Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 45
    1. #1
      Jason bourne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd July 2011
      Posts : 1,385
      Rep Power : 1387
      Likes Received
      610
      Likes Given
      19

      Default Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Baada ya kuwa kwenye mgogoro wa umeme nchini Tanzani yapata miaka karibu 15 sasa, nimeamua kufuatilia hasa tatizo lilianzia wapi na nani waliohusika.

      Nilianzia ndani ya Wizara ya nishati na madini kwa kufuatilia mikataba iliyoyaingiza nchini makapuni ya uzalishaji umeme,

      Taarifa halisi na nyaraka zinabainisha kuwa tatizo hili lilianza baada ya mfanyabiashara maarufu bwana Rugemalia kuiingiza nchini kampuni ya IPTL kutoka Vietnam!

      Mchakato unatajwa kuwa ndugu Rugemalila alikuwa akifanya biashara ya Mchele kutoka Vietnam mwaka 1995, katika harakati zake za kibiashara huko Vietnam aliweza kuunda urafiki na wanaotajwa kuwa wamiliki wa IPTL hii ya sasa.

      Mwaka 1997 kulianza kutokea uhaba wa umeme tanzania ambapo ndani ya Wizara ya nishati na Madini kulipendekezwa itafutwe kampuni itakayozalisha umeme wa dharula wa haraka zaidi ili kunusuru taifa:

      Kamishna wake alikuwa ni Ndugu Patrick Rutabanzibwa ambae katika uchunguzi umebaini ni ndugu na Rugemalila ambae ni mfanyabiashara na mmiliki wa Mabibo Heineken ya Ubongo,

      Baada ya Rutabanzibwa kuona kuwa pale wizarani kuna mwanya wa kupiga hela aliweza kuongea na mdogo wake ambae katika nyaraka nyingi anatajwa zaidi kwajina moja tu la Rugemalila kuwa atafute kampuni ya kufanya kazi hiyo haraka sana!

      Rugemalila bila kusita akawashtua washikaji zake ambao taarifa kutoka Vietnam zinasema waliokuja si wale waliokuwa na urafiki na Rugemalila bali ni marafiki wa marafiki wa Rugemalila kutoka Malaysia.

      Na hawakuwa na sifa ya kiushawishi ya kufanya mradi wa kimataifa ingawa waliweza kushirikiana pamoja bila tatizo kwakuwa yalikuwa ndio malengo yao ya pamoja!

      Makubaliano ya mkataba ilikuwa ni mashine zitakazoletwa na IPTL, zitakuwa na mfumo wa kutumia gesi na mafuta, hilo liliingizwa katika makubaliano ya mkabata kwakuwa tayari kulikikuwa na mradi wa songas uliokuwa ukiendelea kujengwa .

      Katika uchunguzi ulioenda sambamba na mahojiano ya kijasusi, bwana Rutabanzibwa anasema miezi miwili baada ya kusaini mkataba ule alishangazwa kubaini kuwa IPTL inaleta mitambo inayotumia mafuta tu na alipouliza wasaidizi wake wakamuambia mkataba unasemaje? Akaamua kwenda kuangalia upya mikataba aliyohusika na yeye kuisaini lakini anasema "nilishangaa kuona kipengele kilichokuwa kikisema kuwa genereta hizo zitakuwa na uwezo wa kutumia gesi kimetolewa" nakuwa generata za mafuta mazito tu.

      Baada ya kupandishwa nakuwa Katibu mkuu, anasema "nilizuia kuletwa kwa mitambo hiyo kwakuwa nilizungukwa na kubadilishiwa mkataba feki"

      Uchunguzi umebaini Bwana Rutabanzibwa hakuzuia ama lengu la kuzuia halikutimilika na alihongwa!

      Ukweli unabainika katika dokezo la 12/6/2001 toka kwa JK (rais sasa) likiwa limeandikwa kwa mkono na kalamu ya wino mwekundu "Kama nilivyokuahidi jana katika kikao chetu, waambie wailete hiyo mitambo kama ilivyo na mimi nitafanya kama tulivyokubaliana" chini ikasainiwa J Kikwete

      Licha ya hivyo bado uchunguzi unazi kubaini ushirika wa karibu wa Jakaya Kikwete na mtu anaetajwa kuwa ni Rugemalila anaeonekana alikuwa na nguvu ya ushawishi kwa Rutatabanzibwa na wavietnam wa IPTL.

