Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

    Report Post
    Page 1 of 17 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 332
    1. #1
      Gambas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2011
      Location : Malimbe, Nyegezi Mwanza
      Posts : 955
      Rep Power : 2450
      Likes Received
      191
      Likes Given
      17

      Default UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      "NI saa 12:45 asubuhi, bado kiza kimetanda katika eneo hili la Msitu wa Mabwepande. Mbele yangu namwona mtu akiwa amekaa chini, pembeni ya barabara akiwa amelowa damu mwili mzima.

      "Ninapomkaribia nasikia sauti ya mtu huyo ikisema kwa taabu; naomba msaada jamani… naomba msaada jamani", hivi ndivyo anavyoanza kusimulia Juma Mgaza Abdallah, mtu wa kwanza kumwona Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka baada ya kutekwa, kupigwa na kutupwa katika Msitu wa Mabwepande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

      Abdallah, anasema mara baada kumwona daktari huyo akiwa katika hali hiyo, alijaribu kumkokota kumtoa eneo hilo, lakini alishindwa kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo.

      Baada ya hapo, aliamua kusubiri mtu mwingine apite eneo hilo ili amwombe wasaidiane kumpeleka Kituo cha Polisi Bunju.

      Anasema muda mfupi baadaye aliona gari likija mbele yao, akalinyooshea mkono kulisimamisha. Liliposimama, akamweleza dereva hali aliyokuwa nayo Dk Ulimboka na kwamba anahitaji msaada wa haraka.

      Abdallah ambaye hadi wakati huo alikuwa hamfahamu mtu ambaye alikuwa akimsadia kuwa ni kiongozi wa madaktari kutokana na sura yake kuvimba, anasema walimwingiza katika gari hilo na kumpeleka Kituo Kidogo cha Polisi Bunju.

      Anasema, Dk Ulimboka wakati huo alikuwa akiendelea kuvuja damu katika baadhi ya majeraha yake huku akiwa hana suruali na kubaki na bukta tu, huku akizungumza kwa taabu.

      Kituo cha Polisi Bunju

      Baada ya kumfikisha kituoni hapo, walitoa maelezo namna walivyomwokota na kumsaidia kumfikisha hapo.

      Polisi baada kumhoji Dk Ulimboka, aliwatajia namba ya simu ya rafiki yake aitwaye Dk Deo. Walipompigia na kumweleza tatizo hilo, aliamua moja kwa moja kwenda Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, kutoa taarifa hizo na hatimaye kuandamana na watu kadhaa kutoka hapo akiwamo Mkurugenzi wake, Hellen-Kijo Bisimba.

      Wawasili kituoni
      Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania wa kituo hicho, Onesmo Olengurumwa, anasema waliwafika Polisi Bunju saa 3:36 asubuhi na kumkuta Dk Ulimboka akiwa amekalishwa kwenye benchi huku damu ikiwa imeganda kwenye majeraha mwilini.

      Olengurumwa anasema waliwahoji polisi waliokuwa kituoni hapo kwa nini wakae na mtu aliyeumia kiasi hicho muda mrefu bila ya kuita gari la wagonjwa kumchukua ili kuwahi kupatiwa matibabu.

      Olengurumwa anasema polisi walisema kwamba, walikuwa wanawasubiri ndugu zake wafike.

      Baada ya muda mfupi, akiwa ameingizwa kwenye gari kupelekwa hospitali, Dk Ulimboka aliomba maji ya kunywa akisema ana kiu sana, lakini alipopewa, alikunywa kidogo akashindwa.

      Anasema wakiwa njiani, alikuwa akilalamika kuwa anasikika maumivu makali huku akisisitiza kuwa tukio la kutekwa na kupigwa lilikuwa la kumuua.

      "Jamani hawa watu walitaka kuniua walikuwa wamepanga kuniua," alisikika mara kwa mara akisema Dk Ulimboka wakati anapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupatiwa matibabu.

      Maelezo ya Dk Ulimboka
      Baada ya Dk Ulimboka kuokotwa aliweza kuzungumza na kurekodiwa muda mfupi baada ya kutolewa msituni na mazungumzo yake yalikuwa hivi;

      “Nilikamatwa na watu hao usiku wa Jumanne nikiwa maeneo ya Leaders Club, Kinondoni na daktari mwenzangu baada ya kupigiwa simu na mtu mmoja ambaye alidai kuwa anafanya kazi Ikulu.

