Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 26
    1. #1
      mwinukai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2011
      Posts : 656
      Rep Power : 538
      Likes Received
      134
      Likes Given
      51

      Default Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Waandishi Wetu, Dodoma| Mwananchi | 19, Juni 2012

      WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Esther Bulaya, juzi walizozana katika kile kinachoonekana kuwa ni kuwania madaraka katika Jimbo la Bunda mkoani Mara, katika uchaguzi mkuu 2015.

      Sakata hilo lilitokea nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao juzi usiku, ambapo Wassira alimfuata Bulaya na kumhoji kwamba kwanini alitoa maneno ya kuipinga bajeti ya Serikali.

      Wassira ambaye pia ni Mbunge wa Bunda (CCM) alimwambia Bulaya: “Mimi ndiye Mbunge wa Bunda, wewe huwezi kujifanya ndiye uliyetumwa na wananchi kuja kusema maneno ya uwongo hapa, eti unaipinga bajeti ya Serikali, ni nani aliyekutuma?”

      Waziri huyo alikwenda mbali na kumwambia mbunge huyo kijana kwamba, “wewe tunakufahamu una pande mbili (upinzani na CCM) na kila siku unashirikiana na Halima Mdee (Kawe-Chadema), tunakujua kwamba uko CCM na Chadema.”

      Kutokana na kauli hizo, Bulaya alijibu mapigo akimwambia Wassira kwamba yeye akiwa mbunge wa CCM ana wajibu wa kukikosoa chama chake na hakuwa mtu wa kwanza kukataa kuunga mkono bajeti hadi hapo marekebisho yatakapokuwa yamefanywa.

      “Mimi nina haki ya kuzungumza ndani ya Bunge na kusema kile ninachokiamini kama mbunge, wala hakuna mtu wa kuniwekea mipaka. Halafu kama ni uhusiano na wabunge wengine mbona wabunge wengi tu wa CCM wanashirikiana na upinzani?” alihoji Bulaya.

      Wakati hayo yakiendelea Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na mbunge mwingine wa Viti Maalum (CCM), Rosemary Kirigini walikuwa wakishuhudia.

      Nahodha alitumia dakika chache kumsihi Bulaya kutojibu mashambulizi ya Wassira.

      Msingi wa mvutano

      Msingi wa mvutano huo ni mchango wa Bulaya alipochangia hotuba ya bajeti ya Serikali na kuhoji sababu ya kutotengwa kwa fedha za kuwalipa fidia wananchi wa Bunda waliohama katika maeneo yao kupisha utekelezaji wa mradi wa maeneo maalum ya uwekezaji (EPZ).

      “Nitahitaji majibu sahihi katika hili, kwani wananchi wa Bunda wamenituma na bila majibu sina haja ya kuunga mkono hoja,” alisema Bulaya.

      Mbali na suala hilo, mbunge huyo pia aliiponda bajeti ya Serikali kwamba haina jipya kutokana na kushindwa kuandaliwa kwa vipaumbele, ambavyo vitasaidia maendeleo ya Watanzania, badala yake bajeti hiyo, bado imetenga fedha nyingi kwa matumizi ya kawaida, imeendeleza misamaha ya kodi na kukuwa kwa deni la Taifa.

      Akichangia hotuba ya bajeti ya Serikali, Bulaya alisema bado hajaridhishwa na serikali kutenga fedha nyingi katika matumizi ya kawaida na kwenda kinyume na mpango wa serikali wa miaka mitano ambao ulieleza wazi fedha za maendeleo zitaongezeka walau kwa asilimia 35 kila mwaka.

      Mbunge huyo alisema ni lazima Serikali iwe na vipaumbele vichache ili iweze kutekeleza kwa fedha za ndani, kuliko kuwa na vipambele vingi ambavyo haviwezi kutekelezeka.

      Bulaya alisema pia inahitajika mchanganuo wa deni la Taifa kwani bado linaongezeka mwaka hadi mwaka na sasa limefikia trilioni 20.

      Alisema pia inashangaza wakati fedha za maendeleo zinapunguzwa matumizi mengineyo katika wizara yameongezeka hadi kufikia 583 fedha ambazo ni nyingi sana.

      “Haiwezekani zikatengwa Sh583 bilioni kwa ajili ya kula katika wizara, wakati miundombinu muhimu kama Reli ya Kati inahitaji zaidi ya Sh1.3 trilioni kuboreshwa na wizara nzima imepangiwa trilioni 3.8,” alisema Bulaya na kuongeza:

      “Nina mhurumia sana Waziri wa Uchukuzi, Dk Mwakyembe (Harrison) kwani hawezi kutekeleza mipango yake kwa bajeti hii,” alisema.

      Mgogoro wahamia bungeni

      Katika kile kinachoonekaka kwamba ni mvutano wa kisiasa baina ya Wassira na Bulaya, suala lao liliibuka kwa sura nyingine katika kipindi cha maswali na majibu jana asubuhi.

