Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchini

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 30
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,210
      Rep Power : 3557
      Likes Received
      3059
      Likes Given
      462

      Default CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchini

      JUMATATU, JUNI 25, 2012 05:16

      NA BENJAMIN MASESE, DAR ES SALAAM

      Na Gazeti la MTANZANIA

      CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewataka viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi nchini, kuwatambua wajumbe wa nyumba 10 wa chama hicho cha upinzani, kwa kuwa nao ni viongozi halali.

      Pia kimesema kuwa, kitendo cha wajumbe hao kubaguliwa, hakiwezi kukubaliwa kwa kuwa wamechaguliwa kwa mujibu wa sheria.

      Akizungumza na wandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Uchaguzi CHADEMA, Msafiri Mtemelwa, alisema hivi sasa kuna mvurugano mkubwa wa kiutawala ndani ya jamii kuhusu wajumbe wa nyumba 10.

      “Sisi zamani hatukuwa na wajumbe wa nyumba 10, lakini baada ya kuona hatuwezi kuchukua nchi bila kuwa na mizizi hadi chini, tumeweka viongozi hao na wanatambuliwa kisheria.

      “Pamoja na kwamba wanatambulika, jambo la ajabu ni kwamba, mtu akipata shida na kuwenda kwa mjumbe wa nyumba 10 wa Chadema kisha akapeleka barua hiyo kituo chochote cha polisi, hatapokelewa.

      “Lakini mtu huyo huyo akienda kituo cha polisi na barua ya mjumbe wa nyumba 10 wa CCM, anasikilizwa vizuri na kupewa kila aina ya msaada anaotaka.

      “Sasa tunahoji kwa nini mjumbe wa Chadema asitambuliwe na mjumbe wa CCM atambuliwe wakati wote hao ni wawakilishi wa vyama vya siasa?

      “Huu ni ubaguzi wa hali ya juu na hatuwezi kuukubali, bila shaka hii ni mbinu ya CCM kutaka kuendelea kuwalazimisha wananchi kwamba mabalozi wa CCM, ndio wenye uhalali wanaotambulika katika maeneo husika.

      “Kwa kifupi hatuwezi kukubali hali hii, wajumbe wetu wa nyumba 10 wapo kisheria na wanatambuliwa kama ilivyo kwa wajumbe wa CCM,” alisema Mtemelwa.

      Mtemelwa alisema kuwa, tangu Juni mosi mwaka huu, Chadema ilipoanza kuwaweka mabalozi katika maeneo mbalimbali nchini na kufanya kazi kama mabalozi wa CCM, baadhi ya wananchi wamekuwa wakikosa huduma pale wanapofika katika vituo vya polisi, ofisi za mtendaji wa kata na sehemu nyingine za Serikali, wakiwa na barua zilizotolewa na viongozi hao.

      Kutokana na hali hiyo, alitoa wito kwa viongozi wasiowatambua wajumbe wa nyumba 10 wa Chadema, kutoendelea na tabia hiyo vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria.

      DEUS NSHANGE likes this.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,210
      Rep Power : 3557
      Likes Received
      3059
      Likes Given
      462

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Polisi tuache ubaguzi, hatujifunzi ya Zambia?

    4. #3
      Filipo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Kiding'a
      Posts : 6,349
      Rep Power : 18614
      Likes Received
      3508
      Likes Given
      1663

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Ingekuwa uamsho, makanisa yangechomwa moto!

    5. #4
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,982
      Rep Power : 2589
      Likes Received
      637
      Likes Given
      776

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Hata wajumbe wa nyumba kumi wa CCM ni wa CCM hawatakiwi kuandika chochote kwenda serikalini. Mjumbe wa nyumba kumi anayejishughulisha na maswala ya watu wasio wanachama wake anafanya utapeli tu. CDM angalieni hii vita kwa umakini. police anayepokea barua ya mjumbe wa nyumba kumi anatakiwa kushitakiwa, maana anakua ameingiza siasa sehemu ya kazi. Washitakini wjumbe wa CCM kwa kuingilia shughuli za serikali za mitaa.