      “Kuna jamaa mmoja anafanya kazi Ikulu, kama siku tatu mfululizo alikuwa akitaka kukutana na mimi ila nilishindwa kukutana naye kwa kuwa nilikuwa na kazi nyingi na wakati mwingine mpaka usiku,” alisema Dk Ulimboka.

      Huku akizungumza kwa taabu kutokana na mdomo wake kuvimba, alisema siku hiyo mtu huyo alimpigia tena simu na kumtaka wakutane.

      “Jana (Jumanne) alinipigia simu na nikamwambia daktari mwenzangu twende tukaonane naye, wakati huo alitueleza kuwa alikuwa maeneo ya Kinondoni Stereo,” alisema Ulimboka na kuongeza:

      “Tulipofika maeneo hayo tukampigia simu na akatueleza kuwa alikwisha ondoka, baadaye tukamweleza sehemu tulipo mimi pamoja na mwenzangu.”

      Alisema kuwa, wakati anakutana na mtu yule maeneo ya Leaders Club, hakuwa na amani.

      “Kwa kweli siku ile nilivyoonana na mtu yule sikuwa na amani kabisa ya kukaa eneo lile,” alisema Dk Ulimboka.

      Alisema kuwa wakati wakiendelea na maongezi ya kawaida, bado aliendelea kuwa na mashaka na mtu yule.

      “Katikati ya maongezi nikaona ameanza kuzungumza na simu, kila tukitaka kuagana alikuwa akizungumza na simu, sijui nini kilikuwa kinachelewesha sisi kuagana,” alisema Dk Ulimboka na kuongeza:

      “Ghafla walitokea watu kama watano na kusema kuwa hawana tatizo na mtu yeyote katika eneo hilo isipokuwa mimi.

      Wakati sijakaa sawa, waliniburuza hadi barabara ya lami kwa kuwa eneo hilo lilikuwa karibu na barabara.”

      Aliongeza, “Nilipowauliza wananipeleka wapi, wakaniambia kuwa mimi nasumbua sana na nitajua hukohuko, waliniingiza katika gari jeusi, lakini halikuwa na namba. Niliwauliza kosa gani nimefanya? Hawakunijibu kitu na kusema, we twende utajua hukohuko.’’

      Alisema alipokuwa ndani ya gari hilo watu hao walimpiga na kwamba walipofika maeneo ya Victoria, walichukua sweta nyeusi na kumfunga usoni, jambo lililomfanya ashindwe kuona kinachoendelea ikiwa ni pamoja na alikokuwa akipelekwa.

      “Walinipiga mateke ya mbavuni, wakati mwingine walitumia vitako vya bunduki, kila nilipokuwa najaribu kuangalia ninapokwenda nilishindwa,” alisimulia Dk Ulimboka.

      Alisema kuwa watu hao walimpeleka katika nyumba moja ambayo hakujua iko sehemu gani ambapo walimshusha na kuanza kumshambulia kwa mateke mfululizo kila sehemu ya mwili. Wakati huo, wote walimshinikiza awaambie nani yupo nyuma ya mgomo wa
      madaktari.

      “Tangu saa sita usiku mpaka saa 9:00 alfajiri walikuwa wananipiga tu, kuna wakati nilijaribu kukimbia wakapiga risasi juu nikasimama na sikuweza kukimbia tena,” alisema Dk Ulimboka na kuongeza:

      “Nilisimama, wakaendelea kunipiga, niliwasikia wakisema ama wanichome sindano ya sumu nife au kunikanyaga na gari. Baadaye wakaanza kuning’oa meno na kucha kwa kolea huku wakinilazimisha kusema nani yupo nyuma ya mgomo wa madaktari."

      Alisema kuwa, watu hao walikuwa na bunduki kubwa ambayo hakuweza kuitambua ni aina gani.

      “Waliniambia kuwa ninajua ninachokifanya hivyo wanaweza kunichoma sindano ya sumu nife au wanikanyage na gari nife,” alisimulia.

      Dk Ulimboka alisema kuwa awali hakuwa na shaka na watu hao kwa kuwa alidhani ni polisi, lakini baadaye alishindwa kuwaelewa kwani watu hao walimchanganya.

