Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

    Report Post
    Page 7 of 9 FirstFirst ... 56789 LastLast
    Results 121 to 140 of 172
    1. #1
      Vancomycin's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 168
      Rep Power : 461
      Likes Received
      108
      Likes Given
      22

      Default Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Taarifa ambazo zimethibitishwa zinatabanaisha kuwa madaktari walio katika uzoefu kazini, INTERN doctors wameanza kufukuzwa katika hospitali mbalimbali ambapo katika hospitali ya DODOMA madaktari 11 kati ya 33 wamefukuzwa na madaktari wote 70 waliokuwepo hospitali ya rufaa mbeya chini ya ulinzi mkali wa polisi wameambiwa waondoke kufikia saa 11 jioni ya leo wakati huo huo mkurugenzi wa hospitali ya BUGANDO amewafukuza madaktari wote 44 na kuwataka warudi wizarani wakati madaktari waliosajiriwa wameamuriwa kufika kesho wawe kazini au la wanafukuzwa.

      Wakati huo huo madaktari wakazi waliitwa na senate ya BUGANDO na kulazimishwa kurudi kazini lakini walikataa mbele ya senate hiyo hivyo wakaambiwa watafutiwa udahili wao na wote kwa pamoja wakapiga makofi wakisema wako tayari kwa hilo.

      Habari zaidi zinazidi kupasha kuwa hospitali ya Mwananyamala wameletewa fomu za kujaza kama wako tayari kuendelea na kazi au la,ila madaktari wamesimamia msimamo wao huo kuwa mgomo uko pale pale.

      Katika hatua nyingine CHUO CHA TIBA BUGANDO NA KILE CHA MUHIMBILI VIKO MBIONI KUFUNGWA kutoka na walimu wao ambao ni madaktari kugoma na mazingira kutokuwa rafiki kwa kujifunzia.

      Wakati hayo yakiendelea taarifa zinasema hsopitali ya Tanga BOMBO imeingia rasmi kwenye mgomo na ile ya MOUNT MERU

      Habari zaidi madaktari wanajiandaa kwa mass resignation muda wowote


      BAK, Papizo, Bantugbro and 14 others like this.
      'Kuuza Ardhi ni kuuza uhuru wetu na haki zetu kwa sababu tu viongozi wamechoka kufikiri' Said A. Arfi,CDM 22/11/'11


    2. Miaka 50

    3. #121
      Makala Jr's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th August 2011
      Posts : 1,616
      Rep Power : 714
      Likes Received
      334
      Likes Given
      0

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Mungu ibariki Tanzania na watu wake japokuwa kati yao haoni alama za nyakati. Uwezo wa viongozi wa ccm ndo ulipofikia!

    4. #122
      MWANA WA UFALME's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th September 2010
      Posts : 365
      Rep Power : 514
      Likes Received
      65
      Likes Given
      34

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      kwahili nani ni mshindi?

    5. #123
      jouneGwalu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Location : Studio
      Posts : 2,341
      Rep Power : 969
      Likes Received
      1314
      Likes Given
      1755

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Quote By BAK
      Nani amekwambia kuna watu tunasheherekea mgomo wa madaktari? Madaktari wanaomba kulipwa mishahara ambayo inaendana na taaluma yao ili waweze kukidhi gharama za maisha na pia kupewa vitendea kazi na kuboresha hospitali zetu ambazo zote ziko katika hali ya kutisha...Iweje Mbunge ambaye hajaenda shule apate mshahara mkubwa kuliko daktari aliyesota vyuoni miaka chungu nzima ili kuhitimu katika taaluma yake?

      Hakuna hata Mtanzania mmoja anayesherehekea mgomo wa madaktari bali tunawaunga mkono kwa vile tunayaona madai yao yote yana umuhimu mkubwa katika kuboresha sekta ya afya nchi.
      Mkuu umenifanya nitie neno hapa!

      Huyo mtu uliyemjibu anawakilisha fikra halisi za mtanzania wa kawaida....

      Mkuu wangu BAK, jamii hii inaundwa na aina ya watu wenye fikra dhoofu, zilizojaa uoga na unyonge wa hali ya juu.
      Sijui Mungu alitumia sample ya udongo wa wapi kuumba watu wa namna kama yetu watanganyika (Ndio wazenji nimewatoa wao hawapo kama sisi).....

