Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

    Report Post
    Page 7 of 13 FirstFirst ... 56789 ... LastLast
    Results 121 to 140 of 247
    1. #1
      vimon's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd April 2008
      Posts : 141
      Rep Power : 810
      Likes Received
      156
      Likes Given
      17

      Default Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Kamanda aliyehusika kumtesa Dr. Ulimboka na mmoja kati ya watu wanaounda tume ya kuchunguza unyama aliofanyiwa Dr. Ulimboka ameaibika mara alipoingia chumba alicholazwa Dr. Ulimboka aliweza kumtambua na kumwambia "Nirudishie simu na wallet yangu".

      Kamanda alitoka wodini kainamisha kichwa.

      Source (Mimi mwenyewe-nilikuwepo)

      =======

      Kutoka Gazeti la Mtanzania

      NI UNYAMA!

      *Dk. Ulimboka atekwa nyara, avunjwa taya na mikono
      *Ang'olewa meno na kucha kwa koleo, apasuka kichwa
      *Amtambua mmoja wa watekaji, asema aliwahi kumuona
      *Dk. Nchimbi alaani tukio, aahidi uchunguzi utafanyika


      MGOMO wa madaktari unaoendelea nchini umechukua sura mpya. Juzi usiku wa kuamkia jana, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Stephen Ulimboka, alitekwa na watu wasiojulikana.

      Baada ya kutekwa na kupigwa vibaya na watekaji hao, Dk Ulimboka alitelekezwa katika msitu wa Mabwepande, uliopo katika Manispaa ya Kinondoni, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

      Kutokana na tukio hilo, daktari huyo aliokotwa jana saa 12 asubuhi na wananchi waliofika eneo alikokuwa ametelekezwa.

      Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo, Msaidizi wa Dk. Ulimboka, Dk. Deogratius Michael, alisema:

      “Jana (juzi) usiku, tulikuwa na Dk. Ulimboka maeneo ya Leaders Club Kinondoni na ghafla walifika watu watano wakiwa ndani ya gari aina ya Suzuki Escudo lenye rangi nyeusi lisilokuwa na namba za usajili.

      “Watu hao walikuja mpaka mahali tulipokuwa na kujitambulisha kuwa ni askari polisi na wanamhitaji Dk. Ulimboka Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Dar es Salaam.

      “Baada ya askari hao kumchukua Dk. Ulimboka na kuondoka naye, sisi tulikwenda kituo hicho cha polisi ili kujua kwa nini wamemchukua, lakini tulipofika hatukumkuta na badala yake tulitoa maelezo na kuondoka.

      “Pamoja na kutomkuta, tuliendelea kumtafuta kwa njia ya simu lakini hakupatikana hadi tulipopigiwa simu leo asubuhi na msamaria mwema akitueleza kuwa Dk. Ulimboka yupo Mabwepande ametelekezwa na amejeruhiwa vibaya.

      “Nilipopokea taarifa hiyo, niliwatafuta watu wengine, tukaondoka kwenda Mabwepande na kumkuta Dk. Ulimboka akiwa na majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake na meno yote pamoja na kucha zikiwa zimeng’olewa na inaonekana walitumia ‘plaizi’ na tulipomchunguza vizuri, tuligundua pamoja na kung’olewa meno na kucha pia amevunjwa taya.

      “Nilipomuona sikuamini kama yule ni Dk. Ulimboka, alikuwa uchi na mwili mzima ulikuwa na majeraha makubwa, nilizungumza naye akawa anaongea kwa shida, lakini nilimuelewa.

      “Kwa mujibu wa Dk, Ulimboka, anieleza kuwa baada ya kuchukuliwa pale walianza kumpiga sehemu mbalimbali za mwili na kuishiwa nguvu na walipoona yuko hoi walianza kushauriana.

      “Walikuwa wanashauriana kwamba wampige risasi, wengine wanakataa, wakapendekeza wamweke barabarani na kumgonga na gari ili ionekane amegongwa na gari, mwingine akakataa, akasema wamdunge sindano yenye sumu na kumuua lakini pia hawakukubaliana.

      “Dk Ulimboka alinieleza kwamba, baada ya kutafakari yote walifikia uamuzi wa kumpeleka msitu wa Mabwepande baada ya kuonekana muda wowote anaweza kufariki na kumvua nguo zote na kuchukua simu zake zote,” alisema Dk. Deo.

