Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 34
    1. #1
      Allien's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2008
      Posts : 4,192
      Rep Power : 10788
      Likes Received
      1237
      Likes Given
      473

      Default Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Source: Ulimboka ana siri nzito

      Ulimboka ana siri nzito


      ASEMA ATAANIKA KILA KITU BAADAYE, ASEMA ACHWE APUMZIKE, MKUU WA JOPO LA MADAKTARI WANAOMTIBU ASEMA ALING'OLEWA KUCHA, MENO MAWILI NA KUPATA MTIKISIKO WA UBONGO



      MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari aliyetekwa nyara na kuumizwa vibaya usiku wa kumkia juzi, kisha kutupwa Msitu wa Pande, Dk Steven Ulimboka amesema atazungumza kwa kina yote yaliyomsibu baadaye na kuomba sasa aachwe auguze maumivu makali yanayomkabili.

      Dk Ulimboka aliokotwa na wasamaria wema juzi asubuhi katika Msitu wa Pande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, baada ya kutekwa nyara na watu waliokuwa na silaha akiwa katika Viwanja vya Klabu ya Leaders, Kinondoni.

      Jana, Dk Ulimboka ambaye amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili huku hali yake ikiwa haijatengemaa vyema, alitoa kauli akisema ingawa ana maumivu makali anaendelea vizuri ikilinganishwa na siku ya kwanza.

      Dk Ulimboka alitoa kauli hiyo baada ya kutakiwa aeleze mkasa huo uliomfika wa kukamatwa, kuteswa na kutupwa msituni.

      Hata hivyo, hadi sasa wingu zito la nani alimteka na watekaji walitaka kujua nini kutoka kwa kiongozi huyo wa madaktari, bado limetanda.

      Siri nzito

      Akisimulia mkasa huo kupitia Kituo cha Redio cha Clouds FM, Dk Ulimboka alisema, akiwa katika klabu hiyo ya Leaders alipigiwa simu na rafiki yake ambaye alikuwa atokee Tandika na baada ya kumsubiri ndipo alipofika kwenye klabu hiyo, lakini, alianza kujisikia vibaya tofauti na siku nyingine na kuongeza; "Yaani sikuwa na amani."

      Alisema, "Mara, katikati ya maongezi tukaona mtu anaongea na simu. Ghafla tukiwa tunasema tuagane, wakaja watu kama watano hivi na bunduki, wakasema wewe na yule bwana mko free (huru), tunakuchukua wewe (Dk Ulimboka)," alieleza na kuongeza:

      "Sijakaa sawa, nikaona nimeshaburutwa nikaanguka kwenye lami, wakaniinua na kuniingiza kwenye gari nyeusi, lakini halikuwa na namba."

      Hata hivyo, jana Dk Ulimboka hakuonana na mwandishi wa habari hii, badala yake alirekodiwa, na Mwananchi kupata sauti yake akijibu swali kuhusu hali yake na tukio hilo, baada ya uongozi wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi) kuzuia watu kumwona.

      Daktari huyo wa magonjwa ya binadamu, amelazwa katika chumba cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU).

      "Kidogo najisikia nafuu ikilinganishwa na nilivyokuja ingawaje, bado nina maumivu makali. Kwa hivyo, ingependeza niendelee na mapumziko na mtu yeyote anayetaka kuniona pengine hilo jambo lisifanyike sasa. Hivi sasa ni vizuri nipumzike," ilisikika sauti hiyo ya Dk Ulimboka.

      Lakini, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa wodini alikolazwa Dk Ulimboka, kuna ulinzi mkali wa madaktari na hairuhusiwi watu kumwona kiholela siyo tu kwa sababu za kutaka aachwe apumzike, bali pia kutowaamini watu ovyo.

      Madaktari wanaolinda eneo hilo walisikika jana wakisema, “Huyu tunamlinda wenyewe na haiwezekani mtu asiyefahamika kuingia humu ndani, na hilo tutahakikisha sisi wenyewe,”alisikika akisema mmoja wa madaktari hao.

      Kiongozi jopo la madaktari

      Katika hatua nyingine, kiongozi wa jopo la madaktari wanaomuhudumia Dk Ulimboka, Profesa Joseph Kahamba aliwaambia waandishi wa habari kuwa Dk Ulimboka ana majeraha mwili mzima.

