Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 59
    1. #1
      Nyetk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2012
      Posts : 1,011
      Rep Power : 678
      Likes Received
      562
      Likes Given
      576

      Default Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      UJUMBE WA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA KWA WAAMINI WAKATOLIKI NA WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA

      Sisi Maaskofu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania tumekutana katika Mkutano wetu Mkuu wa 65 wa kawaida tangu tarehe 23 – 30 Juni 2012 uliowajumuisha Wakuu wa Mashirika ya Kitawa, wakuu wa Idara, Tume na Taasisi za Baraza pamoja na wawakilishi Walei. Lengo la Mkutano huu lilikuwa kutathmini shughuli na kazi zetu za Kichungaji na za huduma za jamii kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita (2009-2012) na vile vile kupanga mikakati ya kuboresha shughuli hizo za Kichungaji na za huduma za Jamii katika Nyanja za Afya, Elimu, Maji, misaada kwa wasiojiweza, utetezi na ushawishi, kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo (2012-2015).

      Pamoja na kufanya tathmini ya kina ya utendaji wa Baraza letu katika kipindi hicho kilichopita, na kupanga mipango kabambe kwa ajili ya utendaji wa Baraza kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo, Mkutano wetu Mkuu umekuwa fursa ya kujadiliana na kushirikishana baadhi ya matukio/mambo ambayo, kwa hakika, yameitikisa jamii yetu ya Watanzania na kuidhalilisha mbele ya Jumuiya ya kimataifa.

      Kwa namna ya pekee kabisa, tumetafakari juu ya vuguru za kidini za hivi karibuni zilizotokea katika Visiwa vya Zanzibar kuanzia 26-28 Mei, 2012 na kupelekea kuchomwa moto kwa baadhi ya Makanisa Visiwani humo pamoja na uharibifu mkubwa wa mali na uvunjifu wa amani. Bila kupenda kurudia matamko ya Wadau mbali mbali waliyoyatoa katika nyakati tofauti kulaani bila kusita hali hiyo ya kutisha na kusikitisha iliyojitokeza Visiwani humo, tunaunga mkono kwa nguvu zote kauli na jitihada za wale wote wenye mapenzi mema walioguswa na vitendo hivyo na hivyo kuvilaani. Tunatoa pole na kueleza mshikamano wetu wa kindugu kwa wale wote walioathirika kwa namna moja au nyingine na vitendo hivyo vya vurugu ambavyo vimefanya sehemu ya jamii ya wakazi wa Visiwani humo, hasa Wakristo, kuishi kwa wasi wasi mkubwa kutokana na vitisho vinavyoendelea kutolewa na baadhi ya vikundi pamoja na hali ya kutopewa ulinzi wa kutosha na vyombo husika. Tunaendelea kuwaahidi Sala na mshikamano wetu katika kipindi hiki kigumu.

      Pamoja na hayo, tunapenda kuwakumbusha Watanzania wenzetu, hasa mamlaka husika kutafakari na kuzingatia busara ya wahenga waliosema kwamba “mwanzo wa makubwa ni madogo” na kwamba “mdharau mwiba mguu huota tende”. Kumbu kumbu zinatwambia kwamba, chuki za wazi za kidini zilianza kuinyemelea nchi yetu miaka ya 1990, pale mihadhara ya kashfa za kidini ilipoanza kuruhusiwa. Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, kwa kuongozwa na busara ya kichungaji, kwa nyakati tofauti, liliandika barua kuziomba na kuzihimiza Mamlaka husika kuingilia kati na kuhakikisha kwamba mihadhara kama hiyo haipati nafasi ya kuendelea katika nchi yetu kwani kamwe haiwezi kuwa na tija isipokuwa kuamsha hisia kali za kidini, jazba na kujenga chuki miongoni mwa waamini wa dini tofauti. Kwa bahati mbaya, ushauri huo wa Baraza la Maaskofu ulipuuzwa na mamlaka husika.

      Hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko kubwa la vyombo vya habari ambavyo vimeanzishwa na ambavyo badala ya kuzingatia malengo mazuri ya vyombo vya habari ya kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha, vimeonyesha malengo ya wazi ya kueneza uzushi, kashfa, chuki na uchochezi. Bado kuna CD/DVD na Kanda chungu nzima zilizozagaa mitaani zenye malengo kama hayo ambapo, kwa mshangao mkubwa wa raia wema wa nchi hii, licha ya wahusika kufahamika na kuonekana wazi wazi, hakuna hatua za kisheria zinazochukuliwa dhidi yao. Tunachelea hata kudhani kwamba mamlaka za dola zinawakingia kifua wadau wa harakati hizo.

      Mkusanyiko wa mambo yote haya ndio uliotufikisha hapa tulipo. Kwa upendo tulio nao kwa nchi yetu na kwa kuzingatia historia ya mlolongo wa matukio yaliyotufikisha hapa tulipo, tunahofu, lakini kwa uwazi tunapenda kuziambia mamlaka husika, watu wote wenye mapenzi mema na Watanzania wote kwa ujumla kwamba, iwapo hatua madhubuti hazitachukuliwa mara moja ili kurekebisha hali hii, baada ya miaka michache, hakika kwamba nchi yetu inaweza kuingia katika machafuko makubwa ya kidini. Ili kuepuka hali hiyo isitokee, kwa moyo wa unyenyekevu kabisa, tunapendekeza hatua zifuatazo zichukuliwe:-

      • Sisi Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania tutaendelea kusali ili kuiombea nchi yetu amani. Licha ya sala na maombi ya kawaida kwa ajili ya lengo hilo, Mkutano Mkuu umeamua kwamba, tutakuwa na siku moja ya kusali kitaifa kwa ajili ya kuomba amani;
      • Tutaendelea kutumia sauti yetu ya kinabii kuonya, kukemea na kukaripia vitendo vyote vile vinavyoashiria kueneza chuki miongoni mwa watu wa dini mbali mbali;
      • Kwa kutumia Tume na Idara zetu, tutaendelea kujenga na kueneza mazungumzano na Waamini wa dini mbali mbali tukiheshimu tofauti zilizopo. Hii ni kwa sababu tunaamini kwamba, suala la dini ni wito na hiari ya mtu na hakuna mtu yeyote aliye na haki ya kumlazimisha mwingine ajiunge na dini yake.


      Kwa upande wa wadau wengine na hasa kwa Serikali yetu pamoja na vyombo vyake vya usalama tunapendekeza yafuatayo:-

      • Mihadhara, makongamano na mikutano yenye lengo la kutoa kashfa na kuchochea chuki miongoni mwa dini mbalimbali ipigwe marufuku;
      • Vyombo vya habari vinavyoeneza uzushi, kashfa na uchochezi vidhibitiwe kwa kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufungiwa;
      • Uzushi na uongo unaoenezwa na vyombo vya habari na watu wenye lengo la kuwachonganisha Watanzania na waamini wa dini mbali mbali utolewe ufafanuzi mara moja na Wizara na vyombo vingine vinavyohusika;
      • Kuweko na mpango kabambe wa kutoa elimu ya uraia yenye kina na upana katika nafasi zote, itakayowawezesha vijana wetu kuwa wazalendo kwa nchi yao na kuepuka propaganda za kuwagawa Watanzania kwa misingi ya kidini;
      • Suala la ukosefu wa ajira, hasa miongoni mwa vijana, liangaliwe kwa makini kwani linaweza kuwa moja ya sababu zinazowafanya vijana wengi kujiingiza katika vikundi vya kidini vinavyojenga chuki na kutoa matumaini ya uongo;
      • Lakini, zaidi ya yote, iwapo Serikali yetu na mamlaka husika inataka kuwa na imani mbele ya jamii kwamba ina nia thabiti ya kuhakikisha kwamba vurugu za kidini hazipati nafasi katika Nchi yetu, wale wote wanaohusika na vurugu hizo wachukuliwe hatua za kisheria mara moja! Ni vigumu kuamini kwamba katika kipindi cha kuanzia mwaka 2001 mpaka sasa, Makanisa 25 yamekwisha chomwa moto Visiwani Zanzibar lakini hakuna aliyekamatwa na kuchuliwa hatua za kisheria!


