Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...

By
abou
wakati tunasheherekea mgomo wa madaktar tusisahau kua wamegoma kututibu sisi watanzania wa kawaida kbs ambao apollo tunaisoma kwenye magazeti tu....kwa hali hii tuombe na magonjwa nayo yagome
Nani amekwambia kuna watu tunasheherekea mgomo wa madaktari? Madaktari wanaomba kulipwa mishahara ambayo inaendana na taaluma yao ili waweze kukidhi gharama za maisha na pia kupewa vitendea kazi na kuboresha hospitali zetu ambazo zote ziko katika hali ya kutisha...Iweje Mbunge ambaye hajaenda shule apate mshahara mkubwa kuliko daktari aliyesota vyuoni miaka chungu nzima ili kuhitimu katika taaluma yake?
Hakuna hata Mtanzania mmoja anayesherehekea mgomo wa madaktari bali tunawaunga mkono kwa vile tunayaona madai yao yote yana umuhimu mkubwa katika kuboresha sekta ya afya nchini.
Last edited by BAK; 29th June 2012 at 04:20.
Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action
Follow Us Here