Hana jipya,
Mh. Zambi anahoji kuwa japokuwa kesi mahakamani madaktari wameendelea kugoma serikali inasemaje?
Pinda kasema kesho watalitolea maamuzi na kasema LITAKALO KUWA NA LIWE. Hivi kwa kauli hii tuna waziri mkuu kweli??
Hana jipya,
Mh. Zambi anahoji kuwa japokuwa kesi mahakamani madaktari wameendelea kugoma serikali inasemaje?
Pinda kasema kesho watalitolea maamuzi na kasema LITAKALO KUWA NA LIWE. Hivi kwa kauli hii tuna waziri mkuu kweli??
Last edited by dosama; 27th June 2012 at 10:57.
ndugu zanguni
hakuna aneunga mkono kupigwa na kuteswa kwa Dr ulimboka! lkn aliefanya hivyo hajulikani. suala la madaktari limekua la kisiasa. siasa ni mchezo mchafu
NIMEJIFUNZA JAMBO MOJA
Nimejifunza kuwa DAKTARI HARUHUSIWI KUGOMA KUTOKANA NA KAZI YAKE INAYOHUSU UHAI. mbona huyu dr ulimboka amekimbizwa mhimbili!!! kwa nini? jibu ni rahisi, KUOKOA MAISHA YAKE. sasa kwa nini wanagoma!? ina maana wantaka watanzania wafe? mboa serikali imetatua maombi yao kwa 70% bado TC SCan pekee na mambo madogo madogo. WANATAKA NIN HAWA MADAKTARI? WANATUMWA NA IFRITI (JINI) YUPI? waziri mkuu amesema bungeni kuwa serikali kesho itatoa msimamo wake.
USHAURI WANGU
Nashauri waziri wa utumishi awafukuze wote ambao HAWATARIPOTI KESHO ASUBUHI KAZINI. tuache kuvuruga nchi yetu yenye amani kwa MAMBO YA UCHU WA MADARAKA
Ni kweli madaktari wanahaki ya kudai maslahi yao!!! hiyo ni haki yao kwani siku hizi hata kazi za kanisa watu hulipwa. ila inapofika hatua ya kuibana serikali kwa staili ya kumdhuru mwananchi wa kawaida tena ambaye hata hiyo PANADOL kuipata kwake ni ishu nadhani hiyo si sawa!
Serikali yetu nafikiri kuna maeneo inabidi ilaumiwe ila kwa hili tuitetee, sioni sababu ya msingi ya maana ambayo inaweza kunifanya nishawishike kuwa serikali haijafanya kitu kabisa kwenye hili la madaktari. Nafikiri imejitahidi, kuwasomesha bure tu madaktari tena kwa kodi za wananchi hilo si dogo, nafikiri sasa serikali itathmini sheria zake, hii dekezadekeza hii ndiyo inaleta matatizo haya mambo ya upole huu itaifikisha nchi pabaya sasa nidhamu irudi.
Kesho nitashangaa kama nitasikia kauli za chondechonde! Liwalo na liwe. CHONDECHONDE basi, hii chekecheka hii kwa nchi maskini kama hii haitatufikisha popote. Upole na Hekima za Rais wetu kunawatu wanataka waipandie kichwani.! wakati shuleni watoto wa wakulima wanakalia mawe kunamtu anataka atimiziwe na serkali haki zake kwa asilimia 100%
Ninaandika maneno haya maana ninamgonjwa (nadiklea intrest)
I say No! liwalo na liwe! uwepo wa mabingwa hauzuii kifo!!!
nimesikitika sana
tuingie msituni
"Look Deep into Nature and then you will Understand Everything Better" - ALBERT Einstein
nchi nyingine zimeweka sheria inayozuia madaktari kugoma. wamesomeshwa na serikali. dktr bingwa mshahara wake na marupurup kwa ss unafikia milioni 8. WANATAKA NINI HAWA WATU!? WALIMU WASEMEJE NA MSHAHARI WA LAKI 3?
huyu bwana amekaidi amri ya mahakama. wanatufundisha kuwa kuanzia leo watanzania tuanze kudharau mahakama zetue?
acheni kauli ya kuwa kikwete ni dhaifu. atakuonesheni kuwa siyo dhaifu. chezea serikali wewe? (huu ni utani)
umetumwa na pinda nashangaa raia wengine hapo wa kumbana ni serikali na sio madaktari maana wakienda kazini kwa shingo upande na hizo panadol ndo mtakufa kama mbu wakipuliziwa dawa.
nchi nyingine zimeweka sheria inayozuia madaktari kugoma. wamesomeshwa na serikali. dktr bingwa mshahara wake na marupurup kwa ss unafikia milioni 8. WANATAKA NINI HAWA WATU!? WALIMU WASEMEJE NA MSHAHARI WA LAKI 3?
huyu bwana amekaidi amri ya mahakama. wanatufundisha kuwa kuanzia leo watanzania tuanze kudharau mahakama zetue?
acheni kauli ya kuwa kikwete ni dhaifu. atakuonesheni kuwa siyo dhaifu. chezea serikali wewe? (huu ni utani)
Sasa nimegundua,kumbe Pinda akipata kauli inayomsikitisha huwa analia (Unafiki) lakini linapotekea suala zito lenye kuwagusa wananchi masikini anasema liwalo na liwe.Ndiyo maadili ya wadhaifu!
