Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

    Report Post
    Page 3 of 8 FirstFirst 12345 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 151
    1. #1
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 485
      Rep Power : 670
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Kufuatia tuhuma zilizo elekewa kwake juu ya matumizi shangingi la kambi ya upinzan mbowe alikua na haya yakusema:

      "Mimi nilikataa gari kwa kipindi cha miezi sita na nikawa natumia gari langu kwa shughuli zote za vikao vya bunge,lakini nataka umma uelewa kuwa kwa nafasi yangu natakiwa kulipwa posho ya madaraka sh 200000 kila mwezi,kupewa nyumba ya kuishi ikiwa samani zake.

      Ila mpaka sasa sina nyumba ya serekali,wala mlinzi,wala kulipwa fedha za mawasiliano,vyote natumia fedha zangu...kama ningetaka ningedai mambo mengi ambayo natakiwa kupata lakini kulingana na hali ya uchumi wa nchi ni lazima nitumie fedha zangu ili kunusuru uchumi" alisema.

      Source: Tanzania daima 22 june, 2012
      Oluoch, REMSA, mamajack and 1 others like this.

    2. Miaka 50

    3. #41
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 18,330
      Rep Power : 12591
      Likes Received
      5858
      Likes Given
      775

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Sasa zile kelele za Mbowe hakuna kulala, mpaka kieleweke, Pipozz power, wao wana pesa sie tuna Mungu...

      Siasa hizi usanii mtupu...

    4. #42
      Satanic_Verses's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th September 2011
      Posts : 37
      Rep Power : 397
      Likes Received
      3
      Likes Given
      22

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Katuhumiwa nini kwa maana halisi ya neno tuhuma!!

      Quote By Pinokyo Jujuman
      Hapo tuhuma haijajibiwa; badala yake ameibua malalamiko yake ingawa hajaiweka kimalalamiko zaidi; suala la kutofuatilia stahiki yako ya makazi,Samani na Mlinzi hilo laweza kuwa ni tatizo pia kwa namna mbili tofauti.

      Moja ana uhakika gani kama stahiki yake aloiacha inaingia kwenye kusaidia uchumi wa Taifa na hauliwi na walafi kwa maana upo ndani ya utaratibu!!
      Kwa uelewa wako mwajibikaji ni mtu asitefuatilia haki na wala mdhulumaji wa haki??!!

      Quote By Pinokyo Jujuman
      Pili kwa kutofuatilia haki yake haoni kwamba kuna haja pia ya kuja kututhibitishia kuwa hata House allowance nayo hapokei!!
      Kama wafanyakazi wa TANZANIA DAIMA hawalipwi mshahara basi ni ujinga wao hawamfikishi mahakamani mwajiri wao.

      Quote By mpinga shetani
      Maadam kaamua kujibu. Mbowe pia atueleze kwa nini waandishi wa gazeti lake la Tanzania Daima linalosimamiwa na mkewe hawalipwi mishahara.

      Na aseme kwa nini mkewe hivi karibuni aliwajibu wahariri wake kifedhuli kuwa "asiyetaka kazi bila malipo aache! "

    5. FJM
      #43
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,179
      Rep Power : 2569
      Likes Received
      5331
      Likes Given
      4587

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      CCM wanahangaika na Mbowe wakati leo wamejitwisha bomu? Hiyo bajeti italipuka muda si mrefu.

    6. #44
      georgeallen's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd June 2011
      Location : Seattle, WA, USA
      Posts : 2,055
      Rep Power : 0
      Likes Received
      516
      Likes Given
      260

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Mchagga akatae gari, "fesa"(200K), "numba", mlinzi? Labda mbowe siyo mchagga

    7. #45
      georgeallen's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd June 2011
      Location : Seattle, WA, USA
      Posts : 2,055
      Rep Power : 0
      Likes Received
      516
      Likes Given
      260

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Mchagga akatae gari, "pesa"(200K/mo), "numba", mlinzi? ......Labda mbowe siyo mchagga

    8. RukaaJuu Final

    9. #46
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 485
      Rep Power : 670
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default

      Quote By zomba
      Nilifikiri matatizo ya kuzuwa kwenye tarakimu za mahesabu ni tatizo la waziri wenu kivuli kumbe wote mnatatizo hilo?

      Hiyo hesabu yako (niliyokuwekea nyekundu hapo juu) ni uongo na uzushi. Weka hesabu za ukweli.
      mkuu nilijua kabisa watu kama wewe hawakosekani ndio maana nikaweka source hapo..kama unalo gazeti soma kwenye habari inayohusu baraza jipya kivuli mwisho wa hiyo habari ndio utakuta matamshi yake haya(hawakuiweka kama habari kamili)..au tembelea website yao

    10. #47
      Kabembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2009
      Location : ITETE-Kandwesi
      Posts : 878
      Rep Power : 703
      Likes Received
      170
      Likes Given
      170

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Wanasiasa wanaifirisi nchi kwa mbwembwe zao.