      Kwakuwa baada ya kufuatilia kwa kina imegundulika kuwa katika account ya bank (CRDB) ya biashara ya mchele ya Rugemalila, kila mwezi kiasi cha pesa Shilingi milioni 130 kilikuwa kikihamishwa kwenda kwenye account mbili tofauti lakini za mtu mmoja aliyefahamika kwa jina Asha Salum Mohamed mkazi wa Arusha mjini,

      Jambo la kuvutia zaidi nikuwa pesa hizo zikifika kwenye hizo account zilikuwa zikitolewa ndani ya masaa 48, na kuingizwa kwenye akaunti ya ya Abas Zuberi Musa (NMB) na hapo hutolewa siku hiyohiyo (Cash) na kupelekwa mojakwa moja katika akaunti ya siri ya Rais Jakaya kikwete iliyopo Standard Chartered Bank,

      Abas Z. Musa kwa sasa ni mmoja wa usalama wa taifa watiifu kwa rais Jk na anaaminiwa sana kwa mambo binafsi ya rais!

      Huo ndio ushikiano wa JK na Rugemalila katika biashara ya mchele,

      Bado naendelea kufuatilia kwa undani kujua mambo makuu mawili kwanza:

      (1) Kwanini aliamua kufanya biashara hiyo ya mchele kwa siri na kuchukua faida kwa siri kubwa hivyo?

      (2) Iwapo Jakaya Kikwete alihusika moja kwa moja au kwa aina yoyote ya biashara ya IPTL

      Nitafanya uchunguzu huu kwa undani na kujua nini hasa kipo kwenye tatizo la umeme Tanzania, ninaanza na IPTL kisha wengine watafuata!

      Kwasababu za kiuchunguzi nyaraka sitaziweka hapa mpaka uchunguzi ukamilike wote!
      Last edited by Jason bourne; 24th June 2012 at 01:09.
      mzamifu, Topical, FJM and 2 others like this.

    2. Study Abroad

    3. #2
      Godfrey Electronics's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 13th March 2012
      Posts : 184
      Rep Power : 398
      Likes Received
      24
      Likes Given
      2

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Uuwiii.....! Kweli JK sio DHAIFU

    4. Nzi
      #3
      Nzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Location : 740 Park Avenue
      Posts : 3,313
      Rep Power : 21622
      Likes Received
      924
      Likes Given
      822

      Default Re: Uchunguzi: Huyu ndie aliileta IPTL nchini Tanzania, Je nani yupo nyuma yake?:

      Quote By Jason bourne
      Ukweli unabainika katika dokezo la 12/6/2001 toka kwa rais likiwa limeandikwa kwa mkono na kalamu ya wino mwekundu "Kama nilivyokuahidi jana katika kikao chetu, waambie wailete hiyo mitambo kama ilivyo na mimi nitafanya kama tulivyokubaliana" chini ikasainiwa J Kikwete
      Chifu Jason bourne, hapo juu sijakuelewa vizuri. Unamaanisha Kikwete ndiye aliyesaini kama rais tarehe hizo? Kikwete si amekuwa rais toka mwaka 2005?!

      Ebu fafanua hili chifu kabla haujaendelea na uchunguzi wako.
      "You can't make a scene if you don't have little green"-------Jim Carrey

    5. #4
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 573
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Kaka kweli we kamanda hapo Jk alikuwa waziri wa mambo ya nje

    6. #5
      Jason bourne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd July 2011
      Posts : 1,385
      Rep Power : 1387
      Likes Received
      610
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By Nzi
      Chifu Jason bourne, hapo juu sijakuelewa vizuri. Unamaanisha Kikwete ndiye aliyesaini kama rais tarehe hizo? Kikwete si amekuwa rais toka mwaka 2005?!

      Ebu fafanua hili chifu kabla haujaendelea na uchunguzi wako.
      Alikuwa Waziri nimeweka mabano kuonyesha sasa ni rais!

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      zumbemkuu's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 11th September 2010
      Location : street dweller
      Posts : 5,317
      Rep Power : 1998
      Likes Received
      2114
      Likes Given
      7786

      Default Re: Uchunguzi: Huyu ndie aliileta IPTL nchini Tanzania, Je nani yupo nyuma yake?:

      Quote By Nzi
      Chifu Jason bourne, hapo juu sijakuelewa vizuri. Unamaanisha Kikwete ndiye aliyesaini kama rais tarehe hizo? Kikwete si amekuwa rais toka mwaka 2005?!

      Ebu fafanua hili chifu kabla haujaendelea na uchunguzi wako.
      alikuwa mambo ya nje na kuna kipindi alikuwa waziri wa nishati na madini.
      DHAIFU
      "watakaotubeza na kututukana wasameheni wanahitaji ukombozi wa fikra" Mh.G.Lema

    9. Nzi
      #7
      Nzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Location : 740 Park Avenue
      Posts : 3,313
      Rep Power : 21622
      Likes Received
      924
      Likes Given
      822

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Quote By Jason bourne
      Alikuwa Waziri nimeweka mabano kuonyesha sasa ni rais!
      Sawa. Sasa endelea na uchunguzi chifu.
      "You can't make a scene if you don't have little green"-------Jim Carrey

    10. #8
      Jason bourne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd July 2011
      Posts : 1,385
      Rep Power : 1387
      Likes Received
      610
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By Nzi
      Sawa. Sasa endelea na uchunguzi chifu.
      Asante!

