Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

    Report Post
    Page 1 of 7 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 121
    1. #1
      Mongoiwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Posts : 478
      Rep Power : 669
      Likes Received
      51
      Likes Given
      23

      Default Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Leo Jumamosi, Juni 30, aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, atakuwa na mkutano wa hadhara Ilala Bungoni.

      Vyanzo vyangu vya habari, kutoka karibu na Lema vinasema kuwa leo atalipuka sana. Mojawapo ya masuala atakayolipua ni kuwataja vigogo/kigogo waliohusika katika suala la Dkt. Ulimboka.

      Jamani wenzetu wa habari, sijui vyombo vingapi viko maeneo hayo, mtupatie taarifa hizi mapema iwezekanavyo kama ni kweli. Hatuwezi kusubiri mpaka kesho au usiku.

      Nawasilisha.
      Elli, Saint Ivuga, Nyunyu and 6 others like this.
      Nchi yangu inaangamia kwa kukosa maarifa ya Viongozi

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Kayoka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Posts : 427
      Rep Power : 490
      Likes Received
      94
      Likes Given
      2

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      anaingilia uhuru wa jeshi la polisi, wacha naye atulie huku tukimwomba mungu amponyeshe mapema dr. Ulli aje awataje waliomteka na kumuumiza.

    4. #3
      Kiumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th February 2012
      Posts : 484
      Rep Power : 464
      Likes Received
      77
      Likes Given
      0

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Jembe letu hilo. Eti pimbi wewe ndio msangi nini?

    5. #4
      MMASSY's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 98
      Rep Power : 443
      Likes Received
      10
      Likes Given
      12

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Wewe unayemwitalema pimbi inawezekana kweli wewe ni msangi!!

    6. #5
      thatha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 5,050
      Rep Power : 0
      Likes Received
      227
      Likes Given
      1

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni


      Madaktari 146 watimuliwa kwa mgomo Send to a friend
      Saturday, 30 June 2012 10:04
      0digg

      Mgonjwa akiwa nje ya geti la Taasisi ya Mifupa MOI jijini Dar es Salaam jana akiwa ajui chakufanya baada kukuta geti hilo limefungwa kutokana na mgomo wa madaktari unaoendelea nchini.Picha na Venance Nestory

      Waandishi Wetu
      MADAKTARI 146 wamefukuzwa katika hospitali mbalimbali nchini kutokana na kushiriki mgomo unaoendelea nchi nzima kwa lengo la kuishinikiza Serikali kutekeleza madai yao.

      Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa, madaktari hao walitimuliwa katika Hospitali za Bugando na Sekou Toure mkoani Mwanza na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya na ile ya Rufaa Dodoma.

      Wakati Serikali ikichukua hatua hiyo, mgomo huo jana uliendelea katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Ocean Road, Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) za jijini Dar es Salaam, Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na Hospitali ya Rufaa ya KCMC mkoani Kilimanjaro.

      Katika kile kinachoonekana kuwaunga mkono wenzao, madaktari bingwa wa MOI, MNH na Ocean Road jijini Dar es Salaam, jana walitangaza rasmi kuingia kwenye mgomo huo hadi madai hayo yatekelezwe.

      Madai ya madaktari ni hali bora ya mazingira ya utoaji huduma nchini, ongezeko la mishahara, posho za kufanya kazi katika mazingira magumu, posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi na posho za kuitwa kazini.

      Tamko la madaktari hao bingwa, lilitolewa jana na msemaji wao, Dk Catherine Mng'ong'o muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao chao kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

      Tamko hilo limekuja siku moja baada ya baadhi yao kuanza kushiriki mgomo huo juzi, kushinikiza pamoja na mambo mengine, Serikali itoe tamko juu ya tukio la kutekwa na kujeruhiwa kwa Dk Ulimboka.

      Hata hivyo, wakati madaktari hao wakitoa tamko hilo, uongozi wa Moi jana ulitoa tangazo kuwataka madaktari wote walioshiriki mgomo huo kurejea kazini ifikapo Julai 2, mwaka huu, vinginevyo watafukuzwa kazi.