      “Ingawa kwa sasa anaendelea vizuri, Dk Ulimboka ameumia sana, kwani mwili wake mzima una majeraha kutokana na kupigwa na watekaji hao,”alisema Profesa Kahamba na kuongeza:

      “Aliumia mbavuni,kifuani, miguuni, mikononi ambako aling’olewa baadhi ya kucha za vidole na kichwani na kinywani, ambako aling’olewa meno mawili,”alisema.

      Alifafanua kwamba, kutokana na maumivu hayo ya kichwa, Dk Ulimboka alipata tatizo la mtikisiko wa ubongo, lakini akasisitiza kuwa madaktari bingwa wanaendelea na harakati za kuokoa maisha yake.

      Uongozi wa Moi watoa neno

      Uongozi wa Taasisi ya Mifupa (Moi) umeeleza kuwa hali yake inaendelea vizuri ingawa bado amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi cha taasisi hiyo.

      Msemaji wa Moi, Almas Jumaa aliwaambia waandishi wa habari kuwa licha ya hali yake kuendelea vizuri, lakini haingewezekana kwa waandishi wa habari kuingia ndani ya chumba alikolazwa na kumwona Dk Ulimboka.

      “Mgonjwa anaendelea vizuri ukilinganisha na jana (juzi), anaongea, anawatambua watu wanaokwenda kumwona, lakini utaratibu wa kwenda kumwona kwa ninyi imeshindikana kwa sababu yupo (ICU) ni chumba chenye utaratibu wake,”alisema Jumaa.

      Jumaa aliongeza kwamba ili mtu aweze kuingia wodini analazimika kuvaa vazi maalumu na mavazi yaliyopo, yasingetosha, lakini pia wapo watu wanaoendelea kumpatia huduma ya matibabu.

      Tamko la Jumuiya ya Madaktari

      Wakati hali ya Dk Ulimboka ikiwa hivyo, madaktari wameipinga tume ya uchunguzi iliyoundwa na Jeshi la Polisi kuchunguza suala hilo, wakidai mazingira ya tukio hayaliondoi jeshi hilo kuhusika.

      Katibu wa Jumuiya hiyo, Dk Edwin Chitage aliwaambia waandishi wa habari kuwa wangependa kuundwa kwa tume huru itakayofanya kazi ya kuchunguza tukio hilo na kutoa taarifa kwa umma.

      “Madaktari kwa ujumla wetu tunalaani tukio la kutekwa nyara,kupigwa na kutupwa katika Msitu wa Pande, lakini pia hatuna imani na tume iliyoundwa na Jeshi la Polisi kwa sababu mazingira ya tukio hayaondoi kuhusika ama kutohusika kwa jeshi hilo,”alisema Dk Chitage.

      Chitage alitoa msimamo wa madaktari kuwa ni kuendelea na mgomo, huku akionya Serikali kuacha vitendo vya kuwatisha, kwa madai kuwa vitendo hivyo haviwezi kuwa suluhu ya mgogoro kati ya pande hizo mbili.

      “Kumekuwa na vitisho kwa madaktari katika maeneo mbalimbali nchini, hususan Dodoma, Mbeya, Arusha na Mwanza. Tunaionya Serikali kuacha mara moja na itambue kuwa mgogoro huo hauwezi kumalizwa kwa namna nyingine yoyote bali ni kwa Serikali kutekeleza madai ya madaktari,”alisema Chitega na kuongeza:

      “Sisi madaktari kwa umoja wetu, tumechoka kushuhudia Watanzania wakipoteza maisha kwa magonjwa tunayoweza kuyatibu, kufanya kazi katika mazingira magumu huku kukiwa hakuna mipango ya kuboresha mazingira ya kazi, kukosekana kwa dawa na vifaa tiba.”

      Mgomo huo wa madaktari leo unaingia siku ya saba tangu ulipotangazwa na mwenyekiti huyo kuwa, ungeanza rasmi Jumamosi iliyopita.