      “Sikuweza kuwatambua ila naweza kusema ni askari, walipokuwa wananipeleka niliwauliza mnanipeleka wapi na wakati huo nilikuwa sioni mbele ila ilikuwa kama maeneo ya Mwenge hivi,” alisema Dk Ulimboka.

      Alisema kuwa baadaye alipoteza fahamu na hakuweza kuona chochote zaidi ya kusikia sauti za watu hao kwa mbali.

      “Nilikuwa sioni na nilipoteza fahamu nikawa nasikia tu wakinibeba, gari lilitembea muda mrefu, sikujua ni wapi tunakwenda, kumbe ndio huko Mabwepande,” alisema.

      Alisema kuwa walifika maeneo ya barabara ya vumbi na baadaye wakamshusha na kumbeba hadi msituni.

      “Waliniburuza na kuniacha huko na muda wa saa kumi alfajiri ndipo nikazinduka na kuanza kujiburuza kuelekea barabarani ambako nilisaidiwa na mtu mmoja ambaye simtambui,” alisema Dk Ulimboka.

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      kelvito's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th May 2012
      Posts : 388
      Rep Power : 522
      Likes Received
      97
      Likes Given
      74

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Kweli udhaifu wa JK ni tatizo kubwa sana. Dr Slaa alisema kuichagua ccm ni maafa, hv JK kwanini anaamini mgomo wa ma dr unasababishwa na maadui zake? Kwani usalama na majeshi wanamsaidiaje mwenyekiti wa chama cha mapinduzi?

    4. #3
      artorius's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 527
      Rep Power : 478
      Likes Received
      100
      Likes Given
      0

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      At the beggining I thought this was just a conspiracy theory but now I have realised,this was really a conspiracy,the government now has a lot to explain,NO Doubt the government had its hand on dr.ulimboka
      Mtumishi Wetu, makungas and Thanda like this.

    5. #4
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,530
      Rep Power : 1799
      Likes Received
      656
      Likes Given
      0

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Wao wajipange haraka wanunue XRay CT Scan machines hospitali zote Utra Sound na waboreshe hali za hospitali zetu waone kama Dr wataendelea na mgomo!kwa nini wanaboresha bungeni tu?wangepunguza matumizi bungeni na kuboresha sekta zingine

    6. #5
      jigoku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2011
      Posts : 1,458
      Rep Power : 1005
      Likes Received
      365
      Likes Given
      537

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Walaaniwe wale wote waliomtesa ,waliopanga kumtesa na waliwatuma kumtesa huku wakidhani angelikufa kabla ya kusema neno kwa watu wakalisikia,sasa tumesikia kamtaja Msangi na taarifa zingine zimetupa kujua kumbe serikali inahusika.
      Liwalo na liwe
      Marumia likes this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Lukolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Location : Iringa
      Posts : 3,881
      Rep Power : 7038
      Likes Received
      2048
      Likes Given
      1573

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Tungependa kupata waandishi wa habari shujaa watakaoweza kuweka hizi story kwenye magazeti na kwenye redio, ili kila mwananchi ajue serikali ya Kikwete ni serikali ya aina gani. Yafaa pia taarifa kama hii ifikishwe kwenye vyama vya wanaharakati, ili wasiendelee kusema watu wasiojulikana bali waseme moja kwa moja kwamba alitekwa na kuumizwa na serikali, ieleweke moja.
      MwanaCBE likes this.
      Mtaji mkubwa kabisa wa CCM katika chaguzi zake ni umaskini na ujinga wa watanzania. CCM haitafanya kosa la kuyamaliza matatizo hayo kwa kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wamehatarisha nafasi yao ya kuendelea kutawala

    9. #7
      Baba V's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Location : Buguruni Mnyamani
      Posts : 10,962
      Rep Power : 30234
      Likes Received
      4722
      Likes Given
      3477

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      IKULU ina laana,imechafuka,if i was to be the next president nahisi nisingekaa pale,UDHAIFU ni hatari!

    10. #8
      georgeallen's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd June 2011
      Location : Seattle, WA, USA
      Posts : 2,055
      Rep Power : 0
      Likes Received
      516
      Likes Given
      260

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Hata tukijua (100%) ni serikali imefanya hivyo kuna lolote la kuifanya? nauliza tu.
      tripojo, michosho and jamiif like this.

