Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Hongera Tundu Lissu: Hoja ya kurudisha Tanganyika!

    Report Post
    Page 2 of 5 FirstFirst 1234 ... LastLast
    Results 21 to 40 of 99
    1. #1
      masopakyindi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 3,728
      Rep Power : 4193
      Likes Received
      1000
      Likes Given
      416

      Default Hongera Tundu Lissu: Hoja ya kurudisha Tanganyika!

      Watanganyika tuwe na misimamo mingine ambayo ni ya kizalendo kama hoja hii ya Tundu Lissu Bungeni.
      Nmeipenda hoja ya Tanganyika.
      Kama Wazanzibari wameweza kujitoa katika muungano na wakawa na sera moja juu ya muungano(iwe CCM au CUF).

      Gazeti la Nipashe leo 5 Julai 2012, (uk. wa 4)lina kichwa cha habari:

      "Lissu ataka Serikali ya Tanganyika irudi

      Na Muhibu Said, Dodoma
      Kambi ya upinzani Bungeni imesema muungano wa Tanganyika na Zanzibar unakabiliwa na hatari kubwa ya kuvunjika kutokana na kitendo cha Zanzibar kujitangazia uhuru, na kwa hiyo ni wakati mwafaka sasa wa kuanzishwa tena kwa Seikali ya Tanganyika."

      Mh Lissu ametoa argument yenye mantiki ya kutosha Bungeni kutetea hoja hii.
      Kama walivyokubaliana kule Zanzibar(CCM na CUF) , kambi ya CCM Bungeni tunawaomba waone mantiki ya hoja ya Mh Lisuu katika hili suala la Muungano na hatma yake.
      Tanganyika inabidi irudishwe kutokana na yaliyotokea Zanzibar , na kuelekea kukubalika na viongozi wote.
      Wabunge wa CCM tafadhali walione hili bila woga.
      Nawasilisha
      "If you don't know where you are going, any road will get you there-nowhere”

    2. FemaTV & Radio

    3. #21
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,606
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2866

      Default Lisu amwaga tindikali bungeni


      1. Ataka Serikali ya Tanganyika irudi
      2. Asema Zanzibar ilijitangazia uhuru


      Lissu awasha moto

      Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imesema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unakabiliwa na hatari kubwa ya kuvunjika kutokana na kitendo cha Zanzibar kujitangazia uhuru, na kwa hiyo ni wakati mwafaka sasa wa kuanzishwa tena kwa Serikali ya Tanganyika. Msemaji wa Kambi kwa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Tundu Lissu, alisema hayo wakati akitoa maoni ya kambi hiyo kuhusu Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) kwa mwaka 2012/2013, bungeni jana.

      Alisema misukosuko ambayo imeukumba Muungano tangu mwaka 1964 hailingani na hatari kubwa inayoukabili hivi sasa. Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alisema jambo hilo waliwahi kumueleza pia Rais Jakaya Kikwete katika waraka wao wa Novemba 27, mwaka jana.

      Hatari ya kuvunjika Muungano

      Alisema hatari ya kuvunjika kwa Muungano inatokana na mabadiliko makubwa ya kikatiba yaliyofanyika katika Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na kutokana pia na Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

      “Hii ni kwa sababu Sheria ya Mabadiliko ya Kumi ya Katiba ya mwaka 2010, inaashiria tafsiri mpya ya Makubaliano ya Muungano na ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambayo inahoji misingi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano kama nchi moja, mamlaka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, na mambo muhimu ya Muungano,” alisema Lissu na kuongeza:

      “Katiba ya sasa ya Zanzibar inaelekea kuwa ni tangazo la uhuru wa Zanzibar zaidi kuliko waraka wa mwafaka kati ya vyama viwili (CUF na CCM) vilivyokuwa mahasimu.”

      Serikali itoe tamko kuhusu Zanzibar kujitangazia uhuru kutoka Muungano

      Lissu ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alichambua vifungu mbalimbali vya Katiba ya sasa ya Zanzibar na kuitaka serikali kutoa tamko bungeni sababu zilizoifanya kuiruhusu Zanzibar kujinyakulia mamlaka juu ya mambo ya ulinzi na usalama ambayo alisema kwa historia yote ya Muungano yamekuwa ni mamlaka pekee ya serikali ya Muungano.