      Hii ni matatazo ya chama dhaifu. Hakioni haya kufanya mambo ya ajabu. Wamefanya makusudi kutoingiza uchaguzi wa wajumbe wa nyumba kumi katika uchaguzi wa serikali ya mitaa ili waendelee kuburuza wananchi, shame, shame, shame on you. Lakini sasa wameshajitengenezea jinai. Police wanachanganywa maana wanaenda kwa mzoea, hawatakiwi kupokea CCM wala CUF wala CDM katika level ya wajumbe, mpaka sheria zitakaporekebishwa.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    6. #5
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,947
      Rep Power : 888
      Likes Received
      382
      Likes Given
      144

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      CCM walifuikiri watatawala milele nakumbuka wakati tunaingia kwenye mfumo wa vyama vingi upinzani hasa CDM waliitaka serekali kuwatambua rasmi hawa mabalozi kwenye mfumo wa utawala ngazi ya chini kiserekali lakini ccm wakagoma.

    7. Miaka 50

    8. #6
      MANGUNGO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Posts : 1,146
      Rep Power : 620
      Likes Received
      251
      Likes Given
      14

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Watawatambua tu siku moja!!

    9. #7
      ALEX PETER's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 17th January 2012
      Posts : 100
      Rep Power : 391
      Likes Received
      21
      Likes Given
      60

      Default Chadema yatoa tamko kwa serikali


      CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kupitia Kurugenzi ya Kampeni na Uchaguzi inapenda kutoa taarifa kwa umma na kukemea ubaguzi unaofanywa na baadhi ya watendaji wa serikali dhidi ya viongozi wa vyama vya siasa, hususan wale wa chama kikuu cha upinzani na chama mbadala, CHADEMA.

      Chama kupitia Kurugenzi ya Kampeni na Uchaguzi kimepata taarifa kutoka ngazi ya chini ya uongozi, yaani misingi na matawi kwamba mabalozi wa nyumba kumi wa CHADEMA wamekuwa wakibaguliwa katika utendaji kazi wao wa kila siku na watendaji wa serikali, huku watumishi hao wakiendelea kutoa ushirikiano kwa mabalozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

      Ndugu wanahabari kupitia kwenu, tunaomba umma wa Watanzania ufahamu mambo mawili muhimu hapa;

      Kwanza; balozi wa nyumba kumi wa chama cha siasa si sehemu ya uongozi wa kiserikali. Suala hili limewahi kusisitizwa na serikali yenyewe kwa kutoa kauli bungeni. Ngazi rasmi ya uongozi wa kiserikali inaanzia serikali za mitaa/kitongoji.

      Lakini pia suala hili la ngazi za uongozi wa kiserikali na kuwa mabalozi si sehemu ya uongozi huo linaoneshwa pia katika katiba yetu ya sasa (pamoja na ubovu wake uliotusukuma tudai iandikwe upya).

      Pili; Sheria ya Vyama vya Siasa ya Mwaka 1992, inavitambua vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu kuwa vyote viko sawa mbele ya sheria. Halikadhalika kutokana na sheria hiyo, katiba za vyama vyote vya siasa ni sawa, hasa baada ya kuwasilishwa na kupitishwa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na kupitishwa.

      Kwa mantiki ya masuala hayo mwili hapo juu, Kurugenzi ya Kampeni na Uchaguzi, inatumia fursa hii kutoa tamko kwa umma kuwa mabalozi wa CHADEMA na CCM, wana haki sawa mbele ya sheria, kwa sababu wanatokana na vyama vilivyo sawa mbele ya sheria, halikadhalika katiba za vyama hivyo ziko sawa mbele ya sheria.

      Mabalozi wa CHADEMA wanapatikana kwa mujibu wa Katiba Mpya ya Chama ya Mwaka 2006, Sura ya Saba, ambayo inazungumzia ngazi, uongozi na majukumu ya vikao.

