Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

    Report Post
    Page 5 of 20 FirstFirst ... 3456715 ... LastLast
    Results 81 to 100 of 399
    1. #1
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Mbunge kijana ambae anaonesha kuwa umaarufu na madaraka ya ubunge yamemlevya amefikia hatua ya kumuingia Kikwete binafsi kwa kumwita, kwa kejeli na dharau eti ni "dhaifu".

      Kwa muono wangu, Mnyika amepotoka na amekosa heshima na adabu kwa sio tu mtu aliyemzidi umri, bali kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa Watanzania wote ambao tumeridhika kwa kumchagua Kikwete kwa kumpigia kura atuongoze.

      Mnyika baada ya kushindwa kuwasilisha hoja kuhusu bajeti akaamuwa kwa makusudi kabisa, kutoa lugha inayokera, si tu kwa Rais, bali kwa bunge pia, kuwa wote ni "wazembe" na CCM yote ni "upuuzi".

      Kweli kabisa, mimi ni mwana CCM na umenitukana, kwa hilo, umetangaza vita binafsi na mimi na wana CCM wote, hali kadhalika na Wabunge wote kwa kuwaita "wazembe". Jee, kijana hicho kiburi cha kututukana wote pamoja na Rais wetu mpendwa kwa ajili ya huo Ubunge? au kuna kinachokufanya ujione kuwa uko juu ya sheria, kwa kuwa upo hapo na watunga sheria wengine?

      Nakuhakikishia, vita uliyoitangaza itakugharimu kupita uwezo wa kufikiri, na majuto ni mjukuu.

      Kikwete humuwezi.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    2. Miaka 50

    3. #81
      nkyalomkonza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2012
      Posts : 668
      Rep Power : 581
      Likes Received
      242
      Likes Given
      75

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Quote By Safari_ni_Safari
      Wewe neno UDHAIFU linakukera nini kwani? Mtu anayepata PASS darasani utesema ni STRONG au WEAK? Hivi unaijua SWOT analysis? Ushawahi kuwa katika interview ya kazi na ukaulizwa weakness zako ni zipi? WEAKNESS ndio UDHAIFU kama hujui! Na ni neno la kawaida sana........Hata Museveni ni dhaifu kwa kudhani familia yake tu ndio ina uwezo wa kutawala. Kila binadamu (akiwemo Mnyika) ANA UDHAIFU WAKE.......sasa labda Kikwete ni jini na si binadamu basi atakuwa hana udhaifu!
      Hatokuelewa unaonge na Huyu ZOMBA ambaye shule imempitia pembeni. We angalia hata kauli zake. Usipoteze muda.

    4. #82
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,389
      Rep Power : 1265
      Likes Received
      1208
      Likes Given
      1253

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      SISIEM mshazoea kupigiwa makofi kwenye kila kitu ndio maana mnapenda kusifiwa hata kama ni wadhaifu..KIMSINGI KIKWETE NI MDHAIFU TENA SANA TUU

    5. #83
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,480
      Rep Power : 19785
      Likes Received
      4300
      Likes Given
      1248

      Default

      Quote By Ngoromiko
      Mnyika ameharibia watoto wetu wanaofuatilia kwa makini Bunge kwa lengo la kujifunza jinsi wawakilishi wetu wanavyoongea na kuijadili bajeti.

      Pamoja na kufurahia bunge, watoto pia wanajifunza jinsi watakavyoongea wakikua iwapo wataamua kuingia kwenye siasa.

      Walichojifunza kwa huyu mpuuzi Mnyika ni jinsi ya kuwatukana baba zao hadharani.

      Aibu sana, nimewapiga marufuku wanangu kuangalia kipindi cha Bunge ....until further notice.
      sasa watoto wako kupitia mnyika wamejua jk ni dhaifu kwani wewe hukuweza kumwambia kwa hiyo acha wenye ujasiri wakufundisha wanao yanayo endelea nchini wawambie.

      Usipowafundisha wanao, jirani zako watawafundisha.

    6. #84
      Chakaza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2007
      Location : everywhere
      Posts : 3,549
      Rep Power : 1475
      Likes Received
      884
      Likes Given
      522

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Quote By papason
      Kweli leo umedhihirisha u zoba wako!
      Mbona hilo alishadhihirisha siku nyingi sana? mkuu wewe umeliona leo? mbona haya madogo!

      Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi

    7. #85
      Gulwa's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th June 2008
      Posts : 138
      Rep Power : 585
      Likes Received
      46
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By mkomatembo
      Nadhani imefika wakati sasa Rais inabidi aoneshe udikteta kama wa Mkapa , enzi zile midono ya watu kama hawa ilifyata kama mikia ! Rais tunaomba uwashikishe adabu watu kama hawa ambao hawana nidhamu kabisa, hata iweje huwezi kuwa na kiburi na dharau kiasi hicho kwa kiongozi wako wa nchi! Rais tunaomba huyu aadabishwe ! na iwe fundisho kwa wengine !
      Enzi hizo zimeshapita, huwezi kuzirudisha, nyoka lazima aitwe nyoka si vinginevyo

    8. FemaTV & Radio

    9. #86
      kibol's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2012
      Location : dar es salaam
      Posts : 1,154
      Rep Power : 587
      Likes Received
      290
      Likes Given
      181

      Default

      Quote By zomba
      Mbunge kijana ambae anaonesha kuwa umaarufu na madaraka ya ubunge yamemlevya amefikia hatua ya kumuingia Kikwete binafsi kwa kumwita, kwa kejeli na dharau eti ni "dhaifu".

      Kwa muono wangu, Mnyika amepotoka na amekosa heshima na adabu kwa sio tu mtu aliyemzidi umri, bali kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa Watanzania wote ambao tumeridhika kwa kumchagua Kikwete kwa kumpigia kura atuongoze.

      Mnyika baada ya kushindwa kuwasilisha hoja kuhusu bajeti akaamuwa kwa makusudi kabisa, kutoa lugha inayokera, si tu kwa Rais, bali kwa bunge pia, kuwa wote ni "wazembe" na CCM yote ni "upuuzi".

      Kweli kabisa, mimi ni mwana CCM na umenitukana, kwa hilo, umetangaza vita binafsi na mimi na wana CCM wote, hali kadhalika na Wabunge wote kwa kuwaita "wazembe". Jee, kijana hicho kiburi cha kututukana wote pamoja na Rais wetu mpendwa kwa ajili ya huo Ubunge? au kuna kinachokufanya ujione kuwa uko juu ya sheria, kwa kuwa upo hapo na watunga sheria wengine?

      Nakuhakikishia, vita uliyoitangaza itakugharimu kupita uwezo wa kufikiri, na majuto ni mjukuu.

      Kikwete humuwezi.
      Alichokosea Mnyika ni kusema mfalme yu uchi hadharani wakati watu wazima wanaona mfalme kavaa vazi lisiloonekana,lakini in reality huo ndio ukweli,km ccm mmeshindwa kumuambia acheni wenye uwezo wa kufanya hivyo wafanye.bravo kijana cuz umefungua uwanja mpya wa kuelezana ukweli pale inapobidi.
      toghocho likes this.

    10. #87
      hacena's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 383
      Rep Power : 513
      Likes Received
      92
      Likes Given
      11

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      du ukija kwa uzinzi nyinyimu hapo si mmeoza mbona dhaifu aliwahi kumfungulia demu aliyezaa nae dodoma grosary, mwigulu oh mzee wa miongozo

    11. #88
      Kimweli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th October 2011
      Posts : 378
      Rep Power : 461
      Likes Received
      65
      Likes Given
      12

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Watu Kama wewe ni wakupeleka Cameroon mkavunishwe Chai na Migambo wakiwasimamia kwa nyuma.

      Soma hapa basi
      MNYIKA ANGEKUWA DHAIFU ZAIDI KAMA ANGEFUTA KAULI YAKE BUNGENI.

      1. Kama udhaifu ni kuto kujua kwa nini wananchi wako ni maskini
      wakati wako nchi tajiri. Mnyika yuko sahihi.

      2. Kama huwezi kumuwajibisha au kuona madudu ya katibu mkuu au katibu
      kiongozi mpaka bunge lishikilie bango na kushinikiza wang'oke ndio
      uzinduke kufanya maamuzi basi mnyika yuko sahihi.