Ndivyo alivyo huyu "mwana wa mkulima" daima huongea bila kufikiri. Bahati mbaya kashindwa hata kutumia usemi wa bosi wakealiosema, "akili ya mbayuwayu ongeza na za kwako". Sisemi hivi kwa kumdhalilisha Pinda; ila kama mtu anamfuatilia huyu jamaa utaweza kumuweka katika ngazi mbili. 1. Huambiwa/ huandikiwa cha kusema na hawezi kusoma wala kufatakari alichoandikiwa. 2. Ni mropokaji, hatafakari athari za kauli zake kwa umma ukizingatia nafasi yake ya uwaziri mkuu.
Hii hapa mifano ya tabia na kauli za Pinda:
1. Akiwa mkoa mmojawapo magharibi mwa nchi wakati tatizo la mauaji ya albino likiendelea aliropoka, "wauaji wakikamatwa wauwawe". Pamoja na uchungu wa mauaji hayo, Waziri mkuu ni wa kwanza kuhimiza wananchi kufuata misingi ya sheria na kutochukua sheria mkononi. Kauli hii ilimcost kulia mbele ya umma wa waTz!
2. Alitishia kuwafukuza kazi madkari wote waligoma; lakini hata mgomo ulipoendelea hakuweza kuwafukuza kazi. Kwa nini? Pinda hakukaa chini na kutafakari kuwa uko utaratibu wa kumuondoa mtumishi katika ajira na pia mchakato wa kusomesha daktari mmoja una gharama kiasi gani. Kibaya zaidi alifikiri hawa madaktari ni kama shamba boy wake. Hakutaka kuangalia nini chanzo cha mgomo huu na kwa kiasi gani yeye na Serikali yake waliwafikisha madaktari mahali pa kugoma.
3. Alisema Dr. Ulimboka si daktari maana hakuna taarifa/ rekodi kuwa alimaliza mafunzo yake baada ya kufukuzwa chuo. Alimuita Dr Ulimboka mhuni; ajabu mgomo ulipopamba moto Mh. Pinda alikaa meza moja na Mhuni huyu (Dr.Ulimboka); wala hakuhoji huyu katokea wapi?
4. Alisema nitamshauri Rais kuwafuta kazi Mh.Mponda, Nkya; lakini hakufanya hivyo hadi Rais alifanya mabadiliko ya baraza kwa shinikizo la wabunge.
Ya Mh. Pinda ni mengi mno. Nadhani hata kauli hii ya "liwalo na liwe" karopoka tu; ila ajue itamgharimu!
EJL
Napata shida kidogo kwamba nikupe pole wewe au wale wagonjwa ambao kwa lengo lenu la kugoma na kuiwajibisha serikali wengi wanateseka,wengine wanakufa,mama zetu wanajifungua kwa uchungu bila ya kua na msaada wowote,haya ni mateso makubwa,
Hemu tujiulize vipi kama ulimboka na yeye kama akitelekezwa aachwe bila ya huduma yoyote?
ni vyema madaktari watafute njia tofauti yakuibana serikali kwani watanzania wasio na hatia wanakufa kwa kosa la serikali
Ningesema Kigumu Chama cha Mafisadi! na wewe utaitikia Kidumu! Karagabaho!
Kitanda usicho kilalia hukijua kunguni wake....
Bravo Madaktari!, Tatizo la kuchangua kiongozi Dhaifu, na kuwa naselekari dhaifu.
Hakuna cha mtoto wa mkulima hapo tena, wamesha m-contaminate,
Arusha ni mwanga wa TUMAINI jipya
Kwa hili lililotokea la Dr. Ulimboka ambalo limehusishwa sana na kauli
yako ya LIWALO NA LIWE ni busara kwako ukiamua kujiuzulu.
Bila shaka umenielewa kwani nina wasiwasi wa kuhusishwa na mengine
makubwa zaidi ambayo pengine utakuwa huhusiki nayo.
Jiuzulu Mheshimiwa ili kulinda Imani ya wapiga kura wako wa Rukwa.
naunga mkono hoja ajiuzuru tu kwa hili hatakiwi kuwa hata mwenyekiti wa kijiji
Follow Us Here