Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 51
    1. #1
      Bangoo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,269
      Rep Power : 0
      Likes Received
      370
      Likes Given
      0

      Default Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Baraza la maaskofu catolic Tanzania limemetoa taarifa kuwa serikali imekuwa ikiwakumbatia watu wanaokashifu dini za wanzao!

      Akitoa taarifa ya baraza la maaskofu Tanzania jana Raisi wa baraza hilo Thadeus Ruwaichi alisema serikali imeshindwa kuwachukulua hatua watu waliochoma makanisa huko zanzibar.

      Alisema toka 2010 mpaka sasa makanisa 25 yamechomwa zanzibar na hakuna mtu yoyote anayechukuliwa hatua!.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Abdalla Khamis's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Posts : 59
      Rep Power : 728
      Likes Received
      8
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Nyinyi viongozi wa Makanisa mnataka Serikali ifanye nini kwa kitu ambacho hata ushahidi haupo?,tokio la kuchomwa kanisa Zanzibar bado ni tete , hajajulikana msababishi, au ndio mwatafuta namna ya kuimrisha serikali ikamate tu watu kama mnavofanya?, kwa Zanzibar tunasema basi tena ,amri zenu toeni Makanisani sio Serikalini, ama kwa serikali yenu ya muungano sio Zanzibar.

    4. #3
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 573
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      BARAZA la Maaskofu Katoliki Tanzania (Tec) limeilaumu Serikali kuwa, inawakingia kifua watu wanaoendesha mihadhara ya kidini inayokashifu dini nyingine.

      Rais wa Tec anayemaliza muda wake, Askofu Mkuu, Yuda Thadeus Ruwa’ichi alisema jana kuwa, licha ya kwamba jambo hilo linaweza* kuleta chuki na vurugu nchini, Serikali haichukui hatua zozote dhidi yake.

      “Serikali na mamlaka za dola zinawakingia kifua wadau wa harakati wanaoendesha mihadhara yenye kukashfu dini nyingine, pamoja na kufahamika lakini hawachuliwi hatua zozote,” alisema.

      Rais huyo ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza, alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati wa ibada maalumu ya kutangaza uongozi mpya wa baraza hilo.

      Katika uchaguzi huo Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo la Iringa, alichaguliwa kuwa rais mpya kwa kipindi cha miaka mitatu.

      Askofu Ruwa’ichi aliitaka Serikali kupiga marufuku mihadhara na makongamano ya kidini, kwani ikiendelea baada ya miaka michache nchi itaingia katika machafuko makubwa yatakayoleta maafa.

      Ruwa’ichi* ambaye alikuwa akitoa tamko hilo kwa niaba ya maaskofu wote, alisema wameshangazwa na ukimya wa Serikali katika kushughulikia vurugu za kidini zinazoendelea kutokea hapa nchini na kuwataka wasiogope kuchukua hatua, kwani hiyo ndiyo dhamana waliyopewa na wananchi.

      “ Tunalaani vikali vurugu na vitendo vya uchomaji moto makanisa vilivyotokea huko Zanzibar na kuwafanya wananchi waishi kwa wasiwasi kwa sababu ya kushindwa kupewa ulinzi na vyombo vya dola,” alisema Askofu Ruwa’ichi.

      Alisema maaskofu wanatoa pole kwa waathirika wa vurugu hizo huko Zanzibar ambao wanaendelea kuishi kwa wasiwasi kutokana na vitisho vinavyoendelea kutolewa dhidi yao.

      Alisema Serikali kama inataka kujenga imani mbele ya wananchi wake, inatakiwa kuchukua hatua ili kuhakikisha vurugu za kidini hazipati nafasi.

      “ Watanzania na mamlaka husika za Serikali zinatakiwa kutafakari kwani mwanzo wa makubwa ni madogo, na mdharau mwiba mguu huota tende,” alisema na kuongeza kuwa vurugu hizo zikiachwa ziendelee zitasababisha matatizo makubwa.

      Askofu Ruwa’ichi alisema kati ya mwaka 2001 na sasa jumla ya makanisa 25 yalichomwa moto Zanzibari, lakini hakuna aliyekamatwa wala kuchukuliwa hatua za kisheria.