      Tumefanya mkutano wetu katika mazingira ya kuwepo mvutano kati ya madaktari na serikali na kwa bahati mbaya sana, kama tulivyokwisha kutamka huko nyuma, mvutano huu unaleta athari kubwa kwa raia wasio na hatia, athari ambayo haiwezi kurudishwa. Uhai wa raia wa Tanzania unaangamia kwa kukosa ulinzi wa tiba. Katika hili tunapenda kukumbusha kuwa kila mmoja ni mdau. Hakuna hata mmoja anayeweza kulikwepa hili. Tunapenda kurudia himizo letu la awali kwamba ni bora ikapatikana njia nyingine iliyo mwafaka zaidi ya kudai haki na mazingira yanayofaa ya kazi bila kuleta madhara ya kupoteza uhai ambao ni haki msingi ya kila mwanadamu.

      Tunaiasa Serikali yetu ikae tena pamoja na madaktari na kuchambua hoja zitakazowekwa mbele yao. Uwazi na ukweli vikitawala hakuna pande itakayokataa kuridhia eti kwa sababu ya kukataa tu bila hoja. Taifa letu limejipatia aibu mbele ya macho ya ulimwengu ya jinsi tunavyoshindwa kuishi kile tunachosema kwenye majukwaa.

      Mwisho, tunaendelea kuwaalika Watanzania wenzetu, hasa viongozi wa dini mbalimbali kuwahamasisha waamini wao wawe raia wema wa nchi hii kwa kuungana pamoja kuhamasisha upendo, haki, amani na maridhiano miongoni mwa Watanzania wote. Licha ya tofauti zetu, tuzingatie hasa yale yanayotuunganisha: ubinadamu wetu na uraia wetu wa nchi yetu Tukufu ya Tanzania ambamo tutake tusitake, ni lazima wote tuishi! Tuepe ushindani ambao hauna tija isipokuwa kutupeleka katika kujenga chuki na hali ya kudhaniana vibaya miongoni mwa Waamini wetu. Iwapo kuna sababu ya kushindana, tushindane katika kubuni mbinu za kujenga Upendo na Amani miongoni mwa Watanzania katika kutafuta njia za kuwaletea maendeleo yatakayowatoa kutoka katika Umaskini, Ujinga na Maradhi ambao ndio adui wetu sote.

      Tunaiombea Nchi yetu Amani na Usalama.



      +Jude Thaddaeus Ruwai’chi
      RAIS: BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA/
      ASKOFU MKUU JIMBO LA MWANZA

      Juni 30, 2012

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Return Of Undertaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Posts : 654
      Rep Power : 539
      Likes Received
      448
      Likes Given
      0

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      No comment
      Yo Yo likes this.

    4. #3
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,496
      Rep Power : 2078
      Likes Received
      1059
      Likes Given
      1568

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Vichwa vimesema. Hakuna Kihiyo hapo
      Yo Yo likes this.
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    5. #4
      Bangoo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,269
      Rep Power : 0
      Likes Received
      370
      Likes Given
      0

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Wasomi wa kikatoliki wakikaa ujue kuna jambo! Hawa ndo wasomi wametoa tamko! Yapasa serikali ichukue hatua dhidi ya wahusika. Hivi vichwa havikurupuki! Hujifungia ndani na kutoka na maneno ya busara.
      Yo Yo, genekai and magistergtz like this.

