Taarifa za Dar, Morogoro, Mwanza, Dodoma kuhusu mgomo wa Madaktari,
WAKATI kukiwa na mgawanyiko mkubwa kwa madaktari nchini katika kushiriki mgomo ulioitishwa na Chama cha Madaktari nchini (MAT), Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salam, Said Meck Sadik amepiga marufuku mikusanyiko ya aina yoyote katika hospitali za Jiji, yenye lengo la kuchochea watumishi wa afya kugoma.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Sadik alisisitiza kuwa Serikali itachukua hatua kali za kisheria kwa watu watakaobainika kushiriki katika kuwashawishi watumishi wa sekta ya afya wakiwemo madaktari na wauguzi kugoma.
Sadik anaungana na viongozi wengine wa kitaifa na Mahakama Kuu ya Tanzania, kutoa amri ya kusitishwa kwa mgomo huo wa madaktari ambao ulianza jana katika baadhi ya hospitali huku huduma katika hospitali nyingine zikiendelea vizuri kutokana na madaktari na wauguzi katika hospitali hizo kutogoma.
“Kufuatia tangazo la Chama cha Madaktari nchini (MAT) la kuanza mgomo siku ya Jumamosi tarehe 23 Juni, 2012, Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Kazi, Dar es Salaam imetoa amri ya kusitisha mgomo huo mpaka hapo pande zote mbili yaani Serikali na Chama cha Madaktari Tanzania yatakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.”
Ilisema taarifa ya Mahakama Kuu kwa vyombo vya habari. Amri hiyo ya Mahakama ilitolewa kufuatia maombi namba 73 ya mwaka 2012 yaliyowasilishwa chini ya hati ya dharura na Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Chama cha Madaktari Tanzania.
Gazeti hili lilipofika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jana asubuhi lilishuhudia madaktari wakiendelea na kazi kitendo kilichoonesha kuwa hawakushiriki katika mgomo.
Wakati hayo yakiendelea, Serikali imeendelea kuwataka madaktari wote nchini kuendelea na kazi wakati suala la kupatiwa suluhisho likiwa katika chombo cha kisheria Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi.
Pia imesema itakuwa tayari kutekeleza maamuzi ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Kazi, kuhusu mapendekezo yatakayotolewa juu ya suala zima la maslahi na haki za madaktari kama maombi yao yalivyowasilishwa.
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Selaman Rashid, aliyasema hayo mjini Morogoro jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufanya ziara ya ghafla katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ili kuona iwapo madaktari wameamua kutekeleza mgomo wao au la.
Akiwa hospitalini hapo, Naibu Waziri huyo alishuhudia madaktari kwa kushirikiana na wauguzi wakiendelea kufanya kazi mbalimbali za kuhudumia wagonjwa licha ya Chama cha Madaktari kutoa tamko la kuwataka wagome nchi nzima kuanzia jana.
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa hiyo ukiongozwa na Mganga Mkuu wa Mkoa , Dk. Godfrey Mtey , ulimtembeza Naibu Waziri maeneo mbalimbali ikiwemo wodini, maabara na chumba cha kujifungulia na kuzungumza na baadhi ya wagonjwa waliokuwa wakipatiwa tiba.
“Nawaomba madaktari wote waendelee na kazi ya kuwahudumia wagonjwa wakati suala lao lipo kwenye chombo cha kisheria ...sote tumekubaliana usuluhishi wa mgogoro huu uamuliwe na Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi. Hata hivyo alisema, Serikali imejipanga kuhakikisha inaboresha maslahi ya wafanyakazi wote si kwa ajili ya madaktari pekee ili wapate mishahara kulingana na kazi wanazozifanya.
Alisema, Serikali inapozungumzia mishahara haizungumzii kwa daktari pekee bali inazungumzia sekta mbalimbali na si kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pekee bali na wizara nyingine za Serikali.
