Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

    Report Post
    Page 4 of 7 FirstFirst ... 23456 ... LastLast
    Results 61 to 80 of 125
    1. #1
      abdulahsaf's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st August 2010
      Posts : 860
      Rep Power : 723
      Likes Received
      123
      Likes Given
      1

      Default Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid





      WASIWASI umetandakuwa huenda kuna watuwanataka kumuuwaSheikh Farid.

      Hiyo ni kutokana na kile kilichojiri hivi karibuniambapo watu waliokuwakatika gari walifukuza gariyake na kuipiga risasi, lakinikwa bahati nzuri Sheikhalikuwa hayupo ndani yagari hiyo.

      Wakati huo huo, mwanamke mmoja aliyekuwa akishikilia bendera ya Uamsho yenye maandishi Laaila ha ilallah, ameshushiwa kipigo kikali na polisi alipokataa kuachia bendera hiyo.

      “Huyo polisi mmoja alikuwa akinilazimisha nimpe bendera, nikamwambia mimi hii siitoi hata kama utaniuwa, basi bora nife nayo mkononi mwangu hii ina Lailahaila llah… sikupi akaendelea kunipiga kwa kile kirungu cha polisi alichokuwa nacho…akanipiga tena nikaanguka chini na akanivuta bendera yangu tukawa tunanyanganyiana.” Amesema Bi Riziki akiongeana mwandishi juzi.

      Bi Riziki Omar Chande(42) ni mmoja wa wanawake kadhaa waliojitokeza na kueleza jinsi walivyopigwana kudhalilishwa na polisi.

      Riziki Omar Chande(42) mkaazi wa Mfenesini anasema kuwa baada ya kusikia kuna mhadhara Donge, yeye alitoka mapema na kwenda kupanda gari kuelekea Donge kama wenzake lakini baada ya kufika Mahonda jeshi la polisi lilisimamisha msafara na kuwataka watu wote warejee mjini.

      Hata hivyo anasema kuwa viongozi wa msafarawaliwataka wasiondoke mpaka viongozi wakuu watakapofika.

      Ilikuwa ni katika muda huo huo Sheikh Farid Hadi Ahmed na wenzake walifika katika eneo la Mahonda na kutaka jeshi la polisi kuacha kuhatarisha amani kutokana na kitendo chaocha kuwazuiya watu waliokuwa wakielekea Donge kuhudhuria mkutano uliokuwa ufanyike katika Msikiti wa Donge.

      Hata hivyo badala ya kuwasikiliza na kujadiliana nao, polisi waliwafukuza kwa mabomu ya machozi na ndipo Masheikh haowalipoingia Msikitini.

      Taarifa kutoka eneo latukio zinafahamisha kuwa polisi waliwafuata huko huko Msikitini kuwatawanya kwa mabomu ambapo Sheikh Farid na wenzake waliruka ukuta na kukimbia kwa miguu katika pori kutoka Mahonda kuelekea njia ya Mwangapwani.

      Huku nyuma, wakidhani Sheikh Farid yupo ndani ya gari alilokuja nalo, watu wasiofahamika walilifukuza gari hilo na kulipiga risasi ambapo lilipinduka na kuharibikia vibaya.

      “Sijui kama walitaka kutuuwa au vipi, lakini bahati mimi sikuwemo katika ile gari ingawa wanadhani kwamba ile gari ni yangu, lakini niseme mimi ile gari sio yangu ila nilipewa kwa kutumia kwa ajili ya shughuli za kuendeleza hizi harakati zetu”, alisema Sheikh Farid muda mfupi baada ya kurudi katika hekaheka hizo ambapo walifanya mhadhara wao Mbuyuni baada ya kutokufanikiwa kupenya kwenda Donge.

      Akielezea juu yakilichomfika Bi Riziki anasema kuwa kwa vile alikuwa kashikilia bendera, ilikuwa rahisi kwake kufuatwa na polisi.

      “Mimi nilikuwa nimekamata bendera yangu polisi alipokuja kunichukua akanikamata mkono ananipeleka kituoni alipofika mbele kuna polisi mwenzake akawambia unampeleka kituo kama BiHarusi, mpige virungu,…yule polisi akajibu kwanini tumpige wakati amekubali kutii amri halali?”

      “Mwenzake akasema, haiwezekani hao hawana adabu lazima apigwe, yeye ndio akaanza kunipiga huku akinambia nimpe bendera yangu ya Uamsho mimi nikamwambia nipige lakini bedera yangu sikupi ndio akaendelea kunipigana kunipiga”, alisema BiRiziki.