      3. Kama kweli watu wamelibia taifa kupitia dili za magumashi halafu
      una watangazia warejeshe fedha ili wasichukuliwe hatua na wakati
      huohuo vibaka wanauwawa au kuchomwa moto kwa kuiba kuku na simu basi
      ni dhahiri kuna udhaifu wa kiungozi. Mnyika yuko sahihi.

      4. Kama ndege inaingia kwenye anga ya nchi yako na kubeba wanyama
      kupeleka Arabuni bila hatua zozote kuchukuliwa ni dhahiri kuna udhaifu
      wa kimfumo ulio kubuhu serikalini. Mnyika yuko sahihi.

      5. Kama rais anafunga safari kwenda kuomba misaada na wakati huohuo
      misaada anayopewa hailingani thamani na raslimali zinazo vunwa kwenye
      nchi yake basi Mnyika yuko sahihi.

      6. Kama rais anadiriki kutoa ahadi 99 ambazo thamani yake ni zaidi ya
      trilion 9 huku akijua kuwa hazitekelezeki ni hadaa kwa wananchi, chama
      na serikali. Mnyika yuko sahihi.

      7. Kama taasisi ya Ikulu na mfumo wake wa utawala umehusika kuingilia
      maamuzi ya mhimili wa haki kwa kutoa hukumu ya upendeleo ili kumkomoa
      au kumnyang'anya mbunge wadhifa kama jinsi ilivyo lalamikiwa. Mnyika
      yuko sahihi.

      8. Kama serikali inatenga 70% kwa matumizi kwenye bajeti yake na 30%
      kwenye maendeleo. Ni dhahiri kuwa ni aina ya serikali dhaifu yenye
      viongozi wavivu wa kufikiri.

      Kama hivyo ndivyo, nasimama na kijana mwenzangu kwa ukakamavu na
      kupaza sauti yenye mwale mkali. Namuunga mkono Mnyika.
      kindafu and Gracious like this.

    12. #89
      mkomatembo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2011
      Location : Bweleo
      Posts : 1,019
      Rep Power : 637
      Likes Received
      228
      Likes Given
      1269

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Quote By Chakaza
      Awaue kama kina Kombe?au wafungwe kama wale wanamuziki? Ulimwengu huu ni mwingine, usimponze amfuate Taylor bure wakati wewe utakuwa unakula maisha kwa mafanikio yatakayo letwa na Chadema baada ya 2015
      Babu yenu Nyerere alokuwa akiua waziwazi kina marehemu Hanga mbona hakuwahi kuuliwa? na matokeo yake amekuja kuuliwa na ambao aliwaamini sana tunavosikia kutoka kwa kina vicent nyerere! kwani adabu ni kuua tu ! kwalipi kubwa mpaka auliwe mnyika? afungwe tu kumshikisha adabu kwa kumdhalilisha kiongozi wa nchi!
      zomba likes this.
      "If the Virgin Mary appears wearing a Veil on all her pictures, how can you ask me to sign on a HIJAB BAN law ?" -Roberto Maroni, Italian Minister.

    13. #90
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,480
      Rep Power : 19785
      Likes Received
      4300
      Likes Given
      1248

      Default

      Quote By Crucial Man
      na mimi pia nasema ni dhaifu.
      namimi na sema jk ni dhaifu.

    14. #91
      SUWI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2010
      Posts : 491
      Rep Power : 537
      Likes Received
      21
      Likes Given
      65

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Na mimi pia nasema RAISI KIKWETE NI DHAIFU TENA SANA!!! haya nasubiri hiyo vita.. kawatishie mafisadi wenzio wewe..

    15. #92
      Mkosoaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th August 2009
      Posts : 331
      Rep Power : 562
      Likes Received
      28
      Likes Given
      43

      Default

      Quote By zomba
      Wewe anza kwa kuonesha ni lipi la maendeleo alilofanya Rais yeyote wa kabla yake, ambalo yeye hajafanya zaidi.

      Mnaleta matusi na ktukana lakini hoja za wazi kabisa zinawashinda. Mnyika kashindwa hoja ya bajeti akaamuwa awatukane wabunge wote, wana CCM wote na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Namwambia hvi; Kikwete asimjaribu, hamuwezi hata kidogo.
      Rais ni binadamu kama wengine, so anaweza kuwa strong au dhaifu. Na kwa mujibu wa katiba yetu ya sasa, ana uwezo wa kukosolewa vilevile.