      Jana jengo la MOI lilikuwa limefungwa kwa makufuli, huku wagonjwa wakielezwa kuwa huduma zote hazitolewi zikiwamo za dharura ambazo awali ziliendelea kutolewa.
      Mmoja wa walinzi aliwambia waandishi wa habari kuwa, amefunga mageti kutokana na amri ya mkuu wake wa kazi.
      “Mimi ninatekeleza amri ya bosi wangu, amenitaka kufunga geti na hakuna mtu kuingia, awe mgonjwa au ninyi waandishi wa habari kwa kuwa hakuna huduma zinazotolewa humu,” alisema.
      Mkoani Mwanza
      Madaktari 63 walio katika mafunzo ya vitendo kazini wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Hospitali ya Mkoa Sekou Toure wametimuliwa na kurejeshwa wizarani kutokana na mgomo huo.

      Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Dk Charles Majinge alisema kuwa, juzi aliwataka madaktari waliokuwa katika mgomo kurejea kazini, lakini hawakufanya hivyo na jana akaamua kuwarejesha 47 wizarani.

      Katika Hospitali hiyo ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure, Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk Valentino Bangi alisema, madaktari 16 wamesimamishwa kufanya kazi kutokana na agizo la wizara.

      Kilimanjaro

      Madaktari walioko kwenye mgomo katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro walisema jana kuwa, kinachofanywa na Serikali kuwafukuza kazi waliogoma, ni njia mojawapo ya vitisho, lakini wakasema kuwa kamwe hawataogopa.

      Madaktari hao ambao hawakutaka majina yao yaandikwe gazetini walisema, wao wanaendelea na mgomo mpaka pale Serikali itakapotekeleza madai yao.

      “Tumesikia wenzetu wa Dodoma na Mbeya wamefukuzwa ….Hiyo haitufanyi turudi kazini na kama Serikali inaona hiyo ndiyo njia ya kumaliza mgogoro huu waendelee sisi tutarudi kazini pale itakapotimiza tunayotaka,” alisema mmoja wa madaktari hao.

      Mbeya

      Juzi Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, ilitoa tangazo la kuwataka madaktari waliopo mafunzoni waliogoma kurejea kazini jana, na endapo wangekiuka agizo hilo wangekuwa wamejifukuzisha kazi. Na hadi jana jioni hospitali hiyo ilikuwa imewafukuza madaktari 72.

      Ocean Road

      Katika Taasisi ya Taifa ya Saratani, (Ocean Road), kutokana na madaktari sita kusitisha kutoa huduma tangu Dk Ulimboka alipojeruhiwa kwa kipigo, waligoma na jana Mkurugenzi wa Tiba na Huduma Diwani Musemo alionekana akitembelea wagonjwa.

      Dodoma
      Madaktari 11 wa mafunzo kwa vitendo katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma nao wamefukuzwa, tukio ambalo jana lilileta usumbufu mkubwa katika upatikanaji wa tiba hospitalini hapo.
      “Kwa hakika matibabu yanaendelea ingawa ni katika hali ya kusuasua. Hatuna uhakika kama kweli kuna mgomo wa chinichini au la, maana mimi nimefika mapema, lakini bado sijahudumiwa," alisema mmoja wa wagonjwa waliozungumza na mwandishi wa habari.
      Arusha
      Katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, huduma zimedorora lakini Mganga Mkuu, Dk Omar Chande alisema jana kuwa, imekuwa ni vigumu kuchukua hatua kuwabana madaktari ambao wanatuhumiwa kufanya mgomo baridi, kwani wote wanaripoti kazini.

      "Ni kweli kuna taarifa hizi za kuwapo mgomo baridi, lakini madaktari wote wapo kazini, ila kama kuna kufanya kazi chini ya kiwango, tumeanza uchunguzi," alisema Dk Chande.
      Amana

      Katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam utoaji wa huduma ulisuasua kutokana na mgomo huo jambo lililofanya uongozi kuweka tangazo kwenye Ofisi ya Mganga Mkuu kuwataka watumishi wote ambao hawakuwapo kazini kuanzia Juni 25, 2012 waandike barua za kurejea kazini.

