHARA maarufu na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mustafa Jaffer Sabodo amekichangia tena Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), sh. milioni 10, huku akitoa ahadi nyingine mpya ya kukipatia chama hicho mradi wa kukiingizia mapato na kuchimba visima kwa majimbo ya chama hicho kwa miaka 10.


      Amesema kuwa kazi inayofanywa na chama hicho kutoa elimu ya uraia hadi vijijini, huku kikizidi kuimarisha mtandao wake kwenye ngazi za vitongoji na mitaa kikidhamiria kuendelea kupigania na kutetea haki za wananchi, inapaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania mpenda maendeleo.

      Mfanyabiashara huyo ambaye amekuwa akijitokeza waziwazi bila uoga kukichangia chama hicho cha upinzani, akisema anafurahishwa na kazi ambayo kinafanya ya kutetea maslahi na rasilimali za Watanzania kutengeneza fursa za maendeleo, ameongeza kuwa amefurahishwa na Operesheni Okoa Kusini, ambayo chama hicho kilifanya karibuni mikoa ya Lindi na Mtwara.

      Akizungumza jana nyumbani kwake ambako alikutana na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa kwa ajili ya kuzungumzia mchakato wa utekelezaji wa ahadi alizotoa kwa chama hicho, Mzee Sabodo aliahidi kuwa baada ya kukamilika kwa jengo la kuegesha magari linalojengwa katikati ya Jiji la Dar es Salaam, sehemu ya mapato yatatumika kuchimba visima kwa miaka 10.

      Mbali ya sehemu ya mapato kutoka katika jengo hilo la kuegesha magari ambalo linajengwa na Taasisi ya Khoja Shia Ithnasheri Jamaat (KSIJAMAAT), pia Mzee Sabodo alisema kuwa sehemu ya chini ya jengo hilo ambayo itakuwa na maduka, CHADEMA itapatiwa duka moja kama mmoja wa miradi ya kukipatia mapato.

      “Mtapata sehemu ya mapato ili kuchimba visima kwenye majimbo yenu kwa miaka kumi…pia mtapata duka pale ili mpate mradi wa mapato. Ili kuharakisha utekelezaji wa ahadi ya visima vile vingine fanyeni survey ninyi wenyewe na mpate mkandarasi, itakuwa sehemu ya gharama ya uchimbaji…hizi milioni 10 mtapata hundi hapa mkafanye kazi za wananchi,” alisema Mzee Sabodo.

      Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Slaa, mbali ya kumshukuru na kumpongeza Mzee Sabodo kwa ujasiri wake wa kuendelea kujitoa kusaidia harakati za kupigania haki za wananchi, mabadiliko ya kiutawala na kimfumo nchini, aliahidi kuwa chama hicho kitaendelea kutimiza wajibu wake kwa maslahi ya Watanzania.

      “Umekuwa mtu wa msaada mkubwa kwetu, umeendelea kuwatia moyo Watanzania wote wa kila namna kuacha uoga wa kuchangia harakati hizi, kwani lengo letu ni kuwatumikia Watanzania katika kila fursa tunayoipata, ambapo kwa sasa tutaendelea kuisimamia na kuiwajibisha serikali ya CCM ambayo ni dhahiri ielekea mwisho na wananchi wameichoka.

      “Nasi tunawaahidi Watanzania wote kuwa tutaendelea kuwatumikia na hatutawaangusha, tunatambua kuwa katika mparanganyiko huu mkubwa, kama ugumu wa maisha, hali mbaya ya uchumi, siasa zinazoyumba, ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma na migogoro katika makundi mbalimbali ya kijamii kwa sababu ya uongozi mbovu, CHADEMA linabaki kuwa ndiyo tumaini pekee kwa Watanzania,” alisema Dkt. Slaa.