    2. Miaka 50

    3. #2
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,858
      Rep Power : 1844
      Likes Received
      593
      Likes Given
      413

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Kichwa cha habari hakiendi sawa na maelezo.............
      jovitha mussa likes this.

    4. #3
      nyabhingi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th October 2010
      Posts : 3,244
      Rep Power : 1295
      Likes Received
      1378
      Likes Given
      2668

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      kwa kauli hiyo ulinzi mkali unahitajika,lazima mkono wa pinda umo kwenye saga hii..
      Every nation in every region now has a decision to make: Either you are with us, or you are with the terrorists.George W. Bush


    5. #4
      Allien's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2008
      Posts : 4,192
      Rep Power : 10788
      Likes Received
      1237
      Likes Given
      473

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Quote By MAMA POROJO
      Kichwa cha habari hakiendi sawa na maelezo.............
      Tafsiri ya: ASEMA ATAANIKA KILA KITU BAADAYE

    6. #5
      Allien's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2008
      Posts : 4,192
      Rep Power : 10788
      Likes Received
      1237
      Likes Given
      473

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Hakuna mwanzo usio na mwisho . . . this too will come to an end in whichever way
      Mafie PM and gfsonwin like this.


    7. bdo
      #6
      bdo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2006
      Posts : 892
      Rep Power : 886
      Likes Received
      140
      Likes Given
      73

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      sitaki kujua Clouds walimuuliza maswali gani Dr.Ulimboka, ila nashangaa how clouds wamepata nguvu ya kumfanyia interview Dr.Ulimboka! wakati katika kipindi chao Power Breakfast - Jumatano/Alhamis)katika segment ya "jicho la Ng'ombe" Clouds FM waliponda, walilaani, na kudhihaki mgomo wa madaktari, na kwa tukio lililompata Dr. Ulimboka naamini kabisa Clouds FM wanaweza kuwa wamefurahi, na kwa mahojiano yao na Dr.Ulimboka ninawaona kama wanajikomba, na wanaona aibu - eti the people's station! Clouds ni kama TBC B
      Mafie PM and waziri/saidi like this.

    8. #7
      mbalu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Location : Ntuzu
      Posts : 214
      Rep Power : 396
      Likes Received
      98
      Likes Given
      68

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Tunamwombea apone haraka ili atutemee cheche hizo, asante sana kwa taarifa mkuu.
      Ong'wizukuru Shimba nawe Shimba.

    9. #8
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,745
      Rep Power : 1920
      Likes Received
      1180
      Likes Given
      972

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Mbo mbo ngafu Tz.
      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    10. #9
      kiogopeni's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th June 2012
      Posts : 31
      Rep Power : 354
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Hichi kinachotokea sasa ni jambo zuri. Natamani madaktari wengine wanaoleta matatizo wapate kipondo

    11. #10
      Inkoskaz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 6th November 2010
      Location : URT
      Posts : 4,435
      Rep Power : 7357
      Likes Received
      1081
      Likes Given
      1115

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Quote By kiogopeni
      Hichi kinachotokea sasa ni jambo zuri. Natamani madaktari wengine wanaoleta matatizo wapate kipondo
      Ufinyu wa kufikiri.....kaanze kipondo na mtoto wa mkulima ama vasco
      Thinking is the hardest work there is,which is probably the reason why so few engage in it!!

    12. #11
      BongoLogik's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2009
      Posts : 254
      Rep Power : 548
      Likes Received
      40
      Likes Given
      40

      Default

      Quote By kiogopeni
      hichi kinachotokea sasa ni jambo zuri. Natamani madaktari wengine wanaoleta matatizo wapate kipondo
      lazima utakuwa unaingiliwa kinyume na maumbile! Maana akili zako ni za hovyo ukidhani ni rahisi kumaliza mgogoro kwa kugawa vipondo, kazi ya udaktari haiwezi kufanyika kwa kulazimisha kama uko jela!
      Mafie PM and waziri/saidi like this.

    13. #12
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 14,976
      Rep Power : 3704
      Likes Received
      3582
      Likes Given
      5771

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Inasikitisha sana
      Allien nadhani ni vyema kichwa cha habari kikaongezwa maneno..
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..

