Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka; Yadaiwa yupo Ujerumani na si Afrika Kusini

    Report Post
    Page 1 of 6 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 106
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,189
      Rep Power : 3552
      Likes Received
      3051
      Likes Given
      461

      Default Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka; Yadaiwa yupo Ujerumani na si Afrika Kusini

      • TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI,
      • RAFIKI YAKE ATOA USHUHUDA MPYA WA JINSI ALIVYOTEKWA


      Waandishi wetu | Mwananchi | 04 July 2012

      WAKATI ikielezwa kwamba Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Steven Ulimboka anatibiwa Afrika Kusini, kuna taarifa kwamba amelazwa katika hospitali moja ya huko Ujerumani.

      Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa Dk Ulimboka alipelekwa Afrika Kusini lakini alikaa kwa muda mfupi tu kabla ya kupelekwa Ujerumani anakoendelea na matibabu yake sasa.

      Awali, jopo la madaktari waliokuwa wanamtibu Dk Ulimboka hapa nchini lilieleza kuwa baada ya hali yake kuendelea kuwa mbaya katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, waliamua kumpeleka Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.

      “Ni kweli alikwenda kwanza Afrika Kusini, lakini hapo alipita tu. Ndege ilitua na akaunganisha ndege nyingine kwenda Ujerumani,” kilisema chanzo kimoja cha habari.

      Hata hivyo wakati chanzo hicho kikieleza hivyo, mmoja wa wanafamilia yake, alisema: “Sisi katika level (ngazi) ya familia tunajua yuko Afrika Kusini lakini hii haiwazuii madaktari kumhamishia kwenye hospitali nyingine wanayoona inafaa.”

      Mwanafamilia huyo ambaye hakutaka kutajwa gazetini, alisema suala la Dk Ulimboka kuhamishiwa Ujerumani si la ajabu kwani anachotafuta ni matibabu ya uhakika.

      Alipoulizwa kuhusu habari hizo, Kiongozi wa Jopo la Madaktari waliokuwa wakimtibu, Profesa Joseph Kahamba alisema: Mimi ndiyo kwanza nasikia, lakini kwa nature (aina) ya tukio lake, si vyema ikaanikwa amepelekwa wapi. Pia si vizuri ikaelezwa yuko wapi ingawa tayari watu wanajua yuko Afrika Kusini.”

      “Kama kiongozi wa jopo la madaktari wanaomtibu Dk Ulimboka ninajua kwamba yuko Afrika Kusini ingawa hata hiyo taarifa tusingependa watu waijue kwa jinsi tukio lilivyokuwa.”

      Mmoja wa madaktari ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alipoulizwa juu ya suala hilo alipinga na kusema; “Habari za aina hiyo mtakuwa mnazipata nyingi, najua mtaandika, ndiyo maana mnaandika madaktari Muhimbili wanafanya kazi wakati si kweli”.

      Alisisitiza kuwa Dk Ulimboka yupo Afrika Kusini anakopatiwa matibabu na kusisitiza kuwa habari alizokuwa nazo tangu juzi jioni ni kwamba anaendelea vizuri.

      Katibu wa Chama cha Taifa cha Madaktari (MAT), Dk Rodrick Kabangila alipoulizwa juu ya hali ya Dk Ulimboka alisema kwa mujibu wa taarifa za juzi jioni alikuwa anaendelea vizuri.

      Alipoulizwa juu ya taarifa za kupelekwa Ujerumani aliguna kisha akasema: “Naomba ieleweke kuwa yupo Afrika ya Kusini kwa matibabu.

      Rafiki asimulia mkasa

      Rafiki wa karibu wa Dk Ulimboka aliyekuwa naye wakati mkasa wa kutekwa ukitokea, Dk. Deogratius Michael ameelezea tukio zima lilivyotokea na kusema ulikuwa wa kitaalamu na ulifanywa na watu wenye ujuzi na mambo hayo.

      Dk Deogratius alisema jana kwamba siku ya tukio walikuwa wametokea kwenye msiba wa ndugu wa mwalimu wao Profesa Yongolo na baada ya msiba walikwenda Viwanja vya Leaders saa moja usiku kuangalia taarifa ya habari na mambo mengine.

