Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

    Report Post
    Page 1 of 4 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 71
    1. #1
      VUTA-NKUVUTE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2011
      Posts : 1,703
      Rep Power : 723
      Likes Received
      892
      Likes Given
      125

      Default Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Ingawa ni maelezo marefu,si vibaya tukajikumbusha mambo haya kutoka kwenye Hansard za MKUTANO WA NANE

      Kikao cha Tano – Tarehe 19 Juni, 2012

      VIDEO:




      MHE. MCH. PETER S. MSIGWA:

      Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi.Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuanza kwa nukuuambayo naipenda sana inayosema:-


      “Insanity is keeping doing the same thing in the same way and expecting different result”

      ambazo zinalikabili taifa lakini kwa bahati mbaya nimeona yaani uwendawazimu nikufanya jambo lilelile kwa njia ileile huku ukitegemea matokeo tofauti.

      Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanafalsafa Albert Einstein anasema:-“Problems can not be solved by the same level of thinking that creates them”. Ndugu zangu, kabla sijawa Mbunge kama alivyosema kaka yangu Mheshimiwa Akunaay, nilikuwa nawa-admire sana Wabunge wanavyokuwa Bungeni, wakivaa suti, nilikuwa naona hapa ni mahali ambapo tuna reason, mahali ambapo tuna question na mahali ambapo tunatoka na solutions


      is the opposite, binafsi najisikia vibaya sana. Kama taifa tupohapa, we are dealing na future ya taifa hili, tunashughulika namamia ya maskini wa Tanzania, tunashughulika na barabarambovu za Watanzania, tunashughulika na hospitali mbovu zaWatanzania, halafu tunakuja hapa tunaongea mambo yakhanga!

      Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma historia, nchi za Ulayakarne ya 14, Marekani na Ulaya na nchi zilizoendelea, zilikuwana fikra na mawazo kama tunavyofanya sasa hivi lakini ilipofikakarne ya 18, inaitwa age of enlightenment, reasoning age, walianza kufikiri, kuhoji na kudadisi. Tunapofika katika karne hiikatika Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania,tunapojadili bajeti maana yake tunazo changamotozinazotukabili kama taifa.

      Badala ya kukaa na kujiuliza kwa ninitupo hapa, tunatokaje hapa tulipo, tunaanza kuongeangonjera na maneno ya uswahiliuswahili yaani unafiki, woga,kujipendekeza na kutokujadili mambo ya msingi.


      (Makofi)


      Mheshimiwa Mwenyekiti, najisikia uchungu sana mamiaya wananchi wametuamini tuje tujadili vitu vya maana hapalakini tunakubaliana akili ndogo itawale akili kubwa. JamesMadison mwaka 1822 alisema, “
      knowledge forever will governignorance”.

      Tumekubali Bunge hili knowledge ndogo i-governknowledge kubwa, tumekubali ignorance i-govern knowledge,tunalipeleka wapi taifa? Akichangia professor hapa hanatofauti na mtu wa darasa la pili. Huwezi kutofautisha mtumwenye masters na mtu wa darasa la pili, where are we takingthis nation? Watu wametupa kura, tunapoteza fedha zaWatanzania, tumekaa hapa tunaacha kujadili mambo yamsingi kwamba tunawezaje kutoka kwenye matope haya? Karne hiyo ya 18 ninayoisema walipoanza kuhoji, walipoanzakudadisi ndipo mapinduzi ya viwanda yalivyojitokeza, no wonder watu wanaosema ni wataalamu wa uchumi wametufikisha hapa tulipo, if that is the case, haya ndiyo masuala ambayo tunapaswa tuyajadili kama taifa.

      Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti inaonyesha hapa, kitabu cha uchumi cha Mheshimiwa Wassira kwamba deni limekuwa shilingi trilioni 20. Ukigawanya ni kama karibu kila Mtanzania anadaiwa shilingi laki nne na themanini na zaidi, hata mimba inadaiwa, ndiyo taifa tulipofika hapa sasa hivi.

      Pianinashangaa katika mpango wake wa bajeti taifa hili kamatunafuatilia na tunakwenda na takwimu, mdogo wangu amezungumza hapa kwamba tunatumia takwimu za nyuma, unawezaje kupanga mambo na takwimu za nyuma?

      Leo hii katika taifa hili 44.2% ni watoto walio chini ya miaka 15 maanayake hawa ni consumers, wanakula zaidi hawa-produce, wakoshuleni na wanao-produce katika nchi hii ni wachache sanakuliko wanaokula ukijumlisha na wazee tuna mzigo mkubwasana. (Makofi)



      Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa utaratibu wabajeti tulio nao hapa,
      there is no way kama tunaweza tukafanya maendeleo, it will take ages kubadilisha taifa hili kama tunaendelea na ngonjera za namna hii na kuruhusu akili ndogo itawale akili kubwa.