    11. #9
      MAN OF CHANGES's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 9th January 2011
      Posts : 185
      Rep Power : 461
      Likes Received
      36
      Likes Given
      19

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Very sad,yani Tz kwa sasa kila kitu kunaumiza na kuendelea kuvunja wananchi moyo na matumaini.viongozi wabovu wasio na utu na wenye kujipenda wenyewe ndio chanxpzo cha matatizo na sababu ya hapa tulipo sasa.TUSIFE MOYO WA TZ WENZANGU,MUNGU YUPO NASI KUTUTETEA,ZAIDI TUENDELEE KUPIGANIA HAKI ZETU BILA KUJALI YANAYOTUKUTA NA YATAKAYOTUKUTA.
      NAKUOMBEA DACTARI ULIMBOKA,MUNGU AKUPONYE.AMINA.
      WA-UKENYENGE and Marumia like this.

    12. #10
      Ruppy karenston's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2011
      Posts : 396
      Rep Power : 482
      Likes Received
      69
      Likes Given
      26

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Aiseee,habari ya huzuni sana mpaka nimelia!
      Marumia and Vadgama like this.

    13. #11
      mkonowapaka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th February 2010
      Posts : 740
      Rep Power : 619
      Likes Received
      291
      Likes Given
      203

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      so sad ndugu zangu...better mtu upigwe risasi ufe kuliko mateso hayo...serikali ya jk inahusika moja kwa moja na tukio hili...ninalaani kwa nguvu zote tukio hili la kikatili na mateso makubwa namna hiyo kwa binadamu huyu...kumtesa mtoto wa mtu aliezaliwa na baba na mama yake;akasoma kwa taabu na kisha kuwatumikia watanzania wenzako kwenye sekta nyeti kama hii ya afya hakukubaliki ata kidogo..na cc watanzania tunakaa kimya kwa tukio kama hili???wanaharakati mnasemaje au na nyie mmetishwa??...hapana.hatupaswi kukaa kimya
      Mkono and jamiif like this.

    14. #12
      dada jane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th December 2011
      Posts : 505
      Rep Power : 478
      Likes Received
      94
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By georgeallen
      Hata tukijua (100%) ni serikali imefanya hivyo kuna lolote la kuifanya? nauliza tu.
      Tunalo sana. Wewe subiri kidogoo!
      Dawa kuchanana tu likes this.

    15. #13
      Mundu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2008
      Posts : 1,680
      Rep Power : 880
      Likes Received
      228
      Likes Given
      22

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Hata wabunge wa upinzani naona ni wanafiki tu katika suala hili la mgomo wa madakatari...kwanini wasigome kuingia bungeni kushinikiza Serikali kutatua tatizo la mgomo wa madaktari upesi.

      Kama ni suala la maslahi hilo ni jepesi na sioni kwa nini Serikali inasuasua kulitatua... Lakini suala la maboresho, hilo ni suala la mipango...lahitaji muda kwani hata kama ni ununuzi wa vifaa ama upanuzi na uboreshaji wa majengo hauwezi kufanyika kwa muda mchache...na ni suala linalogusa maendeleo ya Sekta ya utabibu Tanzania nzima, hususani vijijini. Niliangalia documentary moja, katika kituo kimoja cha TV hapa nchini, kuna hospitali/despensari moja kijijini ambayo inategemewa na watu wengi, hususan akina mama, haina umeme, wagonjwa huitajika kwenda na mafuta ya taa ili wapatiwe huduma nyakati za usiku. Hakuna pia maji na hakuna dawa. Ni gharika kupata huduma katika dispensari ile.

      Sasa kama ni tatizo la maboresho ya miundo mbinu...sijui katika kile kikao cha muafaka na Pinda walipeana ultimatum ama vipi? Sikumbuki kama nilipata kusikia ama kusoma mahali popote kuwa walipeana muda fulani kuhakikisha masuala haya ya miundo mbinu ama yaananza kushughulikiwa , ama yawe yamefikiwa katika kiwango ambacho madaktari watakuwa wamekubaliana nacho! Na hii ni katika hospitali zote, za rufaa, za mikoa na wilaya, za kata na za vijijini.