      “Kama hakuna mtu yeyote aliyechukuliwa hatua kwa uchomaji moto makanisa hayo, unadhani tatizo hili litamalizika,” alihoji.

      Aidha, Askofu Ruwa’ichi* alitaka vyombo vya habari vinavyoeneza uzushi na chuki za kidini vifungiwe vinginevyo ndiyo kitakuwa chanzo cha vurugu.

      “ Baadhi ya vyombo vya habari vinaeneza uzushi na chuki za kidini kama vile hakuna Serikali. Serikali isikae kimya kama vile hakuna linalojiri, ichukue hatua na kutoa ufafanuzi kwa wananchi,” alisema.

      Akizungumzia ukosefu wa ajira, Askofu Ruwa’ichi* alisema Serikali inatakiwa kuangalia suala hili kwa umakini, kwani vijana ni rahisi kujiunga na makundi hayo yenye vurugu kwa sababu za kutokuwa na kazi za kufanya.

      Alisema katika mkutano huo wameamua kutenga siku moja kwa ajili sala ya kuliombea taifa na kwamba wataendelea kutumia idara za kanisa hilo kujenga masikilizano* na dini mbalimbali, ili kujenga umoja licha ya tofauti zao za kiimani.

      Madaktari na Serikali
      Askofu Ruwa’ichi* alisema, Watanzania wanaangamia nchini mwao kwa kukosa tiba na ulinzi, jambo ambalo ni hatari na kuiomba Serikali kukaa meza moja na madaktari ili kumaliza mgomo huo.

      Hata hivyo, aliwaonya madaktari kuangalia njia nyingine za kutumia katika kudai haki zao badala ya mgomo ambao unapoteza maisha ya wananchi wasiokuwa na hatia.

      “ Tungependa matatizo haya ya Serikali na madaktari yafikie mwisho kwa kufanya mazungumzo kwani wanaoumia ni wananchi,” alisema.
      mwisho

      Askofu Malasusa
      Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa amewataka wananchi kuacha tabia ya kujilimbikizia mali,* huku wakishuhudia jamii ikiangamia* kwa kukosa mahitaji muhimu kama elimu na afya.

      “Kuna watu wamejaliwa kuwa na kila kitu hata baadhi ya mali zao hawazifahamu pale zinapopotea, lakini kuna kundi la jamii nyingine kati yao ambalo linaishi maisha magumu ambayo linahitaji msaada wa kutosha,” alisema.

      Askofu Malasusa aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam *wakati wa harambee ya kuchangia mfuko wa kusomesha wanafunzi wasio na uwezo wa ‘Educate The Children’ wa Shule ya Mtakatifu Joseph’s Mbezi Beach kuwa hivi sasa watu wamekuwa na tabia ya kujilimbikizia fedha nyingi.

      “Hivi sasa watu wanajilimbikizia mabilioni ya fedha, huku wakijua kuna kundi la watu ambao linahitaji msaada wao, lakini wamekuwa hawatambui hilo,” alisema Askofu Malasusa.

      Mwenyezi Mungu ametufundisha kugawana kile unachokipata kwa manufaa ya wengine hususan wasio na uwezo, lakini hivi sasa imekuwa tofauti kwa baadhi ya watu kupenda kumiliki mabilioni ya fedha.

      Kauli hiyo ya Askofu Malasusa *inakuja siku chache ambapo Kitengo cha Polisi wa Kimataifa (Interpol) nchini kinachunguza Sh303.7 bilioni ambazo zinadaiwa kukutwa kwenye akaunti sita za Watanzania, wakiwamo Wanasiasa,katika benki mbalimbali nchini Uswisi.