      Tangazo hilo pia linawataka madaktari walioko mafunzoni kuandike barua kwenda kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia kwa mganga mkuu wa hospitali hiyo.


      Habari hii imeandaliwa na Frederick Katulanda, Mwanza, Rehema Matowo, Moshi, Zakhia Abdallah (SJMC), Editha Majura, Israel Mgussi, Dodoma), Victoria Mhagama na Daniel Mwingira, Sam Jacob na Issa lazaro (SJMC, Godfrey Kahango, Mbeya, na Mussa Juma, Arusha.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Elli's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Kijito-Upele
      Posts : 8,571
      Rep Power : 2551
      Likes Received
      2142
      Likes Given
      1862

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      "Solidarity should also mean insistence on the rule of law. To close one's eyes to trampled freedoms, to get used to violence, become inured to political murders, is to approve them and accept that there are people deserving of justice and others deserving of oppression." Utapona Kaka Ulimboka
      MANI and gfsonwin like this.
      ...but what MAN is entirely without Evil intent in the Silence of his Soul???

    9. #7
      thatha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 5,050
      Rep Power : 0
      Likes Received
      227
      Likes Given
      1

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni


      Madaktari 146 watimuliwa kwa mgomo Send to a friend
      Saturday, 30 June 2012 10:04
      0digg

      Mgonjwa akiwa nje ya geti la Taasisi ya Mifupa MOI jijini Dar es Salaam jana akiwa ajui chakufanya baada kukuta geti hilo limefungwa kutokana na mgomo wa madaktari unaoendelea nchini.Picha na Venance Nestory

      Waandishi Wetu
      MADAKTARI 146 wamefukuzwa katika hospitali mbalimbali nchini kutokana na kushiriki mgomo unaoendelea nchi nzima kwa lengo la kuishinikiza Serikali kutekeleza madai yao.

      Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa, madaktari hao walitimuliwa katika Hospitali za Bugando na Sekou Toure mkoani Mwanza na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya na ile ya Rufaa Dodoma.

      Wakati Serikali ikichukua hatua hiyo, mgomo huo jana uliendelea katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Ocean Road, Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) za jijini Dar es Salaam, Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na Hospitali ya Rufaa ya KCMC mkoani Kilimanjaro.

      Katika kile kinachoonekana kuwaunga mkono wenzao, madaktari bingwa wa MOI, MNH na Ocean Road jijini Dar es Salaam, jana walitangaza rasmi kuingia kwenye mgomo huo hadi madai hayo yatekelezwe.

      Madai ya madaktari ni hali bora ya mazingira ya utoaji huduma nchini, ongezeko la mishahara, posho za kufanya kazi katika mazingira magumu, posho za kufanya kazi katika mazingira hatarishi na posho za kuitwa kazini.

      Tamko la madaktari hao bingwa, lilitolewa jana na msemaji wao, Dk Catherine Mng'ong'o muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao chao kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

      Tamko hilo limekuja siku moja baada ya baadhi yao kuanza kushiriki mgomo huo juzi, kushinikiza pamoja na mambo mengine, Serikali itoe tamko juu ya tukio la kutekwa na kujeruhiwa kwa Dk Ulimboka.

      Hata hivyo, wakati madaktari hao wakitoa tamko hilo, uongozi wa Moi jana ulitoa tangazo kuwataka madaktari wote walioshiriki mgomo huo kurejea kazini ifikapo Julai 2, mwaka huu, vinginevyo watafukuzwa kazi.

      Jana jengo la MOI lilikuwa limefungwa kwa makufuli, huku wagonjwa wakielezwa kuwa huduma zote hazitolewi zikiwamo za dharura ambazo awali ziliendelea kutolewa.
      Mmoja wa walinzi aliwambia waandishi wa habari kuwa, amefunga mageti kutokana na amri ya mkuu wake wa kazi.
      “Mimi ninatekeleza amri ya bosi wangu, amenitaka kufunga geti na hakuna mtu kuingia, awe mgonjwa au ninyi waandishi wa habari kwa kuwa hakuna huduma zinazotolewa humu,” alisema.
      Mkoani Mwanza
      Madaktari 63 walio katika mafunzo ya vitendo kazini wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Hospitali ya Mkoa Sekou Toure wametimuliwa na kurejeshwa wizarani kutokana na mgomo huo.

      Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Dk Charles Majinge alisema kuwa, juzi aliwataka madaktari waliokuwa katika mgomo kurejea kazini, lakini hawakufanya hivyo na jana akaamua kuwarejesha 47 wizarani.

      Katika Hospitali hiyo ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure, Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk Valentino Bangi alisema, madaktari 16 wamesimamishwa kufanya kazi kutokana na agizo la wizara.

      Kilimanjaro

      Madaktari walioko kwenye mgomo katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro walisema jana kuwa, kinachofanywa na Serikali kuwafukuza kazi waliogoma, ni njia mojawapo ya vitisho, lakini wakasema kuwa kamwe hawataogopa.

      Madaktari hao ambao hawakutaka majina yao yaandikwe gazetini walisema, wao wanaendelea na mgomo mpaka pale Serikali itakapotekeleza madai yao.

      “Tumesikia wenzetu wa Dodoma na Mbeya wamefukuzwa ….Hiyo haitufanyi turudi kazini na kama Serikali inaona hiyo ndiyo njia ya kumaliza mgogoro huu waendelee sisi tutarudi kazini pale itakapotimiza tunayotaka,” alisema mmoja wa madaktari hao.

      Mbeya

      Juzi Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, ilitoa tangazo la kuwataka madaktari waliopo mafunzoni waliogoma kurejea kazini jana, na endapo wangekiuka agizo hilo wangekuwa wamejifukuzisha kazi. Na hadi jana jioni hospitali hiyo ilikuwa imewafukuza madaktari 72.

      Ocean Road

      Katika Taasisi ya Taifa ya Saratani, (Ocean Road), kutokana na madaktari sita kusitisha kutoa huduma tangu Dk Ulimboka alipojeruhiwa kwa kipigo, waligoma na jana Mkurugenzi wa Tiba na Huduma Diwani Musemo alionekana akitembelea wagonjwa.

      Dodoma
      Madaktari 11 wa mafunzo kwa vitendo katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma nao wamefukuzwa, tukio ambalo jana lilileta usumbufu mkubwa katika upatikanaji wa tiba hospitalini hapo.
      “Kwa hakika matibabu yanaendelea ingawa ni katika hali ya kusuasua. Hatuna uhakika kama kweli kuna mgomo wa chinichini au la, maana mimi nimefika mapema, lakini bado sijahudumiwa," alisema mmoja wa wagonjwa waliozungumza na mwandishi wa habari.
      Arusha
      Katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, huduma zimedorora lakini Mganga Mkuu, Dk Omar Chande alisema jana kuwa, imekuwa ni vigumu kuchukua hatua kuwabana madaktari ambao wanatuhumiwa kufanya mgomo baridi, kwani wote wanaripoti kazini.

      "Ni kweli kuna taarifa hizi za kuwapo mgomo baridi, lakini madaktari wote wapo kazini, ila kama kuna kufanya kazi chini ya kiwango, tumeanza uchunguzi," alisema Dk Chande.
      Amana

      Katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam utoaji wa huduma ulisuasua kutokana na mgomo huo jambo lililofanya uongozi kuweka tangazo kwenye Ofisi ya Mganga Mkuu kuwataka watumishi wote ambao hawakuwapo kazini kuanzia Juni 25, 2012 waandike barua za kurejea kazini.

      Tangazo hilo pia linawataka madaktari walioko mafunzoni kuandike barua kwenda kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia kwa mganga mkuu wa hospitali hiyo.


      Habari hii imeandaliwa na Frederick Katulanda, Mwanza, Rehema Matowo, Moshi, Zakhia Abdallah (SJMC), Editha Majura, Israel Mgussi, Dodoma), Victoria Mhagama na Daniel Mwingira, Sam Jacob na Issa lazaro (SJMC, Godfrey Kahango, Mbeya, na Mussa Juma, Arusha.