      Tofauti pekee ya mabalozi wa CHADEMA na CCM ni kwamba mabalozi wa CHADEMA wanavaa magwanda wale wa CCM wanavaa magamba. Lakini pia wanatofauti ya tabia;
      Mabalozi wetu wanasimamia ukweli, wakati wale wa CCM wanasimamia uongo, mabalozi wa CHADEMA wanasimamia uadilifu, wale wa CCM wanasimamia ufisadi, wakati mabalozi wetu wanasimamia na kutumikia wananchi, wale wa CCM wanatumikia maslahi ya chama chao na yao binafsi.

      Pamoja na kazi zingine, baadhi ya majukumu ya balozi wa CHADEMA ni pamoja na kuwa mwakilishi wa chama na wanachama. Ana wajibu wa kuwatambua wanachama wenzake, wananchi wote na pia anaufahamu wa kutosha wa masuala mbalimbali katika eneo lake la nyumba kumi.

      Tunasema hivyo kwa sababu wakati mwingine kutokana na kukosa mtandao mpana mpaka chini katika kaya za watu na wakati mwingine ukubwa wa maeneo ya kitongoji/mtaa unakuwa kikwazo, mamlaka za serikali katika kutekeleza majukumu mbalimbali zinashindwa kumtambua kila mwananchi, hivyo zinalazimika kuhitaji mtu/watu wa kusaidia kazi hiyo katika nafasi za uongozi walizoaminiwa katika maeneo madogo ambayo ni rahisi watu kutambuana. Hapo ndiyo dhana ya kuwa na kiongozi wa kaya kadhaa kwa jina la balozi unatokea.

      Mabalozi wetu CHADEMA kwa sababu wanatokana na taasisi inayotambulika kisheria, makini na imara wanafanya kazi kwa barua na mhuri wa chama.

      Kupitia tamko hili, Kurugenzi ya Kampeni na Uchaguzi ya CHADEMA, inawataka watendaji wa ngazi zote wa serikali kuacha mara moja tabia ya kuwabagua mabalozi wa CHADEMA kwani wanatokana na watu, wanatambua na wanaweza kutimiza wajibu wanaopaswa kufanya.

      Chama pia kinatumia fursa hii kutoa mwito kwa mabalozi wote wa CHADEMA nchi nzima ambao wanakutana na vikwazo vya watendaji wa serikali katika kutimiza majukumu yao mbalimbali ya kila siku, watoe taarifa rasmi kwa ngazi za juu zao, ili ngazi hizo husika nazo ziwasilishe kunakohusika, kwa ajili ya chama kuchukua hatua zaidi.


      Imetolewa Juni 24, 2012 Dar es Salaam na
      Msafiri Abdulrahaman Mtemelwa
      Mkurugenzi wa Kampeni na Uchaguzi CHADEMA

    10. #8
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,314
      Rep Power : 1199
      Likes Received
      1183
      Likes Given
      1560

      Default Re: Chadema yatoa tamko kwa serikali

      Hivi huyu msafiri naye ni muislamu. au hiki chama ni cha kiislamu jamani?

    11. #9
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2266
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Chadema yatoa tamko kwa serikali

      Quote By Sangarara
      Hivi huyu msafiri naye ni muislamu. au hiki chama ni cha kiislamu jamani?
      Ritz anajua, atakwambia jina la bandia.
      Simple life is healthier than egoism.

    12. #10
      zaleo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2011
      Posts : 791
      Rep Power : 535
      Likes Received
      234
      Likes Given
      528

      Default Re: Chadema yatoa tamko kwa serikali

      Mmm, chichemi mie. chijachikia njomba
      “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri” by Hon Lema, MP - Arusha

    13. #11
      WA-UKENYENGE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2011
      Location : Inside a Smart Grid
      Posts : 2,417
      Rep Power : 5038
      Likes Received
      782
      Likes Given
      1788

      Default Re: Chadema yatoa tamko kwa serikali

      Quote By Sangarara
      Hivi huyu msafiri naye ni muislamu. au hiki chama ni cha kiislamu jamani?
      Huwezi kujua madhara ya hiyo sentensi yako hadi yatakapotokea.
      "The usual conclusion is that you can't put a price on a human life. But you can if you must".

    14. #12
      Nduka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2008
      Posts : 5,580
      Rep Power : 1634
      Likes Received
      381
      Likes Given
      553

      Default

      Quote By Sangarara
      Hivi huyu msafiri naye ni muislamu. au hiki chama ni cha kiislamu jamani?
      Wanawatumia kama kondomu ma yuda iskarioti.