    5. #4
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,646
      Rep Power : 4015
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Quote By Abdalla Khamis
      Nyinyi viongozi wa Makanisa mnataka Serikali ifanye nini kwa kitu ambacho hata ushahidi haupo?,tokio la kuchomwa kanisa Zanzibar bado ni tete , hajajulikana msababishi, au ndio mwatafuta namna ya kuimrisha serikali ikamate tu watu kama mnavofanya?, kwa Zanzibar tunasema basi tena ,amri zenu toeni Makanisani sio Serikalini, ama kwa serikali yenu ya muungano sio Zanzibar.
      Nani sasa anachoma makanisa na amechukuliwa hatua gani?
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    6. #5
      Bangoo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,269
      Rep Power : 0
      Likes Received
      370
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Wakatoliki hukaa na kutafakari, huwa hawakurupuki! Elimu yao huwafanya wawe na busara sana.
      Chilipamwao likes this.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      rugumisa's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th May 2012
      Posts : 38
      Rep Power : 358
      Likes Received
      8
      Likes Given
      12

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Na hao wanaokashifu dini nyingine wajiulize maswali yafuatayo1)Tangu waanze kukashifu wamepata waumini wapya wangapi?(ii)Je kukashifu au kutukana dini ya mtu mwingine ni njia nzuri ya kuoneza dini yako au ni kuonyesha inferiority complex , elimu ndogo uliyonayo ya kujenga hoja,na kuwa roho wa bwana hayuko nawe?(iii)Je na wakristu tukikikashifu dini yao watavumilia-maana tukianza itakuwa noma na tunao ushahidi mwingi wa kimantiki,kihistoria na miujiza kutoka mbinguni yenye ukweli usiotia shaka kuhusu tunaloamini?(iv)Je kuna nabii/mtume wa Mungu aliyeeneza dini au ujumbe wa Mungu kwa lugha ya matusi na kejeli-hapa naongelea manabii wa ukweli wa mungu kama Yohana mbatizaji,paulo,petro,musa?-Ukweli utakuweka Huru.
      Chilipamwao likes this.

    9. #7
      Bobuk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 2,056
      Rep Power : 920
      Likes Received
      829
      Likes Given
      0

      Default

      Labda serikali ya JMT inasubiri waanze kutua kwa mabomu makanisani kama walivyofanya huko Kenya Jana ndiyo ijishebedue!

    10. #8
      Ye Nyumbai's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 24th March 2011
      Posts : 122
      Rep Power : 437
      Likes Received
      35
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Quote By rugumisa
      na hao wanaokashifu dini nyingine wajiulize maswali yafuatayo1)tangu waanze kukashifu wamepata waumini wapya wangapi?(ii)je kukashifu au kutukana dini ya mtu mwingine ni njia nzuri ya kuoneza dini yako au ni kuonyesha inferiority complex , elimu ndogo uliyonayo ya kujenga hoja,na kuwa roho wa bwana hayuko nawe?(iii)je na wakristu tukikikashifu dini yao watavumilia-maana tukianza itakuwa noma na tunao ushahidi mwingi wa kimantiki,kihistoria na miujiza kutoka mbinguni yenye ukweli usiotia shaka kuhusu tunaloamini?(iv)je kuna nabii/mtume wa mungu aliyeeneza dini au ujumbe wa mungu kwa lugha ya matusi na kejeli-hapa naongelea manabii wa ukweli wa mungu kama yohana mbatizaji,paulo,petro,musa?-ukweli utakuweka huru.
      kuna msikiti hapa arusha unaitwa masjid kuba,hapo kuna kijana anuza kanda na cd za dini yao lakini anachokifanya ni kuweka cd zinazokashifu ukristu wakati wote.ni wazi cd hizo waumini wao wanazipenda na bila hizo hauzi kitu.tunawashangaa viongozi wanalijuwa hili kwamba matokeo yake si mazuri huko tuendako lakini wanakaa kimya.jiulizenu wakristu nao wakaweka mambo hadharani,tanzania itakalika.si kwamba wakristu hawajui habari ya dini zingine ila wakristu wanafundishwa kuvumiliana na kuchukuliana kiubinadamu.pelekeni watoto shule acheni kuwakaririsha mabo wasiyoyaelewa matokeo yake ni kulalamika mnaonewa kila uchao.
      rugumisa likes this.