Aliupongeza Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Morogoro kwa watumishi wake wakiwemo madaktari kuendelea na kazi za utoaji wa huduma kwa wagonjwa. Kutoka Dodoma taarifa zinasema kuwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma Dk Ezekiel Mpuya alisema jana kuwa hali ni shwari katika hospitali hiyo na hakuna mgomo.
Akizungumza na gazeti hili, Dkt. Mpuya alisema madaktari na wauguzi walikuwa wanaendelea na kazi zao kama kawaida na hakukuwa na mgomo wowote.
“Hali ni shwari na wale wote wenye zamu wako kazini isipokuwa daktari mmoja aliyeko kwenye mafunzo leo hajaripoti sijui ana tatizo gani, lakini hapa hakuna mgomo,” alisema.
Hata hivyo hali haikuwa shwari jijini Mwanza kwani madaktari zaidi ya 200 waliopo katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando walianza mgomo rasmi jana baada ya Serikali kushindwa kutoa majibu ya kuridhisha kuhusu madai yao mbalimbali.
Katika mahojiano na gazeti hili Mwakilishi wa Kamati ya kufuatilia madai ya Madaktari hao waliyapeleka serikalini, Dk Richard Kirita alisema kwamba madaktari wa kada zote katika hospitali hiyo wapo kwenye mgomo isipokuwa baadhi ya madaktari bingwa pamoja na wakuu wa idara.
Mapema wiki hii, Kamati ndogo ya Madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyokuwa ikifuatilia mgogoro dhidi yao na Serikali ilisema haijaridhishwa na majibu yaliyotolewa na Serikali juu ya madai yao na kuonesha nia ya kufanya mgomo wa nchi nzima kuanzia jana.
“Ni kweli tumeanza mgomo rasmi, madaktari waliokuwa zamu leo (jana) hawajaenda kazini, hata hivyo kwa kuwa leo si siku ya kazi unaweza kudhani hakuna mgomo, lakini njoo Jumatatu ndio utapata picha halisi ya mgomo kwa sababu wagonjwa watakuwa wengi lakini hakutakuwa na huduma,” alisema Dkt. Kirita.
Hata hivyo alisema kwamba wanaendelea na vikao ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na wenzao wa Dar es Salaam ili kujua ni hatua zipi zaidi wachukue kuhusiana na mgomo wao huo.
Dkt. Kirita alisema kwamba katika kikao cha madaktari wa Bugando kilichofanyika hivi karibuni kujadili majibu ya Serikali juu ya madai yao na kuhusisha jumla ya madaktari 202 walikubaliana kwa pamoja kuanza mgomo kuanzia jana iwapo madai yao hayatatekelezwa na Serikali.
Katika mgomo wa kwanza wa madaktari uliofanyika mapema mwaka huu madaktari walikuwa na madai mbalimbali yakiwemo ya kuboreshwa kwa huduma za afya zikiwemo dawa, vitanda na vifaa tiba, mishahara na nyumba za madaktari.
Baadhi ya watu waliokuwa wamepeleka wagonjwa katika hospitali hiyo jana walionekana wakiwaondoa baada ya kukosa huduma kutoka kwa madaktari ambao baadhi walikuwa kwenye kikao na wengine walionekana katika vikundi vikundi wakipiga soga.
Kwa upande wao wagonjwa katika Hospitali hiyo ya Rufaa ya Bugando wameiomba Serikali pamoja na madaktari walio kwenye mgomo kumaliza tofauti zao ili madaktari waweze kurejea kazini na kuwapatia huduma.
Wakizungumza jana katika wodi namba 6 na 8, Yohana Matinde, Abel Joseph, Martha Maduhu na Pendo Saimon walisema kuwa tangu kutangazwa kwa mgomo huo jana, hawajaweza kuonana na madaktari zaidi ya kuhudumiwa na wauguzi kwa kugawiwa vidonge na sindano.
