Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

    Report Post
    Page 3 of 4 FirstFirst 1234 LastLast
    Results 41 to 60 of 71
    1. #1
      VUTA-NKUVUTE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2011
      Posts : 1,703
      Rep Power : 723
      Likes Received
      892
      Likes Given
      125

      Default Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Ingawa ni maelezo marefu,si vibaya tukajikumbusha mambo haya kutoka kwenye Hansard za MKUTANO WA NANE

      Kikao cha Tano – Tarehe 19 Juni, 2012

      VIDEO:




      MHE. MCH. PETER S. MSIGWA:

      Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi.Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuanza kwa nukuuambayo naipenda sana inayosema:-


      “Insanity is keeping doing the same thing in the same way and expecting different result”

      ambazo zinalikabili taifa lakini kwa bahati mbaya nimeona yaani uwendawazimu nikufanya jambo lilelile kwa njia ileile huku ukitegemea matokeo tofauti.

      Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanafalsafa Albert Einstein anasema:-“Problems can not be solved by the same level of thinking that creates them”. Ndugu zangu, kabla sijawa Mbunge kama alivyosema kaka yangu Mheshimiwa Akunaay, nilikuwa nawa-admire sana Wabunge wanavyokuwa Bungeni, wakivaa suti, nilikuwa naona hapa ni mahali ambapo tuna reason, mahali ambapo tuna question na mahali ambapo tunatoka na solutions


      is the opposite, binafsi najisikia vibaya sana. Kama taifa tupohapa, we are dealing na future ya taifa hili, tunashughulika namamia ya maskini wa Tanzania, tunashughulika na barabarambovu za Watanzania, tunashughulika na hospitali mbovu zaWatanzania, halafu tunakuja hapa tunaongea mambo yakhanga!

      Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma historia, nchi za Ulayakarne ya 14, Marekani na Ulaya na nchi zilizoendelea, zilikuwana fikra na mawazo kama tunavyofanya sasa hivi lakini ilipofikakarne ya 18, inaitwa age of enlightenment, reasoning age, walianza kufikiri, kuhoji na kudadisi. Tunapofika katika karne hiikatika Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania,tunapojadili bajeti maana yake tunazo changamotozinazotukabili kama taifa.

      Badala ya kukaa na kujiuliza kwa ninitupo hapa, tunatokaje hapa tulipo, tunaanza kuongeangonjera na maneno ya uswahiliuswahili yaani unafiki, woga,kujipendekeza na kutokujadili mambo ya msingi.


      (Makofi)


      Mheshimiwa Mwenyekiti, najisikia uchungu sana mamiaya wananchi wametuamini tuje tujadili vitu vya maana hapalakini tunakubaliana akili ndogo itawale akili kubwa. JamesMadison mwaka 1822 alisema, “
      knowledge forever will governignorance”.

      Tumekubali Bunge hili knowledge ndogo i-governknowledge kubwa, tumekubali ignorance i-govern knowledge,tunalipeleka wapi taifa? Akichangia professor hapa hanatofauti na mtu wa darasa la pili. Huwezi kutofautisha mtumwenye masters na mtu wa darasa la pili, where are we takingthis nation? Watu wametupa kura, tunapoteza fedha zaWatanzania, tumekaa hapa tunaacha kujadili mambo yamsingi kwamba tunawezaje kutoka kwenye matope haya? Karne hiyo ya 18 ninayoisema walipoanza kuhoji, walipoanzakudadisi ndipo mapinduzi ya viwanda yalivyojitokeza, no wonder watu wanaosema ni wataalamu wa uchumi wametufikisha hapa tulipo, if that is the case, haya ndiyo masuala ambayo tunapaswa tuyajadili kama taifa.

      Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti inaonyesha hapa, kitabu cha uchumi cha Mheshimiwa Wassira kwamba deni limekuwa shilingi trilioni 20. Ukigawanya ni kama karibu kila Mtanzania anadaiwa shilingi laki nne na themanini na zaidi, hata mimba inadaiwa, ndiyo taifa tulipofika hapa sasa hivi.