    14. #13
      SILENT WHISPER's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 2,049
      Rep Power : 918
      Likes Received
      573
      Likes Given
      159

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      kama kweli polisi wanahusika....! madakari wasiwatibu polisi hata kama wakipigwa risasi na majambazi..! WAANDAE KABISA SINDANO ZA SUMU.....! kwa polisi na wanasiasa waliohusika..!
      Unstoppable and maingu z like this.
      POLITICIAN, ONE WHO SHAKES YOUR HAND BEFORE ELECTION AND YOUR CONFIDENCE LATER

    15. #14
      webondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2012
      Location : Chini ya mwembe
      Posts : 1,167
      Rep Power : 589
      Likes Received
      178
      Likes Given
      381

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      "Ulimboka atema cheche" Mbona tofauti na kilichoandikwa??

    16. #15
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,458
      Rep Power : 14610
      Likes Received
      2295
      Likes Given
      1505

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Quote By kiogopeni
      Hichi kinachotokea sasa ni jambo zuri. Natamani madaktari wengine wanaoleta matatizo wapate kipondo
      Nime type na kufuta sijui mara ngapi! Maana kila ninalotaka kukwambia naona halina uzito wa kutosha na nisingependa kupigwa ban. Bora tu nikuombee Mungu akusamehe.
      bakuza and Unstoppable like this.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    17. #16
      denyol's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th March 2012
      Posts : 16
      Rep Power : 365
      Likes Received
      2
      Likes Given
      9

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Quote By kiogopeni
      Hichi kinachotokea sasa ni jambo zuri. Natamani madaktari wengine wanaoleta matatizo wapate kipondo
      hili jukwaa litapoteza tija kwa kujaa watu kama huyu.... watu wanapigania maisha bora kwa kila mtanzania, mbali kabisa na maslahi ya chama au kijikundi fulani cha watu ndani ya serikali au nje. Mgomo huu pamoja na mambo mengine mengi unapata nguvu zaidi kutokana na taarifa mbalimbali za ufisadi wa waziwazi tunazozisikia kila ukicha. Walimu wangekuwa na nguvu pia wangeweza kugoma na cha moto mngekiona watu kama nyie mnaotetea uovu kwa ajili ya kuendelea kuwanyonya wanyonge wa nchi hii. Mabadiliko yatakuja ktk kipindi hiki hiki, mjiandae. It must be now or never!

      denyol
      Unstoppable likes this.

    18. #17
      denyol's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th March 2012
      Posts : 16
      Rep Power : 365
      Likes Received
      2
      Likes Given
      9

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      Quote By SILENT WHISPER
      kama kweli polisi wanahusika....! madakari wasiwatibu polisi hata kama wakipigwa risasi na majambazi..! WAANDAE KABISA SINDANO ZA SUMU.....! kwa polisi na wanasiasa waliohusika..!
      wapo polisi wengine wazalendo wala sio wote wenye nia mbaya sema mfumo unabana sana. Polisi wenyewe wanaishi katika mazingira magumu na ya aibu, unadhani wao hawapendi maisha bora? uhalifu mkubwa hufanywa na polisi wakubwa ambao hao wanatibiwa nje ya nchi wa na familia zao, sie wengine ni huku huku muhimbili.

    19. #18
      Ndakilawe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2011
      Location : Kumasi
      Posts : 470
      Rep Power : 493
      Likes Received
      53
      Likes Given
      63

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      if you want to know the "STATE",, touch it!

    20. #19
      JATULE's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5
      Rep Power : 354
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Dr. Ulimboka Kutema Cheche

      mh mh nawe fikiria kwanza kabla ya kuandika.

    21. Uda
      #20
      Uda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2010
      Posts : 435
      Rep Power : 1819
      Likes Received
      215
      Likes Given
      14

      Default

      Quote By kiogopeni
      Hichi kinachotokea sasa ni jambo zuri. Natamani madaktari wengine wanaoleta matatizo wapate kipondo
      hahahaha!ma dr watajitibu wenywf kwa wenywe hp umeona mfana kwa kamanda Ulimboka ww je nan atakutibu?huna fail bdo unaleta mdomo apa!kapime akili yako!
      Unstoppable and waziri/saidi like this.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...