Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 98
    1. #1
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 19,235
      Rep Power : 12776
      Likes Received
      6455
      Likes Given
      999

      Default Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Wanabodi.

      Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.

      Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

      Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

      Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

      Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.

      JF Daima


    2. #2
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      We koma kutusemea watanzania.

      Ni mjinga peke yake ndie anaweza kuwa na imani na mtu mdhaifu!
      Life without problems never make a strong and good person!

    3. #3
      MtamaMchungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2011
      Posts : 1,553
      Rep Power : 813
      Likes Received
      715
      Likes Given
      64

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Vipi ule utaratibu maalumu aliowaundia wezi wa EPA, aka "rudisha usamehewe wizi"??
      Jasusi likes this.
      No one wants to die. Even people who want to go to heaven don't want to die to get there - Steve Jobs

    4. #4
      simon james's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 277
      Rep Power : 419
      Likes Received
      136
      Likes Given
      8

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Mwache amdanganye kuwa huu ni upepo wa kisiasa utapita alafu asubiria kimbunga kije kumzoa!

    5. #5
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 16,053
      Rep Power : 14671
      Likes Received
      2955
      Likes Given
      2099

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Ritz,

      Kwa hayo hayo ndio Kikwete hapendeki. Ukitazama wengi wa wanaoleta chuki na kejeli utakuta wengi ni wale wale waliozibiwa mianya ya wizi kwa mara ya kwanza toka hii nchi ipate Uhuru katika kipindi hiki cha Kikwete.

      Baada ya muda mfupi, Kikwete anaanza kushughulikia fedha zilizowekwa nje ya nchi na hawa wizi wa mali za umma. Ni kazi ngumu sana, lakini ipo njiani inakuja, tutaona chuki zikizidi. Ukitazama kijuu juu tu hata bila ya uchunguzi wa kina utakuta wote wenye chuki ni wale wale 83%. Hao ndio "wasomi" bila kuelimika, hao ndio walioifikisha nchi ilipofika na hao ndio wezi wakubwa.

      Tunamtakia kila la heri Kikwete kwa hii kazi ngumu aifanyayo sasa, na matokeo tunayaona. Na hapo ndiyo eti "dhaifu".

      Subiri uone majibu sifuri sasa hivi.
      Profesa likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe


    6. #6
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 19,235
      Rep Power : 12776
      Likes Received
      6455
      Likes Given
      999

      Default

      Quote By zomba View Post
      Ritz,

      Kwa hayo hayo ndio Kikwete hapendeki. Ukitazama wengi wa wanaoleta chuki na kejeli utakuta wengi ni wale wale waliozibiwa mianya ya wizi kwa mara ya kwanza toka hii nchi ipate Uhuru katika kipindi hiki cha Kikwete.

      Baada ya muda mfupi, Kikwete anaanza kushughulikia fedha zilizowekwa nje ya nchi na hawa wizi wa mali za umma. Ni kazi ngumu sana, lakini ipo njiani inakuja, tutaona chuki zikizidi. Ukitazama kijuu juu tu hata bila ya uchunguzi wa kina utakuta wote wenye chuki ni wale wale 83%. Hao ndio "wasomi" bila kuelimika, hao ndio walioifikisha nchi ilipofika na hao ndio wezi wakubwa.

      Tunamtakia kila la heri Kikwete kwa hii kazi ngumu aifanyayo sasa, na matokeo tunayaona. Na hapo ndiyo eti "dhaifu".

      Subiri uone majibu sifuri sasa hivi.
      zomba.

      Ni kweli kabisa watu wanamchukia Kikwete sababu kaziba mianya ya rushwa na kulindana...hata hoja inayosimamiwa na Chadema ya Ufisadi haina nguvu tena wanaofanya hivyo wameshulikiwa na ushahidi upo katika mahakama mbali mbali nchini.

    7. #7
      Dingswayo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th May 2009
      Location : Tanzania/Europe
      Posts : 2,747
      Rep Power : 14821
      Likes Received
      1227
      Likes Given
      2771

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Quote By Ritz View Post
      zomba.

      Ni kweli kabisa watu wanamchukia Kikwete sababu kaziba mianya ya rushwa na kulindana...hata hoja inayosimamiwa na Chadema ya Ufisadi haina nguvu tena wanaofanya hivyo wameshulikiwa na ushahidi upo katika mahakama mbali mbali nchini.
      Kuna mwandishi aliandika kitabu ambacho kinaelezea habari kuwa ni 'kinyumbe cha mambo'. Hakika uliyoyaandika hapa ni kinyume cha mambo!
      Semper fi!