    15. #13
      DOUGLAS SALLU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th November 2009
      Posts : 3,598
      Rep Power : 1285
      Likes Received
      315
      Likes Given
      905

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Quote By Ecoli
      Wanawatumia kama kondomu ma yuda iskarioti.
      Kama wewe unavyotumiwa na mafisadi wenye mabilioni huko Uswiss hali wewe unaambulia posho ya ya kuganga njaa toka kwa nepi.
      NI UTAAHIRA MKUBWA SANA KUIUNGA MKONO CCM

    16. #14
      webondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2012
      Location : Chini ya mwembe
      Posts : 1,167
      Rep Power : 589
      Likes Received
      178
      Likes Given
      381

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Nimepita

    17. #15
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,389
      Rep Power : 1265
      Likes Received
      1208
      Likes Given
      1253

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      du...sisiem ina mbinu chafu sana...hata huku kwenye vyombo vya usalama??

    18. #16
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,314
      Rep Power : 1199
      Likes Received
      1183
      Likes Given
      1560

      Default Re: Chadema yatoa tamko kwa serikali

      Quote By WA-UKENYENGE
      Huwezi kujua madhara ya hiyo sentensi yako hadi yatakapotokea.
      Hiyo sentensi ni matokeo ya madhara yaliyopo mpaka sasa mkuu
      WA-UKENYENGE likes this.

    19. #17
      Ndallo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2010
      Location : LaRusa
      Posts : 4,124
      Rep Power : 6362
      Likes Received
      1481
      Likes Given
      415

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Wajumbe wa nyumba 10 CCM wanachojua nikusuluhisha ndoa za watu tu! That is all I know.
      '' Mtu ni Utu sio Kitu''

    20. #18
      Tuko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2010
      Posts : 4,625
      Rep Power : 13836
      Likes Received
      2265
      Likes Given
      2202

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Malalamiko mengine sio hadhi ya chama makini kama CDM. Tujiheshimu

    21. #19
      Uwezo Tunao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2010
      Posts : 6,873
      Rep Power : 2289
      Likes Received
      1140
      Likes Given
      1479

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      MGOGORO WA KI-KATIBA UNANUKIA NCHINI KITENDO CHA CCM KUDAIWA KUKWAMISHA UTENDAJI KAZI WA SERIKALI MASHINANI ETI KWA SABABU TU YA WAJUMBE KUTOKEA UPINZANI

      Haya madai ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) kudaiwa kuwa ni KIKWAZO KIKUBWA KWA UTENDAJI KAZI MURUA hadi mashinani eti kwa madai tu kwamba mjumbe fulani ni wa kutoka chama cha upinzani.

      Hakika hili ni jambo ambalo si adui tu wa dhana zima ya demokrasia ya vyama vingi nchini bali hadi hapo ni kwamba taaifa letu litakua limejielekeza moja kwa moja kuingia kwenye MGOGORO MZITO WA KIKATIBA nchini.

      Hili si jambo la kuchezea kwani ni jambo ambalo ni NYETI kuliko kawaida hili! Demokrasia tayari imeingia mtihani hapa!!! Maana ya kitendo kama hiki ni kwamba Serikali ya CCM haikubali Mfumo wa vyama vingi nchini.

      Hiyo si kazi ya CHADEMA tena bali ni kazi za John Tendwa kuhakikisha kwamba Demokrasia inapewa nafasi kufanya kazi yake kwa vyama vyote kote nchini.

      Ndio nasema ni jukumu la Waziri wa Mambo ya Ndani kuhakikisha kwamba serikali kamwe HAIKIUKI KATIBA YA NCHI inavyosema hivyo ni jukumu lake kuamuru vyombo vyake vyote vya usalama kufuata maelekezo ya katiba katika utendaji wao kazi wa kila siku.