    11. FJM
      #9
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,167
      Rep Power : 2566
      Likes Received
      5317
      Likes Given
      4585

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Jason, kwani IPTL siyo ya Malaysia?

    12. #10
      Pendael laizer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th January 2012
      Posts : 945
      Rep Power : 560
      Likes Received
      90
      Likes Given
      5

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Jk ni kweli naye pia anauhusika kwa umaskini tulionao watanzania

    13. #11
      Bufa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st March 2012
      Posts : 337
      Rep Power : 427
      Likes Received
      56
      Likes Given
      161

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Pongezi kwako mkuu, inahitaji utulivu na ufuatiliaji wa hali ya juu kupata hizi habari. Ama kwa hakika Kikwete kaanza mbali na hii nchi na sembuse katika kila kitu either cha faida au hasara nchini kina mkono wake. Kila la kheri mkuu

    14. #12
      Jason bourne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd July 2011
      Posts : 1,385
      Rep Power : 1387
      Likes Received
      610
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By FJM
      Jason, kwani IPTL siyo ya Malaysia?
      Kuna mkanganyiko mkubwa hapo mkuu, kwenye nyaraka za majadiliano wanatajwa kuwa ni wa Vietnam, watu halisi waliopo sasa ni wa Malaysia, sasa sijui nani wahusika walio kwenye nyaraka au waliopo sasa?

    15. #13
      Sunshow's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th November 2011
      Posts : 689
      Rep Power : 517
      Likes Received
      95
      Likes Given
      2

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Endelea mkuu na uchunguzi zaidi.

    16. #14
      dada jane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th December 2011
      Posts : 503
      Rep Power : 476
      Likes Received
      92
      Likes Given
      0

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Karibu tena JB. We missed u. Hasa kwenye thread za kiintellegencia. Songa mbele ninakuaminia sana. Muda si mrefu Tanzania itarudi mahala pake mara baada kila lililo chini ya kapet litakuwa linawekwa juu kweupe

    17. #15
      Mupirocin's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Tanzania
      Posts : 1,562
      Rep Power : 805
      Likes Received
      523
      Likes Given
      408

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Aminia sana JB, ukimaliza hili tupe majina ya walioweka hela zetu huko duniani kwa siri. Hii habari ya muuza mchele na IPTL si ngeni akilini mwangu nilishaisikia. Thanks again JB. Jamani tuichangie JF iendelee kuwepo coz itatupa majina ya wezi wetu wote ili wakati wa kuichukua iwe rahisi na kunyonga mmoja baada ya mwingine. Big JB

    18. #16
      Mupirocin's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Location : Tanzania
      Posts : 1,562
      Rep Power : 805
      Likes Received
      523
      Likes Given
      408

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      JK mwizi, fisadi. Kumbe udhaifu wake unatokana na madudu haya hawezi kukemea wakati na yeye ni mwizi

    19. #17
      Jason bourne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd July 2011
      Posts : 1,385
      Rep Power : 1387
      Likes Received
      610
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By Sunshow
      Endelea mkuu na uchunguzi zaidi.
      Asante!

    20. #18
      Jason bourne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd July 2011
      Posts : 1,385
      Rep Power : 1387
      Likes Received
      610
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By dada jane
      Karibu tena JB. We missed u. Hasa kwenye thread za kiintellegencia. Songa mbele ninakuaminia sana. Muda si mrefu Tanzania itarudi mahala pake mara baada kila lililo chini ya kapet litakuwa linawekwa juu kweupe
      Nashukuru tupo wote ndugu usiku na mchana tuna ipigania nchi yetu!

    21. #19
      Jason bourne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd July 2011
      Posts : 1,385
      Rep Power : 1387
      Likes Received
      610
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By Mupirocin
      JK mwizi, fisadi. Kumbe udhaifu wake unatokana na madudu haya hawezi kukemea wakati na yeye ni mwizi
      Ukweli utajulikana na kila kitu kila kitu kitakuwa wazi

    22. #20
      Che-lee's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th June 2011
      Posts : 305
      Rep Power : 463
      Likes Received
      85
      Likes Given
      3

      Default re: Uchunguzi: Chanzo cha matatizo katika sekta ya Umeme Tanzania na ujio wa IPTL

      Bila jf haya ningeyapata wapi? Hakika mungu umeileta jf ije kulikomboa taifa letu!

    23. Miaka 50
    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...