Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

    Report Post
    Page 4 of 8 FirstFirst ... 23456 ... LastLast
    Results 61 to 80 of 155
    1. #1
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By NYENJENKURU
      Unakumbuka alipotolewa high table Nkrumah hadi akupoteza kiatu, jamaa alikuwa mkorofi sana, watu wanamvuta aondoke yeye akashikilia meza kidogo aanguke nayo kwenye stage, i think it was 1991 or 92 kama sikosei.
      Quote By NYENJENKURU
      Yaani kuna vijana walioshiriki kumshusha huyo jamaa na kule FOE kaanza kumuita MUTUNGILAHELA aka Mnyamrenge..Siku hizi wengi ni Ma senior Engineers ukiwakumbusha wancheka sanaaaaa...kama John Peter...JP nk

      Thread hii inatofautiana na ile nyingine ya kuuliza kuhusu aliko Benedict Mutungirehi, aliyekuwa mbunge na sasa hatujui yuko wapi.

      {http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la...ia-wapi-3.html}


      Nimeamua kuweka thread mpya ili wengi wajue chanzo cha matukio yale kwa faida ya historia.

      Unajua hata wengi hawafahamu relation ya vijana wale wa Engineering (FOE) na kundi lililomtoa Mutungirehi pale stejini. Haya ni makundi mawili tofauti yaliyounganishwa na ile nia ya kumuondoa Mutungirehi.

      Sakata ya Mutungirehi ilitokea mwishoni mwa October 1994, lakini ili uielewe vizuri inabidi uanze na matukio ya tangu April 1994 yaani miezi sita nyuma. Mimi nilikuwa namalizia first year pale Engineering na hivyo ninalikumbuka suala hili vizuri sana.

      Kwa nini nianzie nyuma vile? Ni kwa sababu ninataka kuweka hisoria sawa kwani baadhi wanapotosha na wanajifanya siku hizi ni wapiganaji kwelikweli.

      Tuanze sasa maelezo. Mwezi April 1994 nikiwa first Year pale FOE tulikuwa na somo linaitwa Engineering Mathematics ambayo ilikuwa inafundishwa na walimu toka Mathematics depertment. Wakati huo ndiyo amemaliza kufunidha topics ngumu kichizi kama vile divergence, curl na kadhalika.

      Kisha yule lecture akatoa test ambayo ilikuwa ngumu haina mfano kwani mtu unafika mwisho wa time hujafanya swali hata moja. Lecture akatangaza kwamba muda wa paper umeisha. Mimi nilikuwa nachukua Civil Engineering nimekaa karibu na Bwana anaitwa Mziray. Mziray akaanzisha fujo kwa kumshika lecturer asikusanye zile paper.

      Mziray simkumbuki jina lake la kwanza ila najua alimaliza Kibaha High School, May 1993, akaenda JKT Oljoro na akaja UDSM. Pale Kibaha alikuwa PCM na aliondoka na Dv. One Point 5 yaani ABB.

      Kwa watu kama huyu kudhalilishwa kuibuka na zero kwenye Mathematics ilikuwa kejeli lakini ukweli ni kwamba test ilikuwa ni ngumu.

      Fujo ya Mziray zikaungwa mkono na wengi tu. Yule mwalimu akarudi Maths Dept. na huko akashitaki kwa mkuu wake yaani Prof. Masenge kwamba kafanyiwa fujo na vijana wa Engineering.

      Kumbuka ile test ndiyo ilikuwa ya mwisho wa mwaka. Si kama siku hizi nasikia wanasoma kwa semester, wakati ule test ile ilikuwa ya mwisho na kilichobaki ni tutorials chache kusubiri Unversity Exam. Vumilieni hadi mwisho maana hadi hapa hakuna connection yoyote na Mutungirehi.

      Hivyo, Prof. Masenge akato quotion kwamba Mathematics dept haitafundisha tena Engineering students hadi wa-apologise. Engineering tukakataa kuapologise.

      April ikaisha May ikaingia. May ndiyo ilikuwa mwezi wa University Exams. Tukafanya exams zingine lakini binafsi nilishapata dalili za kugoma kufanya Maths Exam. Hili niliambiwa na Marehemu Dr. Nzali ambaye nilienda kumfuata kuhusu ugonjwa wangu maana niliugua karibu niage dunia hivyo nikawa namtaarifu kuhusu unafuu wangu. Akaniambia nisijaribu kugoma.

      Kesho yake ikafika yaani siku ya Mathematics Exam. Tukaingia madarasani lakini walimu hawakuleta mitihani. Wakati huo sheria ya chuo inasema kuwa zikipita nusu saa basi unaweza kutoka nje ya chumba cha mtihani na hakuna mwingine kuingia.

      Nusu saa ikafika, tension ya wanafunzi ikaanza kupanda maana walimu hawakuja na hivyo tutaonekana first year wote hatukufanya paper na hivyo tumeji-ABSCOND.

      Tukakubaliana kuwa tutoke nje tujadili cha kufanya. Sasa hapa ndipo vurugu ya kwanza ilipoanzia. Class representatives wetu ninaowakumbuka walikuwa zaidi ya watatu yaani Lugiko Mpelwa karungubare (Chemical Engineering), Sweke (Civil Engieer), Hussein Kitilinga (Electrical Engineer). Wengine nimewasahau.

      Msiomjua Karungubare ni yule aliyegombea uenyekiti NCCR akapata kura moja na James Mbatia akashinda uenyekiti huo. Karungubare sasa hivi ni mwanachama mzuri tu wa CHADEMA.

      Wakati tumekaa pale chini hawa ma-class reps wakaitwa kujadili kwa Dean of faculty. Kumbe huko kwa Dean tayari Prof Masenge yuko huko na yule lecturer aliyefanyiwa vurugu. Binafsi sijui walifikaje kule.

      Pale chini tumeshajadili na kuamua kwamba sisi hatujagoma kufanya paper ila wao ndiyo wamekataa kuleta mtihani. Basi tukakaa tukiwa hatujui nini kitatokea. Mitihani huanza saa 3 lakini hadi wakati huo tayari ni saa 5 mchana.

      Ikafika mahala kila mmoja akaamua kuchukua uamuzi wake. Wapo walioamua kuondoka na kwenda mabwenini. Wakaulizwa “hivi nyinyi mnaondoka mtihani ukiletwa si mtakuwa mme-DISCO”. Wakajibu “fanyeni mtakavyoamua”!

      Wengine wakaamua kujiandaa na mtihani wa mchana au siku nyingine na hivyo wakabaki madarasani.

      Ilipofika nadhani saa 5:30 kumbe yale mazungumzo ya Prof. Masenge, Clas reps na daen yamemalizika na hivyo Prof. Masenge na timu yake wakaamua kugawa paper ili mtihani uanze. Wakaenda madarasani wakawakuta wale ambao walitulia kujiandaa na subjects zingine. Prof. na wenzake hawakujua kuwa kulikuwa na mtawanyiko wakagawa paper na waliomo wakaanza mtihani.

      Class reps wakaiona hali hii na waka-panic na kuja kwetu ambao tulikuwa nje. Ninayakumbuka vizuri maneno ya Karungubare kwamba “Jamani ingieni madarasani mkafanya paper maana tayari wenzetu wameshaana na zinasubiriwa tu dakika 30 milango ifungwe tusiingie tulioko nje

      Hapa ndipo likaanza sokomoko la mwaka. Binafsi nikataka kuhakikisha maneno ya Karungebare na ma-class reps wenzake. Tukaenda vyumba kadhaa. Kweli bwana wenzetu walikuwa wanafanya paper taratibu. Ingekuwa wote hatufanyi paper kwangu isingekuwa tatizo. Lakini tatizo ni pale baadhi walikuwa wanaifanya.

      Nikapiga kelele na wenzangu kadhaa nikisema “Jamani, tufanye moja kati ya mawili, ama tuwatoe kwa nguvu hawa wanaofanya paper ama tuingie na sisi tufanye”.

      Hakuna aliyejisumbua na huu ushauri wetu kwa sababu tulikuwa kama wanne tu kati ya kundi la watu zaidi ya 220. Nilipoona huu ni upuuzi nikatangaza “ni ujinga kusubiri na hivyo napanda ngazi kwenda kufanya paper nisije nikafukuzwa”. Nikaanza kupanda ngazi. Kumbe huyu Ladislaus Malima kanisikia na kuniona.

      Akanifuata amefura ajabu na kunisukuma akisema “Unajua wewe unacheza na Maisha ya watu, wale walioondoka utawafanya nini, unataka wafukuzwe”. Mimi nikajibu bila kujua kauli yangu imevutia wengi, nikasema “Wamekwenda wapi, si tulikubaliana tusiondoke. Sasa na wewe unasemaje kuhusu wanaofanya mtihani na hujawazuia”. Malima nikamzidi hoja na tension ikawa inazidi.

      Kumbe hata kundini mmojammoja akawa anachomoka na kwenda kufanya mtihani. Mimi pia nikapata nafasi nikaenda kufanya mtihani. Kumbe mtihani wenyewe ulikuwa mrahisi maana ndani ya dakika 30 nikawa nimeshanya maswali ambayo nimeshavuka passmark yaani 40%.

      Kumbe wakati tunafanya, kule nje dakika 30 zikawa zimeshapita na wakakubaliana kwamba waingie kwa nguvu kwenye vyumba vya mitihani, huko watatukuta sisi ambao kuanzia dakika hiyo tukaitwa TRAITORS, lakini wakubaliana wasitudhuru bali waichanechane mitihani ile ili ushahidi ukosekane unaoonyesha kuwa tulifanya paper na wao hawakufanya.

      Wakafanya hivyo. Lakini hawakujua wlaichokosea. Nilisema mwanzoni mtu kama mimi nilishajua tangu jana yake kuwa kungekuwa na harufu ya mgomo. Hivyo mtu ulikuwa ukiingia tu kwenye chumba cha mtihani kitu cha kwanza ilikuwa ni kuandikisha jina lako na signature. Hivyo fujo ilipoanza wale walikimbilia mitihani hawakujua kama huo ni ushahidi mwingine.


      Masenge na wenzake walichofanya wakachukua majina yote wakatoa photocopy ya majina ya wote tuliosaini, wakaacha copy kwa Dean of Engineering na original akaondoka nayo Prof. Masenge mwenyewe.

      Wakati Pro. Masenge anapanda kuondoka FOE grounds, mmoja wale wanafunzi akapata wao kwamba ushahidi wa list ya waliosaini hawana na anayo Masenge. Hivyo, akiondoka nayo wamekwisha. Wakaondoka kundi lote wakamzingira Prof. Masenge, wakamnyang’anya ile list ya majina na wakichanachana mbele yake.

      Terrible mistake hawakujua kuwa tayari kopi ipo kule kwa Dean. Hapa ndipo hawa wanafunzi 211 walipokosea na sijui kama walikuja kuligundua hili.

      Baada ya siku mbili, ikatangazwa list ya watu 72 na 211. 72 walikuwa ni sisi ambao tulifanya mtihani na tulitakiwa kuendelea kuwepo chuoni. Na wale 211 ni wale waliofanya fujo zile wakatakiwa kuondoka chuoni kwani walifukuzwa.

