Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Madactari, Dr. Ulimboka anaendelea vizuri. Inasemekana Madactari wameendelea kupokea vitisho kwa njia ya sms. Mgaya (Katibu TUCTA) amesema wapo kwenye mchakato wa kuliwasilisha jambo hilo kwenye shirika la kazi Duniani (ILO)
Sasa mtu mmoja kula kipigo ndio hakuna amani, amani ipo tena kwa sana na CCM itahakikisha kuwa amani itaendelea kuwepo,usipotoshe umma kijana. Mnakaa kulaumu serikali bila hata kupata ushahidi wowote. CCM itatawala milele, na nyie CDM acheni uhaini,mtafia jela.
Kuna ushahidi gani unaouhitaji ili ujue kuwa Serikali ndo "the bad animal of this scandal"?
Suala hapa ni issue ya Dr. Je, Serikali hii inaongozwa na nani? na kwanini uingize CDM hapa?
Wakati fulani kukaa kimya ni HEKIMA kuliko kujibu UTUMBO hapa!! si lazima kila bandiko ukaja kuchangia...
“It’s now the moment for political baboons to see their backsides” - Time for politicians to look at themselves in the mirror! (Kenyan human right's activist)
Mungu amsaidie apone haraka. Mengineyo haki itatendeka hata ikiwa miaka mbele watajulikana, kina Kombe walifanyiwa mchezo kama huu..tumwombee Mungu apone.
Kwa sala na maombi ya yetu Watanzania wote wenye mapenzi mema na akili timamu, kweli Mwenyezi Mungu atamsaidia apone ili aje kuendeleza mapambano ya kudai haki.
MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
SASA NIMEAMINI KUWA TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA!!!!, TUANDAE KABURI LA KUIZIKA MWAKA 2015
Kwani wameumbuka kidogo? Mungu ndiye anayetupa na kuchukua uhai kwa sisi tunaoamini. Haya matishio mengine kama wengine hawatakufa hayana tija. Siamini kabisa katika kuteketeza maisha ya mtu au watu wengine....either kwa siasa, ujambazi, wivu au lolote lile!
Halafu mdunge mmoja akadiriki kusema eti kipigo hicho kinamstahili Huyo mbunge alaaniwe
Mkuu wangu najua sana kwamba nimeandika mambo mazito sana yanayouma lakini Ndivyo Ilivyo! Na tunaytakiwa kujifunza ktk kila jambo linalotupata hapa duniani maana kinachoendelea nchini haikina huruma kwa watu wengineo. Tazma picha utaona Dr.wetu kawekewa vifaa vya kila aina kuhakikisha anapata huduma ambayo kuna watu 100 hawaipati tena kwa sababu ya mgomo wa Madaktari...
Kwa kuhemu matukio tunayoishi sasa nisingeta kugeuza huu uzi uwe wa malumbano, lakini itoshe nikisema kuwa sijasoma hiyo post yako hapo juu. I just decided not to.
Kwa kuhemu matukio tunayoishi sasa nisingeta kugeuza huu uzi uwe wa malumbano, lakini itoshe nikisema kuwa sijasoma hiyo post yako hapo juu. I just decided not to.
Wabongo bana, so ndugu zetu wanaondelea kufa kutokana na mgomo wa akina Ulimboka hawana haki ya kuishi ama, mimi simuonei huruma huyu jamaa honestly, mgomo wao unawaumiza ndugu zetu sana, na simuombei kupona.
Sasa kama hutafahamu wapi ukimbilie kujinasua, basi wanakuponda.
Huyu jamaa anaweza hata kufa kwa mfano, ila bado tatizo halitakwisha.
Endelea kulaani na ghafla utasikia nyundo Mbaaang, wakati wenzio wanakwenda kutibiwa nje.
By Bollo Yang
Wabongo bana, so ndugu zetu wanaondelea kufa kutokana na mgomo wa akina Ulimboka hawana haki ya kuishi ama, mimi simuonei huruma huyu jamaa honestly, mgomo wao unawaumiza ndugu zetu sana, na simuombei kupona.