    11. #9
      Remote's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2011
      Posts : 4,247
      Rep Power : 1356
      Likes Received
      942
      Likes Given
      182

      Default

      Quote By Abdalla Khamis
      Nyinyi viongozi wa Makanisa mnataka Serikali ifanye nini kwa kitu ambacho hata ushahidi haupo?,tokio la kuchomwa kanisa Zanzibar bado ni tete , hajajulikana msababishi, au ndio mwatafuta namna ya kuimrisha serikali ikamate tu watu kama mnavofanya?, kwa Zanzibar tunasema basi tena ,amri zenu toeni Makanisani sio Serikalini, ama kwa serikali yenu ya muungano sio Zanzibar.
      UAMSHO ndio waliochoma makanisa hata polisi wanajua hilo

    12. #10
      Remote's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2011
      Posts : 4,247
      Rep Power : 1356
      Likes Received
      942
      Likes Given
      182

      Default

      Quote By Abdalla Khamis
      Nyinyi viongozi wa Makanisa mnataka Serikali ifanye nini kwa kitu ambacho hata ushahidi haupo?,tokio la kuchomwa kanisa Zanzibar bado ni tete , hajajulikana msababishi, au ndio mwatafuta namna ya kuimrisha serikali ikamate tu watu kama mnavofanya?, kwa Zanzibar tunasema basi tena ,amri zenu toeni Makanisani sio Serikalini, ama kwa serikali yenu ya muungano sio Zanzibar.
      UAMSHO ndio walichoma

    13. #11
      Lyceum's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2009
      Posts : 547
      Rep Power : 599
      Likes Received
      100
      Likes Given
      128

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Quote By Ye Nyumbai
      kuna msikiti hapa arusha unaitwa masjid kuba,hapo kuna kijana anuza kanda na cd za dini yao lakini anachokifanya ni kuweka cd zinazokashifu ukristu wakati wote.ni wazi cd hizo waumini wao wanazipenda na bila hizo hauzi kitu.tunawashangaa viongozi wanalijuwa hili kwamba matokeo yake si mazuri huko tuendako lakini wanakaa kimya.jiulizenu wakristu nao wakaweka mambo hadharani,tanzania itakalika.si kwamba wakristu hawajui habari ya dini zingine ila wakristu wanafundishwa kuvumiliana na kuchukuliana kiubinadamu.pelekeni watoto shule acheni kuwakaririsha mabo wasiyoyaelewa matokeo yake ni kulalamika mnaonewa kila uchao.
      kuna redio inaitwa Imani kule Morogoro. Jamaa wanakashifu balaa. Nina mpango wa kuanzisha kikanisa changu cha kujibu mpigo. LIWALO MA LIWE BANA

    14. #12
      nyabhingi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th October 2010
      Posts : 3,210
      Rep Power : 1288
      Likes Received
      1347
      Likes Given
      2627

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      mihadhara ya waislam kuitupia madongo dini ya kikristo ilianza mara mwinyi alipoingia madarakani,makanisa kuchomwa moto ni baada ya jk kuwa rais...kuna connection flani hapa..
      waziri/saidi likes this.
      Every nation in every region now has a decision to make: Either you are with us, or you are with the terrorists.George W. Bush


    15. #13
      SAGANKA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2012
      Posts : 272
      Rep Power : 241
      Likes Received
      187
      Likes Given
      32

      Default

      Quote By Abdalla Khamis
      Nyinyi viongozi wa Makanisa mnataka Serikali ifanye nini kwa kitu ambacho hata ushahidi haupo?,tokio la kuchomwa kanisa Zanzibar bado ni tete , hajajulikana msababishi, au ndio mwatafuta namna ya kuimrisha serikali ikamate tu watu kama mnavofanya?, kwa Zanzibar tunasema basi tena ,amri zenu toeni Makanisani sio Serikalini, ama kwa serikali yenu ya muungano sio Zanzibar.
      Intelijensia ambayo kila kukicha polisiccm wanahubiri iko wapi.Mbona haijatuletea majibu juu ya uchomaji wa makanisa.Au intelijensia imewekewa king'amuzi kwa ajili ya habari za cdm tu.Halafu wewe kila siku nakukataza tabia zako hizo za kuwaambia viongozi wa dini eti wasivuke maji kuzungumzia habari za znz,mbona wewe unavuka maji na kuwajibu maaskofu wa bara,au una jini mahaba,sikuelewi.