      Dkt. Slaa aliyeambatana na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA, Antony Komu, aliongeza kuwa visima vya ahadi hii mpya kutokana na mapato ya jengo la maegesho ambayo ni tofauti na ahadi za visima vingine alizowahi kutoa mwaka jana na mapema mwaka huu, vitachimbwa katika maeneo mbalimbali ya Tanzania yenye kero kubwa za maji.



      Mbali ya ahadi hizo mpya za jana, Mzee Sabodo na Dkt. Slaa walizungumzia juu ya mchakato wa utekelezaji wa ahadi mbalimbali zingine za mfanyabiashara huyo na kada wa CCM, ambazo amekuwa akitoa kwa CHADEMA mara kadhaa tangu mwaka 2010, zikiwemo za ujenzi wa chuo, uchimbaji wa visima, ofisi za makao makuu ya chama hicho na baiskeli 100 za walemavu.
      Last edited by Tumaini Makene; 5th July 2012 at 22:51.
      "Nothing in the world is more dangerous than sincere ignorance and conscientious stupidity." Martin Luther King

    2. Miaka 50

    3. #41
      WA-UKENYENGE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2011
      Location : Inside a Smart Grid
      Posts : 2,417
      Rep Power : 5038
      Likes Received
      782
      Likes Given
      1785

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Something is very wrong; there is something I don't LIKE about it. Can't point it out yet but it is there...
      I also see that MM!
      mayenga likes this.
      "The usual conclusion is that you can't put a price on a human life. But you can if you must".

    4. #42
      mayenga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th September 2009
      Posts : 1,564
      Rep Power : 806
      Likes Received
      305
      Likes Given
      437

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Iam smelling something fishy.In corporate theory,nothing should go for nothing.
      A man's character may be learned from the adjectives which he habitually uses in conversation.

    5. #43
      Jumakidogo's Avatar
      R I P Array
      Join Date : 16th July 2009
      Location : DOM & DAR
      Posts : 1,868
      Rep Power : 1176
      Likes Received
      390
      Likes Given
      42

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Safi! Lakini mapato na matumizi ya chama tu, ndo kitendawili tega.

    6. #44
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,498
      Rep Power : 46709
      Likes Received
      16345
      Likes Given
      8416

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      sidhani kama kinachonitatiza ni Sabodo kuchangia; la hasha. Kuna vitu ambavyo sidhani kama vimekaa sahihi... ngoja nirudi nyuma kidogo..
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    7. #45
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,476
      Rep Power : 6168
      Likes Received
      3043
      Likes Given
      1016

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By WA-UKENYENGE
      I also see that MM!
      WA-UKENYENGE hujui kwamba pesa sabuni ya roho? Marijani alikuwa na maana kubwa alipoimba ule wimbo penye udhia penyeza rupia. Wacheni pesa iitwe fedha!
      WA-UKENYENGE likes this.
      CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.

    8. FemaTV & Radio

    9. #46
      Rejao's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 4th May 2010
      Location : Long Street
      Posts : 8,756
      Rep Power : 0
      Likes Received
      3343
      Likes Given
      2878

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      CDM inabidi warudi shule wakasome Portfolio Theory. Naona somo la diversification limewakalia kushoto kabisa. Why always wanategemea source moja ya finance? Tena mbaya zaidi kutoka kwa individual!! Hawawezi kubuni njia nyingine za kuraise fund?

    10. #47
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,476
      Rep Power : 6168
      Likes Received
      3043
      Likes Given
      1016

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By mayenga
      Iam smelling something fishy.In corporate theory,nothing should go for nothing.
      Kuna sinema ya Ki Nigeria niliiona inaitwa Nothing for Nothing imeigizwa na kamanda Kanayo O Kanayo! ina maana kubwa kwamba hakuna free lunch katika dunia hii!
      CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.