    10. #8
      mpepalilambo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th June 2012
      Posts : 72
      Rep Power : 362
      Likes Received
      8
      Likes Given
      3

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Quote By mongoiwe
      leo jumamosi, juni 30, aliyekuwa mbunge wa arusha mjini na mjumbe wa kamati kuu ya chadema, godbless lema, atakuwa na mkutano wa hadhara ilala bungoni.

      Vyanzo vyangu vya habari, kutoka karibu na lema vinasema kuwa leo atalipuka sana. Mojawapo ya masuala atakayolipua ni kuwataja vigogo/kigogo waliohusika katika suala la dkt. Ulimboka.

      Jamani wenzetu wa habari, sijui vyombo vingapi viko maeneo hayo, mtupatie taarifa hizi mapema iwezekanavyo kama ni kweli. Hatuwezi kusubiri mpaka kesho au usiku.

      Nawasilisha.
      jambawazi na siasa wapi nawapi? Ubabaishaji mtupu

    11. #9
      nndondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st February 2010
      Posts : 618
      Rep Power : 688
      Likes Received
      149
      Likes Given
      1

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Na ataje tu hatuna sababu ya kusubiri lolote, na pili naomba tafadhali nirudie madaktari wateua wajumbe wa tume yao iunganike na waandishi mahiri wa investigative reporting wafanye utafiti na kutoa matokea, mimi najitolea kuwemo kwenye tume hiyo na haraka sana matokeo yatolewe kwa kupitia press conference. Tunaomba hamasisheni marafiki zetu wote wa ndani na nje kwa kazi hii

    12. #10
      adolay's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th December 2011
      Posts : 1,664
      Rep Power : 777
      Likes Received
      504
      Likes Given
      504

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Subira yavuta kheli, kama lema anao ushahidi pasipo kuacha masha basi na awataje, kama hana bora kunyamaza, wapuuzi huko serikalin wanatafuta pa kuficha aibu. wanasubili mtu ajichanganye waendeleze ufashit na udikiteta wao. Hawanason kwao wauwaji na mafisadi huitwa makada.
      Kibakamande likes this.

    13. #11
      mpepalilambo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th June 2012
      Posts : 72
      Rep Power : 362
      Likes Received
      8
      Likes Given
      3

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Quote By kiumbo
      jembe letu hilo. Eti pimbi wewe ndio msangi nini?
      toka lini jambazi akaweza siasa? Kama ni jembe lenu kweli basi hamna watu.
      Wakuti likes this.

    14. #12
      chitalula's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 428
      Rep Power : 519
      Likes Received
      88
      Likes Given
      40

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      bora nngezaliwa afghanstan kwenye vita kuliko huku kwenye uuaji wa wazi unaofanywa na serikali
      Unstoppable and Kibakamande like this.

    15. #13
      dguyana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th January 2011
      Posts : 426
      Rep Power : 508
      Likes Received
      109
      Likes Given
      66

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Jamaa ni Mafia haogopi ndio maana JK anamgwaya pia. Big up Lema go go go Lema
      Changudoa mwenye wivu a.k.a Jambazi lenye huruma

    16. #14
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,698
      Rep Power : 1915
      Likes Received
      1596
      Likes Given
      677

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Quote By mpepalilambo
      toka lini jambazi akaweza siasa? Kama ni jembe lenu kweli basi hamna watu.
      Ni kweli mkuu ni bonge la jambazi hata zile pesa kule bank za uswisi ni zake alituibia hata ujambazi wa EPA na Rada alishiriki kweli lema ni jambazi la kimataifa
      Kibakamande likes this.

    17. #15
      Emma.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2012
      Posts : 865
      Rep Power : 521
      Likes Received
      111
      Likes Given
      0

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Kamanda anajua siri zote za ccm hata swala la kuwekwa kura kwenye chupa za chai arumeru yeye alitoa ile siri ndo nasema serikal inahusika kwa 99.9%
      mpiganaji86 likes this.