      Watu wenye akili kubwawanaweka akili zao mfukoni kwa sababu ya ushabiki wakivyama badala ya kukaa tuka-discuss namna ya kutatuamatatizo yetu.Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama wanao-consume niwengi na wanao-produce ni wachache maana yake nini?

      Tutaendelea kuomba fedha nje na kukopa fedha nje ilituwalishe kwa sababu ni wajibu wa Serikali kusomesha watoto,ni wajibu wa Taifa kuhakikisha watoto wanavaa na kusomashule nzuri lakini mpango mzima wa uchumi uko kimya,hauzungumzi.

      Hapa watu wasomi ambao tupo 350 taifalimetuamini tukae hapa tunatakiwa tujihoji, ndiyo maananimesema problems can not be solved by the same level ofthinking that created them, you guys you are tired!

      Kwasababu hamuwezi kutetea matatizo haya, mmetuwekakwenye mess ninyi wenyewe, ni lazima akili ya juu zaidi iwezekutatua, ni principle hii yaani huwezi kubadilisha that is theprinciple, iwe ni mwanamahesabu na nikiunganisha na insanityis keeping doing the same thing in the same way andexpecting different results and this is what we are doing.



      Tunafanya hayohayo kila mwaka bajeti ya namna hiyohiyo.Ukienda kwenye elimu ni matatizo, ukienda kwenye kilimo nimatatizo, ukienda kwenye afya ni matatizo mwaka baada yamwaka ni matatizo yaleyale,
      why can’t we think a little bitmore?

      We can’t stretch our brain a little bit more kama taifa?(Makofi)



      Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeongea na watu wengineambao ni ma-professor wanasema mara nyingi wakitoaushauri wa kitaalamu, Serikali hamsikilizi na inawezekanawanakaa watu wachache, wanajifungia halafu wanatoamaamuzi kwa sababu wanajua mambo ni yaleyale, business asusual. Ndugu zangu, where are we going? Where are weheading?

      165

      Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zinaonyesha tenakaribu 42% ya watoto wanaozaliwa wanadumaa,


      they can notthink properly, they can not question, they can not ask.

      Ubongo aliotupa Mungu ni lazima uwestretched ili uwezekuchambua kwani tumeumbwa ili tutatue matatizo hapaduniani na siyo tu-create matatizo. Tulipokuja hapa Bungenitunatakiwa tu-solve problems, Bunge hili naliomba liwe Bungela kimapinduzi, tu-change namna ya kufikiri na tu-change


      namna ya kufanya vitu na wengine wanapata taabu hapakwa sababu tumezoea Bunge la chama kimoja.

      Tuna mfumona traditional ya chama kimoja cha zamani, ulimwengu umechange
      halafu tumesimama mahali pamoja hatuendi naulimwengu unavyokwenda. Maendeleo duniani yamekuja kwakuwa na mawazo tofauti yanayopingana, badala yakutuzomea mtusikilize, huu ndiyo wajibu wetu. Mimi kama opposition

      siwezi kusifia bali nakukosoa ili ufanye kazi yako vizuriili na wewe utimize wajibu wako. (Makofi)



      Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa deni kama hili kila mwakalinaongezeka halafu tunakaa hapa tunasema Serikali ya CCMitaendelea kutawala, so what? Ili iweje? Kwa sababu lengo laSerikali kuwepo ni kutatua matatizo ili tuhakikishe tuna-improve maisha ya watu lakini watu kwa sababu wanalinda vyeo, kunammoja amesema Mchungaji, lakini nitasema tu hata kamamtasema au kunitoa nje ya Bunge lakini kama ukweli unakosewa


      I will speak out kwa sababu hiyo ndiyo kazi ya Wachungaji vilevile. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Mbunge mmoja alishaurihapa tuombewe lakini sioni hata theory ya uchumi inayosemakama unataka kutatua matatizo ya uchumi eti ufanyemaombi, ninashangaa huyu amepata wapi hilo?

      As aTheologians hata Paul anasema asiyefanya kazi na asile siyo aombewe, unamnyima chakula lakini yeye anasema watu waombewe. Mimi kama Mchungaji naombea wazinzi, wanaofumaniwa na wake za watu, ndiyo tunawaombea, mimi kama Mchungaji tunawaombea wenye mapepo na hii ni
      principle tuna apply, una-consumers wengi lakini producers wachache maana yake you have to produce more tafuta njiaza ku-produce zaidi, we don’t pray for this, we don’t have topray for this. (Makofi)


      Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu tumekaa hapatumezalisha taifa la watu waoga, wanafiki nawanajipendekezapendekeza, mimi sijaja hapa kwa kupewafedha bali wananchi wa Iringawamenichangua, wananiaminina ninajua wananiunga mkono, wananisikiliza. Sasa sihitajikujipendekeza nitaeleza ukweli as a nation tupo kwenyematatizo. Wehave to address this problems lakini siyo tunakujahapa tunaweka ngonjera maneno ya khanga halafu watumnawapigia makofi, tunalipeleka wapi taifa hili? (Makofi)


      Mheshimiwa Mwenyekiti, ninajisikia uchungu, naomba

      niachie hapo. Ahsante sana. (Makofi)
      Uongo huonekana na kuaminiwa haraka.Ukweli ndio mwisho wa yote!