      Pianinashangaa katika mpango wake wa bajeti taifa hili kamatunafuatilia na tunakwenda na takwimu, mdogo wangu amezungumza hapa kwamba tunatumia takwimu za nyuma, unawezaje kupanga mambo na takwimu za nyuma?

      Leo hii katika taifa hili 44.2% ni watoto walio chini ya miaka 15 maanayake hawa ni consumers, wanakula zaidi hawa-produce, wakoshuleni na wanao-produce katika nchi hii ni wachache sanakuliko wanaokula ukijumlisha na wazee tuna mzigo mkubwasana. (Makofi)



      Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa utaratibu wabajeti tulio nao hapa,
      there is no way kama tunaweza tukafanya maendeleo, it will take ages kubadilisha taifa hili kama tunaendelea na ngonjera za namna hii na kuruhusu akili ndogo itawale akili kubwa.

      Watu wenye akili kubwawanaweka akili zao mfukoni kwa sababu ya ushabiki wakivyama badala ya kukaa tuka-discuss namna ya kutatuamatatizo yetu.Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama wanao-consume niwengi na wanao-produce ni wachache maana yake nini?

      Tutaendelea kuomba fedha nje na kukopa fedha nje ilituwalishe kwa sababu ni wajibu wa Serikali kusomesha watoto,ni wajibu wa Taifa kuhakikisha watoto wanavaa na kusomashule nzuri lakini mpango mzima wa uchumi uko kimya,hauzungumzi.

      Hapa watu wasomi ambao tupo 350 taifalimetuamini tukae hapa tunatakiwa tujihoji, ndiyo maananimesema problems can not be solved by the same level ofthinking that created them, you guys you are tired!

      Kwasababu hamuwezi kutetea matatizo haya, mmetuwekakwenye mess ninyi wenyewe, ni lazima akili ya juu zaidi iwezekutatua, ni principle hii yaani huwezi kubadilisha that is theprinciple, iwe ni mwanamahesabu na nikiunganisha na insanityis keeping doing the same thing in the same way andexpecting different results and this is what we are doing.



      Tunafanya hayohayo kila mwaka bajeti ya namna hiyohiyo.Ukienda kwenye elimu ni matatizo, ukienda kwenye kilimo nimatatizo, ukienda kwenye afya ni matatizo mwaka baada yamwaka ni matatizo yaleyale,
      why can’t we think a little bitmore?

      We can’t stretch our brain a little bit more kama taifa?(Makofi)



      Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeongea na watu wengineambao ni ma-professor wanasema mara nyingi wakitoaushauri wa kitaalamu, Serikali hamsikilizi na inawezekanawanakaa watu wachache, wanajifungia halafu wanatoamaamuzi kwa sababu wanajua mambo ni yaleyale, business asusual. Ndugu zangu, where are we going? Where are weheading?

      165

      Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zinaonyesha tenakaribu 42% ya watoto wanaozaliwa wanadumaa,


      they can notthink properly, they can not question, they can not ask.

      Ubongo aliotupa Mungu ni lazima uwestretched ili uwezekuchambua kwani tumeumbwa ili tutatue matatizo hapaduniani na siyo tu-create matatizo. Tulipokuja hapa Bungenitunatakiwa tu-solve problems, Bunge hili naliomba liwe Bungela kimapinduzi, tu-change namna ya kufikiri na tu-change


      namna ya kufanya vitu na wengine wanapata taabu hapakwa sababu tumezoea Bunge la chama kimoja.

