WanaJF. Nashindwa kuelewa kwa nini dunia haiko fair kiasi hiki, inakuaje majitu failures (Div IV na O) yawe ndiyo yenye maamuzi makubwa kuliko learned people?
Hakuna mwanasiasa hata mmoja kwenye sayari hii mwenye record ya kuwa mwenye akili bora kati ya wahitimu wote unaowafahamu, isipokuwa kubebwa na kupelekwa.
Walichonacho ma Dr. Kipo kichwani mwao siyo funguo kwamba watanyang’anywa na kupewa mtu mwingine, ni uwezo wao ambao upo ndani yao.
Mgogoro wa maDr. Na serikali unanikumbusha jinsi ambavyo juha anavyojaribu kumpa vitisho mwerevu. Kama zile khadithi za zamani za Abunuwasi.
Tafiti sahihi zimeonyeshwa kwamba, Wakati tukiwa shule tunasoma wanafunzi :
- wale wanoongoza darasani ama wenye uwezo mkubwa wa akili darasani huwa wanaelekezwa kusomea Udakatari na uinjinia,
- wale wa waoshika nafasi za katikati huwa wanaelekezwa kuwa wahasibu, watawala, na masoko,
- wale wanaofeli akina Div. IV and kushuka chini ndiyo huwa wabanagiza kwenye ualimu, siasa,na ukarani. Ambao baadae hubabaisha na kuwa watawala kama hawa tulionao waona leo.
Muundo huu hauko fair wale failures ndiyo wanaopata nafasi ya kuwatawala wenye uwezo kiakili na na wataalamu.
- Kwa ukweli huu kwa nini tusitegemee dharau?
- Kwa ukweli huu kwa nini tusitegemee Udhaifu?
- Kwa ukweli huu kwa nini tusitegemee ufisadi?
- Kwa ukweli huu kwa nini tusitegemee madini yetu na mitaji yetu kuondoka hali tukifurahia?
- Kwa ukweli huu kwa nini tusitegemee watawala badala ya viongozi?
- Kwa ukweli huu kwa nini tusitegemee badget zisiyoeleweka?
- Kwa ukweli huu kwa nini tusitegemee kauli za akina Pinda?
- Kwa ukweli huu kwa nini tusitegemee Gilba na safari nyingi za nje ?
Wabangaizaji (Wasanii) chaka lao ni uongo na uzushi na kukimbilia vyombo vya habari ili wasikike, wahurumiwe, wasifiwe na waonekane kama wao ni wanachapakazi (tunao mawaziri wengi tuu wa design hizi)
Shule iliwashinda wakakwama kidato cha nne ama hata darasa la saba, lakini kwa vile sasa wamepata kujipenyeza wanajitahidi kujustfy kuwa na wao wamesoma kwa kuupenda UDr. Wa uzamili hata kama ni wa kupewa kwa heshima wasizostahili.
hawachelewi kukimbilia digree za uzamili ili waitwe DR. kisa tuu wanapenda wawe na akili ambazo hawana.
Jamani nyinyi wasanii, sis wananchi tunajua kwamba nyinyi mlishindwa shule na ndiyo maana mkapita mlango wa nyuma kufikia hapo mlipo. HHeshimuni taaluma kwa maana yale ambayo nyinyi mlishindwa wenzenu waliyaweza na ndiyo maana wapo hapo kwa ajili ya kuokoa maisha yetu.
Kusoma ni kazi ngumu sana na ndiyo maana nyinyi mlichemsha, kusoma ni gharama kubwa sana ndiyo maana watoto wa wakulima mmebangaiza kufika huko mliko.
Basi angalau jambo dogo tuu mnalotakiwa kulifanya, wasikilizeni Madr. Hawa badala ya kutumia vyombo usanii wenu kuwagombanisha na wananchi. Walichonacho nyinyi hamna na wala hamtaweza kukipata kwa vyovyote.
Punguzeni kutegemea INDIA, SOUTH AFRICA, KENYA,UK ili muwwezeshe maDk. Wetu. Haipendezi hata kidogo na wmnatujengea hasira sana wananchi kama hamjui. Msione vinaelea jamani vimeundwa.
Follow Us Here