      Ndipo yakazuka majina mawili maarufu yaani G211 na TRAITORS. G211 walijiita hivyo kwa sababu mwaka mmoja nyuma bungeni kulikuwa na kundi la G55 la wabunge waliotaka hoja ya serikali ya Tanganyika iliyozimwa na Nyerere.

      Mimi kama na wenzangu 72 tukaendelea na Maisha ya Chuo. Wale G211 wakafungua kesi Mahakamani. Kundi la G211 lilikuwa na watu wengi sana. Nimeshamtaja Karungubare (CHADEMA), Sweke, Kitilinga ambaye sijui yuko wapi lakini mara ya mwisho alikuwa OTIS kampuni inayoshughulika na lifts za majengo.

      Wengine ni Phenihas Magesa ambaye nadhani ni Mwenyekiti wa CHADEMA mkoani Mwanza na mwaka 2009 aligombea ubunge jimbo la Busanda akashindwa na Lorencia Bukwimba wa CCM. Phenihas alikuwa kinara mzuri

      Kesi ya hawa ilendelea hadi nadhani mwishoni mwa September 1994 na wakashinda na wakarudishwa Chuoni. Wakaja huku tunaanza second year na wako very enthusiastic kukishinda Chuo. Hakika walitamba. Wakanunu T-Shirt zimeandikwa G211 kama ambavyo sasa zimeenea zilizoandikwa DHAIFU. Kurudi kwao ilikuwa fahari kwao na huzuni kwetu. Si huzuni kuwa tulipenda, bali walikuwa ni kero kila tulipopita.

      Tukakaa tumenuaniana yaani TRAITORS na G211. Faculty of Engineering au FOE second year tukawa katika makundi hayo mawili. Ninakumbuka siku moja nimeenda kusoma prep darasa moja wakaja wakanifukuza kwa sababu TRAITORS tulipigwa marufuku hakuna ku-study kule FOE.

      Hali ikadumu hivyo kwa nusu mwezi. Ndipo likaja sakata la Mutungirehi. Maadui wa Mutungirehi wakaona kundi pekee lenye uamsho na zuri kulitumia ni hili la G211.

      Kuanzia hapa wengi mnajua yaliyotokea. Mutungirehi akavurumishwa stejini kama thread moja inavyosimuliwa humu. Lakini players wakuu walikuwa ni hawa G211 ingawa wanachuo wengi walidhani ni vijana wote wa engineering. Si kweli, sisi tulioitwa TRAITORS hatukufurahia vurugu kwa Mutungirehi. Kilichofuata ni kufungwa Chuo kwa mgomo uliosababishwa na fujo hizi.

      Tukiwa huko nyumbani tukaletewa barua zenye neon liitwalo INTIMIDATION. Mimi ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kukutana na neno hili na ikabidi nifungue dictionary kulielewa.

      Sitaki kutaja nilipokea barua nikiwa mkoa gani. Lakini G211 nao walikuwa wamejipanga posta zote za miji mikubwa. Wakiona mwanachuo kaenda kupokea barua basi wanakuja na kufanya kavurugu kadogo ili wajue ulichoandikiwa. Walikuwa wameji-organise kama usalama wa taifa.

      Mimi nikaenda posta. Natoka kuchukua barua nikazungukwa na vijana wanne, wote ni katika kundi la G211. Wakata kujua barua niliyopokea. Kwa sababu nilikuwa mkoani na hatuko chuoni na mimi nikapata kiburi sikutaka kuwaonyesha nikawapuuza na kuwatishia kuwaitia polisi wakaachana na mimi.

      Nyumbani nikafanya masharti ya barua ile, kwamba kama nilitishiwa (intimidation) basi ni nani au kikundi gani kilitutishia. Mimi nikaona Mungu akupe nini maana ule mnyanyaso wa kuitwa TRAITORS tangu May 1994 hadi October 1994 nilishauchoka nikataja waziwazi kuwepo kwa kundi la G211 na jinsi walivyokuwa wakitunyanyasa kutufukuza hata madarasani kujisomea usiku (prep).

      Lecturer mmoja alinipa live kwamba barua yangu walii-discus at length.

      Mwanzaoni mwa December 1994 tukaitwa kurudi Chuoni, lakini Mutungirehi akiwa bado President of DARUSO. Effect ni kwamba wanafunzi zaidi ya 200 walisimiamishwa mwaka mzima wengi wao wakiwa ni wale G211.

      Ikaitishwa referendum kuchagua kuendelea na Mutungirehi regime au la na wengi wakachagua kuwa asiendelee na ukaitishwa uchaguzi mwingine.

      Siku moja nimekutana na Lugiko Mpelwa Karungubare akiwa CHADEMA, nikamkumbusha ule woga wake hadi akatuita tuingine madarasani akakataa kabisa kukumbuka.

      Ladislaus Malima aliyekuwa jasiri kunisukuma nisiingie kwenye mtihani mmeeleza kwenye thread nyingine kwamba alipopigwa mkwara kwenye mgomo wa Mutungirehi akanywea na wale wenzake G211 naye wakamuita TRAITOR.


      Haya ndiyo ninayoyakumbuka kuhusiana na sakata lile la wanafunzi wa Engineering { G211} na Benedict Mutungirehi. Samahani kwa Makala ndefu lakini imenibidi niyaseme haya.
      JokaKuu, fide1975, Nyunyu and 10 others like this.
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    2. RukaaJuu Final

    3. #61
      Peele's Avatar
      Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Posts : 13
      Rep Power : 349
      Likes Received
      5
      Likes Given
      3

      Cool Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      SubiriJibu ijapokuwa unataka kuweka historia sawa, unatumia nafasi hiyo kujitakasa kwa dhambi ya U-TRAITOR. Dhambi ile ni kubwa na itaendelea kukutafuna sana, kama usipokiri na kurudi kundini kama wenzio. Nimesoma kwa masikitiko maelezo yako mareeefu yenye ujanja ujanja mwingi. Nimelazimika kujiunga na JF leo kwa ajili yako, ili niweke kumbukumbu sawa. Mimi ni G211 mpaka kifo.

      1. SIO KWELI hata kidogo kuwa G211 ndio tuliompiga maleva pale Nkurumah, kama unakumbukumbu nzuri siku hiyo tulivaa zile Tshirt zetu usizozipenda, tukakaa kule nyuma darini, muda wote tulikuwa pamoja na ki ukweli tulishangilia sana. Mutungirehi aliangushwa na ma ngwini wenzie na FoE 3rd yr uliowataja.(ndio u traitor wenyewe huu)
      2. Nikirudi siku ya tukio SIO KWELI kuwa viongozi wetu walikuwa na kikao na Prof Masenge, Mbona wao hawakufanya mtihani ??? na mpaka leo ni G211?? na wala hawakutushauri tufanye mtihani. Mimi nilikuwepo darasani nikijiandaa na mtihani wa Chemistry, Masenge alilazimisha watu kwa kutugawia mitihani sisi wengine tukakataa. U-taitor tu ndio uliowasumbua.
      3. Ukweli ambao hutaki kuusema ni kuwa mtihani ulishelewa toka saa 2.00 mpaka 5.40 kwa sababu walimu wa Math dpt walikuwa wamegoma kutoa mtihani kwa sababu ya vurugu tulizofanya na wewe wakati wa ile test ngumuuu. Hivyo Dean wa Engineering aliwabembeleza sana ndio maana wakachelewa.
      4. ukweli mwingine ni kuwa wote tulikuwa na mtihani wa Chemistry siku ile saa 8.00 hivyo ilipofika saa 5 tulikubaliana kutawanyika na kujiandaa na mtihani wa mchana kwa kuwa ktk hali ya kawaida tusingeweza kuanza mtihani saa sita na tufanye na mwingine saa nane kwani mitihani ilikuwa ni ya masaa matatu.
      5. Hii habari ya Yustus si ya kweli, alikuwa mtu wangu wa karibu.
      6. Usichokijua ni kwamba baadhi yetu G211 tulipanga mpango mahsusi wa kimapinduzi wa kuongoza chuo mpaka tumalize, ni mpango huu ndio uliomuweka Sweke madarakani na mwaka uliofuata akafuatia mwenzetu mwingine (room mate wa Sweke) aliyekuja kuwa Vice President ambaye kimsingi ndiye aliyeongoza kwani kama unavyojua President wake alikuwa mtu kilaji sanaa.
      7. Prof Masenge alikasirika sana na hamasa yetu, hasa kitendo cha kuingia darasani na Tshirt(I LOVE G211-1994) alitunga UE ngumu ajabu na akakamata 70 kati ya 211 kwa ajili ya sup. (Nyie Ma traitor alikamatwa mmoja tu kati ya 70)
      8. Kwa ushirikiano wetu tulikataa kwenda field ili tusome na wenzetu waliokamatwa na matokeo wote 70 walifaulu akanyakwa TRAITOR na ku DISCO.
      9. Prof Masenge alipopata nafasi na kwa ushahidi wa uongo wa ma TRAITOR kama wewe akiwa VC ADMIN alitukandamiza na kutuchelewesha kumaliza shule kwani kwenye displinary hearing G211 hawakutukuta na makosa.
      10. Niseme tu ijapokuwa alikuwa mahiri kwa mahesabu, Prof Masenge hakuwa mtawala mzuri, laiti angekuwepo Prof Mkude mambo yangekuwa tofauti.
      11. Pamoja na kuwa tulichelewa kumaliza chuo, tukio lile wengi wetu lilitujengea ujasiri unaotusaidia mpaka leo, TAABU ile ilitufundisha mno kuhusu maisha na tuliporejea tulisoma kama watu wazima tukijua dunia ya nje ikoje, MSHIKAMANO ule ulituacha tukiwa watu wenye kuamini katika utafutaji wa haki kwa umoja, tukijua kwa hakika uchungu wa kusalitiwa katika mapambano.
      12. ALUTA continua mapambano yanaendelea.
      KipimaPembe and Baro like this.

    4. #62
      wagaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2012
      Posts : 598
      Rep Power : 479
      Likes Received
      123
      Likes Given
      92

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Traitor huyo hafai kabisa. mwache pombe imalize kazi yake. anapiga viroba sasa hivi.
      "Tanzania ni ya watanzania, na watanzania wenyewe ndo sisi"

    5. #63
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By Peele
      Nimelazimika kujiunga na JF leo kwa ajili yako, ili niweke kumbukumbu sawa. Mimi ni G211 mpaka kifo
      Basi ninashukuru kwamba thread yangu imeongeza idadi ya wanachama wa JF. Mimi niko humu JF mwaka wa tatu sasa. Nakushauri waite na wenzako G211 tuongezeke. JF kuna issues nyingi. Kuna wengine watakujibu kuwa thread kama hii mpelekee mke wako. Hata mimi nimeambiwa lakini muhimu kuna ambao mnakuja.