      Kutokana na hali hiyo, alisema walitoa taarifa Kituo cha Polisi Bunju na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ili kupata gari la wagonjwa.

      “Jambo la ajabu ni kwamba, Muhimbili waligoma kabisa kutoa gari la wagonjwa, hivyo tukalazimika kukodi gari jingine la wagonjwa kutoka Kampuni ya AAR,” alisema.

      Alisema kampuni hiyo iliwapatia gari lenye namba za usajili T 151 AVD na kumleta Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kupata matibabu.

      Hata hivyo alisema hali yake wakati anafikishwa ilikuwa mbaya na alilazwa katika Chumba cha Wagonjwa mahututi (ICU).

      Hali ilivyokuwa Muhimbili

      Dk. Ulimboka alifikishwa hospitalini hapo jana saa nne asubuhi huku akisindikizwa na wanaharakati mbalimbali, wakiwamo Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Haki za Binadamu, Dk. Hellen Kijo Bisimba, Mkurugenzi wa Taasisi ya Sikika, Irenei Kiria na wengine wengi.

      Katika hali isiyokuwa ya kawaida, madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo waliangua vilio baada ya kumuona Dk. Ulimboka akiwa hoi na mwili wake ukiwa unavuja damu kutokana na majeraha mbalimbali.

      Vilio hivyo vilizua taharuki kubwa kwa wagonjwa na kusababisha huduma zote hata za dharura zilizokuwa zikitolewa hospitalini hapo kusimama, huku kila mmoja akitaka kumuona daktari huyo.

      Madaktari hao na wauguzi walipositisha huduma nyingine, walielekeza nguvu na utaalam wao katika kuokoa maisha ya mwenzao huyo, ingawa wengine walisikika wakilia kwa chini chini.

      Katika hospitali hiyo, waandishi wa habari waliokuwapo walizuiwa kufika katika baadhi ya maeneo kutokana na sababu ambazo hazikuwa wazi.

      Wakati hayo yakiendelea, madaktari na wauguzi jana walionyesha umoja wa hali ya juu, kwani walifurika hospitalini hapo kutoka katika hospitali mbalimbali, zikiwamo Amana, Mwanyamala kwa ajili ya kuongeza nguvu za kitabibu.

      Kutokana na wingi wa watu waliokuwa mahali hapo, ilifika wakati waandishi wa habari wakajikuta wamefungiwa ndani ya moja ya korido za Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI).

      Waandishi hao walipofungiwa katika eneo hilo, Dk. Ulimboka alitoroshwa kupitia mlango wa nyuma na kupelekwa kitengo cha maabara na X-ray.

      Askari apigwa na madaktari

      Wakati Dk. Ulimboka akiwa MOI ili kupatiwa matibabu, katika hali isiyo ya kawaida, mtu mmoja aliyekuwa ndani ya chumba cha matibabu alitoka na kuingia chooni na kusikika akizungumza na simu ya mkononi.

      Mtu huyo ambaye alionekana kuhusika moja kwa moja kutekwa kwa daktari huyo, alisikika akisema kuwa ‘Kumbe hajafariki, bado ni mzima, mimi niliwaambia tumchome sindano ya sumu nyie mkakataa, sasa bado yuko hai’.

      Mtu huyo bila kujijua kwamba alichokuwa akikisema kilikuwa kikisikika kwa madaktari, alijikuta akivamiwa na kundi la madaktari ambao walimhoji kisha wakampiga na kuvunja simu yake ya mkononi na simu yake ya upepo (radio call) aliyokuwa nayo.

      Kuna taarifa zinasema kuwa, mtu huyo alipoteza bastola aliyokuwa nayo.

      Kutokana na kichapo hicho, mtu huyo ambaye alikuwa amevalia suti nyeusi aliokolewa na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na kufungiwa kwenye kibanda cha walinzi wa getini na kufanyiwa mahojiano na kubainika ni Mkuu wa Upelelezi Kituo cha Polisi, Salender Bridge, ASP Mokiri.

      Baada ya mahojiano hayo, askari huyo alitoroshwa na askari wenzake kwa kutumia gari la kukodi yenye namba za usajili T 716 BKZ, huku akisindikizwa na gari la polisi lenye namba T 220 AMV lililokuwa na askari wenye silaha na mabomu ya machozi.