      Tuna mfumona traditional ya chama kimoja cha zamani, ulimwengu umechange
      halafu tumesimama mahali pamoja hatuendi naulimwengu unavyokwenda. Maendeleo duniani yamekuja kwakuwa na mawazo tofauti yanayopingana, badala yakutuzomea mtusikilize, huu ndiyo wajibu wetu. Mimi kama opposition

      siwezi kusifia bali nakukosoa ili ufanye kazi yako vizuriili na wewe utimize wajibu wako. (Makofi)



      Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa deni kama hili kila mwakalinaongezeka halafu tunakaa hapa tunasema Serikali ya CCMitaendelea kutawala, so what? Ili iweje? Kwa sababu lengo laSerikali kuwepo ni kutatua matatizo ili tuhakikishe tuna-improve maisha ya watu lakini watu kwa sababu wanalinda vyeo, kunammoja amesema Mchungaji, lakini nitasema tu hata kamamtasema au kunitoa nje ya Bunge lakini kama ukweli unakosewa


      I will speak out kwa sababu hiyo ndiyo kazi ya Wachungaji vilevile. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Mbunge mmoja alishaurihapa tuombewe lakini sioni hata theory ya uchumi inayosemakama unataka kutatua matatizo ya uchumi eti ufanyemaombi, ninashangaa huyu amepata wapi hilo?

      As aTheologians hata Paul anasema asiyefanya kazi na asile siyo aombewe, unamnyima chakula lakini yeye anasema watu waombewe. Mimi kama Mchungaji naombea wazinzi, wanaofumaniwa na wake za watu, ndiyo tunawaombea, mimi kama Mchungaji tunawaombea wenye mapepo na hii ni
      principle tuna apply, una-consumers wengi lakini producers wachache maana yake you have to produce more tafuta njiaza ku-produce zaidi, we don’t pray for this, we don’t have topray for this. (Makofi)


      Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu tumekaa hapatumezalisha taifa la watu waoga, wanafiki nawanajipendekezapendekeza, mimi sijaja hapa kwa kupewafedha bali wananchi wa Iringawamenichangua, wananiaminina ninajua wananiunga mkono, wananisikiliza. Sasa sihitajikujipendekeza nitaeleza ukweli as a nation tupo kwenyematatizo. Wehave to address this problems lakini siyo tunakujahapa tunaweka ngonjera maneno ya khanga halafu watumnawapigia makofi, tunalipeleka wapi taifa hili? (Makofi)


      Mheshimiwa Mwenyekiti, ninajisikia uchungu, naomba

      niachie hapo. Ahsante sana. (Makofi)
      Uongo huonekana na kuaminiwa haraka.Ukweli ndio mwisho wa yote!

    2. FemaTV & Radio

    3. #41
      davidie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2011
      Posts : 328
      Rep Power : 450
      Likes Received
      48
      Likes Given
      5

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By starn
      kazi aliyotumwa kuifanya hapa duniani imemshinda sasa kajikuta yupo sehemu ambayo hakutakiwa kuwepo. Anaanza kuongea utumbo. Ni rahisi binadamu kumsikiliza kiongozi wa dini kuliko viongozi wa nchi, na yeye ameacha kuchunga kondoo kwa kutafuta uongozi wa nchi. Rudi kafanye kazi ya mungu kaombee wazinzi ili wapate kumrudia mungu.
      tunawafahamu wote wapinga ukweli ni wa ccm maana inawauma sana kuona mbunge wa upinzani akimwaga nondo za nguvu lakini ukweli unabaki palepale hivi maji marefu au komba au lusinde watasema nini mbele ya jamii zaidi ya mitusi na kejeli kwa watanzania? Jiulize hao viongozi wako wa ccm wanafanya kazi zao walizosomea? Jk mwanajeshi,huyo bilal ni mtaalamu wanyuklia, mizengo mwanasheria,komba muimba kwaya, maji marefu mganga wa kienyeji, huo ni mfano mdogo tu usikurupuke kuongea maneno mbofumbofu.