      Kwanza Habari ya miaka mingi natumaini Maisha yanaenda vizuri maana ndiyo lengo langu. Sasa najibu hoja zako kama ifuatavyo

      Quote By Peele
      SIO KWELI hata kidogo kuwa G211 ndio tuliompiga Malevapale Nkurumah, kama unakumbukumbu nzuri siku hiyo tulivaa zile Tshirt zetu usizozipenda, tukakaa kule nyuma darini, muda wote tulikuwa pamoja na ki ukweli tulishangilia sana. Mutungirehi aliangushwa na ma ngwini wenzie na FoE 3rd yr uliowataja.(ndio u traitor wenyewe huu)
      Mkuu,

      Maleva nimemtaja kwenye issue nyingine kabisa yaani 1995 alipoukwaa u-Presidency of DARUSO wakati mimi tukio la Nkruma ni lile la October 1994 dhidi ya benedict Mutungirehi.

      Ingawa ni kama vile unapinga lakini unaungana na mimi kwamba mlikaa kwenye balcon mkiwa kama washangiliaji maana ndiyo mlipatikana kwa shughuli hii. Mutungirehi alipoangushwa na viti wasichana ambao wengi ni wa arts (MANGWINI) walianza kulia. Binafsi niliamini amekufa. Nyinyi mlishangilia kwa nguvu zote na inaelekea mlitaka atoke pale maiti! Watu wa ajabu sana nyie. Mnashangilia mtu kufa.

      Ok. Mutungirehi ameshaokolewa akakimbizwa hospitali, je kuna sympathy yoyote mliyoonyesha. Not at all. Kumbuka kwamba hotuba zilikatisha na fujo na kelele zenu. Kilichofuata hapo kinaitwa anarchy yaani utaratibu ambao ni shaghala baghala. Yule bwana mkurya alivyouliza “Sasa Kiongozi ni nani?”. Ukumbi mzima haukujua ujibu nini kwa sababu Hakuna aliyetarajia ile hali. Lakini nyinyi mkajibu kwa sauti moja kutoka kule juu balcon mkisema “Mushi, Mushi, Mushi”.

      Na kweli mkaonekana kana kwamba mmepitisha Azimio. Ndiyo maana tuliporudishwa nyumbani wengi tu waliwataja kwa kusema vijana wa Engineering ndiyo walioleta fujo. Ni kweli walitakiwa kusema hivyo hawakujua kuwa si Engineering wote. Watu kama sisi ndiyo tulifafanua kuhusu nyinyi kule balcon.

      Kwa taarifa yako hata kabla ya vurugu hizi mimi niliona chuoni hapakaliki na nilishatoa taarifa mapema kuhusu harassment zenu. Nafasi ya kuombwa kwenye barua ilikuwa ni mara ya pile tu na sikutaka kuiacha kuwatajeni na kamwe sintakijutia kitendo hicho.

      Kwa taarifa yako. Baadhi ya G211 wenzako tulipokuwa salama niliwahi kuwakebehi kwamba wana ugonjwa wa mob physchology. Kwamba wanakuwa na moral wa kutusakama wakiwa kwenye kundi lakini kamwe hawathubutu wakiwa peke yao. Ndiyo maana baada ya chuo kila ukikutana na mmoja hataki kukumbushwa hili waziwazi maana anajua yuko peke yake na utambana kwenye angel ya ujinga wake




      Quote By Peele
      Nikirudi siku ya tukio SIO KWELI kuwa viongozi wetu walikuwa na kikao na Prof Masenge, Mbona wao hawakufanya mtihani ???
      Hallo, hebu mtafute Sweke au Karungubare pale CHADEMA wakukumbushe vizuri. Kitilinga nina miaka 15 sijui yuko wapi. Tatizo nyinyi G211 hamkujipanga na challenge nyingi ndiyo maana wenzako ambao wanaochangia humu watakushangaa unaposema hakukuwa na mazungumzo wakati ndilo jambo lililopoteza muda yaani saa 03:00 hadi saa 05:30.

      Eti mbona hawakufanya mtihani? Wangafanyaje wakati mliwabana kwa mabavu mkitetea wenzenu walioondokakijeuri wakisema liwalo na liwe hata mtihani ukija hawana time!

      Quote By Peele
      na wala (viongozi) hawakutushauri tufanye mtihani
      Statement yao ya kwanza ilikuwa ni twende tufanye mtihani kwa sababu hawakujua huku nje tumeparaganyika vipi. Nyinyi ndiyo mkawageuzi mawazo kwa kuwauliza IWEJE TUFANYE MTIHANI WAKATI WENGINE WAMEISHAENDA HOME. Hapa ndipo mlipowabana lakini mimi hamkuweza kunibana kwa hoja hii maana hao walioondoka walitujibu kijeuri kwamba tutakalo na tulifanye.

      Quote By Peele
      Mimi nilikuwepo darasani nikijiandaa na mtihani wa Chemistry, Masenge alilazimisha watu kwa kutugawia mitihani sisi wengine tukakataa. U-taitor tu ndio uliowasumbua
      Sikatai kwamba ulikataa. Na kama ulikataa basi ni wazi kuwa ulikuwa ndani ya exam-room mapema na hukuwa nje kama sisi kusikiliza tutakachoamua. Ndiyo maana hata request ya kwanza ya Class reps hukuisikia kwamba twende darasani.

      Lakini hapohapo hujagundua kwamba unajikanyaga. Huelezi kwamba kama ulikataa je uliendelea kukaa exam room au uli-quit. Kwa maana hiyo fujo ndani ya exam room ilianza mlemle kabla ya kule nje. Uongo mkubwa. Sasa kama ulikataa na ikatokea fujo, iweje fujo ichukue zaido ya dakika 40.

      Ukweli ni kwamba fujo ya kuingia kwenye vyumba vya mitihani na kuichanachana ilipoanza haikuchukua hata dakika tano. Mlijigawa kwenye vyumba kadhaa mkahakikisha inafanywa haraka kama umeme kiasi kwamba hamkuwa hata na haja ya kutujua bali mlikuwa na hajaya ya kuchanachana mitihani ukosekane ushahidi. Kwa hili nawapa hongera maana spidi yenu sijawahi kuiona.

      Na ili fujo ikamilike lazima iwe ya muda mfupi maana askari wanegeweza kumwaga muda mfupi kabla hamjamaliza.

      Quote By Peele
      Ukweli ambao hutaki kuusema ni kuwa mtihani ulishelewa toka saa 2.00 mpaka 5.40 kwa sababu walimu wa Math dpt walikuwa wamegoma kutoa mtihani kwa sababu ya vurugu tulizofanya na wewe wakati wa ile test ngumuuu. Hivyo Dean wa Engineering aliwabembeleza sana ndio maana wakachelewa.
      Nashukuru jinsi G211 mnavyojitokeza wengi kulitetea jambo hili mnajikuta mnajigonga humuhumu. Ona mwenzako alivyokana kwamba April 1994 hakukutokea fujo kwa lecturer aliyetoa paper ngumu. Soma comment number 3 ya huyu bwana (Click hapa)


      Quote By Peele
      ukweli mwingine ni kuwa wote tulikuwa na mtihani wa Chemistry siku ile saa 8.00 hivyo ilipofika saa 5 tulikubaliana kutawanyika na kujiandaa na mtihani wa mchana kwa kuwa ktk hali ya kawaida tusingeweza kuanza mtihani saa sita na tufanye na mwingine saa nanekwani mitihani ilikuwa ni ya masaa matatu.
      Mheshimiwa,

      Naomba unapotunga uogo uwe muangalifu. Unajua hamkutarajia kwamba haya mambo iko siku yatawekwa wazi kama humu JF. Ona sasa usivyokumbuka.

      Ni kweli siku hiyo kulikuwa na mtihani mwingine wa Chemistry. Na ni kweli mitihani ilikuwa ni masaa matatu. Hebu hata mtu asiyejua ratiba yetu. Hata kama tungeanza saa 3 maana yake tungemaliza saa 6. Kisha tukaenda kula na foleni ndefu za pale cafeteria! Kumbuka ratiba vizuri. Mtihani wa Chemistry ulikuwepo kweli lakini ulikuwa unaanza saa 01:00 (19:00) jioni hadi saa tatu (21:00) na si saa nane (14:00) kama mnavyotaka kudanganya umma.

      Quote By Peele
      Hii habari ya Yustus si ya kweli, alikuwa mtu wangu wa karibu
      Kama Habari ya Yustus huijui muulize jamaa aliitwa Balozi akusimulie, Huyu najua yuko pale Enginering registration Board. Loti na Chapa sijui wako wapi.
      Mtetezi pekee wa Yustus alikuwa jamaa anaitwa Waziri yaani classmate wake. Unashindwa kukumbuka inabidi ukumbuke kwamba Yustus alikuwa nyuma yetu mwaka mmoja na kama ulivyosema mlitaka G211 kuritishana mkagundua kuwa Yustus si mwenzenu hasa baada ya kugundua kuwa Yustus ana historia ya ulokole. Na ni kweli sasa hivi ana makanisa yake anahubiri alishaachana na u-engineering.

      Quote By Peele
      Usichokijuani kwamba baadhi yetu G211 tulipanga mpango mahsusi wa kimapinduzi wa kuongoza chuo mpaka tumalize, ni mpango huu ndio uliomuweka Sweke madarakani na mwaka uliofuata akafuatia mwenzetu mwingine (room mate wa Sweke) aliyekuja kuwa Vice President ambaye kimsingi ndiye aliyeongoza kwani kama unavyojua President wake alikuwa mtu kilaji sanaa.
      Ona hata unavyotumia terminology hapa. Unasema nisichokijua. Ni kweli nitaendelea kutojua kama mambo yenu mlikuwa mnayafanya kwa siri yaani caucas bila kuwashirikisha wengine. Leo ndiyo nimejua siri hii.

      Haina ubaya caucas zenu za siri. Kosa lenu ni kwamba mkishatoka kwenye huo usiri wenu mlikuwa mnakuja kama tayari ni maamuzi kwa sisi wote, badala ya kutushawishi kwa hoja mnataka kutumia ngumi, mabavu au kuchanachana mitihani.


      Quote By Peele
      Prof Masenge alikasirika sana na hamasa yetu, hasa kitendo cha kuingia darasani na Tshirt(I LOVE G211-1994) alitunga UE ngumu ajabuna akakamata 70 kati ya 211 kwa ajili ya sup. (Nyie Ma traitor alikamatwa mmoja tu kati ya 70
      Ona unarudia mambo ya Exam ngumu kama lile suala lililoanzisha yote haya. Binafsi sijaongelea ugumu wa paper kama concern bali nimeongelea kama chanzo cha vurugu Tofauti na mlivyopotosha kwa miaka 18 sasa.

      Quote By Peele
      Kwa ushirikianowetu tulikataa kwenda field ili tusome na wenzetu waliokamatwa na matokeo wote 70 walifaulu akanyakwa TRAITOR na ku DISCO
      Hebu eleza ni ushirikiano gani unaohitajika ili mtu afaulu kuelewa jambo la kitabu kama vile masomo na afaulu. Unajua kuna dhana kwamba Chuo Kikuu hawafaulu hadi waonyeshe ushirikiano wa kudesa au kuiba mitihani na aina yoyote ya forgery. Je ndiyo huo unaousema, kushirikiana madesa?