      Bulaya aliuliza swali kuhusu wananchi 164 katika Wilaya ya Bunda waliosubiri kulipwa fidia kwa ajili ya kupisha utekelezaji wa mradi wa maeneo maalum ya uwekeza (EPZ).

      Katika majibu yake, Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Gregory Teu alisema wananchi hao watalipwa fedha zao mwezi ujao.

      Akijibu swali la nyongeza la Bulaya, Teu alisema, “napenda kumpongeza Mbunge wa Bunda, Mheshimiwa Wassira kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia suala hili, kwa kweli amekuwa akifuatilia sana ili kuhakikisha kwamba wananchi hawa wanalipwa.”

      Kauli yake hiyo ilizua miguno na minong’ono ya chinichini kwa baadhi ya wabunge, wakiashiria kile kinachoonekana ni vita baina ya Wassira na Bulaya.

      Kuhusu mchakato wa malipo hayo, Teu alisema malipo ya fidia yalilipwa kwa awamu mbili kupitia akaunti ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ambapo mwaka 2009 jumla ya Sh1 bilioni zililipwa kama awamu ya kwanza kwa hundi kutoka EPZ.

      “Awamu ya pili ya malipo ya Sh100 milioni ililipwa mwaka 2010 kwa hundi namba
      6064316 kutoka EPZ, hadi sasa katika awamu hizo mbili, jumla ya watu 116 wameshalipwa,’’ alisema Teu.

      Naibu Waziri alisema fedha zilizobaki, Sh 1,042,852,910, tayari zimetengwa na hazina na inatarajiwa kulipwa Julai 2012 kwa wahusika 164 waliobakia, ili kukamilisha idadi ya watu 280 waliostahili kulipwa.

      Alisema mwaka 2007, wizara kupitia Mamlaka ya EPZ na kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ilitenga eneo la hekta 2,316 katika kijiji cha Tairo Bunda ikijumuisha vitongoji vitatu kwa ajili ya uwekezaji wa EPZ.

      Teu alibainisha kuwa katika mpango huo, jumla ya Sh3.4 bilioni zilihitajika ili kulipa wananchi wanaomiliki maeneo hayo, lakini kutokana na gharama kuwa kubwa EPZ kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara walikubaliana kupunguza na kubakiza kitongoji kimoja cha Kirumi.

      Hata hivyo, Naibu Waziri alisema kuwa malipo yatayotolewa katika kipidni cha sasa, yatakuwa katika bei ya soko la sasa, na kwamba serikali imekwisha wa kuangalia namna ya kufidia deni hilo.


      Habari hii imeandaliwa na Neville Meena, Mussa Juma na Habeli Chidawali

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Janjaweed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2010
      Posts : 3,599
      Rep Power : 1123
      Likes Received
      1378
      Likes Given
      1528

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      hivi wasirra hawezi kutatua chochote bila kugombana??
      Kama Vipi nipotezee tu; ntakuboa....

    4. #3
      MAKAH's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2010
      Posts : 954
      Rep Power : 628
      Likes Received
      116
      Likes Given
      674

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      wasira anataka kuwa mbunge hadi mauti!! waachie watoto - hawa wana full vigour!!

    5. #4
      Zamaulid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Location : PANDAGI CHIZA
      Posts : 3,642
      Rep Power : 1297
      Likes Received
      943
      Likes Given
      401

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      kazi tunayo watanzania!

    6. #5
      MAMMAMIA's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 25th February 2008
      Location : Near You
      Posts : 3,794
      Rep Power : 3256
      Likes Received
      1496
      Likes Given
      1206

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Quote By Janjaweed
      hivi wasirra hawezi kutatua chochote bila kugombana??
      Huyu si yule aliyepachikwa jina la Tyson kwa kumtwanga tu makonde? Sishangai.
      Hawa wananchi katika suala la malipo ya fidia huwa wanaibiwa tu. Nimefanya hesabu ya chap chap, shilingi bilioni 1.1 ukizigawa sawa sawa kwa hao watu 116 wanaodaiwa kulipwa, kila mmoja angepata kiasi cha milioni 9, je ni kweli wamelipwa zote?

      Ukitaka kuona madudu na mizengwe inayofanyika, inakuwaje watu 116 walipwe milioni na watu 164 waliobakia walipwe milioni 6 kila mmoja?
      "JF - SAUTI YA WASIO NA SAUTI ............ na wapayukaji"

    7. Miaka 50

    8. #6
      Van persie's Avatar
      Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 82
      Rep Power : 375
      Likes Received
      17
      Likes Given
      0

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Haya sasa, nchemba yuko wpi?. Mbunge toka ccm asema bajet ni mbovu, mzee wa first class anasemaje?. Au anasubir waseme chadema ndio puvu limtoke?.Au huyo mzee wa igunga hakuwepo wkt sister shupavu anachangia?. Sister wakikuzubaisha hao magamba njoo cdm, ungane na mdee.

