Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 30
    1. #1
      Tuko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2010
      Posts : 4,650
      Rep Power : 13842
      Likes Received
      2295
      Likes Given
      2215

      Default Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Gazeti moja leo limeripoti kwa urefu maoni ya wabunge hawa wawili machachari, wakitetea madereva wa wabunge walipwe na serikali.
      Kwa maoni yangu siwaungi mkono hata kidogo. Ni wakati huu ambapo tunapigia serikali kelele kuwa ipunguze matumizi kwenye magari ya watendaji wake ikiwemo kuondolewa kwa madereva binafsi kwenye payroll ya serikali. Ni wakati huu ambapo napendekeza kuwa katika nchi hii, wawepo watu watano tu wenye madereva binafsi, yaani raisi na makamu wake, waziri mkuu, spika na jaji mkuu. Watendaji na viongozi wengine wote, wajiendeshe wenyewe au waajiri madereva wenyewe katika safari zao za kila siku, isipokuwa kwa safari za kikazi nje ya maeneo yao ya kazi ambapo watatumia madereva wa ofisi na gari za ofisi (maximum cruiser-mkonga).
      Kwa hiyo wakati tayari tukiona kuwa mzigo wa mamia ya magari na madereva serikalini ni mkubwa, itakuwa ni ajabu kama tukiamua kujiongezea tena mzigo wa madereva 320 wa kulipwa na serikali!!!

      Makamanda Zitto, na Deo nawakubali sana, but katika hili... no no no...

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Rich Dad's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th December 2010
      Posts : 741
      Rep Power : 576
      Likes Received
      100
      Likes Given
      12

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Zitto na Filikunjombe wamekurupuka au wanafanya kusudi tu! Serikali inashinikizwa kwa sasa kupunguza gharama za matumizi ktk uendeshaji, leo iweje hawa jamaa wanakurupuka kutaka madereva walipwe na serikali? Hawa jamaa wanajiona wao kuwa wabunge wana hijati kila aina ya upendeleo? Kwa kazi gani hasa wabunge wote wanafanya zaidi ya kupigana vijembe na mipasho ndani ya bunge
      Tuko likes this.

    4. #3
      arabianfalcon's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Location : Nipe tena
      Posts : 2,193
      Rep Power : 874
      Likes Received
      494
      Likes Given
      96

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Quote By Tuko
      Kwa hiyo wakati tayari tukiona kuwa mzigo wa mamia ya magari na madereva serikalini ni mkubwa, itakuwa ni ajabu kama tukiamua kujiongezea tena mzigo wa madereva 320 wa kulipwa na serikali!!!

      Makamanda Zitto, na Deo nawakubali sana, but katika hili... no no no...
      Kuna kitu hujakielewa hapa. Hoja siyo kwamba hawa madereva walipwe au wasilipwe. Bunge linatoa fedha kwaajili ya madereva. Kila mbunge anapewa tshs. Laki 100,000/= kwa mwezi kama mshahara wa dereva na ths. 300,000/= kama posho ya dereva. Pesa hii ya dereva anapewa kila mbunge ili amlipe kwa derevva wake.

      Kinachofanyika wabunge wanaziminya zike pesa na hazifiki kwa madereva. Tatizo ndo linaanzia hapo. Kakam bunge linatoa pesa, kwaaji ya madereva ni haki yao madereva kupewa pesa zao.
      The hunger for love is much more difficult to remove than the hunger for bread - Mother Teresa

    5. #4
      Ileje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th December 2011
      Posts : 1,041
      Rep Power : 583
      Likes Received
      405
      Likes Given
      107

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Kitu muhimu hapa ni kuhakikisha kuwa madereva hawa wanalipwa stahili zao na wabunge. Hili ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa raia wake hawanyonywi!
      Never give up your right!

    6. #5
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Hili la madereva nawaunga mkono, badala ya watu muhimu kukaa wakaendesha wenyewe, ule muda wataoutumia wakiwa ndani ya gari kwa mawasiliano na shughuli zingine ni muhimu sana kuliko mishahara ya madereva.

      Walipiwe madereva, unless kama mnataka kuona yaliompata yule Mbunge wa chadema.

      Ikumbukwe kuwa wabunge wengi hususan vijana hawa, wameyajulia magari baada ya kuingia bungeni, kama mnapenda usalama wao muweke sheria kabisa kuwa hawaruhusiwi kuendesha wenyewe na wapeni madereva.
      Majimoto and Sangarara like this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    7. Miaka 50

    8. #6
      webondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2012
      Location : Chini ya mwembe
      Posts : 1,167
      Rep Power : 589
      Likes Received
      178
      Likes Given
      381

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      well-said!