      Hakuna aliyeongelea uwezo wa akili za darasani hapa. Na kama mlijidhani mnahitaji kushirikiana ili kufaulu basi iliwacost kisaikolojia na ndiyo maana sasa hivi mmeparaganyika sehemu mbalimbali duniani mnakuja humu JF kila mmoja anaongea lwake yaani lugha Tofauti kwa tukio moja.

      Binafsi sihitaji ushirikiano na ubongo wa mtu mwingine kusoma kitabu? Huyo ninayehirikiana naye kuna kitabu gani duniani anaweza kukisoma na kukielewa halafu mimi nikikisoma sintaambua kitu! Jiamini bwana.

      Quote By Peele
      Prof Masenge alipopata nafasi na kwa ushahidi wa uongo wa ma TRAITOR kama wewe akiwa VC ADMIN alitukandamiza na kutuchelewesha kumaliza shule kwani kwenye displinary hearing G211 hawakutukuta na makosa.
      Mlikuwaje sasa mbona hamkukimbilia kupata haki yenu mahakamani ambako ni wiki sita tu zilipita mnasema mlishinda ile kesi yenu ya kituko cha April 1994?

      Quote By Peele
      Niseme tu ijapokuwa alikuwa mahiri kwa mahesabu, Prof Masenge hakuwa mtawala mzuri, laiti angekuwepo Prof Mkude mambo yangekuwa tofauti
      Uamuzi wa kufunga Chuo na kuanza kushughulikia suala la Mutungirehi ulipendekezwa Seneti ya UDSM wakati huo ikiongozwa na Balozi Fulgence Kazaura. Prof. Masenge hakuwa final decision maker.
      Satanic_Verses likes this.
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    6. #64
      NYENJENKURU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Location : Tanganyika Masagati
      Posts : 936
      Rep Power : 606
      Likes Received
      182
      Likes Given
      359

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Nilikuwa G211.Nimekumbuka mbali sanaaaaaa hayo yote nilikuwepo wakati yanatokea.Nakushukuru sana...kwa kunikumbusha hayo.Karungubare namkumbuka sanaaaaa yule msukuma.Magesssa nikuwanaye darasa moja na kwenye yaani namba yake ilikuwa 18X/T93 na mimi ilikuwa 19Y/T93..
      Jamani CCM hamshibi?Mnataka kula mpaka ukoko jamani?2015 byeeeeeeeeeee.

    7. #65
      ezra1504's Avatar
      Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 54
      Rep Power : 444
      Likes Received
      10
      Likes Given
      1

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By SubiriJibu
      Mkuu,

      Kinachogomba ni utaratibu mliotumia wa kumng"oa Mutungirehi. Huwezi kuzitetea kwa sababu ulikuwa ni uhuni ambao wenzako bila aibu wanauita ni ushujaa.

      Kwani hakukuwa na njia ya kidemokrasia ya kumuondoa? Njia ilikuwepo na ndiyo iliyotumika baada ya nyinyi wengi kusimamishwa.

      Njia hiyo ilitumukaje? Kumbuka tulipoitwa kurudi Chuoni kitu cha kwanza tukapewa referendum au tuite vote of no confidence kama wote tunamtaka Mutungirehi abaki au la.

      Tukapiga kura na Mutungirehi akashindwa na ikabidi uchaguzi ufanyika upya kumpata rais mpya wa DARUSO. Sasa, mlishindwa nini kuieleza iwe namna hii na mbona aliondoka ndipo akarithiwa na Lenganasa.

      Kama alikuwa amenunuliwa hata kama ni kweli, mbona kununuliwa kwake hakukuzuia tumuondoe kwa kura kistaarabu. Hivyo, tatizo nisilolitetea ni ule uhuni uliotumika wa kumvamia wakati history imethibitisha tulimuondoa kwa kura na akaondoka.

      Mbona baada ya kumuondoa akabaki analalamika kwa kujificha jina halisi magazetini akiponda kuondolewa kwake magazetini.

      Hivyo, kile kitendo cha pale Nkrumah Hall huwezi kukabtiza jina jingine bali uhuni ambao unahitaji akili ya ajabu kuutetea eti kwa kuuita ujasiri. Ujasiri kwa nani?
      Kazi ya watu usiuite uhuni rafiki yangu. Kwanza nashangaa ilikuwaje ukasoma Engineering wakati huwezi hata kujisimamia ktk maamuzi magumu km hayo. Wewe ungekuwa Doctor ungesema Ulimboka basi mimi naendelea na kazi, CEBE wa aina gani wewe hujaangusha majengo au madaraja kuvunjika?

      Hii nchi kuna jambo gani linaenda bila watu kustrike kwanza?

      Hii serikali inatufanyia mambo mangapi ya ajabu na wananchi wanalalamika umeona nini kinafanyika? Bila huo mgomo hiyo nafasi ya vote of no confidence nani angewapa? CoET oyeeeeee!!

    8. Miaka 50

    9. #66
      muonamambo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2010
      Posts : 553
      Rep Power : 552
      Likes Received
      164
      Likes Given
      936

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Jokakuu heshima mbele kiongozi

      Kwanza napenda kukushukuru kwa kuweza kuona tatizo lilikuwa wapi...TATIZO lilikuwa ni kiburi cha wahadhiri wa dept ya mathematics kwa kutaa kuuleta mtihani na hata baada ya kugundua kuwa wamechemsha walitaka kushinikiza wanachuo kufanya mtihani huo wakitumia ubabe huohuo wa wao kushika mpini na sisi kushika makali. Lakini g211 walishaisoma bylaws and sheria za chuo na kugunda janja yao.

      Subirijibu anatapatapa kuonda doa la utraitor ambalo halitakuja kumtoka maishani.. na kwa jinsi anavyoeleza bado tabia hiyo anayo mpaka leo...Historia ilishamhukumu siku nyingi na kujaribu kusahihisha kwa sasa hakuta msaidia kitu zaidi ya kujaza saver ya JF.

      Quote By JokaKuu
      ..waliokosea ni viongozi/wawakilishi waliokubali mtihani uanze baada ya kuchelewa masaa 3++.

      ..pia lazima tukubali kwamba kuna mahusiano mabaya kati ya waalimu na wanafunzi hapo UDSM.

      ..hali ya kuogopana, kutishana, kuwindana, kupigana, haifai ktk mazingira ya kisomi.
      Peele likes this.

    10. #67
      kkitabu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 27th December 2011
      Posts : 108
      Rep Power : 395
      Likes Received
      24
      Likes Given
      1

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Hata na mimi nakumbuka kisa hicho kwani nilikuwa nasoma Electrical Engineering. Aidha karatasi zetu za kujibia maswali zilichanwa na wenzetu, kwakweli ni kwamba tulinusurika kupigwa. Hata hivyo boom la kwenda "Practical Training" lilipotoka tulichanga hela ya kumlipa Wakili ambaye alikuwa anasimamia kesi iliyokuwa imefunguliwa na wenzetu dhidi ya uongozi wa chuo.
      Peele likes this.

    11. #68
      muonamambo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2010
      Posts : 553
      Rep Power : 552
      Likes Received
      164
      Likes Given
      936

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By Satanic_Verses
      Mkuu SubiriJibu,

      Umemwaga kila kitu na mimi sina cha kuongezea. Binafsi mimi nilikuwa first year yaani nyinyi mlioitwa TRAITORS na G211 mlinitangulia mwaka mmoja.

      Sikuwa Faculty of Engineering mliyozoea kuiita FOE. Bali nilikuwa BA. Economics, yaani wale mliozoea kutuia MANGWINI.

      Wakati naingia hapo kumbuka nyinyi Second Year mlikuwa hamna vyumba na ikabidi ama mkae offcampus ama mpewe hisani na walio na vyumba, yaani mnalala wawili kitanda kimoja, mtindo maarufu kwa jila la MZUNGU WA NNE.

      Mimi jamaa mmoja wa G211 alinieleza kiasi kikubwa kama ulivyoeleza. Yeye binafsi alijilaumu kwa nini hakuingia kwenye exam room na hivyo akajikuta amepachikwa jina G211 ambalo yeye hakuliona kama ni sifa.

      Yeye aliweka wazi kwamba kungekuwa na uwezekano wa ku-rewing ile event ya sikuya exam na wakapewa choice ileile kwamba wachague kuingia kwenye exam room ya Pro. Masenge au wagome basi angechagua kuingia maana hadi leo haoni sababu za msingi bali aliogopa tu kundi la wenzake G211 ambalo sasa hana uoga nalo tena.

      Hongera mkuu kuondokana na woga na kulisimulia kwa uhalisi wake.
      Mkuu SATANIC_VERSES kwanza nashukuru kwa kukiri kwamba hukuwa FOE na kwamba ulikuwa NGWINI .

      FOE walikuwa na misimamo yao ambayo kwatu watu wa ungwinini msingeweza kuielewa na ni misimamo thabiti ya kusimamia ukweli na umoja... lakini kama ulivyosema hapo juu kwamba kuna mwana FOE mmoja eti alijutia kitendo cha G211 basi napenda kukuambia ya kwamba huyo hakustahili kuwa FOE... Kwani kwenye msafara wa mamba na kenge wapo.... kama alivyokuwa SUBIRIJIBU na wenzake 71...

      SUBIRIJIBU anakiri kuwa kulikuwa na tatizo katika idara ya mathematics na kiburi cha kutoleta mtihani... lakini kwa kuwa alikuwa ni kenge kwenye msafara wa mamba alishindwa kutetea haki yake ya kuthaminiwa kama mwana chuo na kukubali kuburuzwa kama mwanafunzi wa sekondari...

      kwa wana FOE hasa g211 waliokuwa na msimamo thabiti wa kupigania haki yao waliweza kuufikisha uongozi wa chuo mahakamani{ kitendo cha nadra sana kutokea enzi hizo na sasa} na kuwashinda na pia kuja kukabiliana nao kwenye academic ambapo walimu hao hao waliamua kuwafanyizia lakini haki ilishinda dhuluma....

      Nakushauri umpe pole subirijibu na wenzake 71 kwa kuwa dhambi ya u traitor itawaandama mpaka siku wanaingia kaburini... hawa hawewezi kuwa hata wajumbe wa nyumba 10 ... watawauza wenzao kwa kukosa msimamo...na kuweka masilahi yao mbele

    12. #69
      Nzenzu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2011
      Posts : 826
      Rep Power : 559
      Likes Received
      155
      Likes Given
      38

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Nimeipenda hii thread sana. Kisa cha G211 Vs TRAITORS ni simulizi fasaha kama vp kiandikwe kitabu!
      MKALIKENYA likes this.