      Wakati wa tukio la kumtorosha askari huyo, waandishi wa habari walikuwa wakizuiwa kupiga picha, huku wengine wakitishiwa kupasuliwa kamera zao na baadhi ya waandishi walipigwa makofi na kusukumwa.

      Katika tukio hilo, askari huyo alichaniwa nguo na kutafutiwa nguo nyingine za kuvaa kwa kuwa zile suti zilichanwa na madaktari wakati wanampiga.

      Madaktari waandamana

      Wakati Dk. Ulimboka akipelekwa katika vyumba mbalimbali kwa ajili ya matibabu, madaktari walikuwa wakilisukuma gari alilokuwamo huku wakiimba nyimbo za mshikamano.

      Baada ya muda mfupi madaktari hao walikutana wenyewe na kuandaa tamko lao lililojumuisha Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) na Jumuiya ya Madaktari na kulitoa mbele ya waandishi hao wa habari.

      Akizungumza na waandishi hao, Rais wa MAT, Dk Namala Mkopi, alisema wamesikitishwa na unyama huo aliofanyiwa Dk. Ulimboka.

      “Kutokana na kitendo hiki cha unyama, tumeamua kuungana pamoja na kupigania maisha ya Dk. Ulimboka na si wengine tena, tunapenda kuwaambia Watanzania tunalaani kitendo hiki cha unyama na tukio hili limetuhamasisha kuwa imara zaidi.

      “Tumegundua hii ni mbinu maalum iliyoundwa na Serikali ya kumuangamiza Dk. Ulimboka na hii imedhihirika katika sura mbili, moja Muhimbili wamekataa kutoa ushirikiano wa kutoa gari la wagonjwa, pili tumempata askari akitoa taarifa kwa wenzake kwamba Dk. Ulimboka hajafariki na alitakiwa kuchomwa sindano ya sumu.

      “Kutokana na haya, sasa natangaza kuwa mgomo uko pale pale, kwani sasa umechochewa zaidi,” alisema Dk. Mkopi.

      Pinda: Liwalo na liwe

      Wakati hayo yakiendelea jijini Dar es Salaam, bungeni Mjini Dodoma, jana asubuhi, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliliambia Bunge, kuwa mgomo wa madaktari ulipofikia sasa ni pabaya na sasa bora litakalokuwa na liwe kuliko kuacha hali hiyo ikiendelea kinyume cha sheria.

      Alisema kuwa, leo Serikali itatoa kauli bungeni kuhusu mgomo huo kwa kuwa Serikali iliamua kukaa kimya ili kuona utekelezaji wa amri ya Mahakama ukitekelezwa.

      Pinda alitoa kauli hiyo baada ya Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi (CCM), kuomba Mwongozo wa Spika kuhusu mgomo wa madaktari unaoendelea nchini.

      Baada ya mbunge huyo kuomba mwongozo huo, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimuomba Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, atoe kauli ya Serikali bungeni hapo.

      Akizungumzia mgomo huo, Waziri Mkuu Pinda alisema Serikali imefanya jitihada kubwa, lakini dhamira kwa madaktari imeondoka na kwamba jana (juzi), serikali ilikutana na kutafakari jambo hilo na leo itatoa kauli yake.

      Dk. Nchimbi alaani tukio

      Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi, amelaani tukio hilo, huku akisema hivi sasa Jeshi la Polisi linaendesha msako mkali kuhusu tukio hilo.

      Dk. Nchimbi aliyasema hayo Mjini Dodoma, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

      “Jana asubuhi katika Kituo Kidogo cha Polisi Bunju, liliripotiwa tukio la mtu kupigwa katika Msitu wa Pande na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Juma Mgaza ambaye alikuwa amembeba Dk. Ulimboka katika gari yake.

      “Baada ya mahojiano ya muda Mgaza, alisema alikuwa akipita katika njia na kumkuta Dk. Ulimboka akiwa amepigwa na kumuomba msaada.

      “Baada ya kupokelewa hatua iliyofuata ni kuhakikisha anakimbizwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu.

      “Katu Serikali haiwezi kuvumilia vitendo hivi vya utekaji watu ambavyo ni kinyume cha sheria zetu za nchi na tunalaani tukio hili na hivi sasa tayari Jeshi la Polisi lipo katika msako mkali wa kuwatafuta wahusika wote wa tukio hili,” alisema Dk. Nchimbi.

