wana jf,
Nathibitisha kua kupigwa kwa Dkt Ulimboka serikali ilihusika au kufahamu na kuruhusu itokee kwa sababu hizi:
Mgomo wa madaktari ni kitu kikubwa, kinahatarisha usalama wa nchi. Kiutaratibu vyombo vyote vya ulinzi vilipaswa kufanya uchunguzi
Katika uchunguzi wao viongozi wote wa madaktari walitakiwa kuchunguzwa masaa 24 haya yafuatayo:
1. Wanajadiliana na kupanga nini
2. Wanawasiliana na nani na kuongea nini
3. Wako wapi na wanafanya nini
Narudia, ni ktk masaa yote 24 na hii inahusisha vinasa sauti, eavesdropping, suprise meetings(kama huyo abeid wa ikulu), top classified field agents ktk taxi, wapiga debe, barmaid etc.
Pia kungekua na physical suspect tracking, kuwafatilia wako wapi na wanafanya nini muda wote.
upelelezi wote huu kitaaluma ungesimamiwa na vyombo vitatu tofauti, kila kimoja kikijiendesha kivyake kwa ajili ya kua na fair analysis wakati wa kumshauri mkuu wa nchi
1. Usalama wa Taifa
2. Idara ya ujasusi jeshini
3. police
kama taratibu hizi hazikufanyika, Tanzania haiko salama!
ushahidi wa kuhusika serikali
1. Abeid kutoka ikulu
2. Kuvamiwa Leaders (kumbe walikua wanamfatilia)
3. Watekaji kudai kawasumbua(ni kweli walikua na hasira kwa kuwalaza nje kumfatilia masaa 24)
4. Gari halikua na Plate no kusafiri umbali mkubwa(sio ishu sana), ila hizo bunduki na mazingira ya nyumba walizompeleka ni safe house
5. Kipigo alichopewa ni very pro, walipiga kama wanampiga jasusi mwenzao. (sina uhakika ilikuaje hawakutumia umeme)
6. Mabishano namna ya kumuua, kama ni kwa sumu au ajali(Kwa mfumo wetu wa ulinzi kama nilivyosema awali unahusisha vyombo vitatu tofauti. Napata hisia waliungana kumtesa ila kumuua wakatofautiana, kila chombo kina kiongozi wake na anafanya kazi kivyake bila kushirikisha upande mwingine)
7. Hakukua na maandalizi(kawaida ya serikali hii haipangilii mambo na viongozi kuamua kwa pamoja kama wanamuua ulimboka au hapana)
kama nimechemka, wanausalama wenzangu mtanisaidia

Reply With Quote




Follow Us Here