    13. #70
      muonamambo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2010
      Posts : 553
      Rep Power : 552
      Likes Received
      164
      Likes Given
      936

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By kkitabu
      Hata na mimi nakumbuka kisa hicho kwani nilikuwa nasoma Electrical Engineering. Aidha karatasi zetu za kujibia maswali zilichanwa na wenzetu, kwakweli ni kwamba tulinusurika kupigwa. Hata hivyo boom la kwenda "Practical Training" lilipotoka tulichanga hela ya kumlipa Wakili ambaye alikuwa anasimamia kesi iliyokuwa imefunguliwa na wenzetu dhidi ya uongozi wa chuo.
      Kaka KKITABU heshima mbele mkuu... Nafurahi kusikia ya kuwa ulikuwa Electrical engineering kama mimi.. pia nafurahi kusikia kuwa uliweza kukiri na kurudisha moyo nyuma na kuamua kuchangia wenzako waliamua kuwa mstari wa mbele kutetea masilahi na kuthaminiwa kama mwanafunzi wa chuo..

      Mchango wako ulifanikisha kurudisha heshima ya wanachuo na tangu wakati huo kukawa na adabu kwa wahadhiri dhidi ya wanachuo... hongera sana ... kwani kumbuka kufanya kosa sio kosa kosa ni kurudia kosa ... kama alivyofanya suburijibu kwa kuandika wenzake kwamba ndio waliosababisha yeye asifanye mtihani ili wenziwe wafukuzwe chuo na yeye aendelee kusoma.. tabia ya kujipenda nafsi yako zaidi kuliko wengine..

    14. #71
      NYENJENKURU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Location : Tanganyika Masagati
      Posts : 936
      Rep Power : 606
      Likes Received
      182
      Likes Given
      359

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Hata mimi siku hiyo nilipoteza Viatu na mvua ilinyesha baadae wakati mabomu yanapigwa ndo maana hayakuwa na nguvu sana.Yaani wewe umenipeleka mbali sanaaaaaaa.
      SubiriJibu likes this.
      Jamani CCM hamshibi?Mnataka kula mpaka ukoko jamani?2015 byeeeeeeeeeee.

    15. #72
      client3's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th August 2007
      Posts : 204
      Rep Power : 643
      Likes Received
      36
      Likes Given
      69

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      SubiriJibu ijapokuwa unataka kuweka historia sawa, unatumia nafasi hiyo kujitakasa kwa dhambi ya U-TRAITOR. Dhambi ile ni kubwa na itaendelea kukutafuna sana, kama usipokiri na kurudi kundini kama wenzio. Nimesoma kwa masikitiko maelezo yako mareeefu yenye ujanja ujanja mwingi. Nimelazimika kujiunga na JF leo kwa ajili yako, ili niweke kumbukumbu sawa. Mimi ni G211 mpaka kifo.


      1. SIO KWELI hata kidogo kuwa G211 ndio tuliompiga maleva pale Nkurumah, kama unakumbukumbu nzuri siku hiyo tulivaa zile Tshirt zetu usizozipenda, tukakaa kule nyuma darini, muda wote tulikuwa pamoja na ki ukweli tulishangilia sana. Mutungirehi aliangushwa na ma ngwini wenzie na FoE 3rd yr uliowataja.(ndio u traitor wenyewe huu)
      2. Nikirudi siku ya tukio SIO KWELI kuwa viongozi wetu walikuwa na kikao na Prof Masenge, Mbona wao hawakufanya mtihani ??? na mpaka leo ni G211?? na wala hawakutushauri tufanye mtihani. Mimi nilikuwepo darasani nikijiandaa na mtihani wa Chemistry, Masenge alilazimisha watu kwa kutugawia mitihani sisi wengine tukakataa. U-taitor tu ndio uliowasumbua.
      3. Ukweli ambao hutaki kuusema ni kuwa mtihani ulishelewa toka saa 2.00 mpaka 5.40 kwa sababu walimu wa Math dpt walikuwa wamegoma kutoa mtihani kwa sababu ya vurugu tulizofanya na wewe wakati wa ile test ngumuuu. Hivyo Dean wa Engineering aliwabembeleza sana ndio maana wakachelewa.
      4. ukweli mwingine ni kuwa wote tulikuwa na mtihani wa Chemistry siku ile saa 8.00 hivyo ilipofika saa 5 tulikubaliana kutawanyika na kujiandaa na mtihani wa mchana kwa kuwa ktk hali ya kawaida tusingeweza kuanza mtihani saa sita na tufanye na mwingine saa nane kwani mitihani ilikuwa ni ya masaa matatu.
      5. Hii habari ya Yustus si ya kweli, alikuwa mtu wangu wa karibu.
      6. Usichokijua ni kwamba baadhi yetu G211 tulipanga mpango mahsusi wa kimapinduzi wa kuongoza chuo mpaka tumalize, ni mpango huu ndio uliomuweka Sweke madarakani na mwaka uliofuata akafuatia mwenzetu mwingine (room mate wa Sweke) aliyekuja kuwa Vice President ambaye kimsingi ndiye aliyeongoza kwani kama unavyojua President wake alikuwa mtu kilaji sanaa.
      7. Prof Masenge alikasirika sana na hamasa yetu, hasa kitendo cha kuingia darasani na Tshirt(I LOVE G211-1994) alitunga UE ngumu ajabu na akakamata 70 kati ya 211 kwa ajili ya sup. (Nyie Ma traitor alikamatwa mmoja tu kati ya 70)
      8. Kwa ushirikiano wetu tulikataa kwenda field ili tusome na wenzetu waliokamatwa na matokeo wote 70 walifaulu akanyakwa TRAITOR na ku DISCO.
      9. Prof Masenge alipopata nafasi na kwa ushahidi wa uongo wa ma TRAITOR kama wewe akiwa VC ADMIN alitukandamiza na kutuchelewesha kumaliza shule kwani kwenye displinary hearing G211 hawakutukuta na makosa.
      10. Niseme tu ijapokuwa alikuwa mahiri kwa mahesabu, Prof Masenge hakuwa mtawala mzuri, laiti angekuwepo Prof Mkude mambo yangekuwa tofauti.
      11. Pamoja na kuwa tulichelewa kumaliza chuo, tukio lile wengi wetu lilitujengea ujasiri unaotusaidia mpaka leo, TAABU ile ilitufundisha mno kuhusu maisha na tuliporejea tulisoma kama watu wazima tukijua dunia ya nje ikoje, MSHIKAMANO ule ulituacha tukiwa watu wenye kuamini katika utafutaji wa haki kwa umoja, tukijua kwa hakika uchungu wa kusalitiwa katika mapambano.
      12. ALUTA continua mapambano yanaendelea.


      nimependa kweli kwenye red
      nimejifunza kitu kwenye thread hii.....niliingia udsm mwaka 2000 tulikuta simulizi za (FoE sasa CoE) na harakati zao....natamani wanavyuo wa sasa wangapata bahati ya kupitia hapa angalau kupata picha ya pande mbili za harakati mbalimbali vyuoni..na jinsi gani mambo huwa before and after revolution.
      Last edited by client3; 4th July 2012 at 16:40.

    16. #73
      muonamambo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2010
      Posts : 553
      Rep Power : 552
      Likes Received
      164
      Likes Given
      936

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By SubiriJibu
      Basi ninashukuru kwamba thread yangu imeongeza idadi ya wanachama wa JF. Mimi niko humu JF mwaka wa tatu sasa. Nakushauri waite na wenzako G211 tuongezeke. JF kuna issues nyingi. Kuna wengine watakujibu kuwa thread kama hii mpelekee mke wako. Hata mimi nimeambiwa lakini muhimu kuna ambao mnakuja.

      Kwanza Habari ya miaka mingi natumaini Maisha yanaenda vizuri maana ndiyo lengo langu. Sasa najibu hoja zako kama ifuatavyo



      Mkuu,

      Maleva nimemtaja kwenye issue nyingine kabisa yaani 1995 alipoukwaa u-Presidency of DARUSO wakati mimi tukio la Nkruma ni lile la October 1994 dhidi ya benedict Mutungirehi.

      Ingawa ni kama vile unapinga lakini unaungana na mimi kwamba mlikaa kwenye balcon mkiwa kama washangiliaji maana ndiyo mlipatikana kwa shughuli hii. Mutungirehi alipoangushwa na viti wasichana ambao wengi ni wa arts (MANGWINI) walianza kulia. Binafsi niliamini amekufa. Nyinyi mlishangilia kwa nguvu zote na inaelekea mlitaka atoke pale maiti! Watu wa ajabu sana nyie. Mnashangilia mtu kufa.




      "Ok. Mutungirehi ameshaokolewa akakimbizwa hospitali, je kuna sympathy yoyote mliyoonyesha. Not at all. Kumbuka kwamba hotuba zilikatisha na fujo na kelele zenu. Kilichofuata hapo kinaitwa anarchy yaani utaratibu ambao ni shaghala baghala. Yule bwana mkurya alivyouliza “Sasa Kiongozi ni nani?”. Ukumbi mzima haukujua ujibu nini kwa sababu Hakuna aliyetarajia ile hali. Lakini nyinyi mkajibu kwa sauti moja kutoka kule juu balcon mkisema “Mushi, Mushi, Mushi”.

      Na kweli mkaonekana kana kwamba mmepitisha Azimio. Ndiyo maana tuliporudishwa nyumbani wengi tu waliwataja kwa kusema vijana wa Engineering ndiyo walioleta fujo. Ni kweli walitakiwa kusema hivyo hawakujua kuwa si Engineering wote. Watu kama sisi ndiyo tulifafanua kuhusu nyinyi kule balcon.

      Kwa taarifa yako hata kabla ya vurugu hizi mimi niliona chuoni hapakaliki na nilishatoa taarifa mapema kuhusu harassment zenu. Nafasi ya kuombwa kwenye barua ilikuwa ni mara ya pile tu na sikutaka kuiacha kuwatajeni na kamwe sintakijutia kitendo hicho.

      Kwa taarifa yako. Baadhi ya G211 wenzako tulipokuwa salama niliwahi kuwakebehi kwamba wana ugonjwa wa mob physchology. Kwamba wanakuwa na moral wa kutusakama wakiwa kwenye kundi lakini kamwe hawathubutu wakiwa peke yao. Ndiyo maana baada ya chuo kila ukikutana na mmoja hataki kukumbushwa hili waziwazi maana anajua yuko peke yake na utambana kwenye angel ya ujinga wake



      "Hallo, hebu mtafute Sweke au Karungubare pale CHADEMA wakukumbushe vizuri. Kitilinga nina miaka 15 sijui yuko wapi. Tatizo nyinyi G211 hamkujipanga na challenge nyingi ndiyo maana wenzako ambao wanaochangia humu watakushangaa unaposema hakukuwa na mazungumzo wakati ndilo jambo lililopoteza muda yaani saa 03:00 hadi saa 05:30."


      "Eti mbona hawakufanya mtihani? Wangafanyaje wakati mliwabana kwa mabavu mkitetea wenzenu walioondokakijeuri wakisema liwalo na liwe hata mtihani ukija hawana time!

      Statement yao ya kwanza ilikuwa ni twende tufanye mtihani kwa sababu hawakujua huku nje tumeparaganyika vipi. Nyinyi ndiyo mkawageuzi mawazo kwa kuwauliza IWEJE TUFANYE MTIHANI WAKATI WENGINE WAMEISHAENDA HOME. Hapa ndipo mlipowabana lakini mimi hamkuweza kunibana kwa hoja hii maana hao walioondoka walitujibu kijeuri kwamba tutakalo na tulifanye.
      "
      .