    4. #42
      eumb's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 116
      Rep Power : 383
      Likes Received
      54
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By Starn
      Kazi aliyotumwa kuifanya hapa duniani imemshinda sasa kajikuta yupo sehemu ambayo hakutakiwa kuwepo. Anaanza kuongea utumbo. ni rahisi binadamu kumsikiliza kiongozi wa dini kuliko viongozi wa nchi, na yeye ameacha kuchunga kondoo kwa kutafuta uongozi wa nchi. Rudi kafanye kazi ya Mungu kaombee wazinzi ili wapate kumrudia Mungu.
      Huyo ndio Mchungaji wa kweli, aliyepambana na kuingia bungeni kwenda kuwaambia wanasiasa ukweli na kuwatetea wanyonge sio kama Mch Mama Lwakatare anayesubiri kusema ndioooooooo!! Acha ujinga!!

    5. #43
      eumb's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 116
      Rep Power : 383
      Likes Received
      54
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By Ramso5
      Kwa kweli inasisimua.sikubahatika kuisikiliza.inasikitisha ujumbe kama huu unapuuzwa na matokeo yake utumbo wa kina mwigulu unajadiliwa zaidi na kuacha mambo ya muhimu kama haya.Nchi hii tunaipeleka wapi?
      Utashangaa wabunge wa CCM walivyowapumbavu wakamchangia na hela eti kuichambua bajeti ya upinzani kumbe wanamchangia hela za kwenda kuharibu ndoa za watu, shame on those ******!!!
      Reply With Quote

    6. #44
      Simbaarobaini7's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th June 2012
      Posts : 19
      Rep Power : 353
      Likes Received
      12
      Likes Given
      0

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Starn
      Kazi aliyotumwa kuifanya hapa duniani imemshinda sasa kajikuta yupo sehemu ambayo hakutakiwa kuwepo. Anaanza kuongea utumbo. ni rahisi binadamu kumsikiliza kiongozi wa dini kuliko viongozi wa nchi, na yeye ameacha kuchunga kondoo kwa kutafuta uongozi wa nchi. Rudi kafanye kazi ya Mungu kaombee wazinzi ili wapate kumrudia Mungu.
      Wewe Starn ni mpumbavu na huna akili kabisaaa. You dont understand what Msigwa is saying. Hata baba yako aliyekuzaa naye hana akili kama wewe. You a stupid pig and it seems you are living like a pig and you will die like donkey. watu wanatoa comment za maana wewe unaongea utumbo umeniudhi sana wewe **** **** nina zako weee.

    7. #45
      Njangula's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 179
      Rep Power : 418
      Likes Received
      16
      Likes Given
      1

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Nimefurahia linkage ya kipindi hiki aliyotoa na age of reasoning and enlightment . Mabadiliko ya kifikra ya enzi hizo ndo yalipelekea mapinduzi ya Ufaransa. Fukuto lililokuwepo Ufaransa enzi hizo ndilo lililopo hapa nchini saa hizi, kweli naogopa. Serikali hii ijirekebishe naionea huruma. Aliyofanyiwa mfalme Louis xvi na mkewe Antonente nahofia viongozi wa nchi kufanyiwa tena na watoto wa walalahoi.

    8. Miaka 50

    9. #46
      Cha Moto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Location : Kijijini
      Posts : 937
      Rep Power : 586
      Likes Received
      131
      Likes Given
      247

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Ukiisoma hii hotuba na au kumsikiliza Msigwa, yaani unaweza TOA machozi .....!!!
      Eeeee Mungu mwenye REHEMA, sisi wana wa TANZANIA tunahitaji watu kama hawa na si kama wale wengine.
      “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri”

    10. #47
      MAN OF CHANGES's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 9th January 2011
      Posts : 177
      Rep Power : 459
      Likes Received
      33
      Likes Given
      19

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      shallom mtumishi wa MUNGU, Mch. P Msigwa.MUNGU AKUPE HEKIMA NA ROHO YA HURUMA ZAIDI KWA WATANZANIA WENZAKO.AMENI

    11. #48
      Bitabo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2011
      Posts : 1,375
      Rep Power : 662
      Likes Received
      447
      Likes Given
      261