“Tunawaomba Serikali na madaktari wamalize tofauti zao, maana endapo hali hii ya mgomo ikiendelea tunaoumia ni sisi, na pia ni vyema Serikali ingesikia madai ya madaktari ili waweze kurejea kazini,” alisema Joseph.
Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na gazeti hili ulibaini kuwa kwa Jiji la Mwanza mgomo huo ulikuwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, tofauti na katika Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure ambapo madaktari na baadhi ya wauguzi walikuwa wanaendelea na kazi kama kawaida.
Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
CCM oyeeee, sisi watawala tunasema punda afe mzigo ufike. Maisha bora kwa kila Mtanzania ndio haya. Tumejaribu, tumeweza, tunasonga mbele. Usisahau kuipigia CCM kura, mafiga matatu hapo 2015
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
By Kadakabikile
Kama hayo kweli yapo, kwa nini msingegoma toka mwanzo kwa ajili ya kupatiwa hivyo vifaa? Badala yake mnadai hayo baada ya kuona kuwa mngegoma kwa ajili ya maslahi yenu tu msingeeleweka. Madaktari acheni kuua watu na badala ya kuendelea na mgomo wa kipuuzi, sasa mrudi kuchapa kazi.
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.
Kwa hiyo kwa maoni yako, kwa kuwa hawakugoma tangu mwanzo, basi waendelee kukubaliana na mazingira haya. Kwa maana rahisi, kwamba wewe unaridhika na hali ilivyo sasa ktk hospitali na vituo vyetu vya afya, siyo? Huenda ikawa wanatumia njia mbaya kujaribu kubadili hali hii, je wewe kwa upande wako umetumia njia gani bora kubadili hali hii, au ndio vile umeridhika nayo, siyo?
Kama hayo kweli yapo, kwa nini msingegoma toka mwanzo kwa ajili ya kupatiwa hivyo vifaa? Badala yake mnadai hayo baada ya kuona kuwa mngegoma kwa ajili ya maslahi yenu tu msingeeleweka. Madaktari acheni kuua watu na badala ya kuendelea na mgomo wa kipuuzi, sasa mrudi kuchapa kazi.
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.
Mkuu mimba hutunga na kujifunguwa wakati wake ukifika baada ya mama kupata uchungu, hapa walipofika ndo mahala pake hata uvumilivuvu hufikia hatua ikashindikana. Sasa niwangapi wanaokufa kwa kukosa madawa? kukosa tiba sahihi kwa kukosa vetendea kazi sahihi kugundua ugonjwa halisi kwa tiba sahihi? kwa makosa yanayotokana na msongo wa kiwawazo ndani ya vichwa vya madakitari wakifikilia watapata wapi fedha kukidhi mahitaji ya familia zao kupelekea kufanya operations za makosa na kuuwa bila kukusudia,wangapi wanakufa kwa kuambukizana magonjwa hospitalini kwa kupagwa kama ndizi mawodini? Je ni waheshimewa wangapi wakizidiwa huendelea kubakia humhum nchini kwa matibabu bila kuenda india kwanini ........
Mkuu hakika wengi mno wanapoteza uhai kwa uzembe wa serikali, imefika wakati tuibane serikali tupate huduma bora mbona kodi tunalipa au wewe mkuu hulipi? naimani unalipa na pia unandugu na jamaa ambao ungependa siku moja waipate haki ya kupata huduma bora kwa afya zao
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
Kipindi hiki serikari ina mkakati wa kupeleka wagonjwa wote India kama mgomo utatokea. Serikari imejipanga kwa udhaifu utakaojitokeza, ndio sababu Mwinyi kapewa hiyo wizara.
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
By Kadakabikile
Kama hayo kweli yapo, kwa nini msingegoma toka mwanzo kwa ajili ya kupatiwa hivyo vifaa? Badala yake mnadai hayo baada ya kuona kuwa mngegoma kwa ajili ya maslahi yenu tu msingeeleweka. Madaktari acheni kuua watu na badala ya kuendelea na mgomo wa kipuuzi, sasa mrudi kuchapa kazi.