      Tumekuwa watu wa kuamini kuwa sisi hadhi yetu ni "kidogo" , sisi ni "masikini" na mambo mengine mbona "kama kawaida tu"...
      Mtu akifuatilia malalamiko tuyowalalamikia Madr leo hii anaweza kudhani kuwa hii nchi tatizo kuu letu kwa sasa ni madr tu ila vitu vingine kwenye sekta hii viko safi...

      Tupate mwanga wa kuona mambo katika picha kubwa watz wenzangu ;


      • hatustahili kulala zaidi ya mtu mmoja kwenye kitanda kimoja hospitali
      • Xrays na mitambo mingine yote ya kiutendaji ifanye kazi kwa wakati wote
      • Madawa yote stahiki yapatikane kwa wakati tena kwenye eneo husika
      • Sehemu yoyote yenye kutolewa huduma ya afya lazima pawe na hadhi na paheshimiwe
      • nk.... nk......nk


      Kama japo kwa udogo tu watz tungekuwa tunaamini katika hayo niliyoyataja hapo basi naamini hamna mtu ambaye angewaona madr ni watu wa ajabu katika madai yao na naamini kuwa watz wote tungewaunga mkono tena kwa msukumo mkubwa sababu tungeona haki yetu kubwa kwenye madai yao ......

      Ila kwa bahati mbaya sana jamii yetu iliyo athirika na utapiamlo wa fikra kwa kubemendwa na utawala wa kichovu wa ccm, haoni mambo katika ngazi hiyo jamii nzima inaamini saiv adui namba moja ni Madr sababu wamezuia aina yao ya maisha ya "kama kawaida"..... Madr wapo kwenye mchakato wa kukata laana ya unyonge na maisha ya kudharirika ambayo yamejishikanisha na maisha ya kila siku ya Mtz...

      Wito kwa waandishi wa habari, wabunge na idara nyingine za fikra za taifa hili si sahihi kuendelea kulisha sumu umma kuwa eti madr wanapigania maslahi yao tuu
      ..

      Pia kwa watz wenzangu tuache kuamini kuwa tunastahili kitu cha chini na cha hovyo... hapana... sisi ni wa thamani kama walivyo wazungu au wahindi au wachina na tunastahili huduma bora kama watu wa mataifa mengine, tukijidharau hakuna anayeweza kutuheshimu!
      BAK, Tekelinalokujia and Communist like this.
      Music affect the lives!!

    6. #124
      Tekelinalokujia's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Location : Planet Earth
      Posts : 344
      Rep Power : 510
      Likes Received
      30
      Likes Given
      166

      Default Re: Madaktari wafukuzwa mbeya,bugando na dodoma......mwananyamala walazimishwa kusaini,vyuo vya udak

      Quote By Kapeleka
      Kufukuzwa madaktari siyo dawa, ila ni funzo. Hakuna haja ya wao kuendelea kuitwa watumishi wa umma wakati hawautumikii umma. 'Fukuza woooteee, kuanza upya si ujinga' Mjomba aliimba. Sifurahii kupigwa Dr. Ulimboka, ila ni funzo kwao na njia ya wananchi kuonesha uchungu wanaoupata kwa mgomo wao. Madaktari hawapaswi kutumia wagonjwa kama kiboko cha kuichapia serikali kwa madai yao hata kama yanamsingi kiasi gani. Sasa je, wamegoma kumuudumia Dr. Ulimboka alipopata matatizo yanayowapata watanzania wengi.

      Nakubaliana na unamuzi wa madakatari kufukuzwa wote wanaogoma, na hata wakitaka kujuizuru wote sawa. Serikali ijipange hata kwa gharama kubwa kuwaleta madaktari kutoka majeshi ya nchi marafiki na mashirika km red cross kusaidia wakati suluhu ikitafutwa ya kudumu.

      Wewe unaongea FYONGO tuu wala hujui unalosema, kwanza sio wananchi waliofanya hayo ili kuonyesha hisia zao na pili kama unadhani madaktari wotee wakifutwa kazi na serekali kuanza moja kwa gharama yoyote unakosea mazima, mpaka sasa haya matatizo ni sababu serekali inashindwa kugharamia hao madaktari na miundombinu bora za huduma ya afya, sasa watawezaje kujipanga kwa gharama kubwa kuanza moja? acha kuwachukulia madaktari kama wako katika fani ya kitumwa, ile ni ajira kama ajira zingine wao sio malaika.

