Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

    Report Post
    Page 5 of 8 FirstFirst ... 34567 ... LastLast
    Results 81 to 100 of 151
    1. #1
      Sigma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2011
      Location : The 2nd House on the Left
      Posts : 4,262
      Rep Power : 1333
      Likes Received
      915
      Likes Given
      615

      Default MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Ni baada ya mabadiliko ya hali ya Ulimboka.

      Wagonjwa waliokwishalipia tu ndo wanaonwa leo.

      Emergence yasimama.

      Source: Mimi niko ground zero

      UPDATE:
      Kutoka gazeti la Mwananchi
      Huduma za matibabu MOI zasimama tena
      Taarifa za kutatanisha kuhusiana na hali ya Dk. Ulimboka, zilisababisha kusitishwa kwa huduma za matibabu katika Kitengo cha Mifupa cha Hospitali ya Taifa Muhimbili (MOI) baada ya madaktari karibuni wote kwenda katika mkutano wa dharura kujadili tukio hilo.

      Habari za kuaminika kutoka MOI, zimethibisha kuwa taarifa za kuzidiwa na hata kuzuka kwa habari nyingine kwamba Dk. Ulimboka alikuwa amefariki, ziliwachanganya kwa kiasi kikubwa madaktari hao, ambao walilazimika kusitisha huduma na kuwapangia wagonjwa tarehe nyingine za kurudi.

      Kutokana na hatua hiyo ya madaktari, wagonjwa waliofika MOI baada ya kusikia kwamba huduma zimerejea, walishindwa kupata tiba badala yake waliandikishwa majina, wakalipia na kupewa tarehe ya kurudi kwa madai kwamba hakuna madaktari wa kuwahudumia.

      Taarifa ya kurejea kwa madaktari hao ilitolewa juzi hospitalini hapo jana na Mwenyekiti wa Bodi ya MOI Balozi Charles Mtalemwa na kusisitiza kwamba hospitali hiyo haiko katika mgomo kwa sasa.

      Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wagonjwa waliokosa tiba, walidai kuchoshwa na usumbufu huo huku wakiwaomba madaktari hao kurejea kazini.

      “Nimekuja hapa tangu saa moja kulikua na foleni; wenzetu waliowahi walionana na madaktari lakini ilipofika saa nne tukaambiwa wote tuliojiandikisha turudi Alhamisi ijayo kwa sababu madaktari wanaenda kwenye kikao,” alisema Abdallah Haji mkazi wa Kimara.

      Kwa upande wake Jenipher Suka alisema inasikitisha kuona hivyo kwa sababu mama yake ambaye ni mgonjwa mkazi wa Dodoma amekuja akitegemea kupata tiba matokeo yake ameambiwa arudi tarehe 10 mwezi huu kwa kuwa hakuna madaktari kwa sasa.

      “Kwa nini serikali isiseme ukweli maana tunahangaika kuja mpaka huku halafu hakuna huduma? Vyombo vya habari vimetangaza kwamba mgomo umesitishwa lakini bado wanatudanganya wananchi kwa faida ya nani?” alilalamika Jenipher.

      Akizungumza kwa sharti la kutochapisha jina lake gazetini mmoja wa maofisa waandamizi wa hospitali hiyo alikiri kutokuwepo kwa huduma baada ya madaktari kupokea taarifa za kuzidiwa kwa Dk. Ulimboka.

      “Unajua huduma zinazoendelea kwa sasa ni kliniki na upasuaji kwa waliowahi lakini hawa madaktari wamechanganyikiwa baada ya daktari mwenzao aliyeongozana na Dk. Ulimboka kuwaeleza kwamba hali ya mgonjwa ni mbaya mno.

      Kukosekana kwa huduma kulichangiwa na madaktari wanafunzi ambao hupokea na kuwahudumia wagonjwa kuwa katika maandalizi ya mitihani ya mwisho wa mwaka itakayoanza Jumatatu ya Julai 9, 2012 hivyo kusababisha huduma utoaji wa huduma kutokuwepo kabisa.
      Daudi Mchambuzi likes this.