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.
unayajua madai ya madaktari kuanzia mwanzo au unadamdia treni kwa mbele?
Kipindi hiki serikari ina mkakati wa kupeleka wagonjwa wote India kama mgomo utatokea. Serikari imejipanga kwa udhaifu utakaojitokeza, ndio sababu Mwinyi kapewa hiyo wizara.
Serikali ianze kwa kumpeleka mhanga wa fumanii bw Simbachawene
Haya sasa! Maisha bora kwa kila Mtanzania ndiyo hivyo sasa!
Halafu unamkuta mtu anaifagilia ccm..........!
Mkuu ni vilaza wa ushabiki kwa ccm, sidhani kama hawayaoni haya ila hujifanya sintofaham na wengine hujikuta kuchanganya madawa vichwani kwa kuingiza udini kwenye maada wazi kabiasa kama hii.
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
Kwa Madaktari kugoma kwa sababu ya maslahi yao ni sawa kwakua silaha ya mwisho walionao wafanyakazi katika kudai haki yao ni Mgomo,wasiwasi wangu ni je madaktari walishaanza mazungumzo na Serikali,kwanini mara hii wamekataa mazungumzo? au labada serikali haitaki kutekeleza makubaliano yao? Kama inawezekana anayejua makubaliano hayo ya Madaktari na Serikali atuwekee hapa pamoja na yale ambayo Serikali imeyakubali.
Sasa mbona waziri wa afya siku ile Bungeni hakugusia kabisa mapungufu ktk hiyo hospital badala yake alizungumzia madaktari wanadai maslahi yao tuu!
hayo mapungufu atayaonea wapi wakati hajawahi kuingia wodini ,hao si wanatibiwa india,tena wangegoma kuandika rufaa kwa viongozi wa serekali ili watibiwe hapa bongo
Kama hayo kweli yapo, kwa nini msingegoma toka mwanzo kwa ajili ya kupatiwa hivyo vifaa? Badala yake mnadai hayo baada ya kuona kuwa mngegoma kwa ajili ya maslahi yenu tu msingeeleweka. Madaktari acheni kuua watu na badala ya kuendelea na mgomo wa kipuuzi, sasa mrudi kuchapa kazi.
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.
ndugu kadakabikile, huwezi kuwalaumu madaktari kwa kutogoma hapo hawali, kumbuka kila jambo na wakati wake, km wewe usingeweza kuamrisha uzaliwe ulaya, hata mgomo haukuwezekana hivyohivyo, wakati wake haukufika. Serikali inafahamu mapungufu yaliyopo ktk hospitali zetu ndo maana wao wanaenda kwa first consultation nje. Waache madaktari wagome km siri kali hawataki mgomo watekeleze madai ya madokta maramoja. Mkuu wa kaya ahamuru maramoja uone km hayajatekelezwa.
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
By adolay
Mkuu mimba hutunga na kujifunguwa wakati wake ukifika baada ya mama kupata uchungu, hapa walipofika ndo mahala pake hata uvumilivuvu hufikia hatua ikashindikana. Sasa niwangapi wanaokufa kwa kukosa madawa? kukosa tiba sahihi kwa kukosa vetendea kazi sahihi kugundua ugonjwa halisi kwa tiba sahihi? kwa makosa yanayotokana na msongo wa kiwawazo ndani ya vichwa vya madakitari wakifikilia watapata wapi fedha kukidhi mahitaji ya familia zao kupelekea kufanya operations za makosa na kuuwa bila kukusudia,wangapi wanakufa kwa kuambukizana magonjwa hospitalini kwa kupagwa kama ndizi mawodini? Je ni waheshimewa wangapi wakizidiwa huendelea kubakia humhum nchini kwa matibabu bila kuenda india kwanini ........