    7. #125
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Kwa nchi maskini kama Tanzania nadhani mgomo huu utakuwa kipimo cha mambo mengi sana na hakika mwisho wake ndio utatupa majibu. Binafsi yangu sintaunga mkono mgomo wa Madaktari ikiwa swala zima linatanguliwa na ongezeko la mishahara yao. Kama kweli sababu nyinginezo ni vyombo vya kutendea kazi, mazingira ya kazi na kadhalika, ilikuwaje walikubali kurudi kazini ambako hakuna vyombo vya kutendea kazi wala mazingira bora kwa afya zao na waginjwa?. Hivi kweli mtu unaweza vaa koti lako la udaktari ukijua fika kwamba mgonjwa unayemtibu hatapona kwa sababu hakuna vifaa, na unayaweka maisha yako hatarini lakini upo radhi kupokea mshahara wako kwa mwezi Ukisubiri JK ataongeza mishahara na kuleta vifaa baadaye!

      Madaktari mtanichukia sana na wala maneno yangu hayampendezi mtu, isipokuwa nashindwa kabisa kuunganisha dots za mgomo huu na ule wa mwanzo kiasi kwamba walitaka kwanza mawaziri wajiuzuru ndipo mazungumzo yafuatie pamoja na kwamba tuliwaonya hapa kijiweni ya kwamba hili ni swala la kimfumo kuondoka kwa waziri na naibu wake hakuwezi badilisha kitu. Wao ni wafanyakazi waliochaguliwa na rais na wanafuata maagizo na mpango wa serikali ktk kutoa fedha za hutuma hiyo.

      Lakini maajabu mkatuona majuha mkaenda Ikulu mkanywa juice na JK mkatoka huko na furaha tele baada ya sisi weniungine potozewa na ndugu na jamaa zetu kwa kile mlichodai ni haki yenu na sijasikia haki ya Wananchi japokuwa vipengele vyenu vinatujumuisha sote. Nasikitika sana kuona hali hii imefikia hapa lakini binafsi yangu nilijua tutafikia hapa. Na kwa bahati mbaya sana watu wamepoteza maisha wengine (kina Ulimboka) ndio mahtuti kwa jambo ambalo lingeweza kabisa kutatuliwa kisiasa zaidi kama vyama vya Upinzani vingehusishwa ktk kujua na kuhoji matumizi ya fedha ktk wizara hii ya Afya na Elimu.
      Exploration of reality

    8. FemaTV & Radio

    9. #126
      IHANDA's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th June 2012
      Location : GOLANI
      Posts : 26
      Rep Power : 353
      Likes Received
      5
      Likes Given
      2

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Hivi hawa jamaa kwa nini wasilipe hayo madai yao

    10. #127
      mojoki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 904
      Rep Power : 615
      Likes Received
      128
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By IHANDA
      Hivi hawa jamaa kwa nini wasilipe hayo madai yao
      hawana ela mkuu

    11. #128
      Noboka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2011
      Posts : 493
      Rep Power : 2248
      Likes Received
      153
      Likes Given
      23

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Siungi mkono kabisa ubabe unaoonyeshwa na serikali yetu, mbona madaktari wanasema wakae meza moja na serikali wamalize haya mambo shida iko wapi? Kinachofanywa na madaktari ni kuonyesha taswira nzima mahali jamii ya kitanzania ilipofika, Serikali wangetakiwa kutumia busara tu kulimaliza hili, lakini kwahiyi ya kuwatishia kufukuza, sijui.
      Ikumbukwe Dr. wa Tanzania kwa haya maslahi wanayopata, tukifukuza wote hatuna uwezo wa kuajiri Dr. toka nchi nyingine, kwahiyo ni vema busara za serikali zikatumika, likiendelea hili kama juma zima wananchi wakitaharuki tu kwisha kazi

    12. #129
      NG'OMBE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th March 2011
      Posts : 290
      Rep Power : 437
      Likes Received
      60
      Likes Given
      125

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Wabunge jiandaeni kwenda kutibu watu.