    8. #8
      WAHEED SUDAY's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2011
      Posts : 2,880
      Rep Power : 2982
      Likes Received
      484
      Likes Given
      320

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Imani gani waliyonayo watanzania kuhusu Kikwete? kuwafanya wajutie kumchagua?
      Just a charcoal, don't expect anything white

    9. #9
      mamajack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 1,153
      Rep Power : 587
      Likes Received
      275
      Likes Given
      71

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Ndugu mtoa mada nadhani hujafanya reseach ya kutisha unachokiongelea.

      Kila siku unasikia watu wanashindwa kusafirisha mazao sababu ya ubovu wa miundo mbinu ya barabara, hata hao wabunge wanaliliamikia hili japo wanakosa uzalendo na wanaogopa kwenda kinyume na maelekezo ya wakuu wao.

    10. #10
      Gwalihenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 2,496
      Rep Power : 910
      Likes Received
      650
      Likes Given
      414

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Quote By Ritz View Post
      zomba.

      Ni kweli kabisa watu wanamchukia Kikwete sababu kaziba mianya ya rushwa na kulindana...hata hoja inayosimamiwa na Chadema ya Ufisadi haina nguvu tena wanaofanya hivyo wameshulikiwa na ushahidi upo katika mahakama mbali mbali nchini.
      Hawa wakulima wadogo (peasants) kule Ruvuma , Njombe, Mbeya, Rukwa, Iringa............ambao hawapati pembejeo za kilimo nao wanamchukia kwa kuwa wamezibiwa mianya ya rushwa?

    11. #11
      kupelwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th August 2011
      Location : DAR-ES-SALAAM
      Posts : 477
      Rep Power : 491
      Likes Received
      129
      Likes Given
      31

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Sikutegemea mchabuzi kama wewe una hoja dhaifu za kuwaelzea chekechea umesahau kuwa hapa ni jamii forum. Tunashukuru kutambua upeo finyu wa fikra yako.Ila punguza kujipendekeza na kuwa mchumia tumbo. Watanzania wa sasa ni waelewa na wanazitambua ghiriba na propanganda za akina TAMBWE HIZA.

      Nchi hii ina matatizo mengi na hasa kwa wananchi walio wengi, kwasas iefikia kuwa nchi iliyo na upungufu wa chakula , wakati ina ardhi kubwa yenye rutuba, mabonde mengi na nguvu kazi inayotosha na asili ni kuchapa kazi za kilimo.

      Sasa kama wananchi hawasaidiwi kwa hili bali bla bla watakuwa na imani naye kivipi? Namna anavyochukua hatua kuhusu kufufua ushurika ni vichekesho tupu. Nakumbuka wakati anatoa mafedha ya kikwete wachambuzi wengi tusihi fedha hizo zitumike kufufua ushirka na kilimo kwa ujumla ndo hapo impact ingeoneka. Leo hii ukiuliza fedha hizo ni blabla tu na nadharia kubwa.

      Kumsifia JK ni uendewazimu. Alingia madarakani kukiwa na tatizo la umeme, leo miak takribani miaka ifikayo 8 bado blabla. Kama angekuwa si dhaifu ingechukua miaka miwili tu lazima tungeona mageuzi katika sekta hii. Tuna tatizo la kupanda bei ya mafuta , lakini maelezo yanatoka bado blabla na hakuna hatua za dhati kuonyesha wanachukua hatua gani.

      Hata hao EWURA ni blbabla tu wameshikiliwa na matajiri wa mafuta, tabu kabisa. Uje sekta ya usafirishaji kama ATCL, TRL jamani tunamzimu gani wa kijinga? Halafu unakuja na hoja za chekechea!inaonyesha shule ulikuwa unabebwa sana kwa degree za chupi wewe

    12. #12
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,798
      Rep Power : 19852
      Likes Received
      4414
      Likes Given
      1744

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Sikuwai kufikiri kama ritz una uwezo wa kumtete JK.

      Kweli nime amini inabidi nichanganyikiwe kwanza ndio nikubali huo utetezi wako!

      Hivi lowasa amefikishwa mahakama gani?

    13. #13
      Mundali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th September 2010
      Posts : 697
      Rep Power : 650
      Likes Received
      144
      Likes Given
      77

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Mwenye data halisi atoe, JK na serikali yake wanasema wamejenga barabara zenye urefu wa km 11,000.