    16. #14
      mopaozi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2010
      Posts : 2,446
      Rep Power : 757
      Likes Received
      258
      Likes Given
      49

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Wazee wa kununua maspika na kubesha kwenye malori kueleza kuwa Yesu c Mungu na watabakia hvy hvy wenzao wanajenga mashule,vyuo,hospitali na wakiumwa makoo kwa kupayuka kweny maspika watatibiwa kwny hizo hosp kwa kulipia
      Chilipamwao likes this.

    17. #15
      mikonomiwili's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th January 2011
      Posts : 119
      Rep Power : 446
      Likes Received
      27
      Likes Given
      199

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      An_nuur na Radio IMani vitazua Vurugu nchini sijui TCRA wanafanya nini ama hawa wamepata Baraka za serikali . Zamani tulizoea kila kitu kinacho Tangazwa kikakua kina angaliwa yaani monitor lakini leo watu wanajitangazia na kuaharibu dini wawengine tu .Nasis tuanze kuwakashfu ili na wao wajisikie vibaya.

      hivi hawawezi kuhubiri kutokana na msaafu bila kugusa ukristo kila kukicha lazima wa seme dini ya wenzao inawahusu nini ?

    18. #16
      Gulwa's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th June 2008
      Posts : 138
      Rep Power : 585
      Likes Received
      46
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      "Religion and violence do not go together but religion and reson do" Benedict XVI

    19. #17
      Ye Nyumbai's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 24th March 2011
      Posts : 122
      Rep Power : 437
      Likes Received
      35
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Napenda niwafahimishe wale wote wanaukashifu Ukristo kwamba Wakristo si wajinga kunyamaza,nikwasababu Wakristo ni watu wanaopenda amani na utulivu uwepo siku zote.

      Lazima watu wote wafahamu (Waislamu) kwamba hata Wakristu wanaijua Quran vizuri na wanajuwa kuichambua kwa kina pia,watakapoanza akina Simbaulanga na wenzake ndani ya miaka michache misikiti yote itageuka makanisa.

      Narudia tena ndugu zangu ninyi wafwata upepo, pelekeni watoto shule wakaelimike si vinginevyo na haya malalamiko ati Wakristo wanapendelewa yataisha.

      Endelea kusema Yesu si Mungu na nguruwe haramu,mimi namkazania mwanangu asome aje amtume mwanao!!!
      Chilipamwao and waziri/saidi like this.

    20. #18
      Makupa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 2,175
      Rep Power : 810
      Likes Received
      249
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Satanic Verses hivi ni nini
      Chilipamwao likes this.

    21. #19
      mzaire's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th April 2012
      Posts : 200
      Rep Power : 398
      Likes Received
      40
      Likes Given
      4

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Quote By Bangoo
      Baraza la maaskofu catolic Tanzania limemetoa taarifa kuwa serikali imekuwa ikiwakumbatia watu wanaokashifu dini za wanzao!

      Akitoa taarifa ya baraza la maaskofu Tanzania jana Raisi wa baraza hilo Thadeus Ruwaichi alisema serikali imeshindwa kuwachukulua hatua watu waliochoma makanisa huko zanzibar.

      Alisema toka 2010 mpaka sasa makanisa 25 yamechomwa zanzibar na hakuna mtu yoyote anayechukuliwa hatua!.


      Kwani ni kwenu huko znz nyinyi maaskofu, whts kanisa in znz???

      wakristo wenyewe ni 0.2%, msituletee fujo hapa Tz. Nani atawasikiliza huko znzbar.

    22. #20
      mzaire's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th April 2012
      Posts : 200
      Rep Power : 398
      Likes Received
      40
      Likes Given
      4

      Default Re: Serikali inawalinda wanaokashifu dini - Maaskofu

      Quote By Remote
      UAMSHO ndio waliochoma makanisa hata polisi wanajua hilo
      Nenda kanyolewe huko na hzo pumba zako, nendeni mkawakamate si mshawajui, zogo la nini tena???

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...