    13. #130
      Micro E coli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2011
      Posts : 552
      Rep Power : 492
      Likes Received
      103
      Likes Given
      88

      Default

      Quote By Kapeleka
      Kufukuzwa madaktari siyo dawa, ila ni funzo. Hakuna haja ya wao kuendelea kuitwa watumishi wa umma wakati hawautumikii umma. 'Fukuza woooteee, kuanza upya si ujinga' Mjomba aliimba. Sifurahii kupigwa Dr. Ulimboka, ila ni funzo kwao na njia ya wananchi kuonesha uchungu wanaoupata kwa mgomo wao. Madaktari hawapaswi kutumia wagonjwa kama kiboko cha kuichapia serikali kwa madai yao hata kama yanamsingi kiasi gani. Sasa je, wamegoma kumuudumia Dr. Ulimboka alipopata matatizo yanayowapata watanzania wengi.

      Nakubaliana na unamuzi wa madakatari kufukuzwa wote wanaogoma, na hata wakitaka kujuizuru wote sawa. Serikali ijipange hata kwa gharama kubwa kuwaleta madaktari kutoka majeshi ya nchi marafiki na mashirika km red cross kusaidia wakati suluhu ikitafutwa ya kudumu.
      Kichaa chako kimepanda.

    14. #131
      Micro E coli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2011
      Posts : 552
      Rep Power : 492
      Likes Received
      103
      Likes Given
      88

      Default

      Quote By mojoki
      hawana ela mkuu
      Hawana hela eeeh subili sasa uone kama hawaja kimbia magogoni.

    15. #132
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2266
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Tatizo la tanzania hatuna viongozi bali tuna watawala. Hili ni tatizo lakuua professional leadership colleges kama mzumbe na kivukoni. Watawala wetu hawana knowledge, skill and aptitude katika leadership. na matokeo yake ndio haya. Irational scheme of services, poor management and distribution of national cake. Sasa moto wayaka, hii ni laana ya kutokusikiliza wazee. CCM inakwenda kufutika kabisa.
      Simple life is healthier than egoism.

    16. #133
      kitero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2012
      Location : Kaskazini
      Posts : 516
      Rep Power : 469
      Likes Received
      97
      Likes Given
      48

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Quote By Mtandu
      Tunakokwenda au tulikofika?
      OK,kama tulipo fikia ni hapa na tunakokwenda itakuwaje? ndiyo maana nikasema tunakokwenda kama tumeweza fikia hapa.

    17. #134
      mdoe mchaina's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st December 2011
      Posts : 136
      Rep Power : 404
      Likes Received
      20
      Likes Given
      0

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Tumsubiri vasco dagama alitolee ufafanuzi swala la madactary akiongea na wazee wa Dar next week.

    18. #135
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 14,971
      Rep Power : 3703
      Likes Received
      3578
      Likes Given
      5769

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Sijui nini kinaenda Tanzania
      Wti nchi ya amani hii??????????????????????????? ??????
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..

    19. #136
      Fugwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Location : Tabata Dampo
      Posts : 847
      Rep Power : 717
      Likes Received
      95
      Likes Given
      43

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Namwomba MUNGU, siku hizi za mgomo nisiugue.
      A Quick Temper Will Make a Fool of You Soon Enough. '' BRUCE LEE''

    20. #137
      Malipo kwamungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Posts : 280
      Rep Power : 419
      Likes Received
      41
      Likes Given
      70

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      Hivi mnamkumbuka Marehemu Aron Kimaro anapaswa kukumbukwa ktk harakati hizi R.I.P

    21. #138
      watu8's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th February 2010
      Location : Juu ya Tukutuku
      Posts : 15,153
      Rep Power : 31303
      Likes Received
      7501
      Likes Given
      7538

      Default Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

      it's getting more interesting now...ifike kipindi wanasiasa waheshimu taaluma za wenzao...
      watu wamehenyeka miaka 6 hadi 7 kuwa tu MD, bado wale wanaobobea....
      mwisho wa siku serikali isiyo sikivu inaishia kuwanyanyasa...
      wengi tunaopinga mgomo huu ni kwa vile mnatambua umuhimu wa madaktari...
      kwa kuwa mnatambua, ni vyema mngeungana nao kila mmoja katika kada yake....
      kufanikisha azma ya kuutokomeza ubeberu wa serikali yetu...
      naomba hili vuguvugu liendelee na kwa wenye vituo vya mafuta(yale mashangingi yao tuone kama yatatumia maji), madereva mabasi ya mikoani, makampuni ya simu(zimeni mitambo tuone kama watawasiliana)...