      Ninazozifahamu ni Minjingu Babati km 160 Babati Singida km 163, Manyoni Singida Kamalizia km 60 zilizobaki katika barabara ya Dodoma mpaka kanda ya ziwa, Ndundu Somanga km 60 alizoacha Ben bado hazijaisha, Handeni Mkata km 110, hazijakamilika, Babati Kondoa km 5 tu zina lami, Kondoa Dodoma imeanza kujengwa km 3 (kuna jumla ya km 290 za barabara hii), Dodoma Mtera Iringa km 320 zimekamilika km 35. Hizo nilizozitaja zina jumla ya km 1,163.

      Tuwekeeni mambo hadharani hizo barabara zenye urefu wa km 10,000 nyingine ni zipi? Au ndio zile za Tabora - Nzega, Tabora - Manyoni, Sengerema, Nyakanazi - Kibondo, Kigoma - Kasulu - Mpanda, Tunduma - Sumbawanga na kadhalika. Tuwekeeni data tupate km 11,000 as per magufuli data.

    14. #14
      Ben Saanane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th January 2007
      Posts : 6,948
      Rep Power : 45018
      Likes Received
      5329
      Likes Given
      6535

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Aachane na hoja Dhaifu za CHADEMA? Kwani yeye ni Imara kuliko hizo hoja?
      Wametuonyesha Jeuri ya ukaburu,tuwaonyeshe jeuri ya Umkhontho we sizwe kupitia Red Brigade.Tukiwaonyesha woga wetu, itakua silaha imara zaidi kwao kutumaliza-Ben Saanane

    15. #15
      TOWNSEND's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th May 2011
      Location : kwa ngulelo
      Posts : 1,160
      Rep Power : 643
      Likes Received
      201
      Likes Given
      31

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Quote By Ritz View Post
      Mkuu wangu TOWNSEND usihamaki unaona sasa ukihamaki na akili inahama hatimaye unatoa lugha za matusi..

      Sio kila shida zetu za maisha kasababisha JK shida zingine ni matokeo ya yale tuliyoyatengeneza kwa mikono yetu wenyewe.
      ritz kuna yale ya mtu mmoja moja na yale ya ujumla ambayo waliomchagua na wasiomchaguwa jk anatakiwa ayafanye kama kiongozi mkuu ...kila mtu anakusanya kodi au anachangia kila ukinunua kitu hata kiberiti mafuta ya taa na bia nk lakini msimamizi mkuu ni yeye
      hebu fikiria hakuna kinachoenda hakuna maji ya uhakika hata hapo anapoishi yeye dar kila siku bomba linapasuka ninahamaki ka vile yapo mengi ya kipuuzi kuliko mazuri...hatuna takukuru wala police wala mahakama ndio maana nasema wewe labda haupo nchini.hujawahi kuibiwa ili police na mahakama itende kazi yake inabidi wewe mwenye kuibiwa utoe pesa ili usaidiwe ..ili mtoto wako asome lazima umpeleke privata au st fulani ndio apate eelimu...nyumba ikiwaka moto unaomba mungu hakuna gari za zimamoto...taka unavizia usiku unatupa kwenye chaka lolote'
      hivi hata wale wanaochota maji kwa ndoo huwaoni wapo pembeni ya ziwa au mito .
      kinachouma zaidi michango yetu wanakula watu wachache yaani rafiki zake waajiriwa serikalini hasa viongozi sio walim na dactari

      For tommorow belonging to those people who prepared fo it

    16. #16
      Ubongo Silaha's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 101
      Rep Power : 384
      Likes Received
      45
      Likes Given
      18

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Unapojenga barabara kwa kuomba misaada badala ya rasilimali unazoachia ziondoke!
      Unaposamehe kodi kiasi kikubwa kuliko misaada ya masharti
      Unapokubali bei ya kujenga barabara kwa kilomita iwe inflated na usiwe na system ya ku-verify
      Unapotoa amri zisitekelezwe mfano kiushusha bei ya sukari na usichukue hatua
      Unapoanzisha mada kama ya kuvua gamba na isitekelezwe na uliruhusu gamba likusute kwenye kikao unachokiongoza wewe
      Unapoita madaktari ukawabembeleza warudi kazini wakakuheshimu na siku ya pili ukawasuta mbele ya 'Wazee wa Dar
      Unaporuhusu mbunge aliyepokea milioni moja akamatwe lakini waliooiingiza Tz kwenye mikataba ya kipuuzi na ikathibishwa wameweka fedha zaidi ya bilioni ughaibuni wapete
      Unapoangalia wasaidizi wako wakipanda na kushabikia udini
      Unapotumia Bakwata kama kipaza sauti chako
      Unaposhindwa kuwaadabisha mawaziri wako hadi ushinikizwe na Bunge

      Nashindwa kuwa na imani na wewe
      MpendaTz likes this.