    18. #16
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,136
      Rep Power : 14291
      Likes Received
      4019
      Likes Given
      3281

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Quote By Emma.
      Kamanda anajua siri zote za ccm hata swala la kuwekwa kura kwenye chupa za chai arumeru yeye alitoa ile siri ndo nasema serikal inahusika kwa 99.9%
      kamanda rejea walaka wa lema kwenda kwa dr dr dr Kikwete




      Ndugu Wananchi;


      Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi na shukrani nyingi kwa ndugu zetu wa Arusha kwa kuwapokea vizuri na kuwakarimu vyema wageni wetu hao. Nawaomba waendelee na moyo huo mpaka watakapoondoka wote. Naomba kuwepo kwa mkutano huu kuwakumbushe umuhimu wa mji wenu kuwa tulivu. Miaka miwili iliyopita isingekuwa rahisi kwa watu au shirika kubwa la kimataifa kama Benki hii kuamua kufanya mkutano wake Arusha. Isitoshe hata sisi wenyewe tusingeshawishika kuomba au kukubali maombi ya namna hiyo. Lakini sasa imewezekana. Naomba kila mmoja wetu aweke azimio moyoni mwake la kuhakikisha kuwa hali ile haijirudii tena. Nyota ya Geneva ya Afrika lazima iendelee kuangaza. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo
      . ( J.K . KIKWETE.)

      “Narudia tena , IKULU iliingilia kesi yangu ya Ubunge”.


      Mh Rais nimekusikiliza kwa makini sana ila nakupa pole kwani bado unafikiri unaongea na Tanzania ya mwaka 1961 , umesema sasa Arusha ni shwari tofauti na miaka miwili iliyopita kwani sasa kuna amani na utulivu wa kutosha ndio maana hata mkutano wa AFDB umefanyika Arusha .


      Mh Rais , najua IKULU iliingilia kesi yangu kama ilivyoonekana na ndio sababu hata Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakati anaapisha Wakuu wa Wilaya alimpongeza Jaji kwa hukumu nzuri aliyowafurahisha wakati kesi hiyo iko mahakama ya Rufaa , lakini jambo moja la msingi ambalo huwezi kulitambua kwa sasa ni kuwa Haki na Ukweli haviwezi kushindwa na dhuluma, ubaya wala mamlaka , natambua wewe ni Rais na unayo mamalaka makubwa katika Taifa hili lakini vile vile nataka utambue kuwa huna mamlaka makubwa dhidi ya haki , utu na ukweli.


      Mh Rais hakuna Amani Duniani inayozidi Haki na usawa ,utu na ukweli , haipo na wala haitakuwepo , ndio maana kila siku nasema ni
      “Afadhali Vita Inayotafuta Haki na usawa kuliko Amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa Mwanadamu “ umefurahia sana mkutano uliokupa fursa ya kutoa maneno ya kebehi na kudhihirisha ila chafu iliyofanywa na Serikali yako na kujaribu kuhadaa Umma kama ilivyo kawaida ya Serikali yako na Chama chako , hata hivyo wakati huu kuna mambo ya msingi yakushughulikia zaidi ya kebehi na hadaa , Uchumi wa Nchi umeyumba, huduma za msingi za jamii zimepuuzwa, Mpasuko katika suala la Muungano na vururugu zinazoendelea Zanzibar , mfumuko wa bei hizi ni sababu chache ambazo haziwezi kuruhusu wakati huu kuwa wakati wa kebehi na mizaha isipokuwa kazi .

      Mh Rais , Mama Theresa , Nelson Mandela , Martin Luther Jr na Malcom X hawakuwa Wabunge kupigania haki za Nchi yao na watu wao , sihitaji Ubunge kupigania ukweli, haki na utu , nahitaji dhamira safi , nia njema na huu utakuwa wajibu wangu mpaka nakwenda kaburini , nitakapomaliza mbio hizi najua nitapata fursa ya kutazama nyuma yangu nione nini nilifanya , ukweli nisingependa kuona vituo vya mafuta , magorofa , magari na viwanja vingi kila kona ya Nchi bali Haki ,Usawa na utu vikiwa kama nguzo ya imani ya watawala wetu watakaokuwepo, pengine sitaishi miaka mingi sana kama utachukizwa sana na waraka wangu huu kwani Polisi , Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi wanakutii wewe , hata hivyo siogopi kufa kwani nisipokufa kesho , nitakufa siku moja ambayo siijui , napenda kuishi maisha marefu nimwone mke wa mtoto wangu kama itawezekana , lakini kuliko iwezekane kwa kuishi kwa hofu ni bora ishindakane kwa kuthamini haki , kwa hiyo kama utakuwa umekasirika sana , unaweza kufanya jambo lolote baya kwa kutumia mamlaka yako , niko tiyari sio kesho wala leo isipokuwa sasa hivi, najua IKULU imewazulumu watu wa Arusha Mbunge wao.