Mkuu hakika wengi mno wanapoteza uhai kwa uzembe wa serikali, imefika wakati tuibane serikali tupate huduma bora mbona kodi tunalipa au wewe mkuu hulipi? naimani unalipa na pia unandugu na jamaa ambao ungependa siku moja waipate haki ya kupata huduma bora kwa afya zao
Mkuu nafikiri umeeleweka sana, watakao bisha ni ujeuri tu.
Hawakumbuki yule mgonjwa alopasuliwa kichwa badala ya mguu muhimbili?! yale ndo matokeo halisi ya frustration za kazini ingawa wenyewe wanaita uzembe.
Watuulize waalimu, ukiingia class ukiwa na msongo-mawazo kinachotokea huwa ni nini! fikiria natakawa niwafundishe vijana wa MBA au MSc Entrepreneurship kuhusu strategic planning huku nawaza mwanangu leo atatibiwa kweli?! maana nina bima ya afya tena ya kijani lakini upuuzi ndio huo, unakutana na daktari hapa, X-ray unaambiwa kapige ahmadiya, unafika pale wanakwambia bima hatupokei inatucheleweshea malipo, unalipa mfukoni mwako, unarudi na Tax kwa dr pale moro mkoa, unaambiwa sijui nini
Mke wangu alifanyiwa upasuaji kwaajili ya uzazi oct 2011, haaaaaaa!! Mungu bariki nilikuwa nimejiandaa mfukoni, pia nikawa na matumaini ka kakadi kangu ka kijani ka bima ya "chafya" maana si afya tena, eti imagine kuanzia sijui kitu gani cha kupokelea mkojo, mpaka drip za baada ya upasuaji unanunua, na duka la dawa liko nje tu pale getini unapoingia hosp mkoa (moro), Mungu wangu, kufika pale, unaambiwa kuna dawa zinazopokea bima na nyingine ambozo ndo muhimu sana unaambia hazipokei bima, KHAAA nikachanganyikiwa, my wife wangu mpenzi yuko theatre,
bado unakuta Dr analalamika hajanywa hata chai, tangu saa 10 usiku anapiga upasuaji tu, na Mrs ndo kaingia kama emergency maana alidevelop severe bleeding. Maskini, kidogo tu mtoto wangu wa kiume angefariki, maana walikuja kukuta mji wa mimba umeshachanika, na mkono wa mtoto ulikuwa unavinjari nje ya tumbo la uzazi, Imagine!!
Mungu saidia ni baada ya kujieleza na kwa kuwa nilisomaga Mzumbe A-Level, nina madaktari nafahamiana nao ambao tulikuwa class moja. so angekuwa asiyefahamika, anakosa my wife wake, na my baby boy wake.
kinachosikitisha, kila mwezi wanakula kama 37,500 hivi za bima ya afya kwa afya ambayo siyo afya hata kidogo, p.u.m.b.a.v.u zenu serikali, ebu waboresheeni kwanza maslahi, pili vitendea kazi madaktari weeeeeetuuuuu eeeeeeeeeeee
natamani kuingia barabarani kuondoa serikali madarakani
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
MGOMO WA MADAKTARI DAWA YAKE NI MABADILIKO YA SERA NA MFUMO WA TIBA NCHINI NA WALA MABAVU KAMWE HAUTOMSAIDIA MTU WALA SERIKALI YETU
Mgomo wa madaktari hauwezi kuzuiliwa kwa mabavu isipokua ni kwa njia moja tu ya kubadilisha sera na mfumo wa uendeshaji wa sekta zima ya tiba nchini.
Kama mtu alijidanganya mahala kwamba hili la madaktari ni upepo tu utapita basi itakua ni masikitiko makubwa sana jinsi gani mambo yatakavyoanza kuzorota mahospitalini.
Hali hii isiposhughulikiwa vema na kwa wakati pengine makundi mengine ya wafanyakazi kama vile walimu nao kuamua kuunga tera - safari hii nao kwa kufanya hivo hadharani badala ya ule mgomo baridi tunaofahamu kwamba unaendelea hadi hivi sasa.