      Hapa ndipo ninapopata taabu ya kuelewa maana ya vikao vya muafaka; vikao hivi vinapaswa viwe na 'critical path' . Kuwe na mtiririko wa matukio, kuanzia hapa tulipo hadi kule tunakotaka kwenda; na nani anahusika na katika suala lipi na anapaswa alitekeleze ndani ya muda gani.

      Vinginevyo vitakuwa kama vikao vya migahawani ambavyo mwisho wa siku watu hukung'uta miguu, na kuamka kesho yake kuwa kama ilivyokuwa jana yake! Hatua tisa mbele, na kumi nyuma!

      Na makubaliano haya yawe ya kimaandishi, na mintaarafu kwa kuwa ni masuala ya kitaifa basi nasi wananchi yapaswa tuelezwe maendeleo yake...ili tuweze kuhoji.


      Vinginevyo watu watabaki kuwa na kizungumkuti na kufikiri kuwa mgomo wa madaktari umechochewa na haja ya madaktari kudai maslahi bora pekee; kumbe nia yao ...ambayo kwa wananchi wengi iko nyuma ya pazia ni kudai maslahi na hali bora ya sekta nzima ya afya hapa Tanzania. Hatuhitaji mama Kijo Bisimba, ama mama Ananilea Nkya kufafanua haja hii nyeti na muhimu (huduma bora, vifaa bora, hali bora) siku ya kumsafirisha Dr. Ulimboka kwenda nje kwa matibabu. Mungu Ibariki Tanzania!
      tripojo likes this.
      Mswahili jambo la kipumbavu likisemwa kizungu, anaona sawasawa kabisa!! J.K.Nyerere

    16. #14
      Remote's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2011
      Posts : 4,281
      Rep Power : 1364
      Likes Received
      952
      Likes Given
      182

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      watanzania nani katurog.. Nasema hapana tumezidisha upole what is the way forwad, TISS,ikulu na polisi intakiwa itueleze kinaganaga

    17. #15
      zubedayo_mchuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2011
      Posts : 3,358
      Rep Power : 1062
      Likes Received
      590
      Likes Given
      43

      Default

      Quote By Lukolo
      Tungependa kupata waandishi wa habari shujaa watakaoweza kuweka hizi story kwenye magazeti na kwenye redio, ili kila mwananchi ajue serikali ya Kikwete ni serikali ya aina gani. Yafaa pia taarifa kama hii ifikishwe kwenye vyama vya wanaharakati, ili wasiendelee kusema watu wasiojulikana bali waseme moja kwa moja kwamba alitekwa na kuumizwa na serikali, ieleweke moja.
      Ukiona mwenzako ananyolewa na wewe tia maji...
      Mhandishi gani huyo wa kuandika haya TZ.

    18. #16
      mhalisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2011
      Posts : 565
      Rep Power : 601
      Likes Received
      140
      Likes Given
      121

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      serikali ya Kikwete ni serikali ya kishetani. wako wapi wale waliosema Kikwete ni chaguo la Mungu?
      waliomtendea Dk.Ulimboka unyama huu hakika laana hiyo itawaandama maisha yao yote na vizazi vyao vyote.
      tripojo, bemg and Marumia like this.

    19. #17
      Mujumba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2011
      Location : Soweto
      Posts : 847
      Rep Power : 592
      Likes Received
      266
      Likes Given
      118

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      this should be a good lesson to other vimbelembele....lazima mjue nchi haichezewi hovyo hovyo eboo
      "The past is a rich resource on which we can draw in order to make decisions for the future, but it does not dictate our choices. We should look back at the past and select what is good, and leave behind what is bad".Nelson Mandela<!--EndFragment-->

    20. #18
      Money stunna's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th August 2011
      Location : BeechGrove City,Indianapolis
      Posts : 2,804
      Rep Power : 954
      Likes Received
      814
      Likes Given
      526

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      alipata mateso makubwa,kutolewa jino bila ganzi uwi sipat picha,apone haraka

    21. #19
      dguyana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th January 2011
      Posts : 426
      Rep Power : 508
      Likes Received
      109
      Likes Given
      66

      Default re: UHALISIA: Kilichomtokea Dr. Ulimboka mwanzo-mwisho...