      "Njia ya ukombozi ni ngumu, inawapasa wenye nia thabiti!"
      "Ingawa tunatumia AVATARS na USERNAMES ambazo ni FAKE, bado haibadilishi uhalisia wa MIOYO YETU"



    22. #139
      Manyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2011
      Posts : 1,721
      Rep Power : 721
      Likes Received
      291
      Likes Given
      262

      Default Madaktari 72 watimuliwa kazi - Mbeya

      BODI ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya, imewasimamisha kazi madaktari 72 kwa kosa la kutoingia kazini kwa siku tano jambo ambalo ni kinyume cha makubaliano ya mkataba.

      Imeelezwa kuwa madaktari hao ambao 54 ni wale wa mafunzo ambao waliingia mkataba wa miaka miwili na hospitali ya Rufaa na madaktari 18 ni wale walioajiriwa na Wizara ya afya.


      Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Bodi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Norman Sigara, alisema kitendo cha madaktari kutoripoti kazini kwa siku tano ni ukiukwaji wa kanuni za utumisha wa umma toleo la 2009 kifungu namba F.16-F17 na F. 27.


      "Hivyo kupitia kanuni hiyo madaktari hao wamesimamishwa kazi na kurudishwa kwa mwajiri wao ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa hatua zaidi za kinidhamu,"alisema Sigara.


      Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo wa Bodi, imeelezwa kuwa siku ya tarehe 23/6/2012 wafanyakazi 15 waliokuwa zamu(Intern Doctors 12 na Registrars3) hawakufika kazini na tarehe 24/6/2012 wafanyakazi 19(Intern doctors 15 na Registrars 4) hawakufika kazini.


      Alisema, kuanzia tarehe 25/6/2012 hadi leo imethibitika kuwa Interns doctor 54 na Registrars 18 hawakufika kazini hadi leo tarehe 28/6/2012 ambapo tarehe 25/6/2012 bodi ya hospitali ilifanya kikao cha dharura kujadili hali ya utendaji kazi na utoaji huduma hospitalini na kutoa uamuzi.


      Sigara, aliyataja maamuzi hayo kuwa ni Mwenyekiti wa Bodi akutane na madaktari ambao hawakufika kazini ili awasikilize sababu za kutofika na kujadili namna ya kumaliza matatizo hayo jambo ambalo madaktari hao waligoma.


      Alisema, baada ya madaktari hao kukaidi ombi hilo, Bodi ya hospitali ili waandikia barua za kujieleza kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuvunja mkataba walioingia na hospitali na pia kukiuka kanuni za kudumu za utumishi wa umma nalo walilikaidi

      "Iwapo madaktari ambao hawakuripoti au kueleza sababu za kuridhisha ifikapo tarehe 28/6/2012. Kwa kuzingatia kanuni za utumishi wa Umma, madaktari hao watasimamishwa kazi na kurudishwa kwa mwajiri wao ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,"alisema.

      Aidha, alisema kuwa kwa ujumala madaktari hao waligomea barua zote mbili yaani ya kuitwa kwenye kikao pamoja na ile ya kuwataka kujieleza hivyo Bodi imechukua hatua za kisheria za kuwafukuza kazi.


      Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa bodi, alisema kuwa tayari hospitali ya Rufaa kwa ushirikiano wa Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, madaktari watano wamepatikana ili kusaidia huduma kwa hospitali hiyo.



      Source: Mbeya Yetu Blog


    23. #140
      webondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2012
      Location : Chini ya mwembe
      Posts : 1,167
      Rep Power : 589
      Likes Received
      178
      Likes Given
      381

      Default re: Madaktari 72 watimuliwa kazi - Mbeya

      Ni maamuzi stahili kabisa, popote duniani ukikiuka terms za kazi lazima uadhibiwe.

    Page 7 of 9 FirstFirst ... 56789 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...