sasa itafika wakati hawa polisi tunaoishi nao mitaani tutawageuzia kibao kwa mishale ndipo watakapooacha kutumikia kila jambo ovu wanalotmwa na viongozi wao.WAKUMBUKE TUNAISHI NAO MITAANI,MAANDAMANO WANATUPIGA TENA HUKU URAIANI KWENY KUTAFUTA HAKI ZETU,AU KWA KUWA WAO HAWANA VYAMA VYA WAFANYAKAZI
Litania ya Huruma ya MunguBwana utuhurumie – Bwana utuhurumie Kristu utuhurumie – Kristu utuhurumie Bwana utuhurumie – Bwana utuhurumie Kristu utusikie – Kristu utusikilize Baba wa mbinguni Mungu – utuhurumie Mwana Mkombozi wa dunia Mungu - utuhurumie Roho Mtakatifu Mungu - utuhurumie Utatu Mtakatifu Mungu mmoja – utuhurumie. Huruma ya Mungu iliyo sifa kuu ya Muumba wetu - Tunakutumainia (iwe kiitikio) Huruma ya Mungu iliyo kilele cha ukamilifu wa Mwokozi wetu Huruma ya Mungu iliyo upendo usiopimika wa Roho Mtakasa Huruma ya Mungu fumbo lisilofahamika la Utatu Mtakatifu Huruma ya Mungu iliyo ishara ya uwezo mkuu wa Mungu Mwenyezi Huruma ya Mungu iliyofumbuliwa katika kuziumba Roho za Malaika wa mbinguni Huruma ya Mungu iliyotuumba na kutuamuru tuwepo bila kutokana na chochote Huruma ya Mungu inayotujalia maisha ya kutokufa Huruma ya Mungu inayotukinga na adhabu tunazostahili Huruma ya Mungu inayotuinua tutoke katika taabu, unyonge na maumivu ya dhambi zetu Huruma ya Mungu inayotufanya wenye haki katika Neno aliyejifanya Mtu Huruma ya Mungu inayofurika kutoka katika majeraha ya Kristu Huruma ya Mungu inayobubujika kutoka ndani ya Moyo Mtakatifu wa Yesu Huruma ya Mungu iliyotupatia Bikira Maria Mtukufu awe kwetu Mama wa Huruma Huruma ya Mungu iliyoonyeshwa katika kuanzishwa Kanisa Katoliki Huruma ya Mungu inayopatikana katika mafumbo ya Sakramenti Takatifu Huruma ya Mungu inayotolewa kwa wanadamu wote kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo na Kitubio Huruma ya Mungu inayotolewa katika Sakramenti ya Ekaristi na Upadrisho Huruma ya Mungu inayoonyeshwa kwetu pale inapotuita na kutuingiza katika kuwatakatifuza wenye haki Huruma ya Mungu inayotimilika katika ukamilifu wa watu watakatifu Huruma ya Mungu chemchemi ya afya kwa wagonjwa na wote wanaoteseka Huruma ya Mungu iliyo faraja ya wote wenye uchungu moyoni Huruma ya Mungu iliyo tumaini la roho zinazosumbuliwa na mkato wa tamaa Huruma ya Mungu iliyo mwenzi wa daima na popote wa watu wote Huruma ya Mungu inayowahi kutuletea neema zake Huruma ya Mungu iliyo amani yao wanaokufa Huruma ya Mungu iliyo burudisho na faraja yao marehemu wa toharani Huruma ya Mungu iliyo furaha ya mbinguni kwa watakatifu wote Huruma ya Mungu iliyo taji la watakatifu wote Huruma ya Mungu chemchemi ya miujiza isiyokauka Mwanakondoo wa Mungu uliyetuonyesha huruma yako kuu katika kuikomboa dunia kwa msalaba wako mtakatifu, - utusamehe ee Bwana Mwanakondoo wa Mungu unayejitolea kwetu kwa mapendo na huruma katika kila adhimisho la Sadaka ya Misa Takatifu,- utusikilize ee Bwana Mwanakondoo wa Mungu anayeondoa dhambi za dunia kwa njia ya huruma yako isiyo na mwisho,- utuhurumie. Kiongozi : Bwana utuhurumie – Wote: Kristu utuhurumie, Bwana utuhurumie. Kiongozi : Huruma anana za Bwana zi juu ya kazi zake zote – Wote: Huruma za Bwana nitaziimba milele. Tuombe: Ee Mungu uliye na huruma isiyo na mwisho, na hazina za wema na upendo wako hazina mipaka. Tunakusihi umtazame Stephen Ulimboka huku duniani na kumuongezea huruma yako tena na tena, ili imsaidie asije akakata tamaa hata mara moja, haidhuru akumbane na majaribu makubwa kiasi gani, bali aweze daima kuzielekea na kuzishika amri zako, kwa matumaini na kutimiza mapenzi yako matakatifu, ambayo ndiyo huruma yenyewe. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristu Mwanao, Mfalme wa Amani na Huruma, aishiye na kutawala nawe, na Roho Mtakatifu, kwa pamoja mkituonyesha huruma, daima na milele. Amina.
mungu wetu aliye kila kona atamponya dr. kama alivyomnusuru katika kifo, hii ni laana hakika, serikali ya mabavu inataka kuharibu amani katika nchi yetu..mungu isaidie tanzania..mungu mponye dr. ulimboka...amen
Mbegu lazima ife, ili izae zaidi. Tunakuombea upone, ingawa hata kama Mungu akipenda vinginevyo, mbegu utakayotuachia haitakufa, bali itazaa zaidi.
"MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBARI, RIP TANZANIA"
Follow Us Here