      Huko walikutana na madaktari wengine na ilipofika saa 4:00 usiku, Dk Ulimboka aliwaambia kwamba kuna jamaa alikuwa akimtafuta hivyo angependa kwenda kukutana naye.

      “Tukamwuliza anamtafutia nini? Akatueleza kuwa kwa siku tatu huyo jamaa anamtafuta. Wenzangu wakasema asiende mwenyewe na mimi ndiyo nikamsindikiza. Mara ya kwanza huyo jamaa alisema anaitwa Abeid na alisema yuko Sterio, tukaenda huko hatukumkuta tukaenda Hugo hatukumkuta lakini baadaye tukakutana naye maeneo ya Barabara ya Tunis karibu na Ofisi za Ultimate Security.”

      Dk Deogratius alisema wakati wakiendelea na mazungumzo, Abeid alikuwa akitaka kujua nini kinachotakiwa ili kutatua mgogoro uliopo wa madaktari.

      “Wakati tunamalizia mazungumzo nilikwenda msalani, niliporudi Abeid alikuwa akizungumza na simu kila wakati, tuliendelea na mazungumzo hadi tukamaliza na kuanza kuagana,” alisema.

      Alisema wakati wakiagana bado walikuwa wamekaa katika viti pamoja na Abeid... “Ghafla kuna watu walifika na kusema kuwa wanamtaka Dk Ulimboka. Walimchukua na kwenda naye katika gari. Walikuwa watano, walikuwa ‘giant’ (miili mikubwa) na ‘very skilled’ ( wenye uzoefu) wakamchukua Dk Ulimboka wakaenda naye kwenye gari,” alisema Dk Deogratius.

      Alisema wakati huo Abeid alikuwa anakimbia hivyo akamkimbilia ili ampe namba yake ya simu ambayo ingemsaidia kwa mawasiliano.

      “Alinipa namba yake nikampigia muda huohuo lakini nilipokuja kumpigia tena sikumpata na mpaka leo hapatikani,” alisema.

      Alisema baada ya tukio hilo alimpigia mke wa Dk Ulimboka na kumweleza na pia alipiga simu polisi kuwaeleza.

      “Nilikwenda polisi kutoa maelezo na nikawapa namba zangu za simu zote ili wanipigie kama watapata chochote, lakini mtu wa kwanza kunipigia asubuhi (kesho yake) alikuwa Juma Mgaza (aliyemwokota Dk Ulimboka) ambaye alinieleza kuwa kuna rafiki yangu amempa hiyo namba na kwamba yuko hoi amepigwa.”

      Alisema baada ya kupata simu hiyo aliwasiliana na watetezi wa haki za binadamu ambao walimtaka waende pamoja na kwamba walipokuwa njiani kuelekea Kituo cha Polisi Bunju alipigiwa simu na polisi wa kituo hicho.

      Kutokana na hali hiyo aliomba iundwe tume huru ikijumuisha wanasheria, madaktari na watu wengine ili ukweli ujulikane.

      Upelelezi wa Polisi
      Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova amesema jopo la upelelezi aliloteua hivi karibuni kushughulikia tukio zima la kutekwa kwa Dk Ulimboka litaendelea na kazi yake hadi mwisho na hatasikiliza kelele za wanaodai kutokuwa na imani nalo.

      Alisema madai yanayotolewa na watu mbalimbali akiwemo Dk Ulimboka mwenyewe kuwa hana imani na jopo hilo hazitabadili chochote kwani kinachofanyika hivi sasa ni kazi ya kawaida ya upelelezi ya jeshi hilo... “Hao wanaosema hawana imani na jopo hilo hawana hoja isipokuwa waliache jeshi la polisi lifanye kazi yake.

      Kiongozi huyo wa mgomo wa madaktari alitekwa na kisha kujeruhiwa vibaya na baadaye kutelekezwa katika Msitu wa Pande.