      Kikwete kakosolewa hajatukanwa.

    16. #93
      muislamsafi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Posts : 73
      Rep Power : 384
      Likes Received
      20
      Likes Given
      4

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      I am very sorry kwa watu wanaoumia kwa kikwete kuitwa legelege mi nafikiri pia nchi hii imemshinda hajui chakufanya na sasa ana iongoza kwa maelekezo toka kwa wapuuzi fulani fulani. kwa sababu kama huwezi kutoa maamuzi kwenye matatizo nyeti na makubwa ndani ya nchi yako, badala yake unaenda kutalii nje, kama hata mpango wa miaka mitano aliouandaa yeye mwenyewe na mawaziri wake na ukapata sifa kedekede bunge likaupitisha. leo mwaka mmoja tu baaadae anashindwa kusimamia budget i reflect mpango ambao hata kuna baadhi wanadiriki kuuita mpango wa kikwete. mwingine kasema eti mnyika aheshimu watu wazima, hata kama ni watu nusu , wazee, wa baba, wa mama na wengine unao wafahamu wewe kama niwapuuzi,legelege, au dhaifu ni msema kwelitu ndie atakae simama na kusema bana wewe ni mpuuzi legelege au dhaifu. Big up mnyika endeleza mapambano ya ukombozi mpaka kieleweke

    17. #94
      hacena's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 383
      Rep Power : 513
      Likes Received
      92
      Likes Given
      11

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Masikini we, kwa bahati mbaya nasikitika kuwa uwezo wako wa kufikiri ni dhaifu kama naibu spika, kusema Rais Kikwete ni dhaifu sio kutangaza vita, naibu spika alitakiwa kumpa nafasi Mh. Mnyika afafanue kwanza ni ndhaifu kwa lipi? pili mwaka 2010 hatukuchagua malaika kuiongoza Tanzania bali tulimchagua binadamu aitwae Jakaya Mrisho Kikwete kutuongoza hivyo binadamu wote tu dhaifu akiwemo Rais Kikwete hivyo, sio sahihi kutuaminisha watanzania kuwa Rais Kikwete hawezi kuwa dhaifu.

    18. #95
      Nyunyu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 9th March 2009
      Location : Here.
      Posts : 3,349
      Rep Power : 2044
      Likes Received
      465
      Likes Given
      2749

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Quote By zomba
      Wewe anza kwa kuonesha ni lipi la maendeleo alilofanya Rais yeyote wa kabla yake, ambalo yeye hajafanya zaidi.

      Mnaleta matusi na ktukana lakini hoja za wazi kabisa zinawashinda. Mnyika kashindwa hoja ya bajeti akaamuwa awatukane wabunge wote, wana CCM wote na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Namwambia hvi; Kikwete asimjaribu, hamuwezi hata kidogo.
      Zomba naomba nitofautiane na wewe kwenye hili!!! JK toka ameingia zilikuwako dalili lukuki tu za kudhihirisha udhaifu wake! Yapo, meeingi tu, katika hayo naomba niongelee moja tu! JK ameshindwa kuongoza taasisi ya UwT. Hii ni taasisi nyeti kwake kama rais, ndiyo inayomuoongeza kwenye mambo meeenigi sana katika utendaji wake.

      Kwa mfumo wetu mbaya, wengi tu wamejitahidi kutumia vibaya taasisi hii kujinufaisha. Sasa JK ameshindwa kuwa taasisi iliyo imara na moja kumsaidia, UwT imegawanyika na ndo maana mambo ya serikali yake, ikiwamo madudu, tunayapata live mitaani!! Kwa hiyo angeweza kutumia taasisi hii kuendesha vita binafsi na Mnyika, nasikitika kukwambia hawezi maana haiko "coherent" iko kama muunganiko wa maji na mafuta!!