    6. #5
      Bangoo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,269
      Rep Power : 0
      Likes Received
      370
      Likes Given
      0

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Kama huna digree huwezi kuwa kiongozi wa kanisa katoliki, hakika huku ndo kuna vichwa!

    7. Miaka 50

    8. #6
      Sn2139's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th April 2010
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 805
      Rep Power : 2867
      Likes Received
      237
      Likes Given
      1400

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      tamko ni zuri na limejaa hekima na nia njema kwa taifa letu...je kuna mtu ansikiliza tamko hili? je kuna moyo unaotamani kutekeleza? Kama hakuna tutaangamia kama nchi
      Yo Yo and Mlitika like this.
      the fool collects facts, the wise selects them

    9. #7
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,496
      Rep Power : 2078
      Likes Received
      1059
      Likes Given
      1568

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Quote By Bangoo
      Kama huna digree huwezi kuwa kiongozi wa kanisa katoliki, hakika huku ndo kuna vichwa!
      Ndo manake mkuu!!!!
      Nikupateje likes this.
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    10. #8
      Wachovu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th June 2012
      Posts : 222
      Rep Power : 1111
      Likes Received
      44
      Likes Given
      0

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Kikwete ni mnafiki sana , kama alikuwa anasema ukweli au kama alikuwa na hoja za msingi kwa nini asisimame na madaktari wote pamoja watueleze kila mtu anasemaje hili tuone mwongo ni yupi . Yeye anakuja peke yake anabwabwaja anadhani wanasiasa wa nchi hii tunwaamini. Mwongo Mkubwa

    11. #9
      Yo Yo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 10,778
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1333
      Likes Given
      2564

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Nimeishi kitume na watawa hawa kwa miaka mingi....nina msingi mzuri wa kitawa uliojengwa vema na mzazi wangu tangu utotoni.....matamko kama haya huwa si ya kubeza.....ukityumia busara za kawaida kabisa unaona kuna ukweli na wahusika wanapaswa kuchukua hatua za haraka sana.....
      Ndahani and Mlitika like this.

    12. #10
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 846
      Rep Power : 963
      Likes Received
      538
      Likes Given
      592

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Quote By Bangoo
      Kama huna digree huwezi kuwa kiongozi wa kanisa katoliki, hakika huku ndo kuna vichwa!
      Sheria za Kanisa Katoliki yaan Canon Laws inasema kwamba ili uwe askofu lazima uwe walau na Phd au equivalent:

      Can. 378(1){5}:
      {To be a suitable candidate for the episcopate, a person must hold a doctorate or at least a licentiate in sacred Scripture, theology or canon law, from an institute of higher studies approved by the Apostolic See, or at least be well versed in these disciplines}
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    13. #11
      Mlitika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd March 2012
      Posts : 402
      Rep Power : 516
      Likes Received
      220
      Likes Given
      311

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Asante mkuu Nyetk kutuletea huu ujumbe jamvini. Mimi nilisiki live jana redioni. Ni ujumbe uliosheheni ukweli, uko very balanced na umetolewa bila 'biace' yoyote. Natamani kungefanyika utaratibu wa kuunga mkono tamko hili kwa mstakabali wa nchi hii. Big-up sana wazee wetu.

      NAUNGA MKONO TAMKO!
      Last edited by Mlitika; 2nd July 2012 at 19:51.
      Nyetk likes this.

