Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...
Taarifa ambazo zimethibitishwa zinatabanaisha kuwa madaktari walio katika uzoefu kazini, INTERN doctors wameanza kufukuzwa katika hospitali mbalimbali ambapo katika hospitali ya DODOMA madaktari 11 kati ya 33 wamefukuzwa na madaktari wote 70 waliokuwepo hospitali ya rufaa mbeya chini ya ulinzi mkali wa polisi wameambiwa waondoke kufikia saa 11 jioni ya leo wakati huo huo mkurugenzi wa hospitali ya BUGANDO amewafukuza madaktari wote 44 na kuwataka warudi wizarani wakati madaktari waliosajiriwa wameamuriwa kufika kesho wawe kazini au la wanafukuzwa.
Wakati huo huo madaktari wakazi waliitwa na senate ya BUGANDO na kulazimishwa kurudi kazini lakini walikataa mbele ya senate hiyo hivyo wakaambiwa watafutiwa udahili wao na wote kwa pamoja wakapiga makofi wakisema wako tayari kwa hilo.
Habari zaidi zinazidi kupasha kuwa hospitali ya Mwananyamala wameletewa fomu za kujaza kama wako tayari kuendelea na kazi au la,ila madaktari wamesimamia msimamo wao huo kuwa mgomo uko pale pale.
Katika hatua nyingine CHUO CHA TIBA BUGANDO NA KILE CHA MUHIMBILI VIKO MBIONI KUFUNGWA kutoka na walimu wao ambao ni madaktari kugoma na mazingira kutokuwa rafiki kwa kujifunzia.
Wakati hayo yakiendelea taarifa zinasema hsopitali ya Tanga BOMBO imeingia rasmi kwenye mgomo na ile ya MOUNT MERU
Habari zaidi madaktari wanajiandaa kwa mass resignation muda wowote
Re: Madaktari wafukuzwa mbeya,bugando na dodoma......mwananyamala walazimishwa kusaini,vyuo vya udak
By Kapeleka
Kufukuzwa madaktari siyo dawa, ila ni funzo. Hakuna haja ya wao kuendelea kuitwa watumishi wa umma wakati hawautumikii umma. 'Fukuza woooteee, kuanza upya si ujinga' Mjomba aliimba. Sifurahii kupigwa Dr. Ulimboka, ila ni funzo kwao na njia ya wananchi kuonesha uchungu wanaoupata kwa mgomo wao. Madaktari hawapaswi kutumia wagonjwa kama kiboko cha kuichapia serikali kwa madai yao hata kama yanamsingi kiasi gani. Sasa je, wamegoma kumuudumia Dr. Ulimboka alipopata matatizo yanayowapata watanzania wengi.
Nakubaliana na unamuzi wa madakatari kufukuzwa wote wanaogoma, na hata wakitaka kujuizuru wote sawa. Serikali ijipange hata kwa gharama kubwa kuwaleta madaktari kutoka majeshi ya nchi marafiki na mashirika km red cross kusaidia wakati suluhu ikitafutwa ya kudumu.
Karibu jamvini, naona umejiunga leo ili nawe "useme openly"....pyuuu!!
Kufukuzwa madaktari siyo dawa, ila ni funzo. Hakuna haja ya wao kuendelea kuitwa watumishi wa umma wakati hawautumikii umma. 'Fukuza woooteee, kuanza upya si ujinga' Mjomba aliimba. Sifurahii kupigwa Dr. Ulimboka, ila ni funzo kwao na njia ya wananchi kuonesha uchungu wanaoupata kwa mgomo wao. Madaktari hawapaswi kutumia wagonjwa kama kiboko cha kuichapia serikali kwa madai yao hata kama yanamsingi kiasi gani. Sasa je, wamegoma kumuudumia Dr. Ulimboka alipopata matatizo yanayowapata watanzania wengi.
Nakubaliana na unamuzi wa madakatari kufukuzwa wote wanaogoma, na hata wakitaka kujuizuru wote sawa. Serikali ijipange hata kwa gharama kubwa kuwaleta madaktari kutoka majeshi ya nchi marafiki na mashirika km red cross kusaidia wakati suluhu ikitafutwa ya kudumu.
Hebu sema ni njia gani wangetumia kuidai serikali yenye kiburi za dharau?
Re: Madaktari wafukuzwa mbeya,bugando na dodoma......mwananyamala walazimishwa kusaini,vyuo vya udak
By Kapeleka
Kufukuzwa madaktari siyo dawa, ila ni funzo. Hakuna haja ya wao kuendelea kuitwa watumishi wa umma wakati hawautumikii umma. 'Fukuza woooteee, kuanza upya si ujinga' Mjomba aliimba. Sifurahii kupigwa Dr. Ulimboka, ila ni funzo kwao na njia ya wananchi kuonesha uchungu wanaoupata kwa mgomo wao. Madaktari hawapaswi kutumia wagonjwa kama kiboko cha kuichapia serikali kwa madai yao hata kama yanamsingi kiasi gani. Sasa je, wamegoma kumuudumia Dr. Ulimboka alipopata matatizo yanayowapata watanzania wengi.
Nakubaliana na unamuzi wa madakatari kufukuzwa wote wanaogoma, na hata wakitaka kujuizuru wote sawa. Serikali ijipange hata kwa gharama kubwa kuwaleta madaktari kutoka majeshi ya nchi marafiki na mashirika km red cross kusaidia wakati suluhu ikitafutwa ya kudumu.
