Re: Azimio la kikao cha CCM Juu ya Watumishi Serikalini

By
FJM
Madhara ya huu mpango ni mbaya sana sana sana. Ukishaingiza siasa kwenye idara za serikali basi nchi haiwezi kupiga hatua hata kidogo. Itaishia kwenye 'state corruption' ya hali ya juu na taaluma za watu zitafunikwa. Jamani dunia inasonga mbele tena kwa kasi kubwa, hakuna atakayesubiri Tanzania imalize siasa zake. Giza tupu.
Mbona kama wewe ni mgeni na Tanzania na siasa zake? ni idara ipi ya serikali ambayo sio politicized? anza na polisi, jeshi, mahakama, benki kuu, hazina, vyuo vikuu, kila taasisi inaendeshwa kisiasa ndio maana hakuna maendeleo nchi hii! Rais na mawaziri hawajui lini wanafanya kazi za serikali lini wanafanya za chama! mawaziri wanaenda kwenye kampeni za chaguzi ndogo mfano Igunga, Arumeru na kutumia nafasi zao za uwaziri kutisha wananchi kuwa wasipochagua ccm hawapati huduma halafu wewe unafikiri hakuna siasa kwenye taasisi za umma??
Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!
Follow Us Here