    2. RukaaJuu Final

    3. #81
      GeniusBrain's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Location : CHADEMA Makao Makuu
      Posts : 3,822
      Rep Power : 1147
      Likes Received
      188
      Likes Given
      0

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Froida
      Si ndio maana wamemuachia Muhimbili yake hawana shida na mshahara wake akawaleta hao wa Iran waliomhonga suti watibu wananchi
      Well done , ndivyo wanavyotakiwa kufanya na mie nawapongeza kwa hatua yao hiyo, ila mpaka sasa hakuna aliyeandika barua yakuacha kazi , na naomba uwashauri sasa waandike barua ili km kuna mafao yao yaweze kuwa processed , wapewe na waondoke wakatafute maslahi wayatakayo.
      Manyi likes this.

    4. #82
      SHEMGUNGA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2012
      Posts : 332
      Rep Power : 437
      Likes Received
      21
      Likes Given
      0

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Oyoo! walimu lin jama tunasubiri? je wafanyakaz? vp kuhusu wanafunz? duu mkulima mbona kimya? na bado bas ziendao mkoan

    5. MTK
      #83
      MTK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th April 2012
      Posts : 934
      Rep Power : 4495
      Likes Received
      302
      Likes Given
      330

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Kengemumaji
      Kwani afya ya Ulimboka ni muhimu sana kuliko afya za wagonjwa walioko hapo muhimbili?
      Tafakari!! utapata jibu.

    6. #84
      Nyakageni's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,248
      Rep Power : 0
      Likes Received
      769
      Likes Given
      52

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      piganieni haki yenu!

    7. #85
      wakuziba's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 24th June 2012
      Posts : 123
      Rep Power : 581
      Likes Received
      42
      Likes Given
      43

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      mi nilikua muhimbili mida ya asubuhi kujionea mwenyewe kinacho endelea. nimefanya ukaguzi wangu kama raia mwenye haki hiyo. mbona kazi inaendelea kama kawaida. madaktari waliovaa makoti meue nimewaona wengi. nimehoja baadhi ya wagonjwa wanahudumiwa. labda kama mgomo umeanza mida hii!

      jambo lingine ni kwamba wale madaktari ni wasomi. sidhani kama wanaweza kukubali kisha baada ya muda wakagoma tena. tuache kupotosha umma wa watanzania
      Manyi likes this.

    8. Miaka 50

    9. #86
      Mtumpole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2010
      Location : Dreamland
      Posts : 522
      Rep Power : 547
      Likes Received
      93
      Likes Given
      327

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Dumela Mbegu
      Msimamo mbona JK aliisha utoa kwenye hotuba yake ? alisema hawana haja yakugoma na kumsumbua mwajiri kuwaandikia barua nk, wao waache kazi waende kwenye maslahi bora wayatakayo,.....
      Yaani awa madaktari kama wangeitisha mgomo wa kutaka bei za bidhaa na kodi zipunguzwe tungewaelewa ila wamekuwa wabinafsi sana, nadhani sio kosa lao ila kumbukeni hii awamu ya JK imezalisha vichaa wengi nadhani kutokana na ugumu wa maisha.
      Mwenye dhambi hana raha

    10. #87
      mopaozi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2010
      Posts : 2,446
      Rep Power : 758
      Likes Received
      258
      Likes Given
      49

      Default

      Quote By pgasper
      Homa inapanda na kushuka,
      Wananchi sasa ndo watagoma barabarani kwa niaba ya madokta
      Peleka mawazo ya ndumu na viroba huko.WAGOME wananchi ili iweje na wagome nini usitufanye na sisi mapoyoyo kama nyie CDM

    11. #88
      aduwilly's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th March 2009
      Posts : 708
      Rep Power : 661
      Likes Received
      110
      Likes Given
      39

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      7.7 m kwa alietoka direct from school, je mwenye miaka 30 ya uzoefu analipwa shilingi ngapi?