    17. #17
      Mwakalinga Y. R's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd October 2008
      Location : UVUNGUNI
      Posts : 2,180
      Rep Power : 980
      Likes Received
      931
      Likes Given
      2307

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Quote By Ritz View Post
      Wanabodi.

      Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.

      Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

      Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

      Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

      Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.

      JF Daima
      Hapo kwenye nyekundu.Naona unajaribu kutudanganya bila mafanikio ,Jk ameingia madarakani fedha za barabaza zilishatengwa na awamu ya tatu.Labda utoe takwimu sahihi kwamba ni barabari ipi mpya ambayo haikuwa kwenye mipango na utekelezaji wa serikali ya awamu ya tatu ameinzisha yeye.Alipoingia madarakani miradi mingi imekwama kutokana na kukosekana kwa fedha.Fedha nyingi amezielekeza kwenye miradi mipya hewa ili wafanye ufiiadi mfano RICHMOND na safari za nje nyingi zisizo na tija kwa taifa.

      Ukweli ni kwamba miradi mingi mikubwa wamepindisha ukweli kuwa hakuiazisha wala kuwekea mipango Jk ila wanadanganya uma kwa kujitafutia umaarufu.Mfano daraja la Umoja (Mpakani na Msumbiji) na EPZ (Export Processing zone).

      Bado nakubaliana na kauli ya J.Mnyika kwamba Jk ni dhaifu.
      MpendaTz likes this.
      “Even the smallest person can change the course of the future.”-Galadriel


    18. #18
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 19,235
      Rep Power : 12776
      Likes Received
      6455
      Likes Given
      999

      Default

      Quote By Mundali View Post
      Mwenye data halisi atoe, JK na serikali yake wanasema wamejenga barabara zenye urefu wa km 11,000. Ninazozifahamu ni Minjingu Babati km 160 Babati Singida km 163, Manyoni Singida Kamalizia km 60 zilizobaki katika barabara ya Dodoma mpaka kanda ya ziwa, Ndundu Somanga km 60 alizoacha Ben bado hazijaisha, Handeni Mkata km 110, hazijakamilika, Babati Kondoa km 5 tu zina lami, Kondoa Dodoma imeanza kujengwa km 3 (kuna jumla ya km 290 za barabara hii), Dodoma Mtera Iringa km 320 zimekamilika km 35. Hizo nilizozitaja zina jumla ya km 1,163. Tuwekeeni mambo hadharani hizo barabara zenye urefu wa km 10,000 nyingine ni zipi? Au ndio zile za Tabora - Nzega, Tabora - Manyoni, Sengerema, Nyakanazi - Kibondo, Kigoma - Kasulu - Mpanda, Tunduma - Sumbawanga na kadhalika. Tuwekeeni data tupate km 11,000 as per magufuli data.
      Hadi kufika mwaka 2015 barabara ya kutoka Nyakanazi-Uvinza- Mpanda- Sumbawanga hadi Tunduma itakuwa imekamilika kwa kiwango cha lami, huku barabara ya kutoka Mwandiga jimboni kwa Zitto Kabwe hadi Kidahwe-Nguruka-Urambo hadi Tabora itakuwaimishakamilika baada ya kukamilika ujenzi wa daraja la Mto Malagalasi ambalo lilizishinda serikali zilizotangulia kabla ya JK.

    19. #19
      joystaff77's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th September 2011
      Posts : 24
      Rep Power : 397
      Likes Received
      12
      Likes Given
      0

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      Pumbaaaaaa!!!! Kwenu kuna wanawake mpe mmoja uone imani yake acha kukurupuka

    20. #20
      Sir R's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2009
      Location : Moshi
      Posts : 1,146
      Rep Power : 720
      Likes Received
      101
      Likes Given
      24

      Default Re: Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

      JK rais dhaifu Africa
      Umaskini wa Tanzania ni Matokeo ya Akili ndogo kuongoza Nchi

    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...