Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana...
Sasa uchokozi umefikia pabaya na hii sasa ni vita!!
Taarifa iliyonifikia hivi punde ni kuwa jemedari Dr. Ulimboka ametekwa majira ya saa sita usiku na watu watatu waliokuwa na silaha za moto na kumpeleka kusikojulikana! Inasemekana alipigiwa simu na jamaa mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la 'Abeid' ambaye tangu mwanzo amekuwa akiwasiliana naye na kujiita afisa wa serikali na kudai kuwa alitaka aonane naye face to face kwa ajili ya reconciliation.
Taarifa zimekwisha fikishwa polisi na sehemu zingine kwa ajili ya ufuatiliaji. (source chanzo cha kuaminika).
UPDATE:
Inaelekea waliomteka si watu wema kabisa, Dr. Ulimboka kaokotwa sehemu akiwa katika hali mbaya sana!
By Riwa
Jamani this is is serious; Nimepigiwa simu sasa hivi na watu wa Legal and Human Rights Center wameniambia wametoka kumchukua Dr. Ulimboka kule Mabwepande amepigwa vibaya sana na ni emergency wanampeleka MOI sasa hivi.
Please tunaomba mtume habari hii kila mahali please!
Ni habari ya uhakika sana nimeomngea na Patience Mlowe wa Legal and Human Rights center.
Chanzo: Colleague ambaye yuko naye sasa!
By DOMA
Kamanda wa polisi Suleiman Kova amekaririwa akisema kwamba Dr. Ulimboka ametekwa akiwa Club na watu wasiojulikana akiwa anakunywa kinywaji na kuahidi kwamba uchunguzi unaendelea kuhusiana na tukio hilo.
Tutaendelea kutoa updates kadiri muda unavyoruhusu.
PICHANI: Dkt. Ulimboka akiwa katika hali mbaya mara baada ya kuokotwa akiwa hajitambui.
Ulimboka alitekwa jana usiku mida ya saa 6 usiku baada ya kupigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Abeid na alitekwa na watu wawili waliokuwa na silaha. Kufuatia hali hii wafanyakazi wa chumba cha maiti Muhimbili nao wamegoma na mgomo huenda ukawa mkubwa zaidi!
Huyo hajatekwa bali kakamatwa kwa "mahojiano zaidi". Hata hivyo, reconciliation ndio aende pekee yake ? Naye alikosea kama kweli alienda pekee yake; maana hata watu wenye nia mbaya na Serikali wanaweza kuchukua hatua kama hiyo ili kuleta taharuki zaidi !!!!
Huyo hajatekwa bali kakamatwa kwa mahojiano zaidi. Hata hivyo, reconciliation ndio aende pekee yake ? Naye alikosea kama kweli alienda pekee yake; maana hata watu wenye nia mbaya na Serikali wanaweza kuchukua hatua kama hiyo ili kuleta taharuki zaidi !!!!
Angekamatwa ingejulikana ni kwa sababu zipi na amepelekwa wapi, unasema amekamatwa kwa mahojiano zaidi,unajua amekamatwa na nani na anahojiwa kuhusiana na nini?
Huyo hajatekwa bali kakamatwa kwa mahojiano zaidi. Hata hivyo, reconciliation ndio aende pekee yake ? Naye alikosea kama kweli alienda pekee yake; maana hata watu wenye nia mbaya na Serikali wanaweza kuchukua hatua kama hiyo ili kuleta taharuki zaidi !!!!
inawezekana wameenda kujadiliana,sidhani kama atafanyiwa kitu kibaya mana utandawazi umeanika kila kitu,lazima waogope hilo
Re: Kiongozi wa Mgomo wa Madaktari: Dr.ulimboka yadaiwa atekwa na watu wasiojulikana
Hapo ndipo tunapokosea, kutumia mbavu katika kusuluhisha migogoro ya aina hii ni kuendeleza migogoro na jamii husika bila ulazima wowote, sitaki kuamini kuwa kwa kumteka/kumkamata Dkt. Ulimboka ndio migomo itakwisha huu ni ubabe ambao hauna nafsi katika nchi zenye demokrasia na utawala wa sheria. Ikitokea Dkt. huyo amedhurika katika kipindi hiki litokuwa doa kwa chama tawala na serikali yake.