    2. Miaka 50

    3. #2
      Ndekirhepva's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Location : Lubumbash
      Posts : 304
      Rep Power : 413
      Likes Received
      27
      Likes Given
      77

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      jamani natamani ningepata ile video clip yake ndio ina msisimko zaidi, nisikie na zile" so what"?
      mwenye nayo atuwekee plz plz
      afwe likes this.

    4. #3
      DOMA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2011
      Posts : 630
      Rep Power : 0
      Likes Received
      183
      Likes Given
      1

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Ah imetulia sana hii. Viva msigwa

    5. mob
      #4
      mob's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th December 2009
      Posts : 594
      Rep Power : 599
      Likes Received
      103
      Likes Given
      34

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Ndekirhepva
      jamani natamani ningepata ile video clip yake ndio ina msisimko zaidi, nisikie na zile" so what"?
      mwenye nayo atuwekee plz plz
      Iko youtube mkuu
      Ndekirhepva likes this.

    6. #5
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 11,952
      Rep Power : 24145
      Likes Received
      4668
      Likes Given
      2639

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Ndekirhepva
      jamani natamani ningepata ile video clip yake ndio ina msisimko zaidi, nisikie na zile" so what"?
      mwenye nayo atuwekee plz plz

      Huyu hapa Jogoo:

      Mhe. Msigwa akifyatuka Juni 20, 2012 - YouTube

      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,679
      Rep Power : 0
      Likes Received
      538
      Likes Given
      273

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Mchungaji msigwa(aka mbunge muongozo), aache nidhamu mbovu bungeni, na nitamshitaki kwa wananchi wa jimbo la iringa -By Naibu spika Job Ndugai

    9. #7
      Lyimo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 1,799
      Rep Power : 1526
      Likes Received
      796
      Likes Given
      450

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      "Wisdom is not a product of schooling, but of the lifelong attempt to acquire it"

    10. #8
      Luiz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd May 2011
      Posts : 342
      Rep Power : 473
      Likes Received
      35
      Likes Given
      0

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      kweli huyu jamaa ananondo za kufa mtu.

    11. #9
      mtanzaniahai's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd October 2010
      Posts : 20
      Rep Power : 442
      Likes Received
      4
      Likes Given
      6

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      I appreciate this extreemly good speech; Nadhani tukiwa na wabunge wenye mawazo kama haya tutaifikisha mbali nchi yetu.. Tujifunze yanayoendelea kwenye nchi ya UK ambapo wabunge walim-question CEO and others management staffs of Barclays Bank kwa benki yao ku-misuse LIBOR. Hivi hapa kwetu tukianza kuwahoji watendaji wa taasisi muhimu za umma wanapokosea au wasipowajika profesionally taasisi zao zikavurunda au nchi ikapata hasara; itakuwaje?? cha kuuliza Je Bunge letu halitaanza tena UCHAMA na mipasho??? Je wabunge wetu walio bungeni, bunge ambalo is one of the parliament with a lot of Professors, Doctors na wasomi wengine wengi in developing countries je are you focusing this?

      Maslahi ya nchi yapewe kipaumbele kwanza na siasa later..

      Nawakilisha wadau..
      "Naipenda nchi yangu Tanzania na nitaitetea daima dumu" Amina!

    12. #10
      Barnabas Shadrack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Posts : 2,055
      Rep Power : 810
      Likes Received
      182
      Likes Given
      11

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Sikubahatika kumsikia ila kwa kusoma hapa nimemsikia tena mstari hadi mstari.
      Kila atajaye jina la Yesu, na auache uovu.

    13. #11
      Kigogo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,195
      Rep Power : 2094
      Likes Received
      1232
      Likes Given
      313

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      huyu baba ana akili sana..mweeee.sasa hawa ndo wanatakiwa kuwa mawaziri..sio akina wassira...
      ______________________________ _
      Niko tayari kufa huku nimesimama kuliko kuishi huku nimepiga magoti....