      Alisema Katiba mpya ya Zanzibar siyo tu kwamba imetangaza uhuru wa Zanzibar kwa kuhoji misingi muhimu ya makubaliano ya Muungano, sheria ya Muungano na Katiba ya Muungano, bali pia imehakikisha kwamba uhuru huo utalindwa dhidi ya tishio lolote la serikali ya Muungano.

      Lissu alisema jambo hilo limefanywa kwa kuweka utaratibu wa kuwapo kura ya maoni ya wananchi wa Zanzibar kuhusu mabadiliko ya vifungu kadhaa vya Katiba ya Zanzibar.

      “Kuweka masharti ya kura ya maoni kuhusu mabadiliko ya vifungu vya Katiba mpya ya Zanzibar kuna athari ya moja kwa moja kwa uhai wa Muungano wetu. Hii ni kwa sababu hata vifungu ambavyo tumeonyesha kwamba vinakiuka misingi mikuu ya Makubaliano ya Muungano na Sheria ya Muungano haviwezi kubadilishwa bila ya kura ya maoni ya Wazanzibari,” alisema Lissu.

      Alisema kwa mujibu wa Katiba ya sasa ya Zanzibar, masuala kama Tanzania ni nchi moja au la, majeshi ya ulinzi, polisi nakadhalika, ambayo yamekuwa mambo ya Muungano na Sheria ya Muungano siyo mambo tena ya Muungano hadi hapo wananchi wa Zanzibar watakapoamua kwa kura ya maoni kuyarudisha kwa mamlaka ya Muungano.

      “Huku ni kutangaza uhuru wa Zanzibar bila kutaja neno uhuru. Huku ni kuua Muungano bila kukiri hadharani,” alisema Lissu.

      Kwa mujibu wa Lissu, kwa mtazamo wa Katiba ya Zanzibar, Watanzania hawana tena nchi moja inayozungumzwa katika Katiba ya Muungano, bali wana nchi mbili.

      Alisema kwa mtazamo huo huo, masuala ya ulinzi na usalama, polisi nakadhalika, siyo tena mambo ya Muungano kwa sababu kila nchi ina majeshi yake na kila moja ina Amiri Jeshi Mkuu wake.

      Tanzania kuna Marais wawili

      Pia alisema Watanzania wana marais wawili, wakuu wa nchi wawili na viongozi wa serikali wawili. Alisema mambo yote hayo yanakiuka moja kwa moja makubaliano ya Muungano, Sheria ya Muungano na Katiba ya Muungano.

      Lissu alisema kwa upande mwingine kwa mtazamo wa Katiba ya sasa ya Zanzibar, Rais wa Muungano hana tena mamlaka ya kugawa mikoa na wilaya kwa upande wa Zanzibar na wala hawezi kumshauri tena Rais wa Zanzibar anapoteua wakuu wa mikoa wa Zanzibar.

      Alisema pia Mahakama ya Rufaa ya Tanzania licha ya kuwa moja ya mambo ya Muungano kwa mujibu wa Katiba ya Muungano, haina tena mamlaka ya kusikiliza na kuamua rufaa zinazohusu haki za msingi na uhuru wa mtu binafsi zinazotoka Zanzibar.

      Mtazamo wa Chadema kuhusu hali ya Muungano

      “Kama ilivyo kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba katika mazingira ambayo upande mmoja wa Muungano umejitangazia uhuru, huu ni wakati mwafaka kuanzishwa kwa Serikali ya Tanganyika,” alisema Lissu na kuongeza:

      “Katika mazingira ambayo upande mmoja wa Muungano siyo tu una serikali kamili, Bunge kamili, mahakama kamili, wimbo wa taifa, bendera ya taifa, na sasa una nchi kamili yenye mipaka na eneo la bahari linalojulikana, una majeshi yake na Amiri Jeshi Mkuu wake, huu ni muda mzuri kwa serikali ya Tanganyika kuzaliwa upya.”

