Basi ninashukuru kwamba thread yangu imeongeza idadi ya wanachama wa JF. Mimi niko humu JF mwaka wa tatu sasa. Nakushauri waite na wenzako G211 tuongezeke. JF kuna issues nyingi. Kuna wengine watakujibu kuwa thread kama hii mpelekee mke wako. Hata mimi nimeambiwa lakini muhimu kuna ambao mnakuja.
Kwanza Habari ya miaka mingi natumaini Maisha yanaenda vizuri maana ndiyo lengo langu. Sasa najibu hoja zako kama ifuatavyo
Mkuu,
Maleva nimemtaja kwenye issue nyingine kabisa yaani 1995 alipoukwaa u-Presidency of DARUSO wakati mimi tukio la Nkruma ni lile la October 1994 dhidi ya benedict Mutungirehi.
Ingawa ni kama vile unapinga lakini unaungana na mimi kwamba mlikaa kwenye balcon mkiwa kama washangiliaji maana ndiyo mlipatikana kwa shughuli hii. Mutungirehi alipoangushwa na viti wasichana ambao wengi ni wa arts (MANGWINI) walianza kulia. Binafsi niliamini amekufa. Nyinyi mlishangilia kwa nguvu zote na inaelekea mlitaka atoke pale maiti! Watu wa ajabu sana nyie. Mnashangilia mtu kufa.
"Ok. Mutungirehi ameshaokolewa akakimbizwa hospitali, je kuna sympathy yoyote mliyoonyesha. Not at all. Kumbuka kwamba hotuba zilikatisha na fujo na kelele zenu. Kilichofuata hapo kinaitwa anarchy yaani utaratibu ambao ni shaghala baghala. Yule bwana mkurya alivyouliza “
Sasa Kiongozi ni nani?”. Ukumbi mzima haukujua ujibu nini kwa sababu Hakuna aliyetarajia ile hali. Lakini nyinyi mkajibu kwa sauti moja kutoka kule juu balcon mkisema “
Mushi, Mushi, Mushi”.
Na kweli mkaonekana kana kwamba mmepitisha Azimio. Ndiyo maana tuliporudishwa nyumbani wengi tu waliwataja kwa kusema vijana wa Engineering ndiyo walioleta fujo. Ni kweli walitakiwa kusema hivyo hawakujua kuwa si Engineering wote. Watu kama sisi ndiyo tulifafanua kuhusu nyinyi kule balcon.
Kwa taarifa yako hata kabla ya vurugu hizi
mimi niliona chuoni hapakaliki na nilishatoa taarifa mapema kuhusu harassment zenu. Nafasi ya kuombwa kwenye barua ilikuwa ni mara ya pile tu na sikutaka kuiacha kuwatajeni na kamwe sintakijutia kitendo hicho.
Kwa taarifa yako. Baadhi ya G211 wenzako tulipokuwa salama niliwahi kuwakebehi kwamba wana ugonjwa wa mob physchology. Kwamba wanakuwa na moral wa kutusakama wakiwa kwenye kundi lakini kamwe hawathubutu wakiwa peke yao. Ndiyo maana baada ya chuo kila ukikutana na mmoja hataki kukumbushwa hili waziwazi maana anajua yuko peke yake na utambana kwenye angel ya ujinga wake
"Hallo, hebu mtafute Sweke au Karungubare pale CHADEMA wakukumbushe vizuri. Kitilinga nina miaka 15 sijui yuko wapi. Tatizo nyinyi G211 hamkujipanga na challenge nyingi ndiyo maana wenzako ambao wanaochangia humu watakushangaa unaposema hakukuwa na mazungumzo wakati ndilo jambo lililopoteza muda yaani saa 03:00 hadi saa 05:30."
"Eti mbona hawakufanya mtihani? Wangafanyaje wakati mliwabana kwa mabavu mkitetea wenzenu walioondokakijeuri wakisema liwalo na liwe hata mtihani ukija hawana time!
Statement yao ya kwanza ilikuwa ni twende tufanye mtihani kwa sababu hawakujua huku nje tumeparaganyika vipi. Nyinyi ndiyo mkawageuzi mawazo kwa kuwauliza
IWEJE TUFANYE MTIHANI WAKATI WENGINE WAMEISHAENDA HOME. Hapa ndipo mlipowabana lakini mimi hamkuweza kunibana kwa hoja hii maana hao walioondoka walitujibu kijeuri kwamba tutakalo na tulifanye.
"
.
"Sikatai kwamba ulikataa. Na kama ulikataa basi ni wazi kuwa ulikuwa ndani ya exam-room mapema na hukuwa nje kama sisi kusikiliza tutakachoamua. Ndiyo maana hata request ya kwanza ya Class reps hukuisikia kwamba twende darasani.
Lakini hapohapo hujagundua kwamba unajikanyaga. Huelezi kwamba kama ulikataa je uliendelea kukaa exam room au uli-quit. Kwa maana hiyo fujo ndani ya exam room ilianza mlemle kabla ya kule nje. Uongo mkubwa. Sasa kama ulikataa na ikatokea fujo, iweje fujo ichukue zaido ya dakika 40.
"
..
"Ukweli ni kwamba fujo ya kuingia kwenye vyumba vya mitihani na kuichanachana ilipoanza haikuchukua hata dakika tano. Mlijigawa kwenye vyumba kadhaa mkahakikisha inafanywa haraka kama umeme kiasi kwamba hamkuwa hata na haja ya kutujua bali mlikuwa na hajaya ya kuchanachana mitihani ukosekane ushahidi. Kwa hili nawapa hongera maana spidi yenu sijawahi kuiona.
Na ili fujo ikamilike lazima iwe ya muda mfupi maana askari wanegeweza kumwaga muda mfupi kabla hamjamaliza.
Nashukuru jinsi G211 mnavyojitokeza wengi kulitetea jambo hili mnajikuta mnajigonga humuhumu. Ona mwenzako alivyokana kwamba April 1994 hakukutokea fujo kwa lecturer aliyetoa paper ngumu. Soma comment number 3 ya huyu bwana (Click
hapa)
"
Mheshimiwa,
Naomba unapotunga uogo uwe muangalifu. Unajua hamkutarajia kwamba haya mambo iko siku yatawekwa wazi kama humu JF. Ona sasa usivyokumbuka.
Ni kweli siku hiyo kulikuwa na mtihani mwingine wa Chemistry. Na ni kweli mitihani ilikuwa ni masaa matatu. Hebu hata mtu asiyejua ratiba yetu. Hata kama tungeanza saa 3 maana yake tungemaliza saa 6. Kisha tukaenda kula na foleni ndefu za pale cafeteria! Kumbuka ratiba vizuri.
Mtihani wa Chemistry ulikuwepo kweli lakini ulikuwa unaanza saa 01:00 (19:00) jioni hadi saa tatu (21:00) na si saa nane (14:00) kama mnavyotaka kudanganya umma.
Kama Habari ya Yustus huijui muulize jamaa aliitwa Balozi akusimulie, Huyu najua yuko pale Enginering registration Board. Loti na Chapa sijui wako wapi.
Mtetezi pekee wa Yustus alikuwa jamaa anaitwa Waziri yaani classmate wake. Unashindwa kukumbuka inabidi ukumbuke kwamba Yustus alikuwa nyuma yetu mwaka mmoja na kama ulivyosema mlitaka G211 kuritishana mkagundua kuwa Yustus si mwenzenu hasa baada ya kugundua kuwa Yustus ana historia ya ulokole. Na ni kweli sasa hivi ana makanisa yake anahubiri alishaachana na u-engineering.
Ona hata unavyotumia terminology hapa. Unasema nisichokijua. Ni kweli nitaendelea kutojua kama mambo yenu mlikuwa mnayafanya kwa siri yaani caucas bila kuwashirikisha wengine. Leo ndiyo nimejua siri hii.
Haina ubaya caucas zenu za siri. Kosa lenu ni kwamba mkishatoka kwenye huo usiri wenu mlikuwa mnakuja kama tayari ni maamuzi kwa sisi wote, badala ya kutushawishi kwa hoja mnataka kutumia ngumi, mabavu au kuchanachana mitihani.
Ona unarudia mambo ya Exam ngumu kama lile suala lililoanzisha yote haya. Binafsi sijaongelea ugumu wa paper kama concern bali nimeongelea kama chanzo cha vurugu Tofauti na mlivyopotosha kwa miaka 18 sasa.
Hebu eleza ni ushirikiano gani unaohitajika ili mtu afaulu kuelewa jambo la kitabu kama vile masomo na afaulu. Unajua kuna dhana kwamba
Chuo Kikuu hawafaulu hadi waonyeshe ushirikiano wa kudesa au kuiba mitihani na aina yoyote ya forgery. Je ndiyo huo unaousema, kushirikiana madesa?
Hakuna aliyeongelea uwezo wa akili za darasani hapa. Na kama mlijidhani mnahitaji kushirikiana ili kufaulu basi iliwacost kisaikolojia na ndiyo maana sasa hivi mmeparaganyika sehemu mbalimbali duniani mnakuja humu JF kila mmoja anaongea lwake yaani lugha Tofauti kwa tukio moja.
Binafsi sihitaji ushirikiano na ubongo wa mtu mwingine kusoma kitabu? Huyo ninayehirikiana naye kuna kitabu gani duniani anaweza kukisoma na kukielewa halafu mimi nikikisoma sintaambua kitu! Jiamini bwana.
Mlikuwaje sasa mbona hamkukimbilia kupata haki yenu mahakamani ambako ni wiki sita tu zilipita mnasema mlishinda ile kesi yenu ya kituko cha April 1994?
Uamuzi wa kufunga Chuo na kuanza kushughulikia suala la Mutungirehi ulipendekezwa Seneti ya UDSM wakati huo ikiongozwa na Balozi Fulgence Kazaura. Prof. Masenge hakuwa final decision maker.
Follow Us Here