      Mh Rais ninajua wazi njama zote na hasira hizi zinaweza kuwa zimetokana hasa na mkutano tuliokaa Osterbay Dar mimi na wewe kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 hata hivyo sikupuuza maongezi yetu isipokuwa nilichagua kufuata dhamira yangu na wito wangu wa utumishi wa kweli katika Jimbo langu na Nchi yangu.


      Mh Rais nimekuelewa na Wananchi wamekuelewa kila mahali , wewe ni Rais unayo mamlaka makubwa na mimi ni mwananchi mamlaka yangu makubwa ni kwa mke wangu tu , sina Polisi wala Usalama wa Taifa lakini nitawaomba wanyonge wafunge na kusali tuone kama mamlaka yako inaweza kushindana na haki na ukweli .


      Mh Rais
      “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri” Serikali na Chama cha Mapinduzi kimepuuza watu na haki zao kwa muda mrefu , lakini wakati umefika ambapo hawatapuuzwa tena hata hivyo kwa kauli yako hii naamnini haiwezi kuwafundisha kazi majaji wa mahakama ya rufaa .

      ONLY TIME WILL TELL”.


      Tafakari chukua hatua
      Ontuzu, Mkono and Kibakamande like this.
      Nobody can give you freedom. Nobody can give you equality or justice or anything. If you're a man, you take it.... Malcolm X Nasubiri 'breaking news... '





    19. #17
      MASIKITIKO's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th December 2011
      Posts : 205
      Rep Power : 478
      Likes Received
      28
      Likes Given
      2

      Default

      [QUOTE=rais wa tano;4150700]
      [TABLE="class: contentpaneopen"]
      [TR]
      [TD="class: contentheading, width: 100%"] Madaktari 146 watimuliwa kwa mgomo [/TD]
      [TD="class: buttonheading, width: 100%, ali
      KWANI LAZIMA KUAJILIWA NA HOSPITAL ZA SERIKALI

    20. #18
      Kiby's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th November 2009
      Posts : 3,504
      Rep Power : 1189
      Likes Received
      599
      Likes Given
      33

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      mimi toka Mwakyembe ataje maofisa wa serikali waliokuwa wamepangwa kumuua na kutoa ushahidi wa aina ya magari na namba waliyotumia na ni nani kawapokea na ni wapi walishukia na akaweka wazi kuwa yupo tayari kuisaidia polisi zaidi kama atahitajika, sina tena imani na hii serikali anymore. Nikikumbuka pia issue ya Bilali, Zombe na kesi ya Mahanga, ni dhahiri na haki kabisa kwa serikali ya ccm kusulubiwa.
      .

    21. #19
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,877
      Rep Power : 1978
      Likes Received
      2357
      Likes Given
      3047

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Suala la Dr Ulimboka unamsubiri Lema akuambie wakati inajulika wazi ACP Hemed Msangi ndiye mhusika mkuu.
      muonamambo and Unstoppable like this.

    22. #20
      Zak Malang's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th December 2008
      Posts : 4,835
      Rep Power : 1922
      Likes Received
      187
      Likes Given
      2

      Default Re: Lema kuwataja waliomteka Dk. Ulimboka leo Ilala Bungoni

      Kwa nini nynyiemu mnam-hara huyu Lema. Akitamka kitu tu matumbo yenu yatonanayo na mapesa ya ufisadi yanaendesha na mnakimbilia chooni.

      Walafi wakubwa. Jambawazi Na 1 ni Mkuu wa Kaya, ndiye alipotufikisha hapa tulipo.

    Page 1 of 7 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...