      “Wakawa wanatuambia maneno ya ovyo kwamba tutakoma, kwa hivyo yule polisi mmoja akawa anaendelea kunipiga alipokuja polisi mwenzake akawambia unampigia nini huyo wakati yeye amekubali umpeleke kituoni ndipo waliponichukua na kunipiga tena”.

      Riziki ambaye aliumia sehemu ya jicho baada ya kupigwa kibao na jicho lote kupiga wekundu, anasema kilichomshangaza ni kwamba kila kituo cha polisi alipokwenda alikataliwa kupewa barua ya kwenda kupata matibabu.

      “Tunafanywa kama sio raia wa nchi hii tulipokwenda kituo walikataa kutupa barua wakati wanajua hatuwezi kutibiwa kama tumeumia mpaka tupate barua ya polisi, tulipotoka Mahonda tukaja mjini tulikwenda Kituo cha Polisi Mkunazini wakakataa kutupa kibali tukenda Malindi pia wakatwambia nyinyi nendeni tu hukohuko hospitali wambieni madaktari kuwa mmepigwa na polisi …hawakutupa.”

      Bi Riziki ambaye aliumia mkono na jicho anasema hata walipokwenda hospitali walikataliwa kupewa tiba hadi watakapokwenda na barua ya polisi.

      Naye Hafsa Mohammed Mahfoudh (19) mkaazi wa Kinuni, Magogoni anasema katika zahma hizo watu wengi walikimbilia Msikitini na ndipo walipoona Polisi wakiingia Msikitini na kuwapiga wanawake na wanaume na kuwatoa nje huku wakitaka wanawake wote wavuliwe mashungi yao.

      “Walikuwa wakisema maneno mabaya mabaya huku wakituvuta mashungi yetu wakitwambia tokeni hapa Waislamu, Waislamu, Waislamu nini, wanafiki wakubwa, na kuna askari wa kike alinivuta sana shungi na kunipiga sana kwa....

      Inaendelea
      Albedo likes this.


    2. #61
      dudus's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2011
      Posts : 2,339
      Rep Power : 1018
      Likes Received
      1323
      Likes Given
      531

      Default Re: Uongo wa Sheikh Farid kutaka kuuawa huu hapa! Kweli uamsho ni hramu!!! Pole sana Sheikh!!!

      Quote By Jabulani View Post
      Jesus said:
      "44 You are of your father the devil, and your will is to do your father's desires. He was a murderer from the beginning, and has nothing to do with the truth, because there is no truth in him. When he lies, he speaks out of his own character, for he is a liar and the father of lies. "

      John 8:44

      EXACTLY! Na hicho ndicho kiini cha tatizo. Sawa sawa na atendavyo baba yao, wana nao hutenda hayo hayo. Kwani alikuwa mwongo na muuaji tangu mwanzo vivyo hivyo na wanaomtumikia. Thank you Jesus.
      Jabulani likes this.

    3. #62
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 16,049
      Rep Power : 14670
      Likes Received
      2954
      Likes Given
      2099

      Default Re: Uongo wa Sheikh Farid kutaka kuuawa huu hapa! Kweli uamsho ni hramu!!! Pole sana Sheikh!!!

      Hiyo picha aliibandika wapi hebu tupe link, isije kuwa wewe ndio uliibandika halafu uje msingizia Sheikh Farid.
      Gaijin likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    4. #63
      RGforever's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2011
      Posts : 2,107
      Rep Power : 1139
      Likes Received
      420
      Likes Given
      123

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      watanganyika wa ARUSHA walivyouawa na Polisi Je? Wao kupigwa virungu tu Kelele nyingi..

    5. #64
      Gaijin's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2007
      Posts : 11,394
      Rep Power : 12973
      Likes Received
      4638
      Likes Given
      2506

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      Quote By ruttashobolwa View Post
      hiyo picha kwanza ni fake, alaf huyu si sheikh wa uamsho kwa hiyo walita kutuambia amekoswa na risasi na hawezi kukoswa na risasi bali atapigwa kama ataendelea
      Picha ni fake ndo iweje?

      Kama mtu ananukuu maelezo ya Sheikh Farid kisha anaweka picha fake ndio kosa la Sheikh Farid?

      Ni sawa na wewe kusema unamiliki gari, kisha mie nikaweka picha ya Mercedes G55 pamoja na nukuu ya maneno yako, kisha nikapita kusema kuwa wewe ruttashobolwa ni muongo kwa sababu humiliki Mecedes G55!