    11. #48
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,476
      Rep Power : 6168
      Likes Received
      3043
      Likes Given
      1016

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Rejao
      CDM inabidi warudi shule wakasome Portfolio Theory. Naona somo la diversification limewakalia kushoto kabisa. Why always wanategemea source moja ya finance? Tena mbaya zaidi kutoka kwa individual!! Hawawezi kubuni njia nyingine za kuraise fund?
      Duh Rejao kumbe wewe mzee wa finance na mambo ya investment? Umenikumbusha mbali
      CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.

    12. #49
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,159
      Rep Power : 24268
      Likes Received
      4670
      Likes Given
      2294

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Precise pangolin
      Labda humpendi kwasababu yaKyerefaso kwi! Kwi! Kwi!
      hahaaaaaaaaaaaa!!!!!!
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    13. #50
      lodrick's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Posts : 61
      Rep Power : 437
      Likes Received
      19
      Likes Given
      7

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Rejao
      CDM inabidi warudi shule wakasome Portfolio Theory. Naona somo la diversification limewakalia kushoto kabisa. Why always wanategemea source moja ya finance? Tena mbaya zaidi kutoka kwa individual!! Hawawezi kubuni njia nyingine za kuraise fund?

      Hivi unataka kutuambia kwamba Sabodo ndio source pekee ya finance kwa CHADEMA tangia kianzishwe? Kaa ukijua hakuna ubaya wowote kwa chama kupata ufadhili kutoka kwa individuals, vinginevyo ungeanza kuwalaumu magamba kwa tabia yao ya kupokea misaada kutoka kwa wafanyabiashara kwa ajili ya kufinance kampeni zao.
      Tumaini Makene likes this.

    14. #51
      MKALIKENYA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 703
      Rep Power : 500
      Likes Received
      281
      Likes Given
      405

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Something is very wrong; there is something I don't LIKE about it. Can't point it out yet but it is there...
      What is that Mwanakijiji na wewe umeanza kuongea kwa mafumbo kama MIZENGO PINDA emu funguka tunakueshimu sana.

    15. #52
      +255's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Posts : 1,079
      Rep Power : 588
      Likes Received
      205
      Likes Given
      0

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Mwisho wa siku hata wanachama wenyewe wa CDM walivyo maz*** hawawezi hata kuulizia kuhusu michango yao inavyofanya kazi.Endeleeni tu kuchangia huo mradi wa watu fulani wa kaskazini kuwapiga pesa, mnadanganywa M4C

    16. #53
      KOMBAJR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th November 2011
      Posts : 3,858
      Rep Power : 5949
      Likes Received
      798
      Likes Given
      227

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Watakayosema kuhusu Sabodo na CDM kwasasa hayatakuwa na Nafasi M4C inasonga kwa mwendo wa light!
      Face Reality As it Is, Not As it Was or As You Wish It To Be.

    17. #54
      Duble Chris's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2011
      Posts : 2,339
      Rep Power : 871
      Likes Received
      382
      Likes Given
      304

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      mpayukaji
      CCDM kupokea pesa toka kwa huyu ndg si kosa kumbuka kuwa CDM kwenye mikutano yake ya hadhara imekuwa ikipokea michango toka kwa wananchi wanahudhuria mikutano hiyo na wenye mapenzi mema na chama pia nchi hii tofauti yake ni kiwango cha pesa tu

      issue ya namna pesa zinavyo patikana hilo ni suala la serikali yetu. Labda sema kinacho weza kuwaua CHADEMA ni transpancy dhidi ya matumizi ya hizi pesa na umakini mkubwa kufanya kile kilicho kusudiwa tena kwa WAKATI kama
      Kimbunga anavyo lalamika.
      frustration is given by expectationdivide by
      outcome
      ie
      frustration = expectation/outcome


    18. #55
      Duble Chris's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2011
      Posts : 2,339
      Rep Power : 871
      Likes Received
      382
      Likes Given
      304