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Shine
      Chakushangaza bado kuna wabunge na watu wengine humu jf wanambeza!
      Kafulila alisema kuna baadhi ya viongozi wetu ambao uwezo wao wa kufikiria unaishia kwenye ngazi ya familia. Mkuu nadhani hao wanaombeza Msigwa, ndo type ya wale aliowasema Kafulila
      Uovu wa siku moja, unaondoa wema wa MWAKA MZIMA

    12. #49
      Starn's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2011
      Posts : 376
      Rep Power : 524
      Likes Received
      51
      Likes Given
      42

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Simbaarobaini7
      Wewe Starn ni mpumbavu na huna akili kabisaaa. You dont understand what Msigwa is saying. Hata baba yako aliyekuzaa naye hana akili kama wewe. You a stupid pig and it seems you are living like a pig and you will die like donkey. watu wanatoa comment za maana wewe unaongea utumbo umeniudhi sana wewe **** **** nina zako weee.
      HAhaha hahaha si unaoa jinsi ustaarabu ulivyowashinda walio pale bungeni na nyinyi wote akili zenu ni matope badala ya kutetea ili nipate kukuelewa kwanini unamtete mch, unaanza kuleta matusi. matusi hayato kusaidia kabisa kuwa mstaarabu.
      UPIU likes this.

    13. #50
      keulankubha's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th May 2012
      Posts : 33
      Rep Power : 361
      Likes Received
      3
      Likes Given
      1

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Itashangaza sana mtu akiongea ukweli akaonekana hana akili. kuna watu wenye akili za kipumbavu ambao
      bado wanalaumu Msigwa aliyo yaongea. huu ni wakati wa kutafakali sisi wananchi

    14. #51
      Mwanyasi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th November 2010
      Location : Karibu na wewe
      Posts : 1,053
      Rep Power : 840
      Likes Received
      503
      Likes Given
      986

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By Tume ya Katiba
      Mchungaji msigwa(aka mbunge muongozo), aache nidhamu mbovu bungeni, na nitamshitaki kwa wananchi wa jimbo la iringa -By Naibu spika Job Ndugai
      Kazi yake ni kuwaombea watu kama nyie, alisema Msigwa!
      "Hata siku moja mkaa hauuzwi supermarket" - Mpoki

    15. #52
      Third Eye's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th January 2012
      Posts : 167
      Rep Power : 461
      Likes Received
      26
      Likes Given
      13

      Default

      Quote By Starn
      Kazi aliyotumwa kuifanya hapa duniani imemshinda sasa kajikuta yupo sehemu ambayo hakutakiwa kuwepo. Anaanza kuongea utumbo. ni rahisi binadamu kumsikiliza kiongozi wa dini kuliko viongozi wa nchi, na yeye ameacha kuchunga kondoo kwa kutafuta uongozi wa nchi. Rudi kafanye kazi ya Mungu kaombee wazinzi ili wapate kumrudia Mungu.
      hvi ulishawah kuskia kuna chuo cha ubunge? Mle si kila mtu ana taaluma yake?tukisema kila mtu arud kwenye utaalamu wake bunge litabaki tupu, mbona Ayman al Zawahir ni daktar kitaaluma ila anaongoza Al Qaida kwa sasa? Kwa kifupi umeongea pumba ndugu, kama alivosema msigwa jaribu kufikiri a bit more

    16. #53
      Ndakilawe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2011
      Location : Kumasi
      Posts : 470
      Rep Power : 492
      Likes Received
      53
      Likes Given
      63

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      "so what"

    17. #54
      Ndakilawe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2011
      Location : Kumasi
      Posts : 470
      Rep Power : 492
      Likes Received
      53
      Likes Given
      63

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      "if that the case" kamanda huwa ananikosha sana na hii misemo yake

    18. #55
      Chenge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Posts : 485
      Rep Power : 482
      Likes Received
      183
      Likes Given
      47

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Quote By yutong
      haya wekeni na ya mwigulu nchemba tuisome hapo
      Hii hapa Mkuu