      Tafakari chukua hatua

      say no to boycott, say no to mob psychology

      say yes to humanity, say yes to logical thinking

    12. #89
      yutong's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 1,356
      Rep Power : 685
      Likes Received
      240
      Likes Given
      97

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Dumela Mbegu
      Hayo maslahi wanayoyataka Rais JK aliisha waambia hayawezekani, na akawapa na suluhisho kuwa kama hayawezekani na wao waache kazi, mbona kitu ni rahisi tu na ww kwa nn usitumie muda wako kuwashauri waache kazi tu?
      Mbona yeye na mawaziri wake wamekuwa wakitakiwa kujiuzuru hawajiuzuru/hawataki unadhani kwa nini? hebu tafakari hapo?
      Sign of Victory - R. Kelly

    13. #90
      Froida's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Posts : 3,744
      Rep Power : 1317
      Likes Received
      720
      Likes Given
      147

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Dumela Mbegu
      Well done , ndivyo wanavyotakiwa kufanya na mie nawapongeza kwa hatua yao hiyo, ila mpaka sasa hakuna aliyeandika barua yakuacha kazi , na naomba uwashauri sasa waandike barua ili km kuna mafao yao yaweze kuwa processed , wapewe na waondoke wakatafute maslahi wayatakayo.
      Waandike barua kwa nani wao siwameondoka Huyo Mbuzi wako Kikwete si awafukuze hana jpya amebaki kutumbua mimacho he has failed the nation poor leader

    14. #91
      Lubaluka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2009
      Posts : 468
      Rep Power : 603
      Likes Received
      20
      Likes Given
      19

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Nadhani sio kujiunga tena na mgomo, la hasha mgomo bado unaendele na hukuwai kwisha toka umeanza!!!! na kwa sasa Lugalo imepewa hadhi ya hospitali ya rufaa....haaaa!!! kuokoa jahazi....!!!!
      Always The Silence of Our Friends Hurts more than the Noise of Our Enemy.

    15. #92
      yutong's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 1,356
      Rep Power : 685
      Likes Received
      240
      Likes Given
      97

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Dumela Mbegu
      Hayo maslahi wanayoyataka Rais JK aliisha waambia hayawezekani, na akawapa na suluhisho kuwa kama hayawezekani na wao waache kazi, mbona kitu ni rahisi tu na ww kwa nn usitumie muda wako kuwashauri waache kazi tu?
      msiongee kwa ushabiki angalieni hali halisi hata hao anajeshi wenyewe wanahali mbaya usifikiri kuwa wanaraha sana. Taaluma za watu ziheshimike sasa wanateua hospitali ya Lugalo kuwa ya Rufaa je inawataalamu wenye sifa za Rufaa? wanavifaa? Kama walishindwa kununua vyombo kuweka muhimbili je wataweza kuweka Lugalo? Ama nini maana ya Hospitali kuitwa ya Rufaa?
      Sign of Victory - R. Kelly

    16. #93
      Froida's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Posts : 3,744
      Rep Power : 1317
      Likes Received
      720
      Likes Given
      147

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By yutong
      msiongee kwa ushabiki angalieni hali halisi hata hao anajeshi wenyewe wanahali mbaya usifikiri kuwa wanaraha sana. Taaluma za watu ziheshimike sasa wanateua hospitali ya Lugalo kuwa ya Rufaa je inawataalamu wenye sifa za Rufaa? wanavifaa? Kama walishindwa kununua vyombo kuweka muhimbili je wataweza kuweka Lugalo? Ama nini maana ya Hospitali kuitwa ya Rufaa?
      Juzijuzi hapa wajerumani ndio waliiboresha Lugalo hata grade one haizidi vyumba 20

    17. #94
      Ndakilawe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2011
      Location : Kumasi
      Posts : 470
      Rep Power : 493
      Likes Received
      53
      Likes Given
      63

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      hatari hatari, maisha ya ndugu zetu hatarini....

