Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

    Report Post
    Page 3 of 9 FirstFirst 12345 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 171
    1. #1
      Jackbauer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : CTU
      Posts : 4,873
      Rep Power : 1690
      Likes Received
      1348
      Likes Given
      277

      Default Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      baada ya kushuhudia migomo ya madaktari kwa awamu mbili na baadaye kufuatiwa na majadiliano yalioyoisha hivi karibuni sasa kuna kila dalili ya kutokea kwa mgomo mwingine mara itakapofika tarehe 23 juni 2012.
      migomo miwili ya kwanza ilipuuzwa hivihivi lakini mwishowe tuliona viongozi wakuu wa nchi wakirudi nyuma na kuomba huruma ya mazungumnzo.
      je iwapo mgomo wa tarehe tajwa utatokea ni nani alaumiwe kwa kushindwa kutatua mgogoro huu uliodumu kwa kipindi cha nusu mwaka sasa??


      haya ni ya morogoro

      TAARIFA KWA UMMA
      Katika kikao cha madaktari na wahudumu wa afya Ifakara kilichofanyika tarehe 16.June 2012, Kwa pamoja kilikataa taarifa iliyotolewa na serikali kuhusu madai ya Madaktari na Wahudumu wa Afya. Kikao kilitoa maazimio yafuatayo
      1. Tunasikitishwa na msimamo wa serikali kutokuonyesha lengo la kutatua madai ya madaktari na wahudumu wa afya.
      2. Tunatangaza mgogoro rasmi dhidi ya serikali kuhusiana na madai yetu kudharauliwa na kutofanyiwa kazi.
      3. Tutaungana na madaktari na wahudumu wengine wa afya Tanzania katika mgomo utakaoanza tarehe 23 Juni 2012. Kama Serikali haitafanyia kazi madai yetu
      4. Tunaukumbusha umma kuwa serikali ilikuwa na muda wa kutosha kufanyia kazi na kutatua madai ya madaktari na wahudumu wa afya

      haya ni ya BUGANDO


      TAMKO:
      Kutokana na kikao cha tarehe 15/06/2012 hapa Bugando na kanda ya Ziwa kwa ujumla tunatamka kwamba:-
      1. Hatukubaliani na namna serikali ilivyo- na inavyoshughulikia suala la madaktari na wahudumu wengine wa afya hapa nchini.

      2. Ni vema serikali itoe tamko lenye tija juu ya mgogoro unaondelea kati yake na wafanyakazi wa sekta ya afya nchini

      3. Tutaungana na madakrai wote pamoja na wahudumu wengine wa afya katika mgomo utakaonza tarehe 23/06/2012 ikiwa hatua madhubuti na zenye tija hazitachukuliwa

      Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika


      na haya ni ya Dodoma karibu kabisa na mjengoni
      TAMKO LA MADAKTARI NA WAHUDUMU WA AFYA DODOMA
      Baada ya kupata muda wa kupitia na kuchambua kwa kina ufafanuzi wa serikali kuhusu madai ya madaktari. Madaktari na wahudumu wa afya Dodoma tunapenda kutoa tamko kama ifuatavyo

      1. Tunaunga mkono maamuzi ya kikao cha madaktari na wahudumu wa afya cha tarehe 9/06/2012 kwa kuukataa ufafanuzi wa madai ya msingi kwani hauna nia ya dhati wa kuleta suluhisho la kudumu katika sekta ya afya. Hivyo tupo katika mgogoro na serikali na tutaungana na wenzetu katika mgomo utakaoanza tarehe 23/06/2012.

      2. Tunaitaka serikali iache mara moja jitahada zake za kutugawa wahudumu wa sekta ya afya kwani kwa kufanya hivyo kutadhorotesha ufanisi wa utoaji wa huduma za afya katika hospitali mbalimbali nchini. Hivyo tunaitaka serikali ianze mara moja kuwalipa wahudumu wote wa afya posho mpya za kuitwa kazini.

      3. Tunawaomba wahudumu wa afya wote na popote walipo kuendelea kuwa pamoja katika kutetea huduma bora na maslahi mazuri katika sekta ya afya.

      MUNGU IBARIKI TANZANIA.

      updates;mahakama kuu divisheni ya kazi imetoa zuio la mgomo huu.
      madaktari washikilia msimamo wao na baadhi yao kusema
      "BASI NASISI HIYO TAARIFA YA SERIKALI TUNAICHAMBUA KWA KINA ,TUNAIFANYIA MPANGO MKAKAKATI KABAMBE,TUNAISHUGHURIKIA,TUTAI FANYIA UPEMBUZI YAKINIFU MBALI NA HAYA MGOMO UKO PALEPALE''

      SIKU YA KWANZA
      hospitali kadhaa zimeingia kwenye mgomo ikiwa ni pamoja na Bugando,Muhimbili,Mbeya na Amana.
      bado ni vigumu ku-assess makali ya mgomo hasa ukizingatia leo haikuwa 'siku ya kazi' tusubiri siku ya jumatatu ambayo ni siku inayohudhuriwa na wagonjwa wengi.

      SIKU YA TATU

      Mbeya,Bugando,Muhimbili,Dodoma ,amana,KCMC,mwananyamala,TMK,i fakara, wako kwenye mgomo.
      kuna tetesi kuwa Ocean road wako mbioni kujiunga.
      Vyombo vya habari mbalimbali vyaanza kuripoti madhara ya mgomo huu.baadhi ya waandishi wakataliwa kuingia hospitali ili kuhabarisha wananchi juu ya mgomo.
      Channel ten yafanya mjadala na madaktari.madaktari wajieleza vizuri kwa nini wamefikia hatua hii.kesho tutegemee mgomo kuwa mkali zaidi.

      SIKU YA NNE
      Mgomo bado unaendelea katika sehemu tajwa hapo juu.pia kuna taarifa kuwa hospitali ya hydom imeingia rasmi kwenye mgomo.
      waziri wa afya amekwepa kufanya mahojiano ya 