      Common sense is not so common after all ....SMH


      *Hayo mengineyo kwenye bold siendei huko

    6. #65
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,798
      Rep Power : 19852
      Likes Received
      4412
      Likes Given
      1744

      Default

      Quote By knaan View Post
      zanzibar itakuwa huru INSHALLAH .makafiri hampendi taifa la kiislam zanzibar.kwani mnangangania kisiwa kidogo kama hiki.
      kwani zanzibar lazima hiwe huru kwa kuchoma makanisa na kuhatarisha amani?

      Sidhani kama unatumia vizuri kichwa chako kufikiri!


    7. #66
      Konya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th June 2011
      Posts : 831
      Rep Power : 573
      Likes Received
      81
      Likes Given
      1

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      picha feki ambayo imetoa uhalisia wa habari yenyewe na kuifanya iwe ya kutunga (feki) ili kuuhadaa uma kwa kinachoendelea huko visiwani

    8. #67
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : Tandhaniya
      Posts : 4,497
      Rep Power : 1291
      Likes Received
      1242
      Likes Given
      1267

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      hivi jamani matundu gani ya risasi yanakua identical yoote??
      halafu mbona hii picha ni ya kudownload from google??

    9. #68
      Bongolander's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th July 2007
      Location : Tandale
      Posts : 4,044
      Rep Power : 1423
      Likes Received
      614
      Likes Given
      44

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      Quote By masopakyindi View Post
      You dissapoint me!
      Do you really think they "missed"him?
      They did not even try to "kill" him. He is white noise any way.

    10. #69
      Chamoto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th December 2007
      Posts : 1,388
      Rep Power : 1237
      Likes Received
      483
      Likes Given
      355

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      Hayo yanayo onekana kama matobo ya risasi ni stika za kubandika kwenye magari zinapatikana kwenye Autopart stores kama NAPA, Autozone, O'rielly na Advaced Auto.
      If numbers are not beautiful, I don't know what is. - Paul Erdős

    11. #70
      masopakyindi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 3,882
      Rep Power : 4228
      Likes Received
      1049
      Likes Given
      429

      Default Re: Uongo wa Sheikh Farid kutaka kuuawa huu hapa! Kweli uamsho ni hramu!!! Pole sana Sheikh!!!

      Quote By Gaijin View Post
      Kaleta uongo wapi?

      Alisema wapi kuwa picha hiyo ni ya gari yake?

      Kama kuna uzembe na uongo ni wa mwandika makala, maana yeye ndiye aliyeweka picha bila ya kutoa maelezo yahusikayo

      Tanabahi:
      Kwa kazi yoyote ya kiuandishi unayowasilisha vielelezo, inatakiwa kwa sheria na kanuni za uandishi kuweka maelezo yanayohusu vielelezo hivyo [chini ya kielelezo], pamoja na chanzo cha vielelezo hivyo

      Kwenye taarifa/makala tuliyoletewa hakuna maelezo wala chanzo cha vielelezo hivyo
      Mbona waitetea sana hii kashafa Gaijin, sitarajii kama utakuwa na unajaribu ku-water down its implications!
      "If you don't know where you are going, any road will get you there-nowhere”

    12. #71
      kichomiz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2011
      Posts : 4,125
      Rep Power : 1251
      Likes Received
      671
      Likes Given
      80

      Default

      Quote By Honolulu View Post
      Angalia walikoitoa hiyo picha. Yaani huyu naye ni Sheikh kweli?

      http://img.auctiva.com/imgdata/1/4/7...46309610_o.jpg

      kama haifunguki copy yote halafu u paste kwenye google..
      Aseee!!! Kumbe si picha halisi wanasingizia tu.

    13. #72
      njiwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2009
      Location : ax^2+bx+c=0
      Posts : 5,193
      Rep Power : 2419
      Likes Received
      998
      Likes Given
      173

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      MNA MHUKUMU SHEKH NI MUONGO .. KWENYE HABARI HAKUNA MAHALA KASEMA HII NI GARI YANGU ... HUYU abdulahsaf ALIYELETA HIZI KHABARI NDIYE MUONGO IKIWEZEKANA AFUNGIWE UNLESS ALETE USHAHIDI SHEKH ALIONESHA HIYO PICHA NDIO GARI YAKE ...
      Gaijin and zomba like this.
      Pure Matrimony >> Purity starts here (Quran 24:26)
      My loyalty is to reason,and as a reasonable person I reserve the right to change my mind when presented with new information that alters my perspective" Njiwa"ᵀᴴᴱ'ᴼᴿᴵᴳᴵᴻᴬᴸ✯


    14. #73
      Gaijin's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2007
      Posts : 11,394
      Rep Power : 12973
      Likes Received
      4638
      Likes Given
      2506

      Default Re: Uongo wa Sheikh Farid kutaka kuuawa huu hapa! Kweli uamsho ni hramu!!! Pole sana Sheikh!!!