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Rejao
      CDM inabidi warudi shule wakasome Portfolio Theory. Naona somo la diversification limewakalia kushoto kabisa. Why always wanategemea source moja ya finance? Tena mbaya zaidi kutoka kwa individual!! Hawawezi kubuni njia nyingine za kuraise fund?
      Rejeo huwezi kukataa pesa zinazo ingia kumbuka kuwa CDM hawaombi msaada kwake bali huyu mzee anaguswa utendaji mzuri wa CDM na anamua kuwasupport
      frustration is given by expectationdivide by
      outcome
      ie
      frustration = expectation/outcome


    19. #56
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,670
      Rep Power : 1909
      Likes Received
      1563
      Likes Given
      676

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Rejao
      CDM inabidi warudi shule wakasome Portfolio Theory. Naona somo la diversification limewakalia kushoto kabisa. Why always wanategemea source moja ya finance? Tena mbaya zaidi kutoka kwa individual!! Hawawezi kubuni njia nyingine za kuraise fund?
      Unataka watumie ile njia ya CCM ya kuiba kodi za wananchi nafikiri ndio diversification unayoizungumzia
      Tumaini Makene likes this.

    20. #57
      Tumaini Makene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2012
      Posts : 1,061
      Rep Power : 8907
      Likes Received
      2231
      Likes Given
      768

      Default Re: Nani atawatoa CHADEMA kwenye mtego wa Sabodo?

      Kabla hamjaanza kusingizia watu wengine kuwa ni mafisadi, wakamateni na kuwashtaki kwanza wale ambao walishatajwa tena kwa ushahidi ulio wazi. Badala ya kuwashughulikia mnazidi kuwapatia nafasi kwenye viti vya mbele, hasa bungeni. Leo watuhumiwa wakubwa Richmond, Kagoda, Rada n.k, ni nani kwenye chama chenu cha magamba/mafisadi na kwenye serikali yenu na kwenye bunge 'lenu'.

      Kabla hamjaanza kusingizia bila ushahidi hata chembe, twambieni mmefikia wapi kujivua gamba na watuhumiwa wa ufisadi mliwataja kwa majina wenyewe...

      Kabla hamjaanza kushusha shutuma zisizo na msingi zikiwa ni dalili ya kuendelea kukubali kushindwa kwenye kila angle ya battle hii, kwanza waambieni Watanzania wale mawaziri waliokabiliwa na shutuma kubwa za ubadhirifu karibuni wako wapi vile, lupango eeh, kule Segerea, si ndiyo.

      Kabla hamjaanza kuhukumu kila mfanyabiashara kwa kumwita ni fisadi bila ushahidi hata wa kuokoteza achilia mbali genuine, waambieni kwanza Watanzania wale wafanyabiashara mnaonedelea kushirikiana nao katika kujitajirisha kupitia rasilimali na ofisi za Watanzania, wako wapi.

      Usitake kulinganisha misaada yenu iliyokuwa ikitolewa kwenye giza totoro, nyuma ya pazia bila Watanzania kujua. Mchangiaji mwenye nia njema na mwenye nia mbaya unamjua kuanzia hapa katika namna anayochangia. Hivi wale wenu walishawahi kukiri na ninyi mkakiri hadharani kuwa waliwachangia mamilioni na mabilioni kwa sababu gani...mpaka mkaamua kuwalipa EPA, Kagoda, TANGOLD, Meremeta, Migodi ya madini, mashirika yetu ya umma, nafasi za uongozi, n.k.

      Mnafikiri mlivyofadhiliwa na ********** kama uliowataja mwenyewe kwenye maandiko yako (umemuacha RA), kila mmoja atafanana na ninyi eeh! Msaada wa Sabodo utaendelea kuchukuliwa kwa thamani ile ile anayopewa Mwananchi wa kawaida kule Mtwara, Lindi, Mwanza, Dar es Salaam

      Kwa CHADEMA anachotoa M4C haitabagua watu hata mmoja kwa sababu ya rangi yake, kabila lake, dini yake au mahali anapotoka au uwezo wake wa kipato. Never. Kila mtu atakuwa na mchango sawa katika hili vuguvugu. Anachotoa Sabodo kitapata thamani ile ile wanayotoa wananchi wanaokuja kwenye mikutano ya hadhara ambao nao wanatoa hadharani bila kificho.