      Alisema wanatambua kwamba sheria ya mabadiliko ya Katiba inaielekeza Tume ya Katiba kuongozwa na misingi mikuu ya kitaifa ya kuhifadhi na kudumisha kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano.

      Jukumu la Tume ya Katiba

      Lissu alisema hata hivyo, baada ya kujitokeza kwa wananchi wanaopinga kuendelea kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba, alisema kwamba wale wanaopinga Muungano nao wajitokeze kutoa maoni yao kwa tume.

      Kutokana na hilo, aliitaka serikali kutoa kauli mbele ya Bunge namna gani maoni ya wale wanaotaka alichokiita “kiini macho” cha Muungano kiishe yatashughulikiwa na tume ambayo imepewa jukumu kisheria la kuhifadhi na kukidumisha kiini macho hicho.

      Alihoji ni kipi kitakachoizuia tume hiyo kupuuza maoni ya watu hao kwa hoja kwamba sheria inaielekeza tume kuratibu na kukusanya maoni na kutoa mapendekezo ya kuhifadhi na kudumisha Muungano.

      Awali, Lissu alisema umefika wakati kwa serikali kuweka wazi nyaraka mbalimbali zinazohusu historia ya Muungano na mapato yake ili Watanzania waelewe masuala yote yaliyotokea yanayouhusu.

      Alisema suala hilo ni muhimu kwa kuzingatia kwamba mataifa ya Magharibi kama vile Marekani na Uingereza yalikwishatoa hadharani nyaraka za mashirika yao ya kijasusi pamoja na balozi zao za Tanzania zinazoonyesha jinsi ambavyo serikali za mataifa hayo zilihusika katika kuzaliwa kwa Muungano.
      Mawenzi, Jacobus and GITWA like this.

    4. #22
      majebere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 2,207
      Rep Power : 0
      Likes Received
      322
      Likes Given
      111

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Hii misemo mnaitoa wapi?mi nilijua tayari mtu kamwagiwa tindikali, unajua tena tangu uchaguzi wa igunga,COMMAND inaonekana ni wazee wa kumwagia watu tindikali

    5. #23
      Nyetk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2012
      Posts : 1,018
      Rep Power : 680
      Likes Received
      568
      Likes Given
      581

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Ni halali kabisa bunge kujadili na kuchambua hotuba za upinzani badala ya bajeti za kifisadi maana kwenye hizo za upinzani ndiyo kuna issues za kujadili. NAUNGA MKONO HOJA YA UPINZANI!
      mizambwa likes this.

    6. #24
      Mwanaweja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 3,464
      Rep Power : 1112
      Likes Received
      457
      Likes Given
      936

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      haya hizi lugha mnazotumia mtayaona madhara yake baadaye

    7. #25
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,472
      Rep Power : 19782
      Likes Received
      4299
      Likes Given
      1235

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Lissu jembe

    8. Miaka 50

    9. #26
      MNYISANZU's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,311
      Rep Power : 0
      Likes Received
      592
      Likes Given
      76

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Muungano wetu unapumua kwa kutumia hirizi. Wananchi hatuutaki.
      mizambwa likes this.

    10. #27
      Jile79's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2009
      Posts : 3,760
      Rep Power : 1264
      Likes Received
      210
      Likes Given
      9

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Goo lisu...go cdm.....

    11. #28
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2266
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Ndiyo, habari ndio hiyo, sasa je.
      Simple life is healthier than egoism.

    12. #29
      Lyimo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 1,799
      Rep Power : 1526
      Likes Received
      796
      Likes Given
      450

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Hata Mh.Nahodha aliunga mkono na kusema ni kweli tupu, ila si vizuri kuusema. Kwakweli hapo alinichanganya kidogo.
      "Wisdom is not a product of schooling, but of the lifelong attempt to acquire it"

    13. #30
      Nyakageni's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,248
      Rep Power : 0
      Likes Received
      769
      Likes Given
      52

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      we need our country back!

    14. #31
      Democracy999's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th May 2012
      Posts : 627
      Rep Power : 477
      Likes Received
      111
      Likes Given
      30

      Default Re: Hongera Tundu Lissu: Hoja ya kurudisha Tanganyika!