      Akizungumzia tukio la kupigwa mtu ambaye alidhaniwa ni moja ya watekaji nyara wa Dk. Ulimboka, Waziri Nchimbi, alisema ni kweli mtu huyo alikuwa ni Ofisa wa Jeshi la Polisi na siyo kati ya waliokuwa wamemteka Dk. Ulimboka.

      “Yule ni Ofisa wa Jeshi la Polisi ambaye ni Mkuu wa Upelelezi wa Kituo cha Polisi Salender Bridge, yule ni ASP Mokiri ambaye alitumwa na mkuu wake wa kazi kwa ajili ya kufuatilia tukio hilo.

      “Kwa mujibu wa tarifa, alipofika pale na kuonekana ana radio call, baadhi ya madaktari walimvamia na kuanza kumpiga kwa kumtuhumu ni moja kati ya watu waliomteka Dk. Ulimboka,” alisema Dk. Nchimbi.

      Zitto Kabwe anena

      Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana jioni, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), alisema kwanza amepokea ujumbe mfupi wa simu.

      “Nimetumiwa ujumbe na daktari mmoja yupo pale MOI akisema hivi, kaka Zitto, hali ya Dk. Ulimboka yuko unconscious, multiple ribs fracture na kwenye mikono pia amevunjika pamoja na taya, yuko ICU wanamstabilise kwanza kwa sababu hapumui vizuri, the situation here is really bad, I agree with you this is outright outrageous,” ulisema ujumbe huo wa Zitto kutoka kwa daktari huyo.

      Pamoja na hayo, Zitto alisema amechukizwa na habari za kutekwa, kupigwa na kuumizwa vibaya kwa Dk. Ulimboka ambaye ni Kiongozi wa Madaktari Nchini.

      “Mambo kama haya tumezoea kuyasikia kwenye nchi za kidikteta na kuongozwa kiimla ambapo watawala badala ya kutumia njia ya kidemokrasia na kisheria, kushughulikia wanaoamini ni maadui zao katika utawala, hutumia wahuni katika taasisi za usalama kuteka raia, kuwatesa, kuwafunga na hata kuwaua.

      “Sitaki kuamini kwamba Tanzania imefikia huko, nimezungumza na baadhi ya madaktari walio karibu na Dk. Ulimboka na kujulishwa kwamba, majeruhi huyu alikamatwa jana usiku mnamo saa sita na watu wasiojulikana na kupelekwa katika msitu wa Mabwepande na kujeruhiwa vibaya. Habari hizi bado hazijathibitishwa na vyanzo huru lakini ndio zilizopo hadi hivi sasa.

      “Serikali inawajibika kueleza kama sasa imeamua kutumia njia za kihuni kumaliza matatizo na wananchi wake.

      “Nimemuomba Waziri kivuli wa Afya wa CHADEMA kufuatilia suala hili kwa karibu sana ili kuhakikisha kwamba ukweli wote na ukweli mtupu unafahamika. Kamwe hatuwezi kuacha Mtanzania yeyote aonewe, anyanyaswe au akandamizwe eti kwa sababu ya kudai haki yake na za wenzake, an injury to one, injuries to all.

      “Naomba madaktari wamwangalie kwa karibu daktari mwenzao ili aweze kupata nafuu. Ulinzi uimarishwe ili kuhakikisha usalama wake,” alisema Zitto katika taarifa hiyo.



      Wanaharakati walaani
      Akizungumzia tukio hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC), Dk. Hellen Kijo Bisimba, alisema wanaharakati wote wamelaani kitendo hicho na kusema kuwa huo ulikuwa ni mpango wa Serikali kwa ajili ya kuwanyamazisha wananchi.

      “Nilipokea simu saa 12 asubuhi kutoka Kituo cha Polisi Bunju, tulipofika tuliishiwa nguvu baada ya kumuona Dk. Ulimboka namna alivyokuwa amepigwa vibaya.

      “Huu unaonekana kuwa ulikuwa ni mpango wa Serikali kwa sababu hata Dk. Ulimboka alipohojiwa na kuzungumza kwa shida alithibitisha kuwa alimtambua mmoja wa watu waliokuwa wakimpiga kwani alimuona Ikulu wakati alipofika katika awamu ya kwanza ya mgomo wao.

      “Kwa sababu Dk. Ulimboka alisema kuna mtu aliyemtaja kwa jina la Abel ambaye alikuwa akimpigia simu mfululizo kwa muda wa siku tatu akitaka waonane ana kwa ana kabla ya kuitikia wito juzi na kutendewa unyama huo.

