Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Watanzania mbona tunakuwa kama Makondoo???

    Report Post
    Results 1 to 8 of 8
    1. #1
      Mantuntunu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 109
      Rep Power : 455
      Likes Received
      9
      Likes Given
      20

      Default Watanzania mbona tunakuwa kama Makondoo???

      Nia yangu sio kutukana ila jamani mimi maongezi yamenichosha, tunaingia humu tunachonga weee, tunaongea weee, tunaandika wee, labda nikubali kuwa hii ni namna ya kupunguza hasira zetu tu. Tuliwachagua wabunge wetu watuwakilishe na kutuhabarisha mambo yote yanayotendeka serikalini. Kwa kweli naomba niseme kwamba, especially wabunge wa upinzani wamejitahidi sana ktk kutuhabarisha na kutujulisha mapungufu na Madhaifu ya serikali yetu. Kuanzia EPA, Richmond, Kiwira, Rada, Ngege ya Rais,fedha za Uswiss, etc, etc.

      Tunaona yaliyotokea kwa Mwakyembe, na sasa Ulimboka na wengine ambao kwa namna moja au nyingine wameadhibiwa katika kujaribu kutetea maslahi ya wananchi. Wengine hata walifikia kuhoji kwa nini aliukubali Uwaziri, na wengine kusema kwamba Mwakyembe kaufyata hivi mlitaka afanye nini?? Sisi kama watanzania tumempa support gani? hata ningekuwa mimi ningeufyata manake wale unaofanya jitihada ya kuwatetea hawaonyeshi hata nguvu angalau nusu ya kukuunga mkono kwenye harakati hizi.

      Tumuangalie Ulimboka, kapigwa karibu ya kuuawa, tusubiri tuone sisi kama watanzania tutafanya nini angalau kuunga mkono ujasiri wake wa kutetea maslahi ya wenzake. Sirikali inasema madaktari watafute njia nyingine ya kudai madai yao na sio mgomo, hiyo sirikali imeona njia ya kumuadhibu Ulimboka ni sahihi? Anyway tuyaache hayo.

      Ninachotaka kusema hapa ni kwamba kuanzia sasa tusiwalaumu wabunge wetu kwa lolote lile tena hapa naongelea pia baadhi ya wabunge wa CCM ambao wameonyesha kuipinga sirikali wazi wazi. Hawa watu wameishafanya ya kutosha kutuhabarisha mabovu ya sirikali yetu, wizi, mikataba mibovu, ubinafsishaji kwa maslahi binafsi, n.k. Sisi kama Watanzania tunawapa support gani?? Jamani kama hatufahamu sisi ndio wamiliki halali wa nchi hii, tuna sauti kubwa na yenye nguvu sana kama tutaamua leo hii kwamba huu upuuzi wa viongozi wetu basi. Tafakari Chukua Hatua!
      Last edited by Mantuntunu; 28th June 2012 at 13:42.

    2. Miaka 50

    3. #2
      masopakyindi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 3,757
      Rep Power : 4199
      Likes Received
      1015
      Likes Given
      417

      Default Re: Watanzania mbona tunakuwa kama Makondoo???

      Mkuu tangulia mwenyewe Mabwe Pande!!
      "If you don't know where you are going, any road will get you there-nowhere”

    4. #3
      Mantuntunu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 109
      Rep Power : 455
      Likes Received
      9
      Likes Given
      20

      Default Re: Watanzania mbona tunakuwa kama Makondoo???

      Quote By masopakyindi
      Mkuu tangulia mwenyewe Mabwe Pande!!
      Na hicho ndo kinachotuharibu, hakuna cha wewe tangulia, ingekuwa sawa kama ungesema tuungane kwa pamoja watanzania wote na tuone hao polisi kama idadi yao itaweza kutumudu!

    5. #4
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,729
      Rep Power : 2267
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Watanzania mbona tunakuwa kama Makondoo???

      Quote By masopakyindi
      Mkuu tangulia mwenyewe Mabwe Pande!!
      Kondoo dhaifu.
      Simple life is healthier than egoism.

    6. #5
      ALEYN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 1,037
      Rep Power : 588
      Likes Received
      126
      Likes Given
      17

      Default

      Quote By masopakyindi
      Mkuu tangulia mwenyewe Mabwe Pande!!
      jishtukie ww


    7. #6
      KISIMASA's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Posts : 38
      Rep Power : 376
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Default Re: Watanzania mbona tunakuwa kama Makondoo???

      Siyo makondoo ni uoga uliokithiri. Halafu kuteteana,halafu kupeana madaraka hata kama hukidhi viwango. Mfano kwenye hili sakata la madaktari bado wapo wenzao tena senior members tu ambao wamekuwepo tangu enzi ndani ya udhaifu huu na wako kimya kabisa. Wanalinda seat zao. Tunahitaji mabadiliko

    8. #7
      Mantuntunu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 109
      Rep Power : 455
      Likes Received
      9
      Likes Given
      20

      Default Re: Watanzania mbona tunakuwa kama Makondoo???

      Quote By KISIMASA
      Siyo makondoo ni uoga uliokithiri. Halafu kuteteana,halafu kupeana madaraka hata kama hukidhi viwango. Mfano kwenye hili sakata la madaktari bado wapo wenzao tena senior members tu ambao wamekuwepo tangu enzi ndani ya udhaifu huu na wako kimya kabisa. Wanalinda seat zao. Tunahitaji mabadiliko
      Na hicho ndo ninachokisema mimi, we need changes and that starts with us! Kinatakiwa kiwe kitu cha pamoja na sio watu wachache!

    9. #8
      measkron's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 1,570
      Rep Power : 11274
      Likes Received
      683
      Likes Given
      1275

      Default

      Quote By Mantuntunu
      Na hicho ndo ninachokisema mimi, we need changes and that starts with us! Kinatakiwa kiwe kitu cha pamoja na sio watu wachache!
      Tukianza na wale wakuu Wa hospitali za Mbeya, Bugando na Dodoma wanaofukuza interns doctors itakuwa mwanzo mzuri

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...