      Quote By Mundu
      Hata wabunge wa upinzani naona ni wanafiki tu katika suala hili la mgomo wa madakatari...kwanini wasigome kuingia bungeni kushinikiza Serikali kutatua tatizo la mgomo wa madaktari upesi.

      Kama ni suala la maslahi hilo ni jepesi na sioni kwa nini Serikali inasuasua kulitatua... Lakini suala la maboresho, hilo ni suala la mipango...lahitaji muda kwani hata kama ni ununuzi wa vifaa ama upanuzi na uboreshaji wa majengo hauwezi kufanyika kwa muda mchache...na ni suala linalogusa maendeleo ya Sekta ya utabibu Tanzania nzima, hususani vijijini. Niliangalia documentary moja, katika kituo kimoja cha TV hapa nchini, kuna hospitali/despensari moja kijijini ambayo inategemewa na watu wengi, hususan akina mama, haina umeme, wagonjwa huitajika kwenda na mafuta ya taa ili wapatiwe huduma nyakati za usiku. Hakuna pia maji na hakuna dawa. Ni gharika kupata huduma katika dispensari ile.

      Sasa kama ni tatizo la maboresho ya miundo mbinu...sijui katika kile kikao cha muafaka na Pinda walipeana ultimatum ama vipi? Sikumbuki kama nilipata kusikia ama kusoma mahali popote kuwa walipeana muda fulani kuhakikisha masuala haya ya miundo mbinu ama yaananza kushughulikiwa , ama yawe yamefikiwa katika kiwango ambacho madaktari watakuwa wamekubaliana nacho! Na hii ni katika hospitali zote, za rufaa, za mikoa na wilaya, za kata na za vijijini.

      Hapa ndipo ninapopata taabu ya kuelewa maana ya vikao vya muafaka; vikao hivi vinapaswa viwe na 'critical path' . Kuwe na mtiririko wa matukio, kuanzia hapa tulipo hadi kule tunakotaka kwenda; na nani anahusika na katika suala lipi na anapaswa alitekeleze ndani ya muda gani.

      Vinginevyo vitakuwa kama vikao vya migahawani ambavyo mwisho wa siku watu hukung'uta miguu, na kuamka kesho yake kuwa kama ilivyokuwa jana yake! Hatua tisa mbele, na kumi nyuma!

      Na makubaliano haya yawe ya kimaandishi, na mintaarafu kwa kuwa ni masuala ya kitaifa basi nasi wananchi yapaswa tuelezwe maendeleo yake...ili tuweze kuhoji.


      Vinginevyo watu watabaki kuwa na kizungumkuti na kufikiri kuwa mgomo wa madaktari umechochewa na haja ya madaktari kudai maslahi bora pekee; kumbe nia yao ...ambayo kwa wananchi wengi iko nyuma ya pazia ni kudai maslahi na hali bora ya sekta nzima ya afya hapa Tanzania. Hatuhitaji mama Kijo Bisimba, ama mama Ananilea Nkya kufafanua haja hii nyeti na muhimu (huduma bora, vifaa bora, hali bora) siku ya kumsafirisha Dr. Ulimboka kwenda nje kwa matibabu. Mungu Ibariki Tanzania!
      Halafu wakigoma kuingia ndio muanze kusema chadema inahusika sio? Serikali yako ni DHAIFU!!!!
      Changudoa mwenye wivu a.k.a Jambazi lenye huruma

    22. #20
      Kiby's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th November 2009
      Posts : 3,506
      Rep Power : 1190
      Likes Received
      599
      Likes Given
      33

      Default

      Quote By Lukolo
      Tungependa kupata waandishi wa habari shujaa watakaoweza kuweka hizi story kwenye magazeti na kwenye redio, ili kila mwananchi ajue serikali ya Kikwete ni serikali ya aina gani. Yafaa pia taarifa kama hii ifikishwe kwenye vyama vya wanaharakati, ili wasiendelee kusema watu wasiojulikana bali waseme moja kwa moja kwamba alitekwa na kuumizwa na serikali, ieleweke moja.
      .
      Hivi gazeti la Kubenea litatoka lini? Nalisubiri kwa hamu kwani ndilo lenye uthubutu thabiti!!
      .

    Page 1 of 17 12311 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...