      Tanzania ya serikali moja ndio suluhisho la kidumu

    15. #32
      Makupa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 2,175
      Rep Power : 810
      Likes Received
      249
      Likes Given
      0

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Lissu.kama anataka Tanganyika atuonyeshe katiba ya Tanganyika

    16. #33
      DOUGLAS SALLU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th November 2009
      Posts : 3,598
      Rep Power : 1285
      Likes Received
      315
      Likes Given
      905

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Hii lugha imenitisha, Pinda alisema liwalo na liwe Dr. Uli akatekwa na kuteswa, sasa uzi huu asije akauona ACP Msangi akaingia kazini na kumwagia tindikali kamanda Lissu, hawa wa Mabwepande akili zao ni kuiba, kutesa na kuua.
      NI UTAAHIRA MKUBWA SANA KUIUNGA MKONO CCM

    17. #34
      Josaa's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 4th July 2012
      Posts : 5
      Rep Power : 348
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      mwanaume wa shoka LISU

    18. #35
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,210
      Rep Power : 3557
      Likes Received
      3059
      Likes Given
      462

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Quote By Candid Scope

      1. Ataka Serikali ya Tanganyika irudi
      2. Asema Zanzibar ilijitangazia uhuru


      Lissu awasha moto

      Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imesema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unakabiliwa na hatari kubwa ya kuvunjika kutokana na kitendo cha Zanzibar kujitangazia uhuru, na kwa hiyo ni wakati mwafaka sasa wa kuanzishwa tena kwa Serikali ya Tanganyika. Msemaji wa Kambi kwa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Tundu Lissu, alisema hayo wakati akitoa maoni ya kambi hiyo kuhusu Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) kwa mwaka 2012/2013, bungeni jana.

      Alisema misukosuko ambayo imeukumba Muungano tangu mwaka 1964 hailingani na hatari kubwa inayoukabili hivi sasa. Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alisema jambo hilo waliwahi kumueleza pia Rais Jakaya Kikwete katika waraka wao wa Novemba 27, mwaka jana.


      Hatari ya kuvunjika Muungano
      Alisema hatari ya kuvunjika kwa Muungano inatokana na mabadiliko makubwa ya kikatiba yaliyofanyika katika Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na kutokana pia na Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

      “Hii ni kwa sababu Sheria ya Mabadiliko ya Kumi ya Katiba ya mwaka 2010, inaashiria tafsiri mpya ya Makubaliano ya Muungano na ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambayo inahoji misingi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano kama nchi moja, mamlaka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, na mambo muhimu ya Muungano,” alisema Lissu na kuongeza:

      “Katiba ya sasa ya Zanzibar inaelekea kuwa ni tangazo la uhuru wa Zanzibar zaidi kuliko waraka wa mwafaka kati ya vyama viwili (CUF na CCM) vilivyokuwa mahasimu.”


      Serikali itoe tamko kuhusu Zanzibar kujitangazia uhuru kutoka Muungano
      Lissu ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alichambua vifungu mbalimbali vya Katiba ya sasa ya Zanzibar na kuitaka serikali kutoa tamko bungeni sababu zilizoifanya kuiruhusu Zanzibar kujinyakulia mamlaka juu ya mambo ya ulinzi na usalama ambayo alisema kwa historia yote ya Muungano yamekuwa ni mamlaka pekee ya serikali ya Muungano.

      Alisema Katiba mpya ya Zanzibar siyo tu kwamba imetangaza uhuru wa Zanzibar kwa kuhoji misingi muhimu ya makubaliano ya Muungano, sheria ya Muungano na Katiba ya Muungano, bali pia imehakikisha kwamba uhuru huo utalindwa dhidi ya tishio lolote la serikali ya Muungano.

      Lissu alisema jambo hilo limefanywa kwa kuweka utaratibu wa kuwapo kura ya maoni ya wananchi wa Zanzibar kuhusu mabadiliko ya vifungu kadhaa vya Katiba ya Zanzibar.