      Mnyika kamlima JK bungeni si kwa vita binafsi, ila ka-ainisha weakness zake! Weakness si tusi!! So Mnyika was and still is right!! Nyie endeleeni tu kucheza ngoma za CDM, najua mtashtuka mmekuwa chama cha upinzani, ndo akili zitarudi!!
      There is no such a thing as part freedom- Nelson Mandela

      e-mail: [email protected]

    19. #96
      toghocho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th March 2011
      Location : here here
      Posts : 1,000
      Rep Power : 615
      Likes Received
      138
      Likes Given
      29

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Quote By mkomatembo
      Babu yenu Nyerere alokuwa akiua waziwazi kina marehemu Hanga mbona hakuwahi kuuliwa? na matokeo yake amekuja kuuliwa na ambao aliwaamini sana tunavosikia kutoka kwa kina vicent nyerere! kwani adabu ni kuua tu ! kwalipi kubwa mpaka auliwe mnyika? afungwe tu kumshikisha adabu kwa kumdhalilisha kiongozi wa nchi!
      hee, hivi kusema rais ni dhaifu ni kudhalilisha?so ukisema ukweli unaouma, umedhalilisha...kama unataka kujua kikwete ni dhaifu angalia hata baraza lake la mawaziri, alilibadilisha lakini kwa malalamiko ya ooh, kuna watendaji ilibidi wawajibike nk, huo ni udhaifu na kukosa maamuzi...

    20. #97
      kindafu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th November 2010
      Posts : 256
      Rep Power : 488
      Likes Received
      83
      Likes Given
      62

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Quote By Kimweli
      Watu Kama wewe ni wakupeleka Cameroon mkavunishwe Chai na Migambo wakiwasimamia kwa nyuma.

      Soma hapa basi
      MNYIKA ANGEKUWA DHAIFU ZAIDI KAMA ANGEFUTA KAULI YAKE BUNGENI.

      1. Kama udhaifu ni kuto kujua kwa nini wananchi wako ni maskini
      wakati wako nchi tajiri. Mnyika yuko sahihi.

      2. Kama huwezi kumuwajibisha au kuona madudu ya katibu mkuu au katibu
      kiongozi mpaka bunge lishikilie bango na kushinikiza wang'oke ndio
      uzinduke kufanya maamuzi basi mnyika yuko sahihi.

      3. Kama kweli watu wamelibia taifa kupitia dili za magumashi halafu
      una watangazia warejeshe fedha ili wasichukuliwe hatua na wakati
      huohuo vibaka wanauwawa au kuchomwa moto kwa kuiba kuku na simu basi
      ni dhahiri kuna udhaifu wa kiungozi. Mnyika yuko sahihi.

      4. Kama ndege inaingia kwenye anga ya nchi yako na kubeba wanyama
      kupeleka Arabuni bila hatua zozote kuchukuliwa ni dhahiri kuna udhaifu
      wa kimfumo ulio kubuhu serikalini. Mnyika yuko sahihi.

      5. Kama rais anafunga safari kwenda kuomba misaada na wakati huohuo
      misaada anayopewa hailingani thamani na raslimali zinazo vunwa kwenye
      nchi yake basi Mnyika yuko sahihi.

      6. Kama rais anadiriki kutoa ahadi 99 ambazo thamani yake ni zaidi ya
      trilion 9 huku akijua kuwa hazitekelezeki ni hadaa kwa wananchi, chama
      na serikali. Mnyika yuko sahihi.

      7. Kama taasisi ya Ikulu na mfumo wake wa utawala umehusika kuingilia
      maamuzi ya mhimili wa haki kwa kutoa hukumu ya upendeleo ili kumkomoa
      au kumnyang'anya mbunge wadhifa kama jinsi ilivyo lalamikiwa. Mnyika
      yuko sahihi.

      8. Kama serikali inatenga 70% kwa matumizi kwenye bajeti yake na 30%
      kwenye maendeleo. Ni dhahiri kuwa ni aina ya serikali dhaifu yenye
      viongozi wavivu wa kufikiri.

      Kama hivyo ndivyo, nasimama na kijana mwenzangu kwa ukakamavu na
      kupaza sauti yenye mwale mkali. Namuunga mkono Mnyika.
      Mkuu nakuunga mkono kwenye hoja zote, na hapo namba 5 ungeongeza ukweli pia kwamba Rais anafunga safari kwenda kutembeza kibakuli ila ukizingatia ukubwa wa msafara anaondamana nao gharama + posho wanazokatiana zinazidi kile anachopata huko!! Hongera Mnyika kwa ujasiri wa kumvika paka kengele!