      Habari hii imeandikwa na Geofrey Nyang’oro, Boniface Meena na Joseph Zablon

    2. Miaka 50

    3. #2
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      So what?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    4. #3
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,189
      Rep Power : 3552
      Likes Received
      3051
      Likes Given
      461

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Ni Vizuri kweli hata Ubalozi wa Afrika Kusini hawajuia aliko... Rais Mwenyewe hajui

    5. #4
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,189
      Rep Power : 3552
      Likes Received
      3051
      Likes Given
      461

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Quote By zomba
      So what?
      Don't be a hater !!!

    6. #5
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,970
      Rep Power : 2977
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By zomba
      So what?
      Unavyohoji utafikiri ni mtoto mdogo,just imagine wewe ndo mkubwa humu jamvini,na jinsi unavojitaidi kujifanya mtoto sijui kama inaleta maana.
      Utapakatwa we leta uzuri.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Quote By nngu007
      Don't be a hater !!!
      Germany or South Africa, what does that help us? he was sent out of the country by his beloved to try and rescue him from death? or is it his health?

      Does he realize now that many were in his position and could not afford to be even transferred to other hospitals?

      I don't give a damn wherever he is. What does that help us?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    9. #7
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,970
      Rep Power : 2977
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By zomba
      Germany or South Africa, what does that help us? he was sent out of the country by his beloved to try and rescue him from death? or is it his health?

      Does he realize now that many were in his position and could not afford to be even transferred to other hospitals?

      I don't give a damn wherever he is. What does that help us?
      kila linapokuja swala la Dr Uli kwa nini unapata msogo wa mawazo?
      Mkono and Mtumishi Wetu like this.

    10. #8
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Quote By Imany John
      Unavyohoji utafikiri ni mtoto mdogo,just imagine wewe ndo mkubwa humu jamvini,na jinsi unavojitaidi kujifanya mtoto sijui kama inaleta maana.
      Utapakatwa we leta uzuri.
      Wewe unajibu kikubwa inatosha. Si mimi, si wewe, si Mtanzania mwingine yeyote, awepo Afrika Kusini, Ujerumani au Uchina inatusaidia nini?

      Mimi nasema sasa ataelewa kuwa uchochezi wake umemfanya ahisi (kama anazo hizo hisia) ni vipi mtu akikosa afya kwa kuumwa anavyokuwa.

      Katika madai 12 aliyoyabuni, 11 ni ya kipato kwa madaktari, sasa hicho kipato kimpe uzima.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    11. #9
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Quote By Imany John
      kila linapokuja swala la Dr Uli kwa nini unapata msogo wa mawazo?
      Tena sana tu, ametuumizia na kutuulia wagonjwa wetu wengi kwa maslahi yake binafsi, halafu eti alikuwa anakwenda kilabu cha pombe kutatua matatizo ya wagonjwa? Huyo alikuwa anakwenda kupokea rushwa. Halafu bado nimhurumie?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    12. #10
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,970
      Rep Power : 2977
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By zomba
      Tena sana tu, ametuumizia na kutuulia wagonjwa wetu wengi kwa maslahi yake binafsi, halafu eti alikuwa anakwenda kilabu cha pombe kutatua matatizo ya wagonjwa? Huyo alikuwa anakwenda kupokea rushwa. Halafu bado nimhurumie?
      Kakuumizia mgonjwa yupi? Acha kujipendekeza wewe.

    13. #11
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,970
      Rep Power : 2977
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By zomba
      Wewe unajibu kikubwa inatosha. Si mimi, si wewe, si Mtanzania mwingine yeyote, awepo Afrika Kusini, Ujerumani au Uchina inatusaidia nini?

      Mimi nasema sasa ataelewa kuwa uchochezi wake umemfanya ahisi (kama anazo hizo hisia) ni vipi mtu akikosa afya kwa kuumwa anavyokuwa.

      Katika madai 12 aliyoyabuni, 11 ni ya kipato kwa madaktari, sasa hicho kipato kimpe uzima.
      Unadhihirisha usiku waleo ulinyimwa unyumba,kwanini usipeleke hasira kwa mkeo? Au Dr Uli alikuumizia na mkeo?
      Sikonge and Nyamizi like this.