      “Kuweka masharti ya kura ya maoni kuhusu mabadiliko ya vifungu vya Katiba mpya ya Zanzibar kuna athari ya moja kwa moja kwa uhai wa Muungano wetu. Hii ni kwa sababu hata vifungu ambavyo tumeonyesha kwamba vinakiuka misingi mikuu ya Makubaliano ya Muungano na Sheria ya Muungano haviwezi kubadilishwa bila ya kura ya maoni ya Wazanzibari,” alisema Lissu.

      Alisema kwa mujibu wa Katiba ya sasa ya Zanzibar, masuala kama Tanzania ni nchi moja au la, majeshi ya ulinzi, polisi nakadhalika, ambayo yamekuwa mambo ya Muungano na Sheria ya Muungano siyo mambo tena ya Muungano hadi hapo wananchi wa Zanzibar watakapoamua kwa kura ya maoni kuyarudisha kwa mamlaka ya Muungano.

      “Huku ni kutangaza uhuru wa Zanzibar bila kutaja neno uhuru. Huku ni kuua Muungano bila kukiri hadharani,” alisema Lissu.

      Kwa mujibu wa Lissu, kwa mtazamo wa Katiba ya Zanzibar, Watanzania hawana tena nchi moja inayozungumzwa katika Katiba ya Muungano, bali wana nchi mbili.

      Alisema kwa mtazamo huo huo, masuala ya ulinzi na usalama, polisi nakadhalika, siyo tena mambo ya Muungano kwa sababu kila nchi ina majeshi yake na kila moja ina Amiri Jeshi Mkuu wake.


      Tanzania kuna Marais wawili
      Pia alisema Watanzania wana marais wawili, wakuu wa nchi wawili na viongozi wa serikali wawili. Alisema mambo yote hayo yanakiuka moja kwa moja makubaliano ya Muungano, Sheria ya Muungano na Katiba ya Muungano.

      Lissu alisema kwa upande mwingine kwa mtazamo wa Katiba ya sasa ya Zanzibar, Rais wa Muungano hana tena mamlaka ya kugawa mikoa na wilaya kwa upande wa Zanzibar na wala hawezi kumshauri tena Rais wa Zanzibar anapoteua wakuu wa mikoa wa Zanzibar.

      Alisema pia Mahakama ya Rufaa ya Tanzania licha ya kuwa moja ya mambo ya Muungano kwa mujibu wa Katiba ya Muungano, haina tena mamlaka ya kusikiliza na kuamua rufaa zinazohusu haki za msingi na uhuru wa mtu binafsi zinazotoka Zanzibar.


      Mtazamo wa Chadema kuhusu hali ya Muungano
      “Kama ilivyo kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba katika mazingira ambayo upande mmoja wa Muungano umejitangazia uhuru, huu ni wakati mwafaka kuanzishwa kwa Serikali ya Tanganyika,” alisema Lissu na kuongeza:

      “Katika mazingira ambayo upande mmoja wa Muungano siyo tu una serikali kamili, Bunge kamili, mahakama kamili, wimbo wa taifa, bendera ya taifa, na sasa una nchi kamili yenye mipaka na eneo la bahari linalojulikana, una majeshi yake na Amiri Jeshi Mkuu wake, huu ni muda mzuri kwa serikali ya Tanganyika kuzaliwa upya.”

      Alisema wanatambua kwamba sheria ya mabadiliko ya Katiba inaielekeza Tume ya Katiba kuongozwa na misingi mikuu ya kitaifa ya kuhifadhi na kudumisha kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano.


      Jukumu la Tume ya Katiba
      Lissu alisema hata hivyo, baada ya kujitokeza kwa wananchi wanaopinga kuendelea kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba, alisema kwamba wale wanaopinga Muungano nao wajitokeze kutoa maoni yao kwa tume.

      Kutokana na hilo, aliitaka serikali kutoa kauli mbele ya Bunge namna gani maoni ya wale wanaotaka alichokiita “kiini macho” cha Muungano kiishe yatashughulikiwa na tume ambayo imepewa jukumu kisheria la kuhifadhi na kukidumisha kiini macho hicho.