      "Sikatai kwamba ulikataa. Na kama ulikataa basi ni wazi kuwa ulikuwa ndani ya exam-room mapema na hukuwa nje kama sisi kusikiliza tutakachoamua. Ndiyo maana hata request ya kwanza ya Class reps hukuisikia kwamba twende darasani.

      Lakini hapohapo hujagundua kwamba unajikanyaga. Huelezi kwamba kama ulikataa je uliendelea kukaa exam room au uli-quit. Kwa maana hiyo fujo ndani ya exam room ilianza mlemle kabla ya kule nje. Uongo mkubwa. Sasa kama ulikataa na ikatokea fujo, iweje fujo ichukue zaido ya dakika 40.
      "

      ..

      "Ukweli ni kwamba fujo ya kuingia kwenye vyumba vya mitihani na kuichanachana ilipoanza haikuchukua hata dakika tano. Mlijigawa kwenye vyumba kadhaa mkahakikisha inafanywa haraka kama umeme kiasi kwamba hamkuwa hata na haja ya kutujua bali mlikuwa na hajaya ya kuchanachana mitihani ukosekane ushahidi. Kwa hili nawapa hongera maana spidi yenu sijawahi kuiona.

      Na ili fujo ikamilike lazima iwe ya muda mfupi maana askari wanegeweza kumwaga muda mfupi kabla hamjamaliza.



      Nashukuru jinsi G211 mnavyojitokeza wengi kulitetea jambo hili mnajikuta mnajigonga humuhumu. Ona mwenzako alivyokana kwamba April 1994 hakukutokea fujo kwa lecturer aliyetoa paper ngumu. Soma comment number 3 ya huyu bwana (Click hapa)
      "


      Mheshimiwa,

      Naomba unapotunga uogo uwe muangalifu. Unajua hamkutarajia kwamba haya mambo iko siku yatawekwa wazi kama humu JF. Ona sasa usivyokumbuka.

      Ni kweli siku hiyo kulikuwa na mtihani mwingine wa Chemistry. Na ni kweli mitihani ilikuwa ni masaa matatu. Hebu hata mtu asiyejua ratiba yetu. Hata kama tungeanza saa 3 maana yake tungemaliza saa 6. Kisha tukaenda kula na foleni ndefu za pale cafeteria! Kumbuka ratiba vizuri. Mtihani wa Chemistry ulikuwepo kweli lakini ulikuwa unaanza saa 01:00 (19:00) jioni hadi saa tatu (21:00) na si saa nane (14:00) kama mnavyotaka kudanganya umma.


      Kama Habari ya Yustus huijui muulize jamaa aliitwa Balozi akusimulie, Huyu najua yuko pale Enginering registration Board. Loti na Chapa sijui wako wapi.
      Mtetezi pekee wa Yustus alikuwa jamaa anaitwa Waziri yaani classmate wake. Unashindwa kukumbuka inabidi ukumbuke kwamba Yustus alikuwa nyuma yetu mwaka mmoja na kama ulivyosema mlitaka G211 kuritishana mkagundua kuwa Yustus si mwenzenu hasa baada ya kugundua kuwa Yustus ana historia ya ulokole. Na ni kweli sasa hivi ana makanisa yake anahubiri alishaachana na u-engineering.



      Ona hata unavyotumia terminology hapa. Unasema nisichokijua. Ni kweli nitaendelea kutojua kama mambo yenu mlikuwa mnayafanya kwa siri yaani caucas bila kuwashirikisha wengine. Leo ndiyo nimejua siri hii.

      Haina ubaya caucas zenu za siri. Kosa lenu ni kwamba mkishatoka kwenye huo usiri wenu mlikuwa mnakuja kama tayari ni maamuzi kwa sisi wote, badala ya kutushawishi kwa hoja mnataka kutumia ngumi, mabavu au kuchanachana mitihani.




      Ona unarudia mambo ya Exam ngumu kama lile suala lililoanzisha yote haya. Binafsi sijaongelea ugumu wa paper kama concern bali nimeongelea kama chanzo cha vurugu Tofauti na mlivyopotosha kwa miaka 18 sasa.



      Hebu eleza ni ushirikiano gani unaohitajika ili mtu afaulu kuelewa jambo la kitabu kama vile masomo na afaulu. Unajua kuna dhana kwamba Chuo Kikuu hawafaulu hadi waonyeshe ushirikiano wa kudesa au kuiba mitihani na aina yoyote ya forgery. Je ndiyo huo unaousema, kushirikiana madesa?

      Hakuna aliyeongelea uwezo wa akili za darasani hapa. Na kama mlijidhani mnahitaji kushirikiana ili kufaulu basi iliwacost kisaikolojia na ndiyo maana sasa hivi mmeparaganyika sehemu mbalimbali duniani mnakuja humu JF kila mmoja anaongea lwake yaani lugha Tofauti kwa tukio moja.

      Binafsi sihitaji ushirikiano na ubongo wa mtu mwingine kusoma kitabu? Huyo ninayehirikiana naye kuna kitabu gani duniani anaweza kukisoma na kukielewa halafu mimi nikikisoma sintaambua kitu! Jiamini bwana.



      Mlikuwaje sasa mbona hamkukimbilia kupata haki yenu mahakamani ambako ni wiki sita tu zilipita mnasema mlishinda ile kesi yenu ya kituko cha April 1994?



      Uamuzi wa kufunga Chuo na kuanza kushughulikia suala la Mutungirehi ulipendekezwa Seneti ya UDSM wakati huo ikiongozwa na Balozi Fulgence Kazaura. Prof. Masenge hakuwa final decision maker.

      Suburijibu;
      Acha kupotosha JF kwamba MUTUNGILEHI alipigwa mpaka anataka kufa huo ni uongo uliodhahiri MUTUNGILEHI alichfanyiwa ni kulazimishwa kujiudhuru na alipogoma ndipo nguvu ilitumika kumtoa madarakani na alipokuwa mbishi watu wote waliamaua mkutoa kwa nguvu ndipo kukatokea fujo kati yake na wanachuo na wengine kuanza kurusha viti na kadharika na ndipo alipotoka...na hata alipotoka aliendelea kuleta ubishi na marafiki zake wakamueleza uwezi kushindana na wengi... MUTUNGILEHI alishanunuliwa na serikali na hivyo FOE tulidhamilia kumtoa na kwa sababu viongozi wengi waliopita walikuwa mangwini na kwa sababu wengi waliishia kununuliwa na serikali... FOE tulidhamiria kumtoa na kuweka mwana FOE... SWEKE..
      SUBURIJIBU:
      Ndugu subirijibu hapo kwenye blue inaonyesha fika jinsi ulivyokuwa informer wa serikali na labda nikuite traitor uliyekubuhu... kumbuka una bahati sana kwamba ulimaliza chuo salama sehemu nyingine matraitor huishia kuchomwa moto...
      Wana FOE Walishagundua janja ya serikali ya kuwarubuni viongozi wa DARUSO na kuwafanya kushindwa kutetea masilahi ya wanafunzi na ku base kwa uongozi ... hivyo jitihada za makusudi ziliitajika ili kuungoa uongozi uliokuwepo ili kuleta uongozi utakaokuwa una msimamamo na kutetea haki za wanachuo wengi ukiwepo wewe.. wewe kwa mshangao mkubwa unadiriki kuandika jinsi ulivyokuwa informer wa kuwafahamisha serikali kuhusu mbinu za kuwakomboa wanachuo... kweli njaa ilianza kukusumbua zamani sana.

      SUBIRIJIBU; Nimekueleza mara nyingi kwamba class reps hawakwenda kudiscus tufanye mtihani huo siku ile ama la... tuliwatuma kuwaeleza watu wa math dept na dean kwamba utaratibu ulikiukwa kwa hiyo waahirishe mtihani... lakini uongozi wa FOE kwa kuwalinda wenzao wakalazimisha mtihani ufanyike masaa 3++ ... na ndio maana utaona ma class reps hawakufanya mtihani kwani walisimamia kauli ya wengi... na wachache matraitor na mainformer kama wewe mkaendelea kuwa wanyonge mbele ya uongozi kandamizi wa chuo...

      SUBURIJIBU; class reps hawawezi kuwaambia watu waende darasani halafu wao wasiende ... msimamo wa pamoja ulikuwa tususie mtihani... na ndio walioufuata.... wachache kama wewe mlitusaliti

      SUBURIJIBU; mimi nilikuwa electrical na kwetu sisi hesabu ni nyumbani kwake huo mtihani unaouita mgumu watu wengi wa electrical waliuona nyanya kabisa na ndio maana nasema sikubaliani nawe kwamba vurugu zilisababishwana mtihani wa calculus ambao kwa watu wa umeme ni nyanya kabisa...

      SUBURIJIBU
      ;sio kweli kwamba tuliwabana mbavu mbona wewe ulikwenda fanya mtihani... ni dhamira yao ya msimamo wa kusimamia maamuzi ya wengi ndio iliyowafanya wasusie mtihani... actually walifanya sahihi kama viongozi wanavyotakiwa kufanya ku sacrify kwa ajili ya wengi... na ndio maana nasema wewe haufai hata kuwa mjumbe wa nyumba 10


      nakutakia kazi njema
      Last edited by muonamambo; 2nd July 2012 at 16:14.
      KipimaPembe likes this.

    17. #74
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By NYENJENKURU
      Nilikuwa G211.Nimekumbuka mbali sanaaaaaa hayo yote nilikuwepo wakati yanatokea.Nakushukuru sana...kwa kunikumbusha hayo.Karungubare namkumbuka sanaaaaa yule msukuma.Magesssa nikuwanaye darasa moja na kwenye yaani namba yake ilikuwa 18X/T93 na mimi ilikuwa 19Y/T93..
      Mkuu,

      Nashukuru kwa mara ya kwanza amejitokeza mwana-G211 anakubali kwamba haya yote yalitokea. Huo ndiyo uungwana. Wenzako wamejitahidi vya kutosha kutaka kukana kwamba hayakuwa hivi. Matokeo yake wamejikuta wao kwa wao wanakuja na kauli zinazokinza. Mwingine anasema Lecturer hakufanyiwa fujo baada ya test ngumu na wengine wanakataa hakikutokea kituko hicho.

      Kuhusu namba labda nikukumbushe kwamba ni kweli mwaka ule namba zetu zilikuwa XXXXX/T93 kwa sababu tuliingia UDSM October 1993. Lakini mimi ninachokumbuka namba zetu zili-range kuanzia 14XXX/T93.

      Hivyo hata leo ukienda hiyo range ndiyo utakuta tumo mle japo nakubali kuna deviations kidogo. Karungubare unamuita ni msukuma kwa sababu sauti yake ilikuwa wazi ni ya kisukuma hadi unacheka ukimsikia. Lakini uzuri ni kwamba haikumzuia kutoa point zake kiasi kwamba kwa muda wa miezi michache aliyoishi pale alijulikana Chuo kizima

      Phenihas Magesa siwezi kusema kuhusu namba yake maana yeye ni mmoja wa athari za mgomo ule wa mwaka 1990 chuo kizima kilipofungwa kwa mwaka mzima na hivyo ikasababisha gap ya mwaka mmoja.