      Quote By masopakyindi View Post
      Mbona waitetea sana hii kashafa Gaijin, sitarajii kama utakuwa na unajaribu ku-water down its implications!
      Sijaribu ku-water down chochote, naonyesha flaw/dosari kwenye mantiki ya watu ku-base mjadala wote kwa picha fake ambayo hakuna sehemu inayoonyesha hiyo picha imetolewa na huyo Sheikh

      Sisemi kuwa ameshambuliwa kwa risasi wala sisemi kuwa hajashambuliwa kwa risasi............ninachojarib u ni kutanua wigo wa reasoning kwa Watanzania.

      Ni ukosefu wa mantiki kumwita mtu muongo kwa sababu maneno yake yamenukuliwa na kubadindikiwa picha fake. Tuseme huyo ni muongo kwa sababu nyengine, kuganda kwenye picha ni kujidumaza kifikra

    15. #74
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,798
      Rep Power : 19852
      Likes Received
      4412
      Likes Given
      1744

      Default

      Quote By njiwa View Post
      MNA MHUKUMU SHEKH NI MUONGO .. KWENYE HABARI HAKUNA MAHALA KASEMA HII NI GARI YANGU ... HUYU abdulahsaf ALIYELETA HIZI KHABARI NDIYE MUONGO IKIWEZEKANA AFUNGIWE UNLESS ALETE USHAHIDI SHEKH ALIONESHA HIYO PICHA NDIO GARI YAKE ...
      sasa ni njiwa vs mleta mada

      jana ilikuw muft vs sheikh ponda

      mbona mnatuchanganya sana
      yani mmegawanyika vipande, vipande.

    16. #75
      makwesa's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th June 2012
      Posts : 49
      Rep Power : 362
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      wanzanzibar songeni mbele ili muikomboe nchi yenu wala msiwajali maadui hata wamisri walianza mda mrefu sana hadi leo wamefanikiwa.M/MUNGU YU PAMOJA NANYI

    17. #76
      Fugwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Location : Tabata Dampo
      Posts : 872
      Rep Power : 726
      Likes Received
      109
      Likes Given
      47

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      Quote By Honolulu View Post
      Angalia walikoitoa hiyo picha. Yaani huyu naye ni Sheikh kweli?

      http://img.auctiva.com/imgdata/1/4/7...46309610_o.jpg

      kama haifunguki copy yote halafu u paste kwenye google..
      Ilike this evidence
      A Quick Temper Will Make a Fool of You Soon Enough. '' BRUCE LEE''

    18. #77
      Kima Mchanga's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 3rd October 2011
      Location : Dynamic
      Posts : 4,630
      Rep Power : 11256
      Likes Received
      648
      Likes Given
      551

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      Siasa za Zenji ndivyo zilivyo!
      Ilianza kwa umwagaji wa damu kwenye mapinduzi,na umwagaji damu utaendelea kwani
      auaye kwa upanga atauawa kwa upanga!!!
      Some people are alive only because it is illegal to kill them

    19. #78
      stroke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2012
      Posts : 1,585
      Rep Power : 687
      Likes Received
      176
      Likes Given
      5

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      hadithi njooo

    20. #79
      majorbuyoya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 663
      Rep Power : 2617
      Likes Received
      183
      Likes Given
      238

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      Nani atake kuuwa wewe bhana? ameamua kuweka picha za uongo ili apate kuungwa mkono na wazembe wa kufikiri.

    21. #80
      njiwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2009
      Location : ax^2+bx+c=0
      Posts : 5,193
      Rep Power : 2419
      Likes Received
      998
      Likes Given
      173

      Default Re: Walitaka kuniuwa, asema Sheikh Farid

      Quote By ruttashobolwa View Post
      sasa ni njiwa vs mleta mada

      jana ilikuw muft vs sheikh ponda

      mbona mnatuchanganya sana
      yani mmegawanyika vipande, vipande.
      Sina rival yoyote na mleta mada .. najaribu kusimama kwenye ukweli...! habari aliyoleta athibitishe kama gari kweli shekh alionesha ni yake.. kama sivyo basi mleta mada ni mzushi na kwa sheria za JF afungiwe kwa kipindi fulani
      Pure Matrimony >> Purity starts here (Quran 24:26)
      My loyalty is to reason,and as a reasonable person I reserve the right to change my mind when presented with new information that alters my perspective" Njiwa"ᵀᴴᴱ'ᴼᴿᴵᴳᴵᴻᴬᴸ✯


    Page 4 of 7 FirstFirst ... 23456 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...