      “Kiujumla hiki ni kitendo cha kinyama ambacho hatuwezi kukivumilia, kwani Serikali imethibitisha kuwa kweli haiwajali wananchi,” alisema Bisimba.

      Alisema kutokana na hali hiyo wanaitaka serikali kuunda tume huru kwa ajili ya kuchunguza tukio hilo kwa sababu mazingira yake yana utata.

      Kwa upande wake, Mkurugenzi wa taasisi ya SIKIKA, Irenei Kiria, alisema serikali imeonesha kushindwa kutatua matatizo yaliyopo katika sekta ya afya na badala yake imeamua kutumia mabavu.


      KOVA: Tumeunda tume
      Kutokana na uzito wa tukio hilo, Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limewaomba wananchi Kutoa ushirikiano utakaofanikisha kupatikana kwa watu waliomteka Dk. Ulimboka.

      Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Suleiman Kova, alisema jeshi hilo limeunda jopo la wapelelezi linaloongozwa na Mkuu wa Upelelezi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Ahmed Msangi.

      Alisema kuwa, tukio hilo ni la kipekee na Jeshi la Polisi limejiandaa kukabiliana nalo na wahusika kufikishwa katika vyombo vya sheria.

      “Siku ya tukio walikuja watu akiwa kwenye club moja pale Leaders Club, wakamchukua kwamba wao ni polisi na wanampeleka Kituo cha Polisi.

      “Wakati wanaondoka, kwa mujibu wa maelezo yake, ndani ya gari kulikuwa na watu sita pamoja na yeye ambapo walianza kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili.

      “Dk Ulimboka aliendelea kueleza kwamba, walipofika eneo la Mwenge walimvisha fulana nyeusi usoni na kwamba hakujua tena walikokuwa wakielekea na hatimaye alijikuta yuko Msitu wa Pande.

      “Alisema kuwa, mmoja wa watekaji wake alimwambia watamuua na wakaendelea kumpiga sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kutumia ngumi na mateke na mwishoni walimuacha hapo na kisha wakaondoka zao.

      “Dk Ulimboka alieleza kuwa, baada ya kuwa ameachwa hapo, alijivuta na kufika barabarani na ilipofika majira ya asubuhi, ndipo huyo raia mwema alipomuokoa akiwa amefungwa kamba miguuni na mikononi na kumpeleka hadi Kituo Kidogo cha Polisi Bunju,” alisema Kova akimkariri Dk. Ulimboka.

      Habari hii imeandaliwa na Gabriel Mushi na Benjamini Masese, Dar es Salaam na Bakari Kimwanga, Dodoma.

      Last edited by vimon; 29th June 2012 at 00:10.


    2. #121
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,515
      Rep Power : 14625
      Likes Received
      2344
      Likes Given
      1530

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Quote By tatanyengo View Post
      MwaJ kuna baadhi ya hao wanaomhudumia yawezekana wakawa ni watu wa system, kaazi kwelikweli.
      Kweli kazi ipo! Ni kumuombea salama apone haraka atoke huko.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    3. #122
      zubedayo_mchuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2011
      Posts : 3,380
      Rep Power : 1070
      Likes Received
      601
      Likes Given
      45

      Default

      Quote By Communist View Post
      Mbunge mmuja akkisema bungeni koplo wa JWTZ ni eqivalent na Inspector wa Police. Hata wao hawjionei huruma.
      Hli kweli kbs nlsha ambiwa mwanajeshi mmoja hv

    4. #123
      50thebe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 609
      Rep Power : 540
      Likes Received
      174
      Likes Given
      871

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      aluuuuuuuuuu, Msangi huyu huyu wa kwenye tume ya uchunguzi? lol

    5. #124
      Mpangamji's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th May 2010
      Posts : 484
      Rep Power : 558
      Likes Received
      118
      Likes Given
      70

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Quote By Radhia Sweety View Post
      Katika mazingira kama haya, kila kitu kinachosemwa na Ulimboka kinaweza kuchukuliwa kuwa ni kweli.
      Katika mazingira gani kila kitu anachosema Pinda kitaonekana kuwa ni cha ukweli!!
      The truth speaks for itself, it is always in 3-D

    6. #125
      silver25's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2010
      Location : DSM
      Posts : 700
      Rep Power : 591
      Likes Received
      23
      Likes Given
      18

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Source please


    7. #126
      kikahe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd May 2009
      Location : Kanyi ko Ruwa
      Posts : 1,202
      Rep Power : 832
      Likes Received
      178
      Likes Given
      134

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Quote By Dauphine View Post
      ilitakiwa ale kichapo km mwenzie wa jana jamani
      Hizi ni hadithi zipeleke kwa magazeti ya udaku
      If Life gives you lemon, change it to Lemonade.