      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa
      nafasi hii ili nizungumze na Watanzania. Awali ya yote, Watanzania wanatakiwa wawe makini
      sana na waigizaji. Ukimpata mwigizaji mzuri, unaweza ukalia, kumbe mwenzio anaigiza na hiki
      ndicho ambacho kimetokea muda mfupi uliopita hapa. (Makofi)
      Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa...
      MWENYEKITI: Mheshimiwa, nakuomba ufute neno uigizaji.
      WABUNGE FULANI: Aaah!
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nafuta kama kuna waigizaji hapa.
      MWENYEKITI: Naomba ufute neno uigizaji.
      90
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nafuta neno uigizaji kama kuna
      waigizaji, lakini maana ya kusema hivi ilikuwa ni hii, tatizo linalojitokeza hapa ni kwamba, bajeti
      imeandaliwa na wataalam, lakini watu badala ya kuuliza wajue undani wa bajeti, aliyesomea
      Sheria za Mambo ya Kichawi na yeye anakuwa mchambuzi wa uchumi, mwenye uzoefu wa
      kuendesha disko anakuwa mchambuzi wa uchumi, unawachanganya Watanzania. Sasa uhalisia
      ndio huu, mimi ni Mchumi wa Daraja la Kwanza na Mwandamizi wa Benki Kuu ya Tanzania, ngojeni
      niwaambie uhalisia wa bajeti. (Makofi)
      Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwenye Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano,
      tunapoongelea 35%, tunajumuisha pamoja na uwekezaji kwenye sekta ya elimu lakini
      tunapozungumzia bajeti hii ya leo, sekta ya elimu iko pembeni, fedha zake zimewekwa pembeni,
      zile za maendeleo zimewekwa pembeni. Watanzania tuulizane, hivi kweli tunaposomesha
      wanafunzi vyuo vikuu, hatuwekezi? Hivi kweli tunapojenga maabara, hatuwekezi? Hivi ni kweli
      tunaposomesha vyuo, tunapoandaa Wataalam wa Ugani, tunapoandaa Madaktari, hatuwekezi?
      Tulisoma wapi? Hiyo Sheria iliyokuwa inatenga investiment on human capital, ilikuwa ni ya miaka
      ya 50 na 60 lakini ukisoma David Roma, ukasoma Waive, ukasoma Mankyu, miaka ya 90, Cop
      Douglas Production Function, inatambua human capital kama investiment. (Makofi)
      Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mpango wa Maendeleo huu tunaojadili, umejumuisha
      investiment on human capital ndio ukapata 35%. Ukienda kwenye bajeti ya mwaka huu,
      ukichukua investiment kwenye elimu, uwekezaji tuliouweka kwenye elimu, bajeti ya maendeleo
      inaenda 39% kwenda 40%. Mmesoma wapi nyie? (Makofi)
      Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, ukiingalia kiutaalamu tu bajeti yenyewe, kiutaalamu
      tu, dependency ratio, utegemezi bajeti imepungua. Ukiweka na ile mikopo kwa sababu mikopo
      nayo ni fedha yetu tutalipa, ukiondoa na ile ya mikopo, utegemezi kwenye bajeti imebaki 6.5%.
      Sifa nyingine ya bajeti, ukienda zile fedha zinazoenda kwenye kulipa mishahara, hamna hata senti
      moja inayoenda kwenye mishahara, mishahara inalipwa na fedha za ndani. (Makofi)
      Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu muone sasa hili nililolisema ambalo mmesema nilifute, hebu
      oneni sasa Bajeti ya Kivuli, wameandika kwamba, kima cha chini kitakuwa 315,000/= hawajui
      wanaolipwa kima cha chini ni wangapi, zidisheni mpate hesabu, mimi nitawaambia mwishoni.
      Halafu chukueni Walimu muwapandishie mishahara mara 50, chukua Madaktari uwapandishie
      mara 50, chukua Manesi uwapandishie mara 50, tafuta jumla yake. Halafu chukua walewale,
      makundi matatu haya, uwapandishie mara moja na nusu, bajeti ya matumizi inaenda zaidi ya hii
      shilingi bilioni tisa waliyoandika wao. Hii waliyoandika kwenye matumizi ya kawaida inazidi,
      ukijumlisha na ile wanayosema kwamba watalipa pensheni kwa wazee, hawajui idadi ya wazee,
      ukijumlisha inakuwa zaidi ya shilingi trilioni 15, mmnatumia bajeti ya wapi? (Makofi)
      Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu wanasema...