    14. #12
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Quote By Imany John
      Kakuumizia mgonjwa yupi? Acha kujipendekeza wewe.
      Siyo mmoja, ni wote waliokosa huduma kwa mgomo uliochochewa na huyu mwenzenu anaeonja na kujuwa ni nini kuumwa saa hizi.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    15. #13
      dada jane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th December 2011
      Posts : 503
      Rep Power : 476
      Likes Received
      92
      Likes Given
      0

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Inaelekea toka saga la dr Uli lianze Zoba halali kabisa.

    16. #14
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,970
      Rep Power : 2977
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By zomba
      Siyo mmoja, ni wote waliokosa huduma kwa mgomo uliochochewa na huyu mwenzenu anaeonja na kujuwa ni nini kuumwa saa hizi.
      yamkini hujui aliyekutuma ameshapotea,nawewe umegundua umeshapotezwa na ndio maana unajitaidi kutafuta wakuwapoteza.
      Jaribu tena baadae

    17. #15
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Quote By Imany John
      Unadhihirisha usiku waleo ulinyimwa unyumba,kwanini usipeleke hasira kwa mkeo? Au Dr Uli alikuumizia na mkeo?
      Amewaumiza si wake za watu tu, watoto, wazee, vijana. Kwa ufupi wote waliokosa matibabu kwa uchochezi wake wa kujitafutia umaarufu na tamaa zake binafsi. Sasa hivi anajuwa kuumwa ni nini.

      Matusi hayasaidii, mnajulikana mnapokuwa hamna hoja mnaanza kutukana.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    18. #16
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,970
      Rep Power : 2977
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By dada jane
      inaelekea toka saga la dr uli lianze zoba halali kabisa.
      alale apate hasara.

    19. #17
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,669
      Rep Power : 1908
      Likes Received
      1563
      Likes Given
      676

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Quote By zomba
      So what?
      Kama unaona hii thread haikuhusu hamna haja ya kuifungua na kuanza kuweka viingereza vyako vya ngumbaro mkuu tunaheshimiana usilete chuki zako na ulimboka hapa jamvini utaanza kuwa pm mods sasa hivi kuwa umetukanwa

    20. #18
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Utata watanda nchi anakotibiwa Ulimboka;TAARIFA MPYA ZAELEZA YUKO UJERUMANI SI AFRIKA KUSINI

      Quote By Imany John
      yamkini hujui aliyekutuma ameshapotea,nawewe umegundua umeshapotezwa na ndio maana unajitaidi kutafuta wakuwapoteza.
      Jaribu tena baadae
      Aliyepotea ni huyo asiyejijuwa saa hizi yuko hali gani wala wapi. Na mliyepotea zaidi ni nyinyi mnaoshadidia wagonjwa wazidi kukosa matibabu na mnaodhani kuwa alikuwa akifanya jambo la maana.

      Mnashindwa kufikiri kitu kidogo tu, ni nini kilimpeleka usiku klabu ya ulevi kwa kuitwa "tuyamalize"? Fikiri na uwe mkweli wa nafsi yako.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    21. #19
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,970
      Rep Power : 2977
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By zomba
      Amewaumiza si wake za watu tu, watoto, wazee, vijana. Kwa ufupi wote waliokosa matibabu kwa uchochezi wake wa kujitafutia umaarufu na tamaa zake binafsi. Sasa hivi anajuwa kuumwa ni nini.

      Matusi hayasaidii, mnajulikana mnapokuwa hamna hoja mnaanza kutukana.
      Bado hoja yako ni dhaifu,daktari gani asiyejua maana ya kuumwa? Wanatibu kitu gani kama sio hayo maradhi?

      Kweli Dr Uli kakuumizia,pole sana.

    22. #20
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,970
      Rep Power : 2977
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By zomba
      Aliyepotea ni huyo asiyejijuwa saa hizi yuko hali gani wala wapi. Na mliyepotea zaidi ni nyinyi mnaoshadidia wagonjwa wazidi kukosa matibabu na mnaodhani kuwa alikuwa akifanya jambo la maana.

      Mnashindwa kufikiri kitu kidogo tu, ni nini kilimpeleka usiku klabu ya ulevi kwa kuitwa "tuyamalize"? Fikiri na uwe mkweli wa nafsi yako.
      Kweli Dr Uli kakuumizia.

    Page 1 of 6 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...