    18. #95
      BornTown's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2008
      Location : ???
      Posts : 1,482
      Rep Power : 864
      Likes Received
      283
      Likes Given
      104

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By afwe
      MOI hawakujua kuwa kurudi jana kazini ilikuwa ni mbinu ya kukatisha mwendelezo wa kutokuwepo kazini kwa zaidi ya siku tatu kinyume cha sheria mwajiriwa anahesabika kuwa amejifukuza kazi. Wanaanza tena leo na wataaendelea na mgomo mpaka wiki ijayo ambapo watarudi tena siku moja au mbili wanagoma tena
      Sheria ni siku 5 hujaonekana kazini unajifukuzisha kazi walishaifanyia marekebisho na imeshaanza kutumika muda mrefu, kuwa usipoonekana kazini siku 5 mfululuzo umejifukuzisha kazi. So walichofanya MOI n kuonekana kazini then wanarudi tena kwenye A kama wameanza mgomo leo unaesabu siku 5 za kazi wanarudi tena mchezo huo wataucheza weee hadi watakapo pata majibu ya matakwa yao

      Crashwise likes this.
      "DONT BE A WOMAN THAT NEEDS A MAN BE A WOMAN A MAN NEEDS!!!!"

    19. #96
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,688
      Rep Power : 1913
      Likes Received
      1590
      Likes Given
      676

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Dumela Mbegu
      Msimamo mbona JK aliisha utoa kwenye hotuba yake ? alisema hawana haja yakugoma na kumsumbua mwajiri kuwaandikia barua nk, wao waache kazi waende kwenye maslahi bora wayatakayo, shida iko wapi ? na kwa nn usiwashauri wafuate ushauri wa Rais wakuacha kazi?
      Waache kazi kwasababu ya udhaifu wa mtu ambaye ameshindwa kutawala?

    20. #97
      yutong's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 1,356
      Rep Power : 685
      Likes Received
      240
      Likes Given
      97

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Lubaluka
      Nadhani sio kujiunga tena na mgomo, la hasha mgomo bado unaendele na hukuwai kwisha toka umeanza!!!! na kwa sasa Lugalo imepewa hadhi ya hospitali ya rufaa....haaaa!!! kuokoa jahazi....!!!!
      Ni rahisi tu mbona; sekondari nyingi sasa hivi zinaitwa vyuo, shule za msingi nyingi sasa zinaitwa sekondari, vyuo vingi sasa hivi vinaitwa vyuo vikuu ila hawana majengo na hata vifaa vya maabara hii ndo tanzania bhana. Miji mingi sasa hivi inaitwa majiji. Pale Lugalo wameongeza wodi? maaabara ama wameiita tu ya Rufaa? Tatizo letu la kutibu dalili badala ya chanjo
      MANI likes this.
      Sign of Victory - R. Kelly

    21. #98
      jogi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 4,004
      Rep Power : 1216
      Likes Received
      978
      Likes Given
      247

      Default

      Quote By aduwilly
      7.7 m kwa alietoka direct from school, je mwenye miaka 30 ya uzoefu analipwa shilingi ngapi?

      Tafakari chukua hatua

      say no to boycott, say no to mob psychology

      say yes to humanity, say yes to logical thinking
      wewe umesoma na Mwigulu nchemba, nimeambiwa alikuwa anadesa kwako, naamini kwa jinsi mnavyofanana iq.

    22. #99
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,688
      Rep Power : 1913
      Likes Received
      1590
      Likes Given
      676

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By Tume ya Katiba

      Nasisitiza


      Hakuna mgomo muhimbili, after all wagonjwa wa rufaa wanapelekwa LUGALO.
      Vip ule Mgomo wenu wa Sensa bado mmeshikilia ule msimamo wenu? Naona lile zoezi lenu la kujihesabu limekuwa gumu mlikuwa mnafikiri zoezi la sensa ni sawa na kuhesabu vikombe vya kahawa na kashata?

    23. #100
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,122
      Rep Power : 14288
      Likes Received
      4013
      Likes Given
      3271

      Default Re: MOI Wajiunga Tena na MGOMO

      Quote By GateCrasher
      Ni baada ya mabadiliko ya hali ya Ulimboka.
      Wagonjwa waliokwishalipia tu ndo wanaonwa leo.
      Emergence yasimama.
      Source: Mimi niko ground zero
      Mimi na familia yangu tunawaunga mkono, komaeni.....................
      Nobody can give you freedom. Nobody can give you equality or justice or anything. If you're a man, you take it.... Malcolm X Nasubiri 'breaking news... '





    Page 5 of 8 FirstFirst ... 34567 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...