Re: Katiba: Tanganyika Irudi Kwanza Ndipo Rasimu ya Katiba Ifuate
Ni kweli kwamba "Nyinyiemu" wametumia muda mwingi sana kushughulikia kero ndogo ndogo kiasi cha kuwabore watu lakini bado wanaotaka uvunjike kwa kutoa kauli kali na vitisho ni watu ambao hata Mapinduzi Matukufu ya 1964 ni kero kwao. Ila kama kuna majority nyuma yao kwa nini usivunjwe? It is only fair uvunjike kwa kuwa majority wanataka hata kama ni grave mistake kuuvunja.
Ushauri wangu ni vema tupige kura ya maoni pande zote za Muungano. Wasioutaka kama Uamsho na Mimi binafsi (japo si mwanauamsho) pamoja na wengineo tufanye kampeni kuwashawishi watu waukatae na wale wanaoupenda sana wapewe nafasi ya kushawishi watu waseme wanautaka kisha tutekeleze matokeo bila kinyongo. Kama Muungano utashinda dhoruba hii ni wazi lazima tuulinde bila kujali chochote na kama kuna mtu atafanya chokochoko dhidi yake lazima tumbane kiasi cha kutosha.
Nilijaribu kuelezea mawazo yangu katika thread hii: Kikwete: Wape zanzibar wanachokitaka tuishi kwa amani!
Viongozi Dhaifu na Mafisadi + Wananchi wavivu, walalamishi na wasiojua haki zao + Imani Iliyopotoshwa = Umasikini wetu.
Follow Us Here