Hapo juu kwenye red ndio ambalo haliwezekani kabisa. Serikali hii haijawahi kujipanga kwenye kitu chochote; so far huwa ina-act kwa kukurupushwa tu. The only option waliyonayo kwasasa ni kubakia kuwa omba omba kwa mataifa makubwa. In other-words; wamekidharau cha nyumbani lakini watakubali kudhalilishwa na wafadhili (kwakufanya kile wafadhili wanataka) ili wapate wanachoomba. Kwakifupi tunarudi kwenye ukoloni kwani, tumeshindwa kukaa wenyewe nakutatua matatizo yetu bila nguvu na jazba. Shame!!!!
kwani madaktari wanataka nini hasa mimi mbona sielewi je aliyosema waziri mwenye dhamana dr hussein mwinyi yana ukweli wake? na kama hayana ukweli kwa nini tufike hapa tulipo
Re: Madaktari wafukuzwa mbeya,bugando na dodoma......mwananyamala walazimishwa kusaini,vyuo vya udak
asa una advice watumie iyo gharama kubwa kuleta doctors kutoka nje sioni unasolve vpi tatizo cause madai ya serikali ni kua hawana hela, sijui resources za kuwapa madaktari madai yao, asa wakiwafukuza wote afu wasafarishe doctors kutoka nje wa kutosha tzania nzima wawape na accomodation, tena hao doctors wa nje wa sha zoea vifaa na mazingira yanayofaa ki ka kazi, vitu ambavo hapa tzania hamna, na ndo moja ya sababau doctors wetu wanagoma iyo hela itokea wapi? kama serikali inaeza afford ilo basi izo hela wapewe tu hawa hawa doctors wetu yaishe,,,doctors hawagomi kwa dai moja tu la posho pia kwa vifaa vya hospital na mambo mengine ili waweze kuboresha huduma zao kwa wananchi...wapo upande wetu cause tuna haki ya kupata health service yenye quality na serikali ni duty yake kuprovide
Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...
By kiliochangu
Kazi kweli kweli. sidhani aliyetoa uamuzi wa kuwafukuza anafikiri kama ma doctor wataendelea na msimamo. usishangae kuona serkali iki-haha kutafuta njia za kutibu wagonjwa. Ndio mwanzo wa Movie picha ndo bado.
Mwenye akii atumie akili yake 2015
waache wakishawatimua ndo raha maana baada ya siku 2 watahaha kuwarudisha .. wakiwarudisha watadai mikataba mipya .. wakipewa ile ile watakataa kusaini kuwa hairidhishi... watawawekea matakwa yao halamu movie itaisha kwa serikali kushindwa....duh nimezinduka
Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...
By Puppy
Na kesho Bungeni utasikia wabunge wanasifu na kushukuru kwa hotuba nzuri ya Ofisi ya "Liwalo Na Liwe".
Kama Noma na iwe Noma, nikiugua leo nakuzidiwa na kufariki kwa kukosa matibabu sitajilaum nitajiona shujaa katika mapinduzi haya Liwalo Na Liwe bwana.
Bi. Kiroboto we endeleza kukataa miongozo sisi tutafunga Airpot sijui mtakimbia India kwa Gari au Lah.
Ukiiona hii Bi Kiroboto kumbuka ile ulosema "Asiekuepo Na Lake Halipo", Wewe kichwani mwangu haupo, tukikutana Tahrir na lako ujue haliko.
Getwell Soon Ulimboka
kama sisi wazima tumeshindwa kujitoa mhanga kwa ndugu zetu walioko mahospitalini bsi tusubiri wao watajitoa mhanga kwa ajili yetu na sie tutasema zidumu fikra za serikali dhaifu.
Nobody can give you freedom. Nobody can give you equality or justice or anything. If you're a man, you take it.... Malcolm X Nasubiri 'breaking news... '
Re: Madaktari wafukuzwa mbeya,bugando na dodoma......mwananyamala walazimishwa kusaini,vyuo vya udak
By gorretti54
Mgomo utatengeneza mazingira mazuri ya wanetu kukimbilia fani ya udaktari....
Exactly... Nimeshaanza maandalizi ya kukusanya fungu la kutosha ili My Four Year Old little asome Sayansi tangu Nursery mpaka atakapokuwa Phd ya Udaktari.... Kabisa.... Sio huu Ualimu ambao watu wako kwenye mgogoro na opportunity ime[atikana lakini yenyewe yamelala yanasubiri 10000 za Sensa...
Re: Madaktari wafukuzwa Mbeya, Bugando na Dodoma... Mwananyamala walazimishwa kusaini...
By Elizabeth Dominic
Nilishasema na naendelea kusema Watanzania/Tanganyika tusipoelekeza hasira zetu pahala sahihi tutaendelea kuumizwa, hii ndio nafasi ya ku vent hasira zetu na concern zote tulizonazo. Jamani time is now, Dr Ulimboka katuonyesha jinsi ya kudai haki na maslahi ya madaktari na Watanzania kwa ujumla.....lets follow suitMimi naamini ukombozi wa Mtanzania/Tanganyika utapatikana kwa roho za ujasiri watu kama Dr Ulimboka Kamanda Godbless Lema na wengine wote waliopoteza maisha au wanaoweka maisha yao hatarini ili tupate kushuhudia na kuikomboa nchi yetu
@Elizabeth Dominic ... Jua kuwa nilielewa ulichosema!!
Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
"Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.
Follow Us Here