    8. #127
      Mwana_mapinduzi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th November 2011
      Posts : 15
      Rep Power : 386
      Likes Received
      5
      Likes Given
      0

      Cool Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Huyu msangi ni muuji wa kawaida na ni tabia yake. Kumtambua ni mwanzo mzuri wa kuanza mapambano yetu. Huyu ni adui namba moja wa madaktari na familia yake ni adui namba mbili. Kama aliazimia kuua na akaishia kutesa, kung'oa jino bila ganzi, kung'oa kucha, ni unyama tosha. yeye katumia bunduki, sasa ninyi madaktari bunduki yenu ni sindano. Msangi popote atakapotokea mdungeni sindano. hafai na hatumwihitaji.

    9. #128
      cement's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2012
      Location : Tanganyika-Dar es salaam
      Posts : 438
      Rep Power : 446
      Likes Received
      152
      Likes Given
      173

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Mh hili swala ni zito sana,kama ni kweli basi askari police wakiongozwa na IGP hawatufai watanzania,wamefanya hvy kumlidhisha nani?aliye leta usemi huu za mwizi ni arobaini alikuwa na akili sana na bado wataumbuka sana!ila kikubwa hapo coz mgonjwa wetu bado anaumwa sio busara hao askari kwenda kujulia hali wasubili apone ili awaumbue vizuri!

    10. #129
      JingalaFalsafa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th April 2012
      Location : Africa.
      Posts : 352
      Rep Power : 432
      Likes Received
      229
      Likes Given
      89

      Default

      Huu ni UNAFIKI MKUBWA na USALITI wa NAFSI YAKO na kwa UMMA wa WATANZANIA.
      Quote By vimon View Post
      Kamanda aliyehusika kumtesa Dr. Ulimboka na mmoja kati ya watu wanaounda tume ya kuchunguza unyama aliofanyiwa Dr. Ulimboka ameaibika mara alipoingia chumba alicholazwa Dr. Ulimboka aliweza kumtambua na kumwambia "Nirudishie simu na wallet yangu".

      Kamanda alitoka wodini kainamisha kichwa.

      Source (Mimi mwenyewe-nilikuwepo)
      Ulichukua hatua gani kama mzalendo...utapishanaje na mwizi mlangoni. Kama ni kweli UMEJIDHARIRISHA, na unastahili adhabu! Unategemea nani wa kupigania ustawi wetu kama sio mimi na wewe? Au unalinda kibarua chako, kwa gharama ya vifo vyetu! Fichua hekima yako, na si upuuzi wako! Umejidharaurishwa sana, we si askari wa moto vitani, hautufai.
      Mungu wetu anaita!

    11. #130
      MVUMBUZI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th January 2011
      Posts : 2,732
      Rep Power : 1122
      Likes Received
      726
      Likes Given
      380

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Huyo askari atafutiwe namna la sivyo mahakamani atashinda kama Zombe tu.
      Unstoppable likes this.

    12. #131
      UTAJUA's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th April 2012
      Posts : 66
      Rep Power : 376
      Likes Received
      17
      Likes Given
      82

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      KAMWE shetani hawezi kushinda
      Unstoppable likes this.

    13. #132
      Makame's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd January 2008
      Posts : 513
      Rep Power : 684
      Likes Received
      57
      Likes Given
      23

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Wewe Kama ulikuwepo wakati hayo yanatokea ulifanya NINI?

      Usilete mineno ya PROPAGANDA ZA KIHUNI

      Mtu alisikika akiongea na simu tu akatandikwa ; iwe huyu anayedaiwa wallet na simu???

      JAMANI

      LET US POST SENSIBLE THREADS

      Quote By vimon View Post
      Kamanda aliyehusika kumtesa Dr. Ulimboka na mmoja kati ya watu wanaounda tume ya kuchunguza unyama aliofanyiwa Dr. Ulimboka ameaibika mara alipoingia chumba alicholazwa Dr. Ulimboka aliweza kumtambua na kumwambia "Nirudishie simu na wallet yangu".

