Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Report Post
    Results 1 to 19 of 19
    1. #1
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

      William Lukuvi leo mchana wakati anafanya rewinding kujibu hoja za wabunge ameeleza jambo moja kwamba wabunge wa CCM wasitishwe na kitendo cha wapinzani kuzunguka sasa nchi nzima.

      Lukuvi inaelekea alikuwa anajibu hoja wanayoulizwa kwamba "mbona nyinyi CCM hamzunguki wakati wenzenu wanazunguka nchi nzima".

      Katika majibu yake Lukuvi kaeleza kwamba wao CCM hawazunguki kwa sababu wana kazi ya kufanya. Wao ndiyo wameshikilia serikali na hivyo wako kazini. Wasio na kazi waache wazunguke na huko wanakozunguka watakuta matatito ambayo hawawezi kuyatatua bali watayaleta tena kwenye serikali ya CCM iyatatue.

      Ni kweli CCM ndiyo iko serikalini.

      Sijui kama Lukuvi aliwasiliana na watu kama Nape Nnauye. Kwani wao wenyewe humo ndani ya CCM wamelaumiana kwamba Nape kazi yake ni kuzunguka mara kuwapaka wengine matope, mara kuwaita watu mafisadi, mara kuwaambia watu kuwa wajivue magamba. Yote hayo ni hukohuko ndani ya CCM.

      Lakini kazi nyingine anayofanya Nape na wenzake ni kuzunguka walikotoka wapinzani iwe kimaeneo au kikauli. Kikauli ameanza siku hizi. Wenzake wamebuni VUA GAMBA VAA GWANDA yeye kaiga kwa kusema VUA GWANDA VAA UZALENDO. Hiyo ndiyo CCM. Kila mmoja na kaui yake maadam imetoka ubongoni ikateremka mdomoni.

      Lakini Lukuvi kama walivyo wana CCM wengi wanadhani bado tu wepesi wa kusahau. Lukuvi anasahau kwamba Bunge la Bajeti mwaka 2007 lilipoisha Serikali ilituma Mawaziri wazunguke mikoani kuhubiri umuhimu wa Bajeti. Ni kipindi kile ambacho Zitto kabwe kafungiwa miezi kadhaa na akatumia kifungo hicho kuzunguka huku na kule kama Godbless Lema anavyofanya sasa.

      Kilichotokea ni kwamba mawaziri hao walizunguka lakini wakaishia kuwa wanazomewa ovyo. Matokeo ya kuzomewa tumeyaona, kidogo nchi iwachomoke 2010.

      Sasa, Lukuvi inawezekana kasahau na anafikiri na sisi tunasahau. Anasahau kwamba kuna kitu inaitwa Jamii Forum na mitandao mingine anayoiogopa inakumbushana kila leo na inachambua kila kauli wanayotoa.

      Hivyo, Lukuvi lete kauli nyingine hii umepitwa na hoja. bahat nzuri mawaziri siku hizi mnaangalia JF kila mpatapo nafasi. Hivyo, wakati mnarudi mjengoni jioni leo jua kwamba wananachi tayari tumeshatoa tamko letu kama hili mitandaoni na kauli zenu zinapata majibu palepale hukuhuku mitandaoni mapema ndani ya dakika chache.
      Last edited by SubiriJibu; 29th June 2012 at 13:57.
      Daudi Mchambuzi and Sangarara like this.
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Andrew Nyerere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th November 2008
      Posts : 1,446
      Rep Power : 0
      Likes Received
      358
      Likes Given
      0

      Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

      Lukuvi ana wasiwasi wapo watu wanafikiria yeye sio kiongozi wa nchi hii,kwamba wako viongozi wengine. Sisi tunajua Lukuvi ni kiongozi. Hakuna mtu yeyote aliyekuwa kiongozi wa Tanzania katika siku hizi za karibuni isipokuwa Lukuvi na wenzake. Ndio maana haya makosa yote yanayotokea ni lazima walaumiwe wao.

      Na we sijui umewezaje kuandika all this stuff,kwa sababu Lukuvi amemaliza kuongea sasa hivi.
      SubiriJibu and Sangarara like this.

