Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete
Wakuu, katika uchunguzi wangu nimegundua kuwa Mh. Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete. wa kwanza alikuwa Mbunge wa Urambo - Mh. Samweli sitta alipomwambia KIKWETE live kuwa awe mkali kwa mafisadi nga kidogo, au kama kuna sheria inamtatiza ailete bungeni irekebishwe. NAOMBA KUWASILISHA.
Re: Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete
By mumburya
Wakuu, katika uchunguzi wangu nimegundua kuwa Mh. Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete. wa kwanza alikuwa Mbunge wa Urambo - Mh. Samweli sitta alipomwambia KIKWETE live kuwa awe mkali kwa mafisadi nga kidogo, au kama kuna sheria inamtatiza ailete bungeni irekebishwe. NAOMBA KUWASILISHA.
Katika nukuu yako ya maneno ya Sitta, wapi kuna neno mdhaifu?
Re: Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete
Yaani kama kuna sheria inamtatiza ailete bungeni irekebishwe. Ambayo sitta alikuwa haioni na kifupi anashangaa kwa nini rais alikuwa haadabishi mafsadi. Yaani Sitta alikwisha kuuona udhaifu wa JK na akamwambia wazi wazi, sioni siri hapo.
Re: Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete
soma kwa makini - nimeandika kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete kwa maana hiyo sitta maneno yake yalikuwa juu ya udhaifu wa Kikwete ingawa hakusema direct. unapoambiwa uwe makali kwa wezi maana yake usicheke nao, usijikombe kwao, usiwe legelege bali uwachukulie hatua madhubuti. huo ni udhaifu na wala sio ushupavu kama unavyojilazimisha kuamini.
Na je, ndege ya Qatar inapoingia anga la TZ na kubeba wanyama hai huo si udhaifu wa serikali inayoongozwa na Rais ambaye ni amri jeshi MKUU, Kikwete. Je, huo nao ni ushupavu au udhaifu?
Re: Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete
By mumburya
Wakuu, katika uchunguzi wangu nimegundua kuwa Mh. Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete. wa kwanza alikuwa Mbunge wa Urambo - Mh. Samweli sitta alipomwambia KIKWETE live kuwa awe mkali kwa mafisadi nga kidogo, au kama kuna sheria inamtatiza ailete bungeni irekebishwe. NAOMBA KUWASILISHA.
Ni kweli mkuu hata mimi nakumbuka hayo yote tatizo la wabung wengi wa CCM ni vilaza wao huangalia upande wao tu...na ndiyo maana mimi nawaona ni wachumia matumbo huogopa kusulubiwa wakati wa uchaguzi kuawafika maafa kwa kusimamia ukweli. Ipo haja sasa ya Watanzania kuwakataa watu wanafiki hawa wasio na tija.BTW namkubali MNYIKA ni mpiganaji wa ukweli na amesema ukweli kwa anachokiamini ila ndiyo hivyo tena serikali haitaki kukosolewa hata kwa madudu wanayoyafanya waige nchi za wenzetu wenye maendeleo wanaokubali challenges.
'' The socialism I believe in is everyone working for each other, everyone having a share of the rewards. It's the way I see football, the way I see life.'' By Bill Shankly
Re: Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete
Tatizo la naibu spika bwana Ndungai ni kwamba hakutaka kufafanuliwa nini maana ya udhaifu wa JK!, kwa wana CCM wamekwenda mbali mno kulitafakari neno UDHAIFU, neno UDHAIFU lina maana nyingi kulingana na nini kilichokua kinajadiliwa ndani ya bunge hapo jana! kwamtazamo wangu mimi nilivyomuelewa bwana John Mnyika alichokua anamaanisha ni kua JK ni mdaifu wa kutokufuatilia muenendo mzima wa kiutendaji kama kiongozi wa nchi, sasa wanaCCM nini kinachowauma?? Kwani siku ile pale Dodoma kwenye kikao cha CCM mbona Lowassa alimshupalia JK kua anajua ni nani wamiliki wa Dowans na yeye hakujibu je huo si udhaifu? wa kuwadanganya watanzania kua hausiki na wala hawajui wamiliki wakubwa wa Dowans? je raisi wa nchi unashauriwa vibaya na wasaidizi wako na wewe unakubali je huo si Udhaifu? Kweli JK utamaliza kipindi chako cha uraisi lakini utaondoka kwa aibu kubwa mno.
Re: Mnyika sio wa kwanza kutoa kauli ndani ya Bunge juu ya udhaifu wa Kikwete
Inategemea udhaifu wake upo kwa wapi. Nadhani jamaa si dhaifu ktk nyanja zote. mbona anao vijana wazuri tu wenye afya tele hadi wengine wamezunguka round about?
Mnyika alihitaji muda zaidi awafafanulie wabunge ila haraka za Ndugai zimeharibu.
"Tanzania ni ya watanzania, na watanzania wenyewe ndo sisi"
Follow Us Here