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
hebu tembelea hospitali za mikoa au wilaya ujionee.kwa mfano kanda ya kaskazini hauna kipimo cha CT scan,kilikuwepo KCMC lakini kimekufa.ukienda kanda ya ziwa ni hayo hayo na ukirudi muhimbili vilevile.
hakuna anayeshtuka wala kushughulikia swala hili kwa sababu kiongozi anayehitaji huduma hii mara moja hukwea pipa na kwenda appolo india wewe mlala hoi utajijua mwenyewe!!
Re: madaktari waanza kufunguka!! sasa kuweka wazi hali halisi za mahospitali yetu
By meningitis
kadri mda unavyosonga mbele ndivyo tunavyozidi kuona vimbwanga kati ya serikali na madaktari.sasa madaktari wameamua kuweka hadharani madhambi ya serikali.wameamua kuwaambia wananchi ukweli kwa nini huduma za afya ni mbovu.una mfano huu hapo chini halafu pitia blogs mbalimbali ujionee
No insults but does anybody else smell a rat?! Public being used as a bargaining chip! Who really has the general public interests at heart? Please guys I really want to know, I am kind of confused.
hebu tembelea hospitali za mikoa au wilaya ujionee.kwa mfano kanda ya kaskazini hauna kipimo cha CT scan,kilikuwepo KCMC lakini kimekufa.ukienda kanda ya ziwa ni hayo hayo na ukirudi muhimbili vilevile.
hakuna anayeshtuka wala kushughulikia swala hili kwa sababu kiongozi anayehitaji huduma hii mara moja hukwea pipa na kwenda appolo india wewe mlala hoi utajijua mwenyewe!!
.............Hii serikali kwa kweli itatufikisha pabaya sasa kwa hali inavyoonyesha.
Ingali wameshatufikishaga kitambo lakini kwa sasa wanataka ku2zamisha Watanzania ktk dimbwi la umaskini ambalo hata serikali nyingine ikija chukua madaraka hakika itakutaga wizara zote zimebaki magofu tu!
Juzi ktk kusoma ile bajeti ya mafisadi mbona wizara hii cjasikia waziri mlengwa akilizungumzia hili la kutokuwepo ama kuharibika kwa hz vyombo ktk hosptal hz?
Kweli hawa ccm ni janga lililowazi kwa Watanzania!
Mabadiliko yanawezeka hakika............haiwezekani tukaachiwa majengo tu!
Mgomo sasa inaanza kuzooleka masikioni mwa wananchi wa Tanzania. Jambo ambalo nadhani lapaswa kuangaliwa ni kwanini kuna migomo, Mfano madaktari wadai kugoma, TUCTA, walimu n.k. na maandamano ya wazee wa Afrika mashariki na wanafunzi vyuo vikuu. Najiuliza hivi watawala wanayaona haya? Kama ndiyo hatua gani wanachukua? Au ni funika moto kwa makuti? Migomo na maandamano yasiyoisha ni dalili za serikali kushindwa, ni dalili za viongozi kutokua makini, kushindwa kazi na uzembe. Nadhani ipo haja watanzania kuacha utani, waamke kujitazama upya, walikotoka, walipo na waendako. Migomo na maandamano isiwe za kutishia nyau, msimamo wa dhati uonekane wa kuwaajibisha viongozi, wananchi kuacha ushabiki badala yake palipo na madai ya kweli km haya madaktari, walimu, TUCTA, wanafunzi na wazee wa EAC yaungwe mkono kwa nguvu zote kushinikiza watawala kuwajibika kama hakuna utatuzi, wajuwe maamuzi ni wananchi na kama hawawezi kuleta mabadiliko(wananchi) waache kulalamika. Poleni madaktari kwa madai yenu yamsingi yanayofanyiwa mzaa.
Follow Us Here