      Naam, ni vema ikaeleweka kwa vyombo vya usalma kwamba wao wamewekwa na katiba na wala hawajawekwa na chama cha siasa ofisini. Hivyo ni jukumu lao wenyewe kuhakikisha kwamba wajumbe wa nyumba 10 waliopatikana kwamujibu wa sheria na maelekezo ya katiba ndio wanaokua washirika wao na wadau katika masuala ya kiutawala.

      Ndio, wafanyakazi wote wa serikali ni wafanyakazi wetu sote na wala si mali ya chama fulani na ndio maana kila siku tunawalipa nje ya mipaka ya itikadi zetu za kisiasa kupitia kodi zetu. Sasa pale kunapotokea ripoti eti mtumishi kama huyu sasa anaanza kuwa mbaguzi wa chama gani kukitumikia - ni kosa kubwa hilo!!!!

      Mhe John Tendwa ofisi yako itakua inashindwa kazi jambo hili likionekana kuendelea hata kwa siku moja zaidi nchini.

      Polisi wafanye kazi kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi kwa kushirikiana na wadau wote HALAI na wala si kufuata maelekezo ya chama kimojawapo cha ushindani (interested political party - CCM) kwa maelekezo yanayoweza kuibua mgogoro wa ki-katiba ndani ya nchi kwa sekunde chache tu.

      Nasema hili jambo linaloonekana dogo mbele yetu leo, likiachwaa likaendelea hivo bila kudhibitiwa huenda likasababisha sokomoko ambalo halikutarajiwa hata siku moja.

      Hatari iliopo ni kwamba wale wajumbe halali, ingawaaje ni wa kutoka vyama vya upinzani, waakiendelea kukataliwa sana na kubaguliwa na serikali ya CCM wao huenda wakajitengenezea 'MFUMO USIORASMI' wa kupitishia shughuli zote zao zaa kiutendaji. Na mfumo kama huo ukizaliwa nchini huenda ukawa vigumu kuiondoa baadaye.

      Kuna hatari kubwa y huu ubaguzi wa serikali ya CCM kwa watendaji mashinani ukazaa saratani itakayopanda juu hadi wizarani watu tukawa na mafisa waserikali lakini wa CUF, DC Handeni lakini wa NCCR-Mageuzi, Mlinzi wa Rais lakini akiwa ni mtendaji mwaminifu wa CHAADEMA.

      Nasema Wazee hebu tutafakari kidogo kama kweli hivi sasa baada ya kuwa na VYMA VINGI nchini hivi sasa ni kwamba kweli pia tunatamani uwepo wa SERIKALI NYINGI ndani ya taifa moja???? Ndio mfumo wa wapi huo??

      Kumbukeni kwamba kitendo cha Serikali ya CCM kukataa kuwapa ushirikiano uongozi wa serika za nyumba 10 zilizochaguliwa na wananchi wenyewe huenda ukageuka GHRIKA la serikaali yenyewe nalo KUKATALIWA na wananchi kote kwenye maeneo yao; hakuna hta mmoja wetu anayetamani kuona hali kama hiyo ikitokea nchini.

      Sasa ndio tusema tunafanya mambo gani kwa CCM kuleta mambo ya ukeweza kwenye mfumo rasmi wa kiserikali tunaougharimia sote wana-CUF, NCCR Mageuzi, CHDEMA pamoja na vyama vinginevyo na hali hiyo imepangwa kuendelea hadi lini kabla ya kuleta tafrani miongoni mwa wananchi??

      Ushindani wa kisiasa tukauendeleze kwa sana tu kote nchini lakini KAMWE Busara za kuzaliwa na utaifa mbele kma tai katika kila jambo tulitendalo lisije likatutoka hata siku moja - wadau wote zingatieni maneno haya machche.
      Last edited by Uwezo Tunao; 26th June 2012 at 17:24.

    22. #20
      Ringo Edmund's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2010
      Location : MDAWI
      Posts : 3,670
      Rep Power : 1361
      Likes Received
      885
      Likes Given
      586

      Default Re: CHADEMA yalalamika viongozi wake wa nyumba 10 kutotambuliwa na Serikali na Jeshi la Polisi nchin

      Chadema ianzishe na jeshi lake.
      ​kusema ni fedha na kusikilizwa ni zahabu.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...