    9. #7
      chama's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 6th August 2010
      Posts : 4,934
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1177
      Likes Given
      915

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      kazi rahisi toa posho za wabunge ili kufidia ajira ya madereva

      Chama
      Gongo la Mboto DSM

    10. #8
      Tuko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2010
      Posts : 4,650
      Rep Power : 13842
      Likes Received
      2295
      Likes Given
      2215

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Quote By arabianfalcon
      Kuna kitu hujakielewa hapa. Hoja siyo kwamba hawa madereva walipwe au wasilipwe. Bunge linatoa fedha kwaajili ya madereva. Kila mbunge anapewa tshs. Laki 100,000/= kwa mwezi kama mshahara wa dereva na ths. 300,000/= kama posho ya dereva. Pesa hii ya dereva anapewa kila mbunge ili amlipe kwa derevva wake.

      Kinachofanyika wabunge wanaziminya zike pesa na hazifiki kwa madereva. Tatizo ndo linaanzia hapo. Kakam bunge linatoa pesa, kwaaji ya madereva ni haki yao madereva kupewa pesa zao.
      Laki 1??? Huo ni mshahara kima gani? Ngapi atapewa dereva, ngapi zitanda PAYE, ngapi pension nk??? Sasa hapo ndipo tatizo linapoanzia. Mbunge makini hawezi na hathubutu kuajiri dereva mwenye thamani ya laki 1, + laki 3 posho.
      Msimamo wangu, and I stand for this ni kuwa hata hizo laki nne ziondolewe. Wabunge wajiendeshe wenyewe na kama hawawezi, waajiri madereva kwa hela yao. Majority ya hawa wabunge walikuwa wanajiendesha wenyewe kabla ya kuwa wabunge na watajiendesha wenyewe baada ya ubunge wao kuisha..

    11. #9
      watu8's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th February 2010
      Location : Juu ya Tukutuku
      Posts : 15,236
      Rep Power : 31320
      Likes Received
      7543
      Likes Given
      7609

      Default

      Dawa hapa ni wabunge kupewa magari tu na wala si posho wala mshahara wa hao madereva....atakayehitaji dereva amuajiri kwa hela yake otherwise ajifunze kuendesha gari kwani halina ugumu wowote ni umwinyi tu unawasumbua

    12. #10
      Tuko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2010
      Posts : 4,650
      Rep Power : 13842
      Likes Received
      2295
      Likes Given
      2215

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Penye red, sio ukweli unless uje na data za kitafiti kuwa 'watu muhimu' wanakuwa na shughuli zenye tija zaidi wakiwa kwenye magari zaidi ya mishahara ya madereva.
      Penye blue, sio kweli maana tulishawahi kushudia viongozi wengi wakihusika katika ajali japokuwa walikuwa wanaendeshwa na madereva waliofuzu
      Penye dark red, sio kwenye kuwa wabunge 'wengi' wamayajulia magari baada ya kuingia bungeni..

    13. #11
      zaleo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2011
      Posts : 795
      Rep Power : 536
      Likes Received
      235
      Likes Given
      528

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Wanatikisa kiberiti tu.
      “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri” by Hon Lema, MP - Arusha

    14. #12
      stroke's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th February 2012
      Posts : 1,427
      Rep Power : 0
      Likes Received
      153
      Likes Given
      4

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Ndio maana unaona kila siku bajeti ni matrilioni lakini maendeleo hakuna..kumbe mijihela inapotoea kijinga jinga namna hii....ngoja niwe rais wenu...hakuna cha posho wala nini..kama hutaki kazi serikalini badili uraia....hamia nchi nyingine kabisa ambayo inaendekeza ukondoo

    15. #13
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Quote By Lynix
      Kwani wakiendesha hao madereva ndio hawawezi kupata Ajali hebu ondoa ushabiki wako wa Kizombi hapa
      Dereva kazi yake ni udereva. Mbunge ana mawasiliano mengi ya kufanya, mifano tumeona kwa wabunge wawili waliopata ajali, mmoja amepoteza maisha (alikuwa anaendesha mwenyewe na hajui gari vizuri), mwingine alipakia wazee wake (kuwaringishia shangingi jipya) na matokeo tunayajuwa. Hawa ni watunga sheria, na udereva wapi na wapi? saa ngapi waongee na simu? saa ngapi waendeshe?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    16. #14
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Quote By Tuko
      Penye red, sio ukweli unless uje na data za kitafiti kuwa 'watu muhimu' wanakuwa na shughuli zenye tija zaidi wakiwa kwenye magari zaidi ya mishahara ya madereva.
      Penye blue, sio kweli maana tulishawahi kushudia viongozi wengi wakihusika katika ajali japokuwa walikuwa wanaendeshwa na madereva waliofuzu
      Penye dark red, sio kwenye kuwa wabunge 'wengi' wamayajulia magari baada ya kuingia bungeni..
      Haihitaji utafiti, tunajuwa wanasafiri safari ndefu na fupi muda wote na inabidi wawasiliane na wananchi na shughuli zingine kwenye vi Ipad, sasa fikiria usalama wao hapo. Isitoshe, Mbunge mmoja analipwa fedha nyingi sana, na kutwa moja ukimuacha aendeshe kwa masaa average ya masaa 4 kwa mwaka, ni fedha ngapi hapo umemlipa kwa kuendesha tu? kwani akiendesha ujuwe hata mawasiliano amekata.