      Baada ya kumaliza JKT, Phenihas ilibidi akae mwaka mzima asubiri kuingia Chuoni na ndiyo maana utaona tulikuwa wengi yaani G211 na G72 yaani 211+72=283 per intake.

      Ni hayo tu kwako maadam hutaki kupindisha history kama wenzako sina matatizo na wewe.

      Ila angalia wanaweza sasa na wewe kukuita TRAITOR kuanzia sasa. Maana hawa mabwana G211 hawana definiton nyingine ya TRAITOR zaidi ya mtu asiyekubaliana na mawazo yao!
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    18. #75
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By client3
      [/LIST]

      nimependa kweli kwenye red
      nimejifunza kitu kwenye thread hii.....niliingia udsm mwaka 2000 tulikuta simulizi za (FoE sasa CoE) na harakati zao....natamani wanavyuo wa sasa wangapata bahati ya kupitia hapa angalau kupata picha ya pande mbili za harakati mbalimbali vyuoni..na jinsi gani mambo huwa before and after revolution.
      Mheshimiwa Client3,

      Nakubaliana na hoja yako kuhusu uanaharakati. Binafsi nimeamua kumwaga kila kitu kuonyesha hali ilivyokuwa na hata wanaharakati wa sasa wajue ni nini kinatakiwa unapofanya harakati zako, siyo vyuoni tu.

      Ukisoma post zangu zote kuhusu hili, zilizopita na hata zinazokuja, sijapinga hata sehemu moja uanaharakati.

      Mwanaharakati ni nani? Mwanaharakati ni yule anayeona kuna uonevu hata kama wenzake hawajauona. Baada ya kuuona anachofanya ni kuuanika wazi uonevu ule ili waonevu waaibike ikibidi waache.

      Zaidi anachoweza kufanya ni kuitisha gathering yoyote na ukaiita vyovyote yaani kikao, meeting, mhadhara, semina, au chochote ili mjadili anachowaletea.

      Wakati wa mjadala mwanaharakati anajiamini kwani wanakuwa wamesimamia ukweli na wanaofanya hivi hupata wafuasi wengi tu. Sina haja ya mifano mnawajua wote hata wa hapa nchini.

      Tuje kwa hawa G211. Kama wangekuwa ni wanaharakati basi uanaharakati wao wangeuanza siku ile ile test ilivyoonekana ngumu. Nimetaja waliotaka kumpig lecturer kwa tes ile. Hadi hapa hakuna anayebisha kwamba test haikuwa controversial.

      Niongeze kwamba hata tulipokuwa second year kuna lecturer mmoja wa somo linaitwa Mechanics alikuwa anaitwa Warioba, alitunga test ngumu na kweli kusingetokea marekebisho hali ingekuwa mbaya. Hili hawalikumbuki hawa G211 kwa sababu walikuwa wanatumikia adhabu home.

      Kilichofanyika tulikaa tukajadili coursework wote second year na Warioba akafanya kitu kinaitwa standardisation. Mrks zetu zikapanda na ninakumbuka mimi nilipanda hadi 75% wakati sikuwahi kufika huko.

      Ona tofauti hapa. Ni kwamba mambo ya ugumu wa mitihani yanajadilika. Hata waliokuja nyuma yetu akina Boss Masamila huyu Warioba aliwafanyia hivihivi lakini aka-standardise mambo yakawa sawa tukasahau tukaendelea na biashara nyingine.

      Hawa mabwana yaani G211 kwao haikuwa hivi. Hawakutaka tujadili ile test. Ninachohisi naona tayari kilishazungumzwa humu. Kuna mmoja G211 anadhani kunisema kwamba yeye alikuwa Electrical Engineering kwa hiyo test ile hawezi kuiita ngumu anadhani nitaghafirika.

      Ninakubaliana naye kwamba vector calculus ni nyanya kwa Electrical lakini hata sisi kwenye Fluid Mechanics huwezi kuifaule bila ile subject.

      Lakini huyu anasahau kwamba kama yeye aliona test ni rahisi basi tayari huo ni mparaganyiko na hata wangeitisha kikao kuijadili basi kunngezuka ubishi na huenda wasingekubaliana.

      Kibaya ni kwamba test ile ilikuw ni ya mwisho na hivyo kama ni kweli huyu aliiona rahisi basi coursework tayari ilikuwa imeshamvusha na wapo ambao hata University Exam wangepata sifuri (0) bado wange-pass.

      Ndiyo sababu suala la ile test halukjadiliwa kwa mwezi mzima uliobakia tukisubiri Univ. Exam

      Hivyo, hadi dakika tunakwenda kwenye Mathematics exam hakukuwahi kuwa na kikao kujadili lolote kuhusu hili. Uanaharakati gani huo sasa?

      Lakini kuna jambo wanalolificha wote hawa. Si kwamba hawakumuona Prof. Masenge aki-discuss kwenye ofisi ya Dr. Nzali. Mimi chumba changu kilikuwa opposite kabisa na ofisi ya Dr. Nzali na Prof. Masenge alikuwa humo tangu saa 3:00 hadi saa 5:300 mtihani ulipoletwa.

      Hivyo, kuchelewa kwa mtihani kulitokana na mabishano marefu maana Prof. Masenge alikuwa amedhamiria issue yetu ifikishwe kwenye senate tuadhibiwe kwa kitendo cha kumghasi lecture ambacho hawa G211 hawapendi kabisa tukitaje na hata kukitaja leo wanaona kama tumewaumbua wakati ni kweli kilitokea na sasa hawabishi.


      Hivyo, mimi nakataa concept kwamba hawa G211 walikuwa ni wanaharakati. Maana hata wao kwa wao hawawezi kusema uanaharakati wao ulianza dakika gani na kwa haki ipi.

      Kama kwlei walikuwa wanaharakati basi kwa nini hawakupigania haki ya kupewa upya mtihani baada ya kuuchanachana ule wetu? Kwa nini waliendelea kukaa chuoni wakiwa comfort bila kuchukua hatua nyingine zaidi?

      Je, uanaharakati wao ulianzia wapi? Nimesema hata baada ya kuchancchana mitihani walikaa tu na kuendelea na ratiba zingine. Siku ileile tukafanya paper ya Chemistry jioni ambayo peele alitaka kudanganya kwamba tulifanya mchana.

      Kesho yake tukaendelea na mitihani mingine kama kawaida. Kwa ujumla ratiba nyingine ya chuo na mitihani iliendelea kama kawaida hadi wote tukamaliza mitihani yote.

      tulipomaliza mitihani wote tukajidhani mtihani ule wa Maths utarudiwa kwa wote maana hatukujua kwamba Chuo kilikuwa na akili kuliko wao kwa kuchambua list ya G211 na sisi.

      Hadi hapa chuo hakijatangaza kumfukuza mtu. Hadi hapa hakuna uanaharakati wowote maana hata kutambua nani alifanya au hakufanya ilikuwa vigumu maana nia yao siku ile ilikuwa kuchanachana mitihani tuwea sawa.

      Uanaharakati wa G211 wanaousema ulianza baada ya siku kadhaa ilipotoka list ya wanafunzi 211 waliofukuzwa na list ya 72 wanaobaki.

      Wote hawa G211 wakajikuta hawana option ila kutafuta advocates wa kuwasaidia ili kupinga wasifukuzwe. Hapa inabidi uelewe vizuri. Si kusimamishwa ni kufukuzwa kabisa chuon on grounds za kimasomo yaa ABSCOND.

      Hivyo, hawakuwa na option kabisa isipokuwa kufungua kesi. Ninaamini thread hii inasoma hata na wabunge wengi tu maana wapo wanasheria walipelekewa kusaidia suala hili la hawa G211.

      Tuchambue sasa kwa akili zetu. Umoja wa uanaharakati ulianza lini? Umoja wa uanaharakati huo wanaousema ulianza siku majina 211 ayliotamkwa kwamba wamefukuzwa. Wote sasa mkakati wao ukawa ni kupinga kufukuzwa kwao. Wote sasa wakawa kitu kimoja maana lengo lao ni moja, kurudishwa Chuoni.

      Hivyo, ukichambua vizuri, hawakuwa na umoja ambao waliuunda wakasema huu tuuite G211. Walilazimika wakajikuta wanadai haki yao ya kurudishwa chuoni. Na kwa mara ya kwanza, hilo la kurudishwa chuoni likaanza kuwafanya wakae vikao, wachague viongozi na wasemaji wazuri, watafute wakili, wachangiane nk.

      Hata hela za kuchangia kesi yao mtindo ulikuwaje? Walibuni kwamba kwa sababu hela zinatolewa pale dirishani kwa bursurer basi wakajichagua baadhi wakakaa pale siku nzima, mtu ukitoka foleni kuchukua pesa unamkuta mwamkilishi wa G211 amekaa kama ombaomba unaandika jina lako na unawapa.

      Practical traininga huwa tunaenda Chuo kizima. Hivyo kumbe kwenye foleni walikuwa Chuo kizima. Hivyo kuchangiwa walichangiwa na yeyote yule wa Chuoni na wala si sisi tu waliotuita TRAITOR.

      Nimsema wazi kwamba kwa sababu hawa mabwana walitu-harrass vya kutosha na kupotosha ukweli mzima na kutuita sisi TRAITORS wakati hatujawahi kukubaliana mkakati wowote, binafsi sikuthubutu kuwachangia hata senti moja.

      Najua walinichukia sana lakini sikujali na hata leo sijafikiri kwamba kulikuwa na sababu ya kuwajali hasa wale ambao hadi leo bado wana mawazo yaleyale ya siku zile.

      Turudi kwenye uanaharakati. Uanaharakati gani wa kutumia ngumi, mateke, kuzomea au kupigana kama alivyotwangwa Mutungirehi.

      Au walitaka kumuiga Idi Amin aliyemwambia Julius Nyerere kwamba waacha kutuma wanajeshi wanaokufa bure waingie ulingoni wao wawili na idi Amini ana hakika atampiga Nyerere wakati Amin amefungwa mkono mmoja na Nyerere ana gloves mikono yote!

      Masumbwi, kung-fu, judo, matusi, kuzomea ni sifa ya wahuni na si wanaharakati. halafu hawa ukiwaambia ni wahuni kwa mujibu huo wanakasirika.

      Sijui watu gani hawa.
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    19. #76
      NYENJENKURU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Location : Tanganyika Masagati
      Posts : 936
      Rep Power : 606
      Likes Received
      182
      Likes Given
      359

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By SubiriJibu
      Mkuu,

      Nashukuru kwa mara ya kwanza amejitokeza mwana-G211 anakubali kwamba haya yote yalitokea. Huo ndiyo uungwana. Wenzako wamejitahidi vya kutosha kutaka kukana kwamba hayakuwa hivi. Matokeo yake wamejikuta wao kwa wao wanakuja na kauli zinazokinza. Mwingine anasema Lecturer hakufanyiwa fujo baada ya test ngumu na wengine wanakataa hakikutokea kituko hicho.