    21. #98
      transcend's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 198
      Rep Power : 478
      Likes Received
      17
      Likes Given
      17

      Default

      Quote By zomba
      Nasema hivi, nyinyi hamuelewi msemo wa Kiswahili unaosema "asiyefundwa na mamae hufundwa na ulimengu", huyu kijana hajafudwa kwao, na sasa ulimwengu utamfunda. Kacheza na moto ambao haujuwi joto lake.

      Kajiingiza kichwa kichwa pabaya sana, kavuka mipaka ya demokrasia, kashindwa kuleta hoja kaleta dharau na hilo hatuliwachi likapita ili iwe fundisho kwa wengine.
      Wewe Zomba kwa woga na udhaifu wako hata kikwete akikutaka utamkubalia haraka sana kwa udhaifu ulionao!

    22. #99
      jigoku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2011
      Posts : 1,441
      Rep Power : 1001
      Likes Received
      362
      Likes Given
      536

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Hivi kama raisi JK ni dhaifu mlitaka Mnyika asemeje?hivi kama mtu kaiba utatumia lugha gani,je utasema aa kachukua tu,wakati kaiba?jamani kumwambia mtu mkubwa kwa umri au kicheo kama au mtawala au Tajiri kuwa hili haliko sawa tusidanganyane sio dhambi wala sio utovu wa nidhamu.karne ya leo hatutaweza kufika kama huwezi kumwambia mtu makosa yake au mapungufu yake.ni kweli JK ni dhaifu sana.
      ANGALIZO wewe ZOMBA usijidanganye kwa kuleta vitisho kumtisha Mnyika,hata kama ni umoja wa wanawake Tanzania zamani ikiwa usalama wa Taifa,USIMTISHE MTU KWA KARNE HII.hapo utaamsha mengi yaliyolala,na usidhani watu hawako nyuma ya Mnyika,tena msije kudanganyana kabisa.
      na kwa taarifa yako mnachotakiwa kufanya ni kumshauri JK atende contrary to udahifu wake hapo tutabadilisha lugha,lakini leo hii bado nasema JK ni dhaifu sana

    23. BAK
      #100
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,603
      Rep Power : 44965
      Likes Received
      8354
      Likes Given
      8336

      Default Re: Mnyika huwezi vita binafsi na Kikwete

      Quote By zomba
      Mbunge kijana ambae anaonesha kuwa umaarufu na madaraka ya ubunge yamemlevya amefikia hatua ya kumuingia Kikwete binafsi kwa kumwita, kwa kejeli na dharau eti ni "dhaifu".

      Kwa muono wangu, Mnyika amepotoka na amekosa heshima na adabu kwa sio tu mtu aliyemzidi umri, bali kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa Watanzania wote ambao tumeridhika kwa kumchagua Kikwete kwa kumpigia kura atuongoze.

      Mnyika baada ya kushindwa kuwasilisha hoja kuhusu bajeti akaamuwa kwa makusudi kabisa, kutoa lugha inayokera, si tu kwa Rais, bali kwa bunge pia, kuwa wote ni "wazembe" na CCM yote ni "upuuzi".

      Kweli kabisa, mimi ni mwana CCM na umenitukana, kwa hilo, umetangaza vita binafsi na mimi na wana CCM wote, hali kadhalika na Wabunge wote kwa kuwaita "wazembe". Jee, kijana hicho kiburi cha kututukana wote pamoja na Rais wetu mpendwa kwa ajili ya huo Ubunge? au kuna kinachokufanya ujione kuwa uko juu ya sheria, kwa kuwa upo hapo na watunga sheria wengine?

      Nakuhakikishia, vita uliyoitangaza itakugharimu kupita uwezo wa kufikiri, na majuto ni mjukuu.

      Kikwete humuwezi.

      Mnyika hana sababu yoyote ile ya kushindana na dhaifu Kikwete na alichokisema ni ukweli mtupu na kuna ushahidi chungu nzima kuanzia 2005 hadi hii leo unaothibitisha kauli ya Mnyika. Hata Wabunge wa Magamba waliona Rais wao ni dhaifu ndio maana wakamshikiza awafukuze kazi mawaziri wake. Siyo siri Msanii Kikwete ni dhaifu.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    Page 5 of 20 FirstFirst ... 3456715 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...