    11. #48
      Mr Emmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Posts : 631
      Rep Power : 594
      Likes Received
      74
      Likes Given
      16

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      aibu yao

    12. #49
      Shardcole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th January 2012
      Posts : 4,402
      Rep Power : 1286
      Likes Received
      1032
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By kimboka one
      Mwizi ni mwizi tu,hawa wanasiasa si watu.
      una maana gan? Kwan siasa inafanywa na vyura?
      Be a guy.

    13. #50
      Tumaini Makene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2012
      Posts : 1,064
      Rep Power : 8908
      Likes Received
      2235
      Likes Given
      768

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Quote By Godwinnko
      Kufuatia tuhuma zilizo elekewa kwake juu ya matumizi shangingi la kambi ya upinzan mbowe alikua na haya yakusema:

      "Mimi nilikataa gari kwa kipindi cha miezi sita na nikawa natumia gari langu kwa shughuli zote za vikao vya bunge,lakini nataka umma uelewa kuwa kwa nafasi yangu natakiwa kulipwa posho ya madaraka sh 200000 kila mwezi,kupewa nyumba ya kuishi ikiwa samani zake.

      Ila mpaka sasa sina nyumba ya serekali,wala mlinzi,wala kulipwa fedha za mawasiliano,vyote natumia fedha zangu...kama ningetaka ningedai mambo mengi ambayo natakiwa kupata lakini kulingana na hali ya uchumi wa nchi ni lazima nitumie fedha zangu ili kunusuru uchumi" alisema.

      Source: Tanzania daima 22 june, 2012
      Akizungumzia tuhuma zilizotolewa na wabunge wa CCM, Mwigulu Nchemba (Iramba Magharibi) na Mbunge Livingstone Lusinde (Mtera), kuwa anawahadaa Watanzania kwa kukataa gari kuu kuu la Kiongozi wa Upinzani Bungeni (KUB), lakini akageuka kwa mlango wa nyuma na kuchukua jipya, Mbowe alisema kauli hizo ni za kisiasa.

      Mbowe alisema ni kweli kuwa hivi sasa analitumia gari la KUB ambalo alilikataa kwa kipindi cha miezi sita bila kulitumia, lakini Serikali imekataa kubadili sera yake za kuacha kununua magari ya kifahari.

      “Mimi nilikataa kwa miezi sita, nilikuwa silipwi gharama zozote za mafuta ikiwamo hata hii ya kila siku ya wabunge na gharama ya mafuta ya kutoka jimboni na kwenda jimboni, na nia yangu ilikuwa ni kuionyesha Serikali kuwa tunaweza kukataa haya matumuzi mabaya lakini, wamegoma,” alisema Mbowe.

      Alisema kimsingi, asingeweza kugoma milele kwani lengo lake lilikuwa ni kutoa msukumo ambao ungewezesha magari yote ya kifahari yapigwe mnada.

      “Hawa jamaa hawataki kubadilika, nimeona suluhu hapa sio tu kukataa gari lao bali ni kuungana na wadau wengine kuwang’oa madarakani kwa sababu hata katika bunge la mwaka huu, hawajasema kama kuna sera rasmi ya kupunguza matumizi kwa kununua magari ya kifahari,” alisema Mbowe.

      Kuhusu kugomea posho ya Sh80,000 ya bunge na kuchukua posho ya Sh 2 milioni kwa mwezi kama KUB, alisema suala hilo anayepaswa kuulizwa ni Katibu wa Bunge, lakini mtu anapokuwa kiongozi wa upinzani bungeni ana stahili zake ambazo zimepangwa.

      “Unapokuwa kiongozi wa upinzani kuna stahili nyingi wanapanga sasa zipo kisheria hata kama ukikaa hapa kuna mambo ya kisheria na kiutaratibu, lakini kama nilivyosema awali kikubwa hapa ni kuiondoa Serikali tu, ili kufuta mambo haya,” alisema Mbowe.

      Mwenyekiti huyo, pia alikanusha tuhuma zilizotolewa na Nchemba kuwa anasomesha mtoto wake chekechea katika shule ya kimataifa kwa dola 15,000 (karibu Sh20 milioni) kwa maelezo kuwa hana mtoto anayesoma chekechea, watoto wake wote ni wakubwa.

      Source; Mwananchi Juni 21, 2012.