    9. #7
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,514
      Rep Power : 1794
      Likes Received
      654
      Likes Given
      0

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Kwani Tyson bado anafikiri atarudi bungeni tena?nitashangaa sana sana sana muda wake wa kupumzika umefika 2015 wazee wote wote wapuzike la sivyo wataaibika anzia Makinda,Wassira,Komba,na wengine wanaojua wamekaa bila mafanikio

    10. #8
      Tusker Bariiiidi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd July 2007
      Location : Sinza Dar es Salaam.
      Posts : 3,230
      Rep Power : 1253
      Likes Received
      375
      Likes Given
      51

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      BEAUTY AND THE BEAST! Peabo Bryson na Celine.

    11. #9
      Anheuser's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd March 2011
      Posts : 1,295
      Rep Power : 672
      Likes Received
      335
      Likes Given
      135

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Quote By MAKAH
      wasira anataka kuwa mbunge hadi mauti!! waachie watoto - hawa wana full vigour!!
      kama hao watoto wana hiyo "full vigour" basi wamng'oe ubunge kwa kutumia hiyo "full vigour" badala ya kuomba Wassira "awaachie watoto." Si unasema wana "full vigour"? hahahaha...

    12. #10
      TIQO's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 4,565
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1030
      Likes Given
      131

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Wassira 2015 harudi mjengoni aanze kuaga

    13. #11
      andishile's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 601
      Rep Power : 480
      Likes Received
      144
      Likes Given
      291

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      namkubali sana bulaya,ni mkweli na muwazi!chachu kama hizi ni muhimu sana !keep it up!

    14. #12
      Masabaja's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th March 2012
      Posts : 139
      Rep Power : 391
      Likes Received
      18
      Likes Given
      13

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Yote magamba hakuna la kuchukua jimbo la Bunda 2015

    15. #13
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,158
      Rep Power : 24268
      Likes Received
      4669
      Likes Given
      2294

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Quote By Janjaweed
      hivi wasirra hawezi kutatua chochote bila kugombana??
      Bunda hawataki kumsikia huyu Mheshimiwa wa Gombe!
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    16. #14
      chitambikwa's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Location : KAISHO
      Posts : 3,163
      Rep Power : 1958
      Likes Received
      573
      Likes Given
      424

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Wassira amezeeeka vibaya sana hajui aendako wala kazi yake
      IT IS TO THOSE WITHOUT TEETH GOD GIVES MEAT

    17. #15
      Msongoru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2008
      Location : Japan
      Posts : 305
      Rep Power : 627
      Likes Received
      14
      Likes Given
      37

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Nimempenda Bulaya!!
      A blind person asked me one day: "Can there be anything worse than losing eye sight?" I replied: "Yes, losing your vision."

    18. #16
      MgungaMiba's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 28th August 2011
      Posts : 318
      Rep Power : 565
      Likes Received
      262
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By Tusker Bariiiidi
      BEAUTY AND THE BEAST! Peabo Bryson na Celine.
      Nataka kuzimia kwa kucheka!!! Hakuna anaeweza kutuwekea picha zao ili tupate Taswira linganishi halisi?

    19. #17
      fikirikwanza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Posts : 642
      Rep Power : 497
      Likes Received
      149
      Likes Given
      17

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Nae huyu bulaya, kama ni mpiganaji si aje CDM tu, aache kuonekana ana sura mbili, kweli ni vibaya kwa mtu yeyote kuwa na sura mbili. Wassira is right at least on logical grounds, wabovu wako CCM, wazuri wako CDM. Bulaya acha kuwa na sura mbili itaku-cost mpaka hutakuwepo kushuhudia cost hiyo, take my words.

    20. #18
      MAKAH's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2010
      Posts : 954
      Rep Power : 628
      Likes Received
      116
      Likes Given
      674

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Quote By Anheuser
      kama hao watoto wana hiyo "full vigour" basi wamng'oe ubunge kwa kutumia hiyo "full vigour" badala ya kuomba Wassira "awaachie watoto." Si unasema wana "full vigour"? hahahaha...
      ubabe hautamsaidia

    21. #19
      Las Mas Bobos's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th June 2012
      Posts : 894
      Rep Power : 527
      Likes Received
      294
      Likes Given
      84

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Quote By Anheuser
      kama hao watoto wana hiyo "full vigour" basi wamng'oe ubunge kwa kutumia hiyo "full vigour" badala ya kuomba Wassira "awaachie watoto." Si unasema wana "full vigour"? hahahaha...
      Soon, stay tuned. Kwani unachokiona kinamfanya atoke povu na kutaka kuwakunja ni nini, anajua kinachofuata.

      Mwaka 2015, Ester Bulaya atakuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Bunda kupitia CDM. Mwisho wa Wassira na Hasira zake na mapovu
      By the time a man comes to realize that his father was right, he usually has a son who think he is wrong.

    22. #20
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,739
      Rep Power : 1917
      Likes Received
      1177
      Likes Given
      962

      Default Re: Wassira, Bulaya wazozana bungeni!

      Bulaya na Mdee kulikoni?

      Inasadikika kuwa Bulaya ameolewa na Chadema.
      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...