      Kamanda alitoka wodini kainamisha kichwa.

      Source (Mimi mwenyewe-nilikuwepo)
      God made Man, Man made Money, Money made man mad!

    14. #133
      Shekhe Gorogosi Jr's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Posts : 65
      Rep Power : 367
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Jamani tuhakikishiane habari hizi atiiiiiiiiiiii.... Isijekua na aliyeandika anataka kututeka tuuuu! Plz jamani unauhakika ulikuepo wewe sosi?
      Nitakununulia LAKUCHUMPA LAKUMPALAMA

    15. #134
      Jigsaw's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 17th June 2011
      Posts : 113
      Rep Power : 427
      Likes Received
      47
      Likes Given
      24

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Sioni sababu kwanini Waziri Mwinyi hahusiki katika hili. Katoka Jeshini kaingia Afya na wahuni wenzie. Kama Kova kaunda kikosi kazi nashauri kianze kwa waziri wa AFYA. Hakuna kuficha mambo.!!
      Tuko and Unstoppable like this.
      You think it is over, but the games have just begun !!!

    16. #135
      jigoku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2011
      Posts : 1,505
      Rep Power : 1018
      Likes Received
      377
      Likes Given
      537

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Leteni habari zenye mashiko,sio kupima hasira zetu humu JF.

    17. #136
      mareche's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2011
      Location : arusha
      Posts : 445
      Rep Power : 507
      Likes Received
      58
      Likes Given
      2

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      du ya kweli hayo au ni utaku humu jamvini

    18. #137
      tabu kuishi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Posts : 211
      Rep Power : 397
      Likes Received
      12
      Likes Given
      10

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Quote By wakuziba View Post
      hii thread ina uongo mwingi. kama shahidi ni wewe mwenyewe, jitokeze kwenye vyombo vya habari useme kwa uwazi kisha uende polisi...

      tuach kudanganyana ndugu zanguni
      Ungekuwa wewe ungekwenda kwenye vyombo vya habari?au unaongea tu tujue nawewe upo?wanaweza kuuana viongozi sembuse yeye mtu mdogo akajisemeshe kwenye vyombo ambavyo mwisho wake kifo kisichokuwa cha
      Mungu.Acha kuwm bolizozo kama nchi hii huijui au vinginevyo na wewe ndo wale2

    19. #138
      mtemiwaWandamba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd May 2011
      Location : MTONI RUIPA
      Posts : 429
      Rep Power : 497
      Likes Received
      76
      Likes Given
      66

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Kwa jijuavyo mimi, Utaratibu wa Idara ya Usalama wa Taifa huwa ina watu wametapakaa sehemu mbalimbali, Maofisi ya serikali hata watu binafsi, Shuleni, Vyuoni, Mahospitalini,Taasisi mbalimbali;orgaizesheni tofauti, ndani ya majeshi yote, ili wapate taarifa zao za kishushushu. Hivyo basi kati yao hao Madaktari, wauguzi,wafagizi, na wahudumu wengine ni miongoni mwao.
      Napatwa na shaka kama hadi muda huu huyo daktari ULIMBOKA hajawekewa sumu kwa njia yoyote ile.
      Maajabu ya Kenge; anakimbia Mvua anaingia Mtoni.

    20. #139
      mujuningaiza's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 14th March 2012
      Posts : 7
      Rep Power : 367
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      wiz m2pu nchi inaelekea kubaya, tuzd muombea Dr Ulimboka apate nafuu haraka

    21. DSN is offline
      DSN
      #140
      DSN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2011
      Location : Home Tanzania
      Posts : 1,443
      Rep Power : 4456
      Likes Received
      690
      Likes Given
      576

      Default Re: Dr. Ulimboka amuumbua mmoja wa wahusika wa utekaji wake!

      Quote By Return Of Undertaker View Post
      Nani nimesikia kumbe ni kweli usalama ndio wanahusika
      Ukisema usalama unaanisha POLISI au USALAMA!!Tanabaisha wazi manake POLISI ni usalama kwa maana ya lugha lakni haipaswi kutamkwa Usalama wakati kuna matumizi ya neno POLISI kwa ujumla wake.Usichanganye USALAMA kuwa POLISI.

    Page 7 of 13 FirstFirst ... 56789 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...