      Kuhusu namba labda nikukumbushe kwamba ni kweli mwaka ule namba zetu zilikuwa XXXXX/T93 kwa sababu tuliingia UDSM October 1993. Lakini mimi ninachokumbuka namba zetu zili-range kuanzia 14XXX/T93.

      Hivyo hata leo ukienda hiyo range ndiyo utakuta tumo mle japo nakubali kuna deviations kidogo. Karungubare unamuita ni msukuma kwa sababu sauti yake ilikuwa wazi ni ya kisukuma hadi unacheka ukimsikia. Lakini uzuri ni kwamba haikumzuia kutoa point zake kiasi kwamba kwa muda wa miezi michache aliyoishi pale alijulikana Chuo kizima

      Phenihas Magesa siwezi kusema kuhusu namba yake maana yeye ni mmoja wa athari za mgomo ule wa mwaka 1990 chuo kizima kilipofungwa kwa mwaka mzima na hivyo ikasababisha gap ya mwaka mmoja.

      Baada ya kumaliza JKT, Phenihas ilibidi akae mwaka mzima asubiri kuingia Chuoni na ndiyo maana utaona tulikuwa wengi yaani G211 na G72 yaani 211+72=283 per intake.

      Ni hayo tu kwako maadam hutaki kupindisha history kama wenzako sina matatizo na wewe.

      Ila angalia wanaweza sasa na wewe kukuita TRAITOR kuanzia sasa. Maana hawa mabwana G211 hawana definiton nyingine ya TRAITOR zaidi ya mtu asiyekubaliana na mawazo yao!
      Hapo kwenye red sikutaka kuziweka kwenye actual series maana najua zilanza na xxxx/T93.Kwenye magroup ya workshop FOE kwa mwaka wa kwanza nikuwa na Magesa na wengine INGAWAJE Magessa alikuwa aingie 92 akaingia 93 namba yake ilikuwa tofauti kidogo na za T93 nakumbuka sana...Maana yeye alisubiri mwaka mmoja kujiunga na chuo kutokana na migomo ya miaka ya Tisini.Asante sana mdau naona unawezakuandika kitabu kuhusu maisha wa wanaFOE.Naomba ufanye hivyo kama unaweza..tetetetetetehhh...Nim ekujua wewe ni EEHHHHH
      Jamani CCM hamshibi?Mnataka kula mpaka ukoko jamani?2015 byeeeeeeeeeee.

    20. #77
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By muonamambo
      Kaka KKITABU heshima mbele mkuu... Nafurahi kusikia ya kuwa ulikuwa Electrical engineering kama mimi.. pia nafurahi kusikia kuwa uliweza kukiri na kurudisha moyo nyuma na kuamua kuchangia wenzako waliamua kuwa mstari wa mbele kutetea masilahi na kuthaminiwa kama mwanafunzi wa chuo..

      Mchango wako ulifanikisha kurudisha heshima ya wanachuo na tangu wakati huo kukawa na adabu kwa wahadhiri dhidi ya wanachuo... hongera sana ... kwani kumbuka kufanya kosa sio kosa kosa ni kurudia kosa ... kama alivyofanya suburijibu kwa kuandika wenzake kwamba ndio waliosababisha yeye asifanye mtihani ili wenziwe wafukuzwe chuo na yeye aendelee kusoma.. tabia ya kujipenda nafsi yako zaidi kuliko wengine..
      Bado mko vilevile kama mwaka 1994 mkidhani mtapata wafuasi mnapopindisha ukweli. Nimesema kwamba niliwataja wale wote waliokuwa wanaongza harrasment.

      Sikiliza wewe muonamambo, sikuja hapa duniani kuvumilia uonevu wa maguvu yako kwa sababu mko kikundi kikubwa cha watu 211. Mlikuwa mnatukataza na kutufukuza madarasani wakati wa prep. Solgan yenu ni kwamba TRAITOR HATAKIWI KUINGIA NIGHT STUDY.

      Huu ni uendawazimu ambaye ni mwendawazimu tu anaywezea kuuvumilia. Sasa baada slogans zenu kuwa vitendo mlitaka tuwaache kimya.

      Kuna siku mlisikika baadhi kwamba hata siku ile ya kuchanachana mitihani mlikosea kwani mlitakiwa walau kumuua mmoja ili iwe mfano.

      Je mlitaka nikae kimya.

      Ni kweli niliwataja wengi tu si kwa kutumwa na serikali bali kwa usalama wangu binafsi. Na hata ikijirudia vievile leo nitawataja zaidi kama mtaleta ghasia za kuwaghasi wengine kwa kulazimisha.

      Ninachoshukuru ni kwamba tulichowafanyia G211 kilikuwa fundisho kwamba Engineering mjifunze kujenga hoja tushindane kwa hoja.

      Chuo kizima kilikuwa mmekishinda kwa ubabe. Na kweli ilifika mahala MANGIWNI wakasema "HAO ENGINEERING WANAWEZANA WENYEWE KWA WENYEWE"

      Mangwini waliwaogopa. Sisi hatukuona sababu ya kuwaogopa. Huwezi kutaka mimi nisifanye mtihani eti kwa sababu wewe umeamua. Ok, kama una haki kweli, basi lete hoja yako tuichambue tukusifie uzuri wa hoja hiyo.

      tukikataa endelea mbele na hoja yako na ukidhani utapata solutiona kwa magumi na mateke basi ni lazima tujilinde kwa kukutaja kitu ambacho kwa akili yako unaita ni u-TRAITOR!
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    21. #78
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By NYENJENKURU
      Hapo kwenye red sikutaka kuziweka kwenye actual series maana najua zilanza na xxxx/T93.Kwenye magroup ya workshop FOE kwa mwaka wa kwanza nikuwa na Magesa na wengine INGAWAJE Magessa alikuwa aingie 92 akaingia 93 namba yake ilikuwa tofauti kidogo na za T93 nakumbuka sana...Maana yeye alisubiri mwaka mmoja kujiunga na chuo kutokana na migomo ya miaka ya Tisini.Asante sana mdau naona unawezakuandika kitabu kuhusu maisha wa wanaFOE.Naomba ufanye hivyo kama unaweza..tetetetetetehhh...Nim ekujua wewe ni EEHHHHH
      Wapo ambao wameandika vitabu kuhusu maisha ya Chuoni pale. Kuna dada anaitwa Hoyce Temu aliandika kitabu aliandika sana kuhusu harrassment za UDSM.

      Yeye alimaliza Zanaki High School na akafaulu kwenda UDSM. Wakati anasubiri kuingia pale akaamua kujaribisha mashindano ya Urembo yaani Miss Tanzania kwa kanda ya D'Salaam.

      Ajabau akashinda akawa Miss Dar na hatimaye akawa Miss Tanzania wa mwaka huo yaani 1999. Mwaka huohuo akaingia UDSM yaani sisi tuliomaliza 1997 tukiwa tumeshatoka.

      Hoyce Temu aliandika mengi tu ambayo tuliosma pale tunakubaliana. Aliandika hata jinsi alivyofukuzw apale Chuoni.

      Mkitaka tuandika hili la G211 basi mkubali msiltete ule ubabe wa wenzako ambao naona humu bado wanao. Wakubali tugawane page. Nusu ya kitabu waandike kuhusu upande wao na sisi nusu inayobaki tuandike yetu.

      Kwa taarifa yako mimi ninacho kitabu cha Mzee Punch ambacho kinasimulia lile kunji (mgomo) la mwaka 1990. Hapo kinaelezea kuhusu maisha ya UDSM yote na lile kunji. Mkikitaka wadau niwamwagie kama tulivyomwaga cha Nyerere humu yaani {Uongozi wetu na hatima ya Tanzania}.

      Wasalaam
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    22. #79
      NYENJENKURU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Location : Tanganyika Masagati
      Posts : 936
      Rep Power : 606
      Likes Received
      182
      Likes Given
      359

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Quote By SubiriJibu
      Wapo ambao wameandika vitabu kuhusu maisha ya Chuoni pale. Kuna dada anaitwa Hoyce Temu aliandika kitabu aliandika sana kuhusu harrassment za UDSM.

      Yeye alimaliza Zanaki High School na akafaulu kwenda UDSM. Wakati anasubiri kuingia pale akaamua kujaribisha mashindano ya Urembo yaani Miss Tanzania kwa kanda ya D'Salaam.

      Ajabau akashinda akawa Miss Dar na hatimaye akawa Miss Tanzania wa mwaka huo yaani 1999. Mwaka huohuo akaingia UDSM yaani sisi tuliomaliza 1997 tukiwa tumeshatoka.

      Hoyce Temu aliandika mengi tu ambayo tuliosma pale tunakubaliana. Aliandika hata jinsi alivyofukuzw apale Chuoni.

      Mkitaka tuandika hili la G211 basi mkubali msiltete ule ubabe wa wenzako ambao naona humu bado wanao. Wakubali tugawane page. Nusu ya kitabu waandike kuhusu upande wao na sisi nusu inayobaki tuandike yetu.

      Kwa taarifa yako mimi ninacho kitabu cha Mzee Punch ambacho kinasimulia lile kunji (mgomo) la mwaka 1990. Hapo kinaelezea kuhusu maisha ya UDSM yote na lile kunji. Mkikitaka wadau niwamwagie kama tulivyomwaga cha Nyerere humu yaani {Uongozi wetu na hatima ya Tanzania}.

      Wasalaam
      Naomba mdau ukiweke hicho cha mzee puch bwana maana laaahh CHA MZEEE PANCHI mzee wa fuvu...kweli wewe noma.Kusuhu cha g211 niwazo zuri tukagawana page kama ulivyosema ni wazo zuri sana.Anyway endelea kutupa uhondo wa enzi hizo...za FOE hivi Makoleo yupo jamani yule jamaa wa ME na pia nasikia yule SUZY alikuwa anafundisha electronics workshop course kwa fist year anaPhd kwa sasa?
      SubiriJibu likes this.
      Jamani CCM hamshibi?Mnataka kula mpaka ukoko jamani?2015 byeeeeeeeeeee.

    23. #80
      MKALIKENYA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 714
      Rep Power : 502
      Likes Received
      282
      Likes Given
      409

      Default Re: Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

      Duh kweli iki Chama CHADEMA kimeanzishwa kuikomboa hii nchi watetezi wote wa wanyonge wa kipindi icho wapo CDM wanaendeleza harakati lakina kana kwamba haitoshi bado kizazi changu pale UDSM kimejaa CDM niwataje kwa ufupi SILINDE(MB MBOZI WEST),NASSARI(MB ARUMERU),KILEWO(KATIBU BAVICHA TAIFA),MWITA MWIKABE(MKURUGENZI SERA UTAFITI),DADO IGOGO(KIONGOZI MWANDAMIZI)..hapo bado kile kizazi cha kaka na dada zetu miaka ya 2000 mwanzoni ZITO KABWE,HALIMA MDEE,MUHONGA VIVA CDM ALUTA CONTINUA.
      Baro likes this.

    Page 4 of 8 FirstFirst ... 23456 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...