Huu ndio ufisadi wa fikra. Pamoja na kuwa migomo hii ya madaktari inaendeshwa bila kuwa na mikakati madhubuti ya kuona kama inafanikiwa au la, bado pia serikali inashindwa kujipanga kuwashawishi kwa hicho wanachoamini na matokeo yake ni kuendeleza ubabe wa wenye dola ambao hawataki kufikiria na wasio na nguvu ya dola wanaodai haki yao ambao pia hawajui hatma ya hilo wanalolifanya.
Kukosekana kwa dhamira inayoeleweka zaidi ya kuamini tu kuwa watu wengi wakifa serikali itatusikiliza kwa sababu madaktari ni muhimu, bado ni tatizo katika migomo mingi ya tanzania na ndiyo maana hakuna mafanikio au yanakuwepo kidogo sana kwa kuwa kila upande unachotaka ni ubabe na siyo kuwa na dhamira madhubuti inayoeleweka na hata inayoainisha njia mbadala endapo iliyopo itashindwa katika kipindi fulani.
Re: Kiongozi wa Mgomo wa Madaktari: Dr.ulimboka yadaiwa atekwa na watu wasiojulikana
Wanabodi,
Tuache kuandika lawama tu hapa,tumelalamika sana inatosha inabidi twende hatua moja zaidi.Hili ni tatizo na lazima tudai taarifa rasmi aliko Dr Ulimboka.
Haiwezekani tuambiwe mtu muhimu kama Dr Ulimboka atekwe kihuni alafu tuishie kulalama bila kutafuta suluhisho hasa jukwaa hili likiwa limesheheni wanasiasa,watawala,wanausalama na sisi wananchi. Naomba comments hapa zisiwe za kulaumu tu bali kushinikiza kwa kila njia wapi alipo Dr huyu.
Kama kuna namna ya kudhibitisha hili itakuwa vyema ili nguvu ya umma ifanye kazi.
re: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana...
By Pombekali
Angekamatwa ingejulikana ni kwa sababu zipi na amepelekwa wapi, unasema amekamatwa kwa mahojiano zaidi,unajua amekamatwa na nani na anahojiwa kuhusiana na nini?
Mkuu, ndio maana nimesema hata watu wenye nia mbaya na Serikali au Drs. wanaweza fanya jambo kama hilo au hata maadui zake wanaweza on hii ndiyo loophole ya kukoroga mambo zadi. Wewe hujui Propaganda ziko kila mahali ?
yaan serikali hapo ndo inapochemka!what do u think ikitangazwa kuwa amekamatwa au kitekwa,nchi haitatawalika jamani,mark my word!
hata akiuawa shuguli zitaenda tu Watanzania walishazoeleka kelele mdomoni vitendo zero! tukaeni kimya tufanye kazi watunyonye watufisadi hadi basi tutakuwa tunatumikia adhabu ya sisi kuwa wazembe na wajinga!adaktari wenyewe na usomi na weledi wao wamegawanyika wengine wamegoma wengine wanafanya kazi wengine hawaeleweki lakini wangeamua wakagoma kwa 100% serikali ilishawasikiliza siku nyingi!!
Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!
Kwanza kabisa ili angalau hii habari iwe credible tunaomba RB No. ya kutekwa kwa Dr. Ulimboka. Unadai tukio lime-ripotiwa polisi
Lakini pia sitashangaa sana kwa serikali kufanya mambo iliyofanya miaka zaidi 20 nyuma. Katika ule mgomo mkubwa ya UDSM wa mwaka 1989, serikali pia ilitumia mbinu hiyo hiyo ya kuwateka viongozi wa DARUSO marehemu Bazigiza na Matiko. Lakini wanafunzi tulisimama kidete hadi wakaachiwa!
Follow Us Here