    14. #12
      Sabayi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th December 2010
      Posts : 1,283
      Rep Power : 685
      Likes Received
      415
      Likes Given
      921

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Inachukua miaka 8 kuwa padre baada ya kumaliza form six na kati ya hiyo nane lazima usome philosophy ikusaidie kufikiria vizuri,Tunapaswa kuweka itikadi zetu pembeni na kusikiliza busara za hawa ndugu

    15. #13
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 846
      Rep Power : 963
      Likes Received
      538
      Likes Given
      592

      Default re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Quote By Sabayi
      Inachukua miaka 8 kuwa padre baada ya kumaliza form six na kati ya hiyo nane lazima usome philosophy ikusaidie kufikiria vizuri,Tunapaswa kuweka itikadi zetu pembeni na kusikiliza busara za hawa ndugu
      Kwa miaka hiyo minane ya upadri ni sawa na degree ya miaka mitatu, ukaenda masters miaka miwili na PhD miaka mitatu.

      Kwa padri wa kanisa katoliki ni equivalent na Phd ya huyu niliyemfananisha. Na huyo ujue ni padri wa Jimbo yaani diocesan. Padri wa Mashirika kama majesuit unaweza kufika hata miaka 45 unausotea!!
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    16. #14
      kuro's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 11th June 2012
      Posts : 7
      Rep Power : 350
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      hongereni baraza la maaskofu wakatoliki kwa tamko lililojaa busara.
      Nyetk likes this.

    17. #15
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,663
      Rep Power : 0
      Likes Received
      536
      Likes Given
      272

      Default Re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Tamko la maaskofu halivuki MAJI, znz ni nchi inayojitegemea na haiendeshwi na kanisa.

    18. #16
      Angel Msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Posts : 6,266
      Rep Power : 1825
      Likes Received
      1397
      Likes Given
      0

      Default Re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      nilikua nasubiria tamko lao kwa hamu kubwa sana. NAWAPONGEZA KWA HEKIMA WALIYOTUMIA
      Nyetk likes this.

    19. #17
      Topical's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 5,050
      Rep Power : 1231
      Likes Received
      853
      Likes Given
      707

      Default Re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Quote By Nikupateje
      Kwa miaka hiyo minane ya upadri ni sawa na degree ya miaka mitatu, ukaenda masters miaka miwili na PhD miaka mitatu.

      Kwa padri wa kanisa katoliki ni equivalent na Phd ya huyu niliyemfananisha. Na huyo ujue ni padri wa Jimbo yaani diocesan. Padri wa Mashirika kama majesuit unaweza kufika hata miaka 45 unausotea!!
      Phd halafu unafanya usheraiti wtf
      "Mbowe for Presidency 2015""

    20. #18
      Same ORG's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 10th June 2012
      Location : Dubai
      Posts : 323
      Rep Power : 0
      Likes Received
      19
      Likes Given
      2

      Default Re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Maaskofu hawana kauli kwa nchi yenye waislamu 99% hii kauli iishie Tanganyika.

    21. #19
      Kigogo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,146
      Rep Power : 2084
      Likes Received
      1219
      Likes Given
      313

      Default Re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      kanisa katoliki lina watu wenye akili sana....sio wale wenzetu wanaogomea sensa
      ______________________________ _
      Niko tayari kufa huku nimesimama kuliko kuishi huku nimepiga magoti....

    22. #20
      Topical's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 5,050
      Rep Power : 1231
      Likes Received
      853
      Likes Given
      707

      Default Re: Tamko la Baraza la Maaskofu juu ya hali ya Zanzibar na mgomo wa madaktari

      Quote By Same ORG
      Maaskofu hawana kauli kwa nchi yenye waislamu 99% hii kauli iishie Tanganyika.
      Wanataka serikali ikataze waislamu wasihubiri dini yao...sasa kama wao wameshindwa kueneza dini yao wanataka serikali iwasaidie kwa kuwazuia wengine wasifanye mihadhara??

      Eti vyombo vya habari vifutwe..wako kwenye enzi zile za st. nyerere; vifutwe kwanini unafikiri hizi ni zama za kusikiliza unachotaka..kila moja uko right kuwa maoni yake kama hutaki usisikilize redio hiyo.."SIYO UNALIA KWA Serikali" what a shame..
      "Mbowe for Presidency 2015""

    23. Study Abroad
    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...