      "Nothing in the world is more dangerous than sincere ignorance and conscientious stupidity." Martin Luther King

    14. #51
      Mr Emmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Posts : 631
      Rep Power : 594
      Likes Received
      74
      Likes Given
      16

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      chadema mnanini jamani kila kukicha kashfa mara heche katukana na kudhulum haki ya makamanda, mara lema na kikapu cha...,.., mara mboye na v8/posho, mara slaa na mshahara wa ubunge, mara shibuda, mara mnyika na mituc, mara nasari na uhuru wa kaskazini, mara komu na ufisadi wa epa, nawapenda sana kama wapinzani wetu hebu tatueni hizi kashfa kwanza then ndo mjikite kisawasawa kupambana na sisi

    15. #52
      Mohamedi Mtoi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th December 2010
      Location : Lushoto - Kwemakame.
      Posts : 2,086
      Rep Power : 24556
      Likes Received
      3166
      Likes Given
      358

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Kama ameamua kulirudia na kulichukua gari baada ya kuona kuwa anaweza kulitumia kueneza elimu ya uraia itakayo wakomboa watanzania walioko gizani na hivyo kuwa mtaji kwa 2015 kwangu sioni kuwa ni kitu kibaya maana ni jambo jema hasa ukizingatia kuwa ni moja ya stahili zake kama kub. Mimi nitafurahi kusikia kuwa hata posho wanachukua ili zisaidie kukijenga chama pamoja na michango inayo changwa kwenye m4c kwa ajil ujenzi wa ofisi za chama na matawi nchi nzima kuliko kuwaachia hawa manyang'au waliouza madini yetu kwa bei poa ya mikataba feki, bila aibu wakatuuza na sisi wenyewe kwa kutuweka rehani kwa mamikopo tutakayo lipa mpaka tufe na sasa wamegeukia kuuza na kutorosha mpaka wanyama nje ya nchi.
      Kamanda kanyaga twende usipote muda na watu wanaofikiria kwa jina la mayor wao wa Darisalamu.
      Naipenda chadema, naichukia nyinyiemu.
      Last edited by Mohamedi Mtoi; 22nd June 2012 at 22:20.

    16. #53
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,136
      Rep Power : 14291
      Likes Received
      4019
      Likes Given
      3281

      Default

      Quote By mpinga shetani
      Maadam kaamua kujibu. Mbowe pia atueleze kwa nini waandishi wa gazeti lake la Tanzania Daima linalosimamiwa na mkewe hawalipwi mishahara.
      Na aseme kwa nini mkewe hivi karibuni aliwajibu wahariri wake kifedhuli kuwa "asiyetaka kazi bila malipo aache! "
      si mgeacha kweli au vielimu vya kungaunga..kama hulipwi mshahara unaendeshaje maisha yako au bahasha....

    17. #54
      Mr Emmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Posts : 631
      Rep Power : 594
      Likes Received
      74
      Likes Given
      16

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      hivi ile kashfa ya tecknohama inayomhusu
      mama junior imeshapelekwa kisutu

    18. #55
      Chenge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Posts : 485
      Rep Power : 483
      Likes Received
      183
      Likes Given
      47

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Mbowe apunguza Baraza Kivuli la Mawaziri


      na Danson Kaijage, Dodoma

      KIONGOZI wa Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amelipangua Baraza lake Kivuli la Mawaziri kwa kuunda wizara mpya zinazopunguza ukubwa wa lile la awali.
      Mabadiliko hayo pia yamewaacha nje mawaziri kadhaa na kujaza nafasi zilizoachwa wazi na aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, aliyeenguliwa na Mahakama Kuu na marehemu Regia Mtema wa Viti Maalumu.
      Hata hivyo, Mbowe hakuwaingiza wabunge wa vyama vingine vinavyounda kambi hiyo vya NCCR-Mageuzi, CUF, TLP na UDP kwa maelezo kuwa bado wanaendelea na mazungumzo yenye kuwafanya waaminiane zaidi.
      Wanaounda baraza hilo ni yeye mwenyewe ambaye atakuwa na Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, akisaidiwa na David Silinde, Said Arf anakwenda Miundombinu akisaidiwa na Pauline Gekul, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais atakuwa Profesa Kulikoyela Kahigi, Fedha, Uchumi na Mipango ni Zitto Kabwe akisaidiwa na Christina Mughwai.
      Katiba, Sheria na Muungano itaongozwa na Tundu Lissu, Maliasili, Utalii na Mazingira ni Mchungaji Peter Msigwa, Mambo ya ndani ya Nchi, Vincent Nyerere, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ezekiah Wenje atakayesaidiana na Raya Ibrahim Khamisi.
      Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ni Mchungaji Israel Natse, Maji Mifugo na Uvuvi, Sylvester Kasulumbayi ambaye atasaidiwa na Sabreena Sungura wakati Kazi, Habari, Utamaduni na Michezo ikiongozwa na Joseph Mbilinyi akisaidiwa na Cecilia Pareso.
      Nishati na Madini anaendelea kubaki John Mnyika, Viwanda na Biashara, Highness Kiwia na Afya, Jinsia na Jamii ni Dk. Gervas Mbassa, akisaidiana na Conchester Rwamlaza, Elimu, Sayansi na Teknolojia, Suzan Lyimo atasaidiwa na Joshua Nassari.
      Wizara ya Kilimo na Ushirika itaongozwa na Rose Kamili wakati Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inabakia kwa Halima Mdee.
      Pia, Mbowe alifafanua sababu za kuendelea kutumia gari la serikali ambalo alikuwa amelikataa, akisema kuwa amelazimika kufanya hivyo kutokana na maelekezo ya serikali iliyopo madarakani.
      Alisema kuwa alikuwa amelikataa ili kuishinikiza serikali kupunguza matumizi ya magari na kutaka apewe gari dogo lakini kutokana na kutosikilizwa alilazimika kuendelea kulitumia.
      “Mimi nilikataa gari kwa kipindi cha miezi sita na nikawa natumia langu kwa shughuli zote za vikao vya Bunge, lakini nataka umma uelewe kuwa kwa nafasi yangu natakiwa kulipwa posho ya madaraka sh 200,000 kila mwezi, kupewa nyumba ya kuishi ikiwa na samani zake.
      Ila mpaka sasa sina nyumba ya serikali wala mlinzi, kulipwa fedha za mawasiliano, vyote natumia fedha zangu….kama ningetaka ningedai mambo mengi ambayo natakiwa kupata lakini kulingana na hali ya uchumi wa nchi ni lazima nitumie fedha zangu ili kunusuru uchumi,” alisema.