      Alihoji ni kipi kitakachoizuia tume hiyo kupuuza maoni ya watu hao kwa hoja kwamba sheria inaielekeza tume kuratibu na kukusanya maoni na kutoa mapendekezo ya kuhifadhi na kudumisha Muungano.

      Awali, Lissu alisema umefika wakati kwa serikali kuweka wazi nyaraka mbalimbali zinazohusu historia ya Muungano na mapato yake ili Watanzania waelewe masuala yote yaliyotokea yanayouhusu.

      Alisema suala hilo ni muhimu kwa kuzingatia kwamba mataifa ya Magharibi kama vile Marekani na Uingereza yalikwishatoa hadharani nyaraka za mashirika yao ya kijasusi pamoja na balozi zao za Tanzania zinazoonyesha jinsi ambavyo serikali za mataifa hayo zilihusika katika kuzaliwa kwa Muungano.

      Mimi niliweka hotuba Nzima ya Mh. Lissu naona imeondolewa, hii inaleta HOJA inaleta mtafakuru
      Mkandara likes this.

    19. #36
      mnduoeye's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Posts : 111
      Rep Power : 369
      Likes Received
      36
      Likes Given
      0

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Wana JF wakati mwingine najiuliza hivi viongozi wanapojaribu kukwepa ukweli wanafanya hivyo kwa maslahi ya nani?
      Zanzibar tayari wameshaamua kujitenga wameshakuwa na katiba yao na bado tunaendelea kuzungumzia muungano ni kujidanganya.Hebu tufikirie hatua mpya ya kuwa na serikali ya tanganyika, ya zanzibar na mwisho shirikisho kama inahitajika.
      Nawaambieni wana JF.Mimi si mtabiri wala mpiga ramli lakini yakini nawaambia itawagharimu sana Wazanzibar kwa sababu hata mafuta wanayoyazungumzia kitaalamu yahitaji takribani miaka 6 kama yapo ndo waanze kuyaona wasifikiri ni kitu cha kusema kipo kikawepo.

    20. #37
      mizambwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2008
      Posts : 1,438
      Rep Power : 975
      Likes Received
      367
      Likes Given
      1808

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Quote By Makupa
      Lissu.kama anataka Tanganyika atuonyeshe katiba ya Tanganyika
      Sasa wewe unnataka akuonyeshe katiba ipi!!!!

      Bunge liamue kisha tutengane ndipo upande wa Tanganyika watengeneze Katiba yao, kama walivyotengeneza WaZNZ.


      KIYAMA YA CCM IMEFIKA!!!!!!!!



      MIZAMBWA
      NABII MTARAJIWA!!!
      SASA NIMEAMINI KUWA TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA!!!!, TUANDAE KABURI LA KUIZIKA MWAKA 2015

    21. #38
      MKUNGA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th December 2009
      Location : SIRTE
      Posts : 425
      Rep Power : 565
      Likes Received
      54
      Likes Given
      21

      Default Re: Lisu amwaga tindikali bungeni

      Ka hili ka kuuchukia Muungano waziwazi ni moja ya mambo yanayowapunguzia credit...Watanzania wanawaona na kuwasikia mrengo wenu wa chokochoko kuanzia ile ya nchi haitatawalika, kuchochea social unrest etc.
      Hakika wanaokula mali ya mayatima kwa dhuluma, bila shaka wanakula moto matumboni mwao na wataungua katika huo moto.
      The Holy Quran 4:10

    22. #39
      Barnabas Shadrack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Posts : 2,055
      Rep Power : 810
      Likes Received
      182
      Likes Given
      11

      Default

      Quote By ruttashobolwa
      Lissu jembe
      Siku Lisu na wenzake wakipata madaraka ya kuongoza nchi, ndipo itakapofahamika kama ni jembe, koleo au nirungu.
      WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.

    23. #40
      Angel Msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Posts : 6,266
      Rep Power : 1826
      Likes Received
      1397
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By MNYISANZU
      Muungano wetu unapumua kwa kutumia hirizi. Wananchi hatuutaki.
      muungano uko icu

    Page 2 of 5 FirstFirst 1234 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...