    14. #12
      Saharavoice's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 30th August 2007
      Posts : 2,141
      Rep Power : 1027
      Likes Received
      379
      Likes Given
      478

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Tume ya Katiba
      Mchungaji msigwa(aka mbunge muongozo), aache nidhamu mbovu bungeni, na nitamshitaki kwa wananchi wa jimbo la iringa -By Naibu spika Job Ndugai
      Hizo ndizo ngonjera zenyewe mr. gamba.
      Msome tena Mh. Msigwa pengine itakusaidia kubadilika, maana elimu uliyonayo ni ya kujipendekeza pendekeza tu...
      A conclusion is the place where you got tired of thinking



    15. #13
      Starn's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2011
      Posts : 376
      Rep Power : 524
      Likes Received
      51
      Likes Given
      42

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Kazi aliyotumwa kuifanya hapa duniani imemshinda sasa kajikuta yupo sehemu ambayo hakutakiwa kuwepo. Anaanza kuongea utumbo. ni rahisi binadamu kumsikiliza kiongozi wa dini kuliko viongozi wa nchi, na yeye ameacha kuchunga kondoo kwa kutafuta uongozi wa nchi. Rudi kafanye kazi ya Mungu kaombee wazinzi ili wapate kumrudia Mungu.

    16. #14
      yutong's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 1,352
      Rep Power : 684
      Likes Received
      240
      Likes Given
      97

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      haya wekeni na ya mwigulu nchemba tuisome hapo
      mk83 likes this.
      Sign of Victory - R. Kelly

    17. #15
      Shine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Posts : 9,182
      Rep Power : 2428
      Likes Received
      944
      Likes Given
      377

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Chakushangaza bado kuna wabunge na watu wengine humu jf wanambeza!

    18. #16
      yutong's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 1,352
      Rep Power : 684
      Likes Received
      240
      Likes Given
      97

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Starn
      Kazi aliyotumwa kuifanya hapa duniani imemshinda sasa kajikuta yupo sehemu ambayo hakutakiwa kuwepo. anaanza kuongea utumbo. ni rahisi binadamu kumsikiliza kiongozi wa dini kuliko viongozi wa nchi, na yeye ameacha kuchunga kondoo kwa kutafuta uongozi wa nchi. Rudi kafanye kazi ya Mungu kaombee wazinzi ili wapate kumrudia Mungu.
      Ni baada ya kuona ktk kipindi zaidi ya miaka 40 watu wanasinzia na kulala bungeni na kupitisha bajeti hewa na huku maisha ya watz yakizidi kuporomoka unafikiri afanyaje sasa? Mbona rwakatare hamumsemi? wapeni nafasi kwanza hata hivyo hapa tulipofika ni kwa sababu ya upinzani
      Sign of Victory - R. Kelly

    19. #17
      yutong's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 1,352
      Rep Power : 684
      Likes Received
      240
      Likes Given
      97

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Sisi tuanendelea na maneno yaleyale tu tu ya mbayuwayu, mara waombewe sasa mtu kama huyu anainput gani kwa taifa?
      Sign of Victory - R. Kelly

    20. #18
      MNYISANZU's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,311
      Rep Power : 0
      Likes Received
      592
      Likes Given
      76

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Msigwa = wabunge 200 wa magamba!

    21. #19
      Ibrah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2007
      Location : TZ
      Posts : 2,883
      Rep Power : 1199
      Likes Received
      402
      Likes Given
      46

      Default

      Quote By Starn
      Kazi aliyotumwa kuifanya hapa duniani imemshinda sasa kajikuta yupo sehemu ambayo hakutakiwa kuwepo. anaanza kuongea utumbo. ni rahisi binadamu kumsikiliza kiongozi wa dini kuliko viongozi wa nchi, na yeye ameacha kuchunga kondoo kwa kutafuta uongozi wa nchi. Rudi kafanye kazi ya Mungu kaombee wazinzi ili wapate kumrudia Mungu.
      Sad comment. Aliyemwita ndiye anajua amwemwita kwa kusudi lipi. Biblia inaniambia sote tu watumishi wa Mungu, hata hapo Bungeni kondoo ni wengi.

    22. #20
      Mimibaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Posts : 3,171
      Rep Power : 1533
      Likes Received
      761
      Likes Given
      592

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Starn
      Kazi aliyotumwa kuifanya hapa duniani imemshinda sasa kajikuta yupo sehemu ambayo hakutakiwa kuwepo. Anaanza kuongea utumbo. ni rahisi binadamu kumsikiliza kiongozi wa dini kuliko viongozi wa nchi, na yeye ameacha kuchunga kondoo kwa kutafuta uongozi wa nchi. Rudi kafanye kazi ya Mungu kaombee wazinzi ili wapate kumrudia Mungu.
      Ameitika wito wakuhudumia kondoo (Chama cha Mabwepande) waliopotea. Aliowatumikia katika nyumba za Mungu waqnaendelea vizuri. Imesemwa dawa hupewa mgojwa si mzima
      Ukweli utakuweka huru daima

    Page 1 of 4 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...