      Source: Tanzania Daima Ijumaa, 22 juni 2012
      Last edited by Chenge; 22nd June 2012 at 22:34.

    19. #56
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 485
      Rep Power : 670
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default

      [QUOTE=Tumaini Makene;4103715][SIZE=4]Akizungumzia tuhuma zilizotolewa na wabunge wa CCM, Mwigulu Nchemba (Iramba Magharibi) na Mbunge Livingstone Lusinde (Mtera), kuwa anawahadaa Watanzania kwa kukataa gari kuu kuu la Kiongozi wa Upinzani Bungeni (KUB), lakini akageuka kwa mlango wa nyuma na kuchukua jipya, Mbowe alisema kauli hizo ni za kisiasa.

      Mbowe alisema ni kweli kuwa hivi sasa analitumia gari la KUB ambalo alilikataa kwa kipindi cha miezi sita bila kulitumia, lakini Serikali imekataa kuba
      magamba mna lingine.??

    20. #57
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 485
      Rep Power : 670
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default

      Quote By Chenge
      hiyo habari iko ukarasa wa ngapi mbona sijaiona kwenye hilo gazeti lililotajwa?
      mkuu mimi nimeisomaa kwenye website yao kwahiyo sijui kurasa..ila nenda kwenye habari inayohusu baraza jipya kivuli,mwisho wa hiyo habari ndio utakuta taarifa hii(waandishi hawakuiweka kama habari kamili,ilionganishwa na habari ya baraza jipya)

    21. #58
      watu8's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th February 2010
      Location : Juu ya Tukutuku
      Posts : 15,285
      Rep Power : 31331
      Likes Received
      7559
      Likes Given
      7615

      Default

      Quote By MESTOD
      Jibu bado halijaonekana hapo sababu ya kulirudia. Ni kwa sababu hajapewa nyumba na samani zake? Ni kwa sababu hjataka hela ya mawasiliano? Ni kwa sababu anatumia ulinzi binafsi?
      Nafikiri hapa mwenyekiti wetu ukiri kuwa ni ajali ya kisiasa. Ulirudisha mbele ya waandishi wa habari, ilibidi ulirudie hivo hivo.
      mkuu unaelewa kiswahili kweli au taarifa umeisoma juu juu tu?...mbona kila kitu kimeainishwa

    22. #59
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,136
      Rep Power : 14291
      Likes Received
      4019
      Likes Given
      3281

      Default

      Quote By Mr emmy
      hivi ile kashfa ya tecknohama inayomhusu
      mama junior imeshapelekwa kisutu
      nape unahangaika sana..

    23. #60
      Barnabas Shadrack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Posts : 2,056
      Rep Power : 810
      Likes Received
      182
      Likes Given
      11

      Default Re: Mbowe ajibu tuhuma dhidi yake juu ya matumizi ya gari la KUB.

      Chezea mchaga weye tena akiwa kachanganya uchaga wake katika siasa, watanzania jiandaeni kuumia zaidi endapo huyu mchaga na kampuni lake(Chadema) watapata sehemu ya kula kivulini(serikalini) baada ya kusota juani(upinzani).
      The unseen is illustrated by the seen.

    Page 3 of 8 FirstFirst 12345 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...