Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

    Report Post
    Page 1 of 9 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 165
    1. #1
      SirBonge's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 18th July 2010
      Posts : 167
      Rep Power : 581
      Likes Received
      91
      Likes Given
      32

      Default Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Mshahara wa wabunge umepanda kutoka Tsh 6,000,000/- kwa mwezi mpaka Tsh 10,000,000/- kwa mwezi mbali na marupurupu mengine!..

      Hii inakuja ikiwa wadaktari tayari wameshatangaza mgogoro na serikali na kuipa wiki 2 kutimiza madai yao la sivyo watatangaza mgomo mkubwa nchi nzima kuanzia 23/6/2012...

      Source: Mtanzania ya leo

      "Hatuwezi kutatua matatizo kwa akili ile ile ambayo ilisababisha yawepo"..Mch. Peter Msigwa


      Quote By Molemo
      Wabunge wazidi kuongezewa marupurupu:Monday, 30 July 2012 - Boniface Meena, Dodoma

      MARUPURUPU ya wabunge ikiwamo mishahara imeongezwa kutoka Sh7.4 milioni kwa mwezi hadi takriban Sh11milioni kwa mwezi, hatua ambayo imeibua mjadala mwingine mzito miongoni mwao.

      Tangu mwaka jana, wabunge wamekuwa katika vita ya kupokea au kutopokea posho ya vikao ambayo imekuwa ikikolezwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe ambaye alizikataa akisema mbunge anapokuwa kazini hahitaji kulipwa.
      Hata hivyo, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba sasa vita kubwa ipo katika marupurupu mapya ambayo pamoja na kuchanganya na mshahara yanafikia Sh11milioni kwa mwezi.

      Spika wa Bunge, Anne Makinda alipoulizwa jana alithibitisha kuhusu kuongezeka kwa malipo jumla ya wabunge kwa mwezi lakini akasema hafahamu kiwango halisi kilichoongezwa. Makinda alisema nyongeza iliyopo siyo kwa wabunge tu, bali watumishi wote wa Serikali na ilitangazwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), wakati wa Bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka 2012/13.

      “Hiyo nyongeza siyo tu kwa wabunge, bali ni kwa watumishi wa Serikali. Tena hiyo ilitangazwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma). Sasa ukiniuliza kiasi gani hapo ndipo sielewei, ila najua nyongeza ipo,” alisema Spika. Lakini, vyanzo kutoka ndani ya Bunge vilisema kwamba nyongeza hiyo ambayo tayari imeingia katika mshahara wa Julai ni Sh3.6milioni, hivyo kufanya jumla ya fedha anazochukua mbunge kufikia kiasi hicho cha Sh11milioni.

      “Hiyo ni vita, kuna wabunge wana hasira kweli hawataki wananchi wajue kama marupurupu yameongezeka. Wanaona wananchi wakijua itakuwa ni tatizo kubwa, watapigiwa kelele lakini nyongeza hiyo ipo. Tayari wengine wamechukua tangu Ijumaa,” kilisema chanzo kimoja kwa sharti la kutotajwa jina gazetini.

      Hata hivyo, kwa mujibu wa chanzo hicho, baadhi ya wabunge kutoka kundi la wanaopinga posho kwa wabunge wamepinga pia nyongeza hiyo wakitaka fedha hizo zielekezwe katika sekta nyingine za kijamii.

      Marupuru ya sasa

      Hadi mwezi uliopita, mbunge alikuwa akipokea Sh7.4milioni kwa mwezi ambazo kati ya hizo Sh2.5milioni ni kwa ajili ya mafuta, Sh2.3 mshahara, Sh170,000 kwa ajili ya mshahara wa dereva, 100,000 kwa ajili ya katibu wa mbunge na posho ya jimbo.
      Hata hivyo, katika nyongeza hiyo ya sasa haijawekwa wazi kwamba kiasi gani ni kwa ajili ya mshahara, fedha za mafuta ya gari la mbunge, za dereva, katibu na za posho ya jimbo na tayari baadhi ya wabunge wameanza kufuatilia mchanganuo wa nyongeza hiyo.

    2. Study Abroad

    3. #2
      mayenga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th September 2009
      Posts : 1,564
      Rep Power : 805
      Likes Received
      305
      Likes Given
      437

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Nimeisikia,siku yangu imeharibika mapema kabisa leo,sijui wapi tunaelekea .
      Mamndenyi likes this.
      A man's character may be learned from the adjectives which he habitually uses in conversation.

    4. #3
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,644
      Rep Power : 4014
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Haaahaaa! Nchi hii namna pekee ya kulindana ni kwa wanasiasa kula mali ya walipa kodi kwa kumegeana. Watu wanajaribu kula hata wasichopanda.
      Madaktari kwa wana siasa wana umuhimu gani? Wakiumwa serikali inawapeleka fasta india
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    5. #4
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,697
      Rep Power : 2260
      Likes Received
      599
      Likes Given
      779

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Eti Zitto, hii ni kweli?
      Mamndenyi likes this.

    6. #5
      MANGUNGO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Posts : 1,146
      Rep Power : 619
      Likes Received
      251
      Likes Given
      14

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Kwa akili ile ile ya wapuumbavu kutaka kutatua matatizo kwa njia zilezile wakitegemea matokeo tofauti.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      pmwasyoke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2010
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,449
      Rep Power : 969
      Likes Received
      319
      Likes Given
      419

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      kwa kweli nitagombea ubunge 2015 ili nikale kwa niaba ya wapiga kura wangu.

    9. #7
      TajiriMutoto's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th June 2012
      Location : Kaunta ya juu
      Posts : 85
      Rep Power : 365
      Likes Received
      35
      Likes Given
      48

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      2015 nalitaka jimbo la Lusinde.
      Mamndenyi likes this.
      Liwalo na liwe

    10. #8
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,590
      Rep Power : 1101
      Likes Received
      996
      Likes Given
      744

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Quote By Communist
      Eti Zitto, hii ni kweli?
      Sisi Watanzania in the first place ni waongo, hatujui haki zetu na ni watu wa kulalamika tu mafisadi yanaiba tunalalamika tu, mikataba ya madini, tunalalamika tu, wawekezaji wanatunyanyasa tunalalamika tu, tunaibiwa kura tunalalamika tu!

      Wabunge wanajipandishia mishahara tunalalamika tu, kodi zinanyonga wafanyakazi na wafanya biashara ndogondogo tunalalamika tu! tunakufa kwa kukosa huduma za afya huku tunachangia bima ya afya tunalalamika tu??Watoto wetu wanakaa chini shuleni wakati tunatoa michango ya dawati na ujenzi tunalalama tu??

      Mafisadi yanatamba tunalalamika tu? serikali inadharau maazimio ya bunge ambalo ndio midomo yetu wananchi tunalalama tu??watoto wa viongozi wanapewa madaraka na kujiimbikizia mali tunalalama tu??

      Huwezi kufanya kitu kimoja kila siku kwa mbinu ileile ukitarajia matokeo tofauti(mch. Msigwa) na sisi Watanzania hatuwezi kuendelea kulalamika tu tukitegemea mambo yatabadilika! Bila kuingia mitaani na kuitikisa serikali hii dokozi na bunge lililojaa vilaza wa magamba hatutaweza kubadili kitu!

      Tuamke tuache kulalama tuchukue hatua tena wakati huu wa budget ndio wakati muafaka wa kuonyesha hasira zetu!!kinyume cha hapo tuvumilie haya na mengine makubwa zaidi yanayokuja!
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    11. #9
      daby mouser's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 9th February 2012
      Posts : 127
      Rep Power : 392
      Likes Received
      17
      Likes Given
      15

      Default

      Quote By Communist
      Eti Zitto, hii ni kweli?
      zitto ndo mtafunaji wako na we ndo mmezaji??acha uumin wa kibwatere ushapewa source unataka upigiwe tarumbeta uamin???
      Unstoppable likes this.

    12. #10
      Black Bat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Abbottabad
      Posts : 2,479
      Rep Power : 9580
      Likes Received
      682
      Likes Given
      575

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      kama wangekuwa hawapelekwi india haya yote yasingetokea

    13. #11
      Barnabas Shadrack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Posts : 2,055
      Rep Power : 809
      Likes Received
      182
      Likes Given
      11

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Ina maana hata Dr Slaa ataongezewa mshahara ili ufanane na wa wabunge?
      The unseen is illustrated by the seen.

    14. #12
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1809
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Quote By SirBonge
      Mshahara wa wabunge umepanda kutoka Tsh 6,000,000/- kwa mwezi mpaka Tsh 10,000,000/- kwa mwezi mbali na marupurupu mengine!..Hii inakuja ikiwa wadaktari tayari wameshatangaza mgogoro na serikali na kuipa wiki 2 kutimiza madai yao la sivyo watatangaza mgomo mkubwa nchi nzima kuanzia 23/6/2012...
      Source: Mtanzania ya leo

      "Hatuwezi kutatua matatizo kwa akili ile ile ambayo ilisababisha yawepo"..Mch. Peter Msigwa
      Je bado bajeti ya 2012/2013 haikidhi haja za Watanzania? teh teh tehe, Wabunge bana wapige kelele basi wagomee na hivyo viwango vipya vya mishahara yao

    15. #13
      Nzenzu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2011
      Posts : 826
      Rep Power : 558
      Likes Received
      155
      Likes Given
      38

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Najiandaa kuchukua jimbo labda naweza jisikia kuwa sehemu ya watanzania!
      Mamndenyi likes this.

    16. #14
      frema 120's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Posts : 1,056
      Rep Power : 1003
      Likes Received
      276
      Likes Given
      62

      Default

      Quote By Barnabas Shadrack
      Ina maana hata Dr Slaa ataongezewa mshahara ili ufanane na wa wabunge?
      The unseen is illustrated by the seen.
      Slaa ni mbunge? una maneno ma......

    17. #15
      Barnabas Shadrack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Posts : 2,055
      Rep Power : 809
      Likes Received
      182
      Likes Given
      11

      Default

      Quote By frema 120
      Slaa ni mbunge? una maneno ma......
      We hujui kuwa aliamua kujilipa mshahara sawa na ule wa wabunge baada ya kuukosa Urais 2010?
      The unseen is illustrated by the seen.

    18. #16
      Uparo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th May 2012
      Posts : 34
      Rep Power : 361
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Serikali ya ccm mnatupeleka wapi jamani? Mbona mnatunyanyasa wazi ndani ya nchi yetu?tofauti ya kipato inazidi kuongezeka,tizama wabunge mishahara mikubwa waalimu ambao ndo nguzo na msingi wa kila kitu wamesahauliwa na kutengwa pia wananchi wa vijijini mmewasaliti oneni aibu na pia msitegemee kurudi bungeni ktk uchaguzi ujao na pia muache unafiki kuwa mnawapenda watanzania wengi mpo kwa manufaa yenu na cyo yetu tuliowachagua

    19. #17
      christine ibrahim's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2012
      Posts : 2,690
      Rep Power : 902
      Likes Received
      430
      Likes Given
      440

      Default

      Quote By Barnabas Shadrack
      We hujui kuwa aliamua kujilipa mshahara sawa na ule wa wabunge baada ya kuukosa Urais 2010?
      The unseen is illustrated by the seen.
      ...acha uongo ww!aliamua kujilipa lini?ww unajua kinachoendelea au unaongea tu?uliza uambiwe c o kuandika vitu usivyo na uhakika navyo

    20. #18
      +255's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Posts : 1,073
      Rep Power : 586
      Likes Received
      205
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By christine ibrahim
      ...acha uongo ww!aliamua kujilipa lini?ww unajua kinachoendelea au unaongea tu?uliza uambiwe c o kuandika vitu usivyo na uhakika navyo
      Nadhani haujui lolote...

    21. FJM
      #19
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,167
      Rep Power : 2566
      Likes Received
      5317
      Likes Given
      4585

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Quote By Barnabas Shadrack
      We hujui kuwa aliamua kujilipa mshahara sawa na ule wa wabunge baada ya kuukosa Urais 2010?
      The unseen is illustrated by the seen.
      Barnabas Shadrack, kuna uhusiano wowote kati ya hii nyongeza ya mshahara kwa wabunge (kama ni kweli) na mbadiliko wa ghafla wa wabunge wa CCM kuanza kuitetea budget wakati week iliyopita walikuwa wanaongea na vyombo vya habari wakisema hawataikubali?

      Pili, unaweza kutuambia Mukama analipwa kiasi gani kwa mwezi?

    22. #20
      decruca's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 18th June 2012
      Posts : 164
      Rep Power : 380
      Likes Received
      33
      Likes Given
      14

      Default re: Mshahara wa wabunge wapanda mpaka 11,000,000/-

      Quote By TajiriMutoto
      2015 nalitaka jimbo la Lusinde.
      Umeendaa timu ya kujibu matusi?

    23. Miaka 50
    Page 1 of 9 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...