      MBUNGE FULANI: Silly thinking.
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi hili nitalirudia tu, halafu
      wanasema kujenga, wanasema kupunguza mzigo wa matumizi ya magari. Mwaka jana
      Mwenyekiti wao, Mheshimiwa Mbowe, alirudisha gari akisema kwamba, kupunguza matumizi,
      akawahadaa Watanzania. Baada ya muda fulani, kumbe alilikataa lile gari kwa sababu
      limechakaa, lilikuwa linatumiwa na Kiongozi aliyepita, baada ya muda fulani kachukua
      kimyakimya gari lingine analitumia. Amelirudisha kimyakimya hajawaambia Watanzania kama
      ameshalichukua. (Makofi)
      Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa watu wanatakiwa kwa kweli Wachamungu wote, mimi
      tangia nizaliwe sijawahi kuona Kambi ya Upinzani yenye pepo mtaka vyeo kama hawa hapa.
      (Makofi)
      Mheshimiwa Mwenyekiti, wanatakiwa waombewe, watalipeleka Taifa pabaya, mimi
      nawaambia Watanzania mkiendelea kushabikia watu ambao haijulikani kama wako normal au
      wanatakiwa wawe Mirembe mtapata kiongozi kama Iddi Amini hapa.
      91
      MBUNGE FULANI: Mwongozo wa Spika!
      MBUNGE FULANI: Mwehu huyu!
      MBUNGE FULANI: Mwongozo! Anatutukana huyu!
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Nimesema niseme na Watanzania, ngojeni niwaambie,
      jambo lingine ambalo wanalolikataa hapa, ngojeni mjue unafiki uko wapi.
      Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine wanalolikataa wanaongelea OC kama vile ni
      dhambi kubwa kwelikweli, angalieni OC kuna nini, OC Serikali imetenga shilingi bilioni 140 kupeleka
      vijana JKT, hivi kweli hiyo ni dhambi kupeleka vijana JKT. (Makofi)
      MBUNGE FULANI: Waambie!
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Serikali imetenga OC kwenda kwenye Tume ikakusanye
      maoni ya Katiba Mpya, mnataka Katiba Mpya hamtaki tuweke bajeti, mnataka Katiba mpya kwa
      kutumia fedha gani.
      MBUNGE FULANI: Mwongozo wa Spika!
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Serikali imetenga fedha kwenye OC kwa ajili ya sensa,
      mnataka sense, hamtaki tuweke bajeti. Serikali imetenga fedha kwenye OC kwa ajili ya fidia za
      watu wanaondolewa kwenye maeneo kupisha miradi ya maendeleo, mnataka zisiwekwe, wale
      watu mtawapatia hela gani mnapowaondoa pale? Serikali imetenga fedha kwenye OC kwa ajili
      ya chakula, wanafunzi, wafungwa, wagonjwa mnataka ziondoke mtawapa nini? (Makofi)
      MBUNGE FULANI: Mwongozo wa Spika!
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Mimi sijawahi kuona Bajeti Kivuli ya aina hii, this is concisely
      and precisely rubbish. (Makofi)
      MWENYEKITI: Samahani kaa chini, Mheshimiwa naomba ukae.
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
      (Kicheko/Makofi/Vigelegele)
      MWENYEKITI: Ngojea Mheshimiwa Mwigulu, order in the House, Mheshimiwa Mwigulu
      naomba ufute neno pepo kwa sababu ni kinyume…
      (Hapa baadhi ya Wabunge walizomea)
      MWENYEKITI: Order in the House.
      MBUNGE FULANI: Mbona walipotaja Mungu mpya hukusema?
      MWENYEKITI: Order in the House.
      MBUNGE FULANI: Afute.
      MWENYEKITI: Order in the House, naomba ufute neno pepo halafu tuendelee.
      MBUNGE FULANI: Mwongozo!
      MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwigulu futa neno pepo tuendelee.
      MBUNGE FULANI: Mwongozo wa Spika!
      92
      MHE. MWIGULU L. M. MADELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa humu ndani nafuta lakini watu
      wa aina hiyo wakaombewe, nafuta neno hilo. (Makofi)
      MBUNGE FULANI: Mwongozo wa Spika.
      MWENYEKITI: Naomba tuendelee.
      MBUNGE FULANI: Kuhusu utaratibu!
      MWENYEKITI: Naomba tuendelee, sasa namwita Mheshimiwa Ahmed Ally Salum na
      Mheshimiwa Amina Clement ajiandae na atafuatia Mheshimiwa Komba. Yupo au hayupo?