      Madereva ni muhimu sana kwa hawa waunga sheria, hiyo tukipenda tusipende.

      Lets think of productivity and safety for a while.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    17. #15
      POMPO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2011
      Posts : 3,027
      Rep Power : 1189
      Likes Received
      1112
      Likes Given
      646

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Zitto na FK acheni kuleta hoja dhaifu....
      "Tumefika hapa kutokana na UDHAIFU wa Rais Jakaya Kikwete.." J.J. Mnyika, Bungeni,June,2012.

    18. #16
      bodachogo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 14th April 2011
      Posts : 89
      Rep Power : 428
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      sio hoja dhaifu bali posho/mshahara wa dereva unalipwa na serikali kupitia kwa mbunge ,nadhani wazo litakuwa na mashiko kama huo mshahara utaenda moja kwa moja kwa dereva na sio kupitia kwa mbunge.

    19. FJM
      #17
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,178
      Rep Power : 2569
      Likes Received
      5329
      Likes Given
      4587

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Quote By zomba
      Dereva kazi yake ni udereva. Mbunge ana mawasiliano mengi ya kufanya, mifano tumeona kwa wabunge wawili waliopata ajali, mmoja amepoteza maisha (alikuwa anaendesha mwenyewe na hajui gari vizuri), mwingine alipakia wazee wake (kuwaringishia shangingi jipya) na matokeo tunayajuwa. Hawa ni watunga sheria, na udereva wapi na wapi? saa ngapi waongee na simu? saa ngapi waendeshe?
      zomba, wabunge ni binadamu kama walivyo watu wengine. Na si kweli kwamba wabunge wana mambo mengi kutushinda sisi tunaofanya kazi na kujiendesha wenyewe. Tuachane na tabia za kitumwa, anayetaka dereva amwajiri yeye mwenyewe na siyo haya mambo ya kusema kuwa wabunge wana mambo mengi? Hivi Vicky Kamata na Lucinde wana mambo gani?

    20. #18
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Quote By FJM
      zomba, wabunge ni binadamu kama walivyo watu wengine. Na si kweli kwamba wabunge wana mambo mengi kutushinda sisi tunaofanya kazi na kujiendesha wenyewe. Tuachane na tabia za kitumwa, anayetaka dereva amwajiri yeye mwenyewe na siyo haya mambo ya kusema kuwa wabunge wana mambo mengi? Hivi Vicky Kamata na Lucinde wana mambo gani?
      Wewe una wananchi wangapi jimboni kwako wanaokupigia simu kila siku kutaka kutatuliwa matatizo yao? wewe una wasiliana na wizara na idara ngapi kwa siku kufatilia matatuzi ya wananchi wa jimbo lako? wewe una safari ngapi kwa mwaka kwenda majimboni kusikiliza wananchi wako?

      Nyie ndi mnaona kuwa kuwapa madereva ni "luxury", haujui maana ya productivity, mawazo kama yako ndio yalikuwa ya Nyerere na matokeo katuwacha maskini wa mwisho duniani.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    21. #19
      masopakyindi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 3,748
      Rep Power : 4197
      Likes Received
      1011
      Likes Given
      416

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Charity begins at home.
      Mtu unateteaje hoja za kupinga ufisadi wakati hata dereva wako unamnyonga!
      Hili suala ndio linaonyesha unafiki wa wabunge wengine kudhani good governance iko serikalini tu, na haiko kwa mtu mmoja mmoja.
      Mbunge anaye pewa fungu la kumlipa dereva wake, naye hafanyi hivyo, basi huyo ni fisadi tu na hafai kupewa madaraka yoyote nchini.
      "If you don't know where you are going, any road will get you there-nowhere”

    22. #20
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kwa hili la Madereva, Zitto na Filikunjombe siwaungi mkono

      Quote By masopakyindi
      Charity begins at home.
      Mtu unateteaje hoja za kupinga ufisadi wakati hata dereva wako unamnyonga!
      Hili suala ndio linaonyesha unafiki wa wabunge wengine kudhani good governance iko serikalini tu, na haiko kwa mtu mmoja mmoja.
      Mbunge anaye pewa fungu la kumlipa dereva wake, naye hafanyi hivyo, basi huyo ni fisadi tu na hafai kupewa madaraka yoyote nchini.
      Hilo ni suala lingine kabisa.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...