      Hebu leo hii acheni kuwatisha wafanyabiashara wengi tu wasafi na wafanyakazi wengine, wakiwemo watumishi wa umma na sekta binafsi, lakini bado wamejaa uoga kwa kutishwa na vyombo vya serikali kama TRA na vyombo vya dola...mkiwaacha na wakaona wazi mazingira yako safi wao kuchangia harakati hizi kwa chochote kidogo/kikubwa walichonacho, mtakwisha saa 2 asubuhi.

      Na kitu muhimu zaidi kwa Sabodo inaweza isiwe michango yake pekee, bali staili yake ya utoaji ambayo inasukuma kwa kasi sana dhana ya kuondoa uoga miongoni mwa Watanzania wa kada mbalimbali ambao mpaka leo wanapenda kweli mabadiliko lakini bado hawajaweza kuogopa na kuukimbia UOGA...nothing to fear but fear itself.

      Mwacheni Sabodo awatie ujasiri wengi zaidi walio wasafi wachangie M4C, maana Watanzania kuondolewa uoga na kutiwa ujasiri ndicho kitu kinachowaogopesha kabisa ninyi.
      POMPO and FortJeasus like this.
      "Nothing in the world is more dangerous than sincere ignorance and conscientious stupidity." Martin Luther King

    21. #58
      jogi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 3,981
      Rep Power : 1212
      Likes Received
      968
      Likes Given
      247

      Default

      mpayukaji Ni vizuri kuchukua tahadhari.

    22. #59
      kichomiz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2011
      Posts : 4,053
      Rep Power : 1232
      Likes Received
      652
      Likes Given
      80

      Default

      Quote By mpayukaji
      Naona kama Sabodo anawadhalilisha Chadema kwa faida zake binafsi na chama chake cha mafisadi. Huwa siamini wafanya biashara ambao ukiwauliza walivyochuma huo utajiri utakuta ni mafisadi wa kunuka. Hakika penye udhia penye rupia. Chadema wanazidi kuingia kwenye tope la ufisadi.
      Mkuu kwa hilo la biashara zake nadhani hakuna shaka,kama ingekuwa ni fisadi yule mlopokaji original aka vuvuzela angepiga kelele mpaka angelazwa,si unamjua alivyo na kihelehele?

    23. #60
      Mr.Professional's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th October 2010
      Location : Dar
      Posts : 1,491
      Rep Power : 736
      Likes Received
      206
      Likes Given
      92

      Default Re: MZEE Mustafa Jaffer Sabodo achangia tena M4C (CHADEMA) na ahadi zingine za miradi

      Quote By Kimbunga
      Mimi nimekuwa nikisikia Sabodo anachangia n kusema atachimba visima lakini sioni am kusikia siku moja CDM wakisema leo tunazindua visima vilivyochimbwa kwa pesa za Sabodo. Hivi mchakato wa kuchimba visima unachukua miaka mingapi?
      Mkuu Kimbunga uchimbaji wa visima huamki tu asubuhi na kuanza kuchimba ni lazima kuwe na survey ya kutosha na uhakika wa maji yatakayokuwepo kwa muda mrefu. Otherwise utajikuta mmetumia raslimali pesa vibaya na tutaanza kuwanyooshea vidole chadema kwa matumizi mabaya ya pesa. Ndo maana hata yeye kawaambia hiyo jana kuwa watafute wakandarasi wenyewe wa wafanye detailed survey wenyewe ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa ahadi.
      for further assistance please press "CTRL + W"

    Page 3 of 13 FirstFirst 12345 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...