      Some people are simply alive because it's illegal to kill them


    19. #56
      piper's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th January 2012
      Posts : 1,593
      Rep Power : 765
      Likes Received
      244
      Likes Given
      39

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Maneno haya aliyosema ni kweli kabisa yatupasa tujithathimini kama taifa, tuangalie tulipotoka, tulipo na tunapoelekea bila kuweka parties ideology mbele, siku zote Tanzania yapaswa kuwa ya kwanza ndo mambo mengine yafuate, viva Mh. Msigwa

    20. #57
      UPIU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2012
      Posts : 503
      Rep Power : 448
      Likes Received
      74
      Likes Given
      8

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Mhe. kwa sasa amebadilika na anajipanga kwenye hoja zake, hususan hoja yake ya leo kuhusu Wizara ya Ujenzi.

    21. #58
      Ntuya's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 18th January 2011
      Posts : 113
      Rep Power : 445
      Likes Received
      14
      Likes Given
      2

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Yap yap ni kweli kabisa haiwezekani akili ndogo iongoze akili kubwa halafu uone maendeleo. Mch Msigwa mwaga nondo, mpaka 2015 lazima watanzania watakuwa wameamka na magamba yote lazima tuyapige chali. Hapana akili ndogo kuongoza akili kubwa mana ni sawa na kipofu kuongoza lazima mtadumbukia wote shimoni. shame on you magambas

    22. #59
      Hofstede's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2007
      Posts : 3,604
      Rep Power : 21341
      Likes Received
      981
      Likes Given
      988

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Kwa wale ambao tuanweza kusikiliza mpate hapa


    23. #60
      makoye2009's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2009
      Posts : 1,416
      Rep Power : 796
      Likes Received
      382
      Likes Given
      266

      Default re: Mch. Msigwa 'afyatuka' Bungeni...

      Mhe. Msigwa(Rev), umenena,umesikika na umeeleweka. Hongera sana.

      Hii ni kuthibitisha kwamba CHADEMA kina wabunge vichwa ambao wako makini sana.Najua wabunge mazezeta wa CCM kina Mwigulu,Bi Mkora Manyanya,Kapteni Komba a.k.a Mkata mauno,Wassira a.k.a Tyson wa usingizi n.k wanaweza wakabeza sana ukweli huu lakini haiwasaidii!

      Kapteni Komba a.k.a. mkato mauno juzi alibwatuka na kusema wabunge wote wa upinzani ni vichaa wakapimwe akili Mirembe, sasa basi swali linakuja kwake Komba na majuha wenzake wa CCM, WA KUPIMWA AKILI HAPA NI NANI KATI YA KOMBA NA MHE.MSIGWA???Ni nani anayeongea points zenye mashiko?

      Jibu mnalo.

    Page 3 of 4 FirstFirst 1234 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...