    4. #3
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

      Quote By Andrew Nyerere
      Na we sijui umewezaje kuandika all this stuff,kwa sababu Lukuvi amemaliza kuongea sasa hivi.
      Mkuu Andrew,

      Kwanza Shikamoo.

      Eti nimewezaje kuandika yote haya wakati Lukuvi kaongea dakika hii. Baba yako mzazi watu walikuwa wanamshangaa hivyohivyo. Kuna story nilisikia Marehemu Prof. Haroub Othman anasema student wa UDSM walimfuata pale Ikulu kumpelekea vitabu vipya kabisa halafu wavijadili.

      Akawapa time ya wiki moja warudi. Wanafunzi wale walidhani kwa sababu ya majukumu mengi ya ukuu wa kila kitu yaani head of state, head of CCM, Head of frontline states wakadhani hatapata muda wa kuvisoma.

      Wiki ikaisha, wakakaribishwa state house. Wakajadili na Kambarage kana kwamba ndiye alikuwa mwandishi wa vile vitabu.

      Huo ndiyo urithi tulioufuata wa tabia ya huyu marehemu mzee wetu kipenzi chetu, kipenzi cha watanzania, aliyeipenda Tanzania kuliko hata familia yake yaani watoto wake wa kuzaa kama nyinyi.
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    5. #4
      Maseto's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd April 2012
      Posts : 180
      Rep Power : 606
      Likes Received
      90
      Likes Given
      3

      Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

      Kile kitendo cha Lukuvi kumpongeza mwenyekiti wa kijiji aliyemzuia mbunge wa viti maaluma wa upinzani kufanya mkutano wa hadhara katika jimbo la Ismani la Lukuvi,hakikuwa sahihi na kilaaniwe kabisa.Mbaya zaidi Lukuvi ameahidi kwenda kumuona mwenyekiti huyo.Nadhani anataka kumpatia takrima.
      Mtu hatalaumiwa akidhani kuwa mwenyekiti huyu alitumwa na mbunge wake

    6. FJM
      #5
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,170
      Rep Power : 2568
      Likes Received
      5320
      Likes Given
      4585

      Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

      Quote By SubiriJibu

      Lukuvi kaeleza kwamba wao CCM hawazunguki kwa sababu wana kazi ya kufanya. Wao ndiyo wameshikilia serikali na hivyo wako kazini. Wasio na kazi waache wazunguke na huko wanakozunguka watakuta matatito ambayo hawawezi kuyatatua bali watayaleta tena kwenye serikali ya CCM iyatatue.
      Kazi nyingi za kufanya kama Mabwepande? Hata hivyo hao wanaozunguka wamekutana na tatizo, ni Dr Ulimboka, CCM wanatakiwa watatue ili tatizo.
      Mtumishi Wetu likes this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

      Quote By Maseto
      Kile kitendo cha Lukuvi kumpongeza mwenyekiti wa kijiji aliyemzuia mbunge wa viti maaluma wa upinzani kufanya mkutano wa hadhara katika jimbo la Ismani la Lukuvi,hakikuwa sahihi na kilaaniwe kabisa.Mbaya zaidi Lukuvi ameahidi kwenda kumuona mwenyekiti huyo.Nadhani anataka kumpatia takrima.
      Mtu hatalaumiwa akidhani kuwa mwenyekiti huyu alitumwa na mbunge wake
      Mkuu, naomba tusivuruge mada niliyoleta na kuwapa nafasi watu ambao mada imewafanya wakae kimya tofauti na tabia zao humu JF.

      Nimesikiliza vizuri ni kwamba yule aliyenyimwa nafasi kuhutubia hakuwa na kibali. Sasa utamtetea vipi. Mbona kwingine wengi wamenyimwa vibali na wakarudi. Jangwani wamenyimwa vibali mara ngapi.

      Cha msingi yule dada kama ni wa CHADEMA au vinginevyo basi aende aombe kibali arudi kuhutubia kijiji hichohicho alichonyimwa ndiyo utakuwa mwisho wa yote yale.

      Washabiki wa upinzani ndipo hapa mnapopotoka. Nchi nzima ina-sympathise kwa hoja zenu. Lakini msipitilize hadi kudhani kukosea taratibu kama vile kukosa kibali mtapata washabiki wa ku-sympathize na hilo.
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52
    #7
    Bajabiri's Avatarstyle="display:none;visibility:hidden;" data-cfsrc="images/icons/icon1.png" alt="Default" />
    Lukuvi ana wasiwasi wapo watu wanafikiria yeye sio kiongozi wa nchi hii,kwamba wako viongozi wengine. Sisi tunajua Lukuvi ni kiongozi. Hakuna mtu yeyote aliyekuwa kiongozi wa Tanzania katika siku hizi za karibuni isipokuwa Lukuvi na wenzake. Ndio maana haya makosa yote yanayotokea ni lazima walaumiwe wao.
    Na we sijui umewezaje kuandika all this stuff,kwa sababu Lukuvi amemaliza kuongea sasa hivi.
    huyu anaweza akabeba mikoba ya Pinda(endapo watafanikiwa 2015)

  • #8
    Nkba's Avatar
    Member Array
    Join Date : 8th December 2010
    Location : Wahapa hapa
    Posts : 25
    Rep Power : 434
    Likes Received
    2
    Likes Given
    5

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    hebu wapeni vidonge hao mahayawani sisiemu!!!

  • #9
    Nkba's Avatar
    Member Array
    Join Date : 8th December 2010
    Location : Wahapa hapa
    Posts : 25
    Rep Power : 434
    Likes Received
    2
    Likes Given
    5

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Lukuvi simpendi tangu akiwa RC wa Dom, coz alinichukulia demu wangu pale Udom alaf akamharibia maisha tu binti wa watu kwa kuridhika na kufuatwa na shangingi chuoni!

  • #10
    Sangarara's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 29th September 2011
    Posts : 3,312
    Rep Power : 1199
    Likes Received
    1182
    Likes Given
    1558

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Quote By SubiriJibu
    Mkuu Andrew,

    Kwanza Shikamoo.

    Eti nimewezaje kuandika yote haya wakati Lukuvi kaongea dakika hii. Baba yako mzazi watu walikuwa wanamshangaa hivyohivyo. Kuna story nilisikia Marehemu Prof. Haroub Othman anasema student wa UDSM walimfuata pale Ikulu kumpelekea vitabu vipya kabisa halafu wavijadili.

    Akawapa time ya wiki moja warudi. Wanafunzi wale walidhani kwa sababu ya majukumu mengi ya ukuu wa kila kitu yaani head of state, head of CCM, Head of frontline states wakadhani hatapata muda wa kuvisoma.

    Wiki ikaisha, wakakaribishwa state house. Wakajadili na Kambarage kana kwamba ndiye alikuwa mwandishi wa vile vitabu.

    Huo ndiyo urithi tulioufuata wa tabia ya huyu marehemu mzee wetu kipenzi chetu, kipenzi cha watanzania, aliyeipenda Tanzania kuliko hata familia yake yaani watoto wake wa kuzaa kama nyinyi.
    Mkuu, Haujatoa jibu. Na we sijui umewezaje kuandika all this stuff,kwa sababu Lukuvi amemaliza kuongea sasa hivi?
    SubiriJibu likes this.

  • #11
    SubiriJibu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 26th June 2009
    Posts : 270
    Rep Power : 768
    Likes Received
    192
    Likes Given
    163

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Quote By Sangarara
    Mkuu, Haujatoa jibu. Na we sijui umewezaje kuandika all this stuff,kwa sababu Lukuvi amemaliza kuongea sasa hivi?
    Mbona nilijiona kama nimetoa jibu. Baba yake Andrew aliturithisha elimu. Elimu kujizoeza hata kuandika au kusoma kilicholetwa mbele ya uso wako.

    Kama ni jibu mnalohitaji basi labda sijawaelewa, maana nimetumia dakika kama saba ku-draft na ku-click send button ya laptop yangu.

    Niko likizo wiki hii na hivyo naangalia bunge na mbele yangu kuna laptop.

    Labda mimi nimshange Andrew kwa sababu ameishi na baba ambaye huwa tunashangaa aliwezaje kutoa hotuba nyingi bila kuandika wakati viongozi wote waliomrithi hakuna mwenye uwezo kama huo.
    Sangarara likes this.
    ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

  • #12
    Daudi Mchambuzi's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 25th November 2010
    Posts : 6,175
    Rep Power : 1950
    Likes Received
    2994
    Likes Given
    13624

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Quote By SubiriJibu
    Mkuu, naomba tusivuruge mada niliyoleta na kuwapa nafasi watu ambao mada imewafanya wakae kimya tofauti na tabia zao humu JF.

    Nimesikiliza vizuri ni kwamba yule aliyenyimwa nafasi kuhutubia hakuwa na kibali. Sasa utamtetea vipi. Mbona kwingine wengi wamenyimwa vibali na wakarudi. Jangwani wamenyimwa vibali mara ngapi.

    Cha msingi yule dada kama ni wa CHADEMA au vinginevyo basi aende aombe kibali arudi kuhutubia kijiji hichohicho alichonyimwa ndiyo utakuwa mwisho wa yote yale.

    Washabiki wa upinzani ndipo hapa mnapopotoka. Nchi nzima ina-sympathise kwa hoja zenu. Lakini msipitilize hadi kudhani kukosea taratibu kama vile kukosa kibali mtapata washabiki wa ku-sympathize na hilo.
    mkuu kwa hiyo kibali cha mkutano kinatolewa na mwenyekiti wa kijiji?
    "Serikalii hii ni IMPOTENT kuanzia yule wa juu hadi walioko chini" by Dr. Slaa

  • #13
    SubiriJibu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 26th June 2009
    Posts : 270
    Rep Power : 768
    Likes Received
    192
    Likes Given
    163

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Quote By Daudi mchambuzi
    mkuu kwa hiyo kibali cha mkutano kinatolewa na mwenyekiti wa kijiji?
    Hoja ya Lukuvi ilikuwa ni kwamba yule kama mkuu wa serikali kwa kijiji hakuwa anajua lolote kuhusu huo mkutano.

    Huwezi kulitetea hili hadi uje na maelezo kwamba inapotokea hali hii kinatakiwa kufanywa nini.

    Huwezi kuukwepa ukweli anaoutete Lukuvi lakini na wewe eleza ni nini mipaka ya huyu mtawala kiserikali wa kijiji ama ile kata.

    Ni bora ukalichukulia hili kama precidence lifanyiwe kazi maana likiigwa kote yaweza kuwa balaa.
    ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

  • #14
    Daudi Mchambuzi's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 25th November 2010
    Posts : 6,175
    Rep Power : 1950
    Likes Received
    2994
    Likes Given
    13624

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Quote By SubiriJibu
    Hoja ya Lukuvi ilikuwa ni kwamba yule kama mkuu wa serikali kwa kijiji hakuwa anajua lolote kuhusu huo mkutano.

    Huwezi kulitetea hili hadi uje na maelezo kwamba inapotokea hali hii kinatakiwa kufanywa nini.

    Huwezi kuukwepa ukweli anaoutete Lukuvi lakini na wewe eleza ni nini mipaka ya huyu mtawala kiserikali wa kijiji ama ile kata.

    Ni bora ukalichukulia hili kama precidence lifanyiwe kazi maana likiigwa kote yaweza kuwa balaa.
    Bado hujajibu swali husika, je, kibali cha kufanya mikutano kinatoka kwa mwenyekiti wa kijiji???
    "Serikalii hii ni IMPOTENT kuanzia yule wa juu hadi walioko chini" by Dr. Slaa

  • #15
    SubiriJibu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 26th June 2009
    Posts : 270
    Rep Power : 768
    Likes Received
    192
    Likes Given
    163

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Quote By Daudi mchambuzi
    Bado hujajibu swali husika, je, kibali cha kufanya mikutano kinatoka kwa mwenyekiti wa kijiji???
    Sina hakika kama ni yeye anayetoa kibali. Ila nina hakika kwamba kama hakujua lolote kuhusu kuwepo kwa mkutano ana haki na uwezo wa kukataa.

    Labda nikuulize. Mwenyekiti wa Kijiji hana maguvu ya mwili kuzuia mkutano usifanyike. je, kama alikataa alitumia chombo gani kukataza mkutano? Kama ni polisi ambacho ni chombo cha dola, unadhani ilikuwaje chombo cha dola yaani polisi kikashindwa ku-sort out controversy ndogo ya kuruhusu mkutano kama kulikuwa na kibali rasmi.

    Kama kibali kilitoka juu na kisitoke kwa Mwenyekiti polisi wangeshindwa nini kulinda mkutano huo.

    Vinginevyo kama justice was not served basi hata wewe usingeishia kumtaja Mwenyekiti na ungeenda mbali hadi kuwataja polisi kwa irresponsibility ya kulinda mtu aliyekuwa ni halali kutumia eneo kwa mkutano.
    ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

  • #16
    IsayaMwita's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 9th March 2008
    Location : Tarime
    Posts : 1,046
    Rep Power : 871
    Likes Received
    82
    Likes Given
    6

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Unakosea, hakuna kibali chochote, isipokuwa unayetaka kufanya mkutano huu ni lazima utoe taarifa polisi, na hii ni kwa sababu ya kupewa ulinzi

  • #17
    maingu z's Avatar
    Senior Member Array
    Join Date : 2nd April 2012
    Posts : 136
    Rep Power : 387
    Likes Received
    20
    Likes Given
    101

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Quote By Maseto
    Kile kitendo cha Lukuvi kumpongeza mwenyekiti wa kijiji aliyemzuia mbunge wa viti maaluma wa upinzani kufanya mkutano wa hadhara katika jimbo la Ismani la Lukuvi,hakikuwa sahihi na kilaaniwe kabisa.Mbaya zaidi Lukuvi ameahidi kwenda kumuona mwenyekiti huyo.Nadhani anataka kumpatia takrima.
    Mtu hatalaumiwa akidhani kuwa mwenyekiti huyu alitumwa na mbunge wake
    Kwanza mkoa wenyewe anaotoka ndo wamechoka mbaya na baado wamekumbatia kijani ni wakuwaonea huruma angalia hata wabunge wanaotoka huko kama wakina LUSINDE, kweli hao watu wana akili timamu. waacheni wameshazoea kuishi kwenye vichuguu wameridhika. Kwahivyo ni wakusaidiwa tu njia rahisi wanayojua kuja kutusumbua kuomba omba.

  • #18
    KIJOME's Avatar
    Banned Array
    Join Date : 7th June 2012
    Posts : 1,324
    Rep Power : 0
    Likes Received
    244
    Likes Given
    220

    Default

    Quote By SubiriJibu
    Mkuu, naomba tusivuruge mada niliyoleta na kuwapa nafasi watu ambao mada imewafanya wakae kimya tofauti na tabia zao humu JF.

    Nimesikiliza vizuri ni kwamba yule aliyenyimwa nafasi kuhutubia hakuwa na kibali. Sasa utamtetea vipi. Mbona kwingine wengi wamenyimwa vibali na wakarudi. Jangwani wamenyimwa vibali mara ngapi.

    Cha msingi yule dada kama ni wa CHADEMA au vinginevyo basi aende aombe kibali arudi kuhutubia kijiji hichohicho alichonyimwa ndiyo utakuwa mwisho wa yote yale.

    Washabiki wa upinzani ndipo hapa mnapopotoka. Nchi nzima ina-sympathise kwa hoja zenu. Lakini msipitilize hadi kudhani kukosea taratibu kama vile kukosa kibali mtapata washabiki wa ku-sympathize na hilo.
    Tunatoa taarifa na si kupewa kibali.

  • #19
    SubiriJibu's Avatar
    JF Senior Expert Member Array
    Join Date : 26th June 2009
    Posts : 270
    Rep Power : 768
    Likes Received
    192
    Likes Given
    163

    Default Re: Lukuvi, CCM wanaogopa kuzunguka nchini, watazomewa kama September 2007

    Quote By KIJOME
    Tunatoa taarifa na si kupewa kibali.
    Unalotoa ni jibu rahisi sana ambalo sidhani kama brilliant people like CHADEMA mle bungeni wasingeweza kuinuka na kumpa Lukuvi kiitwacho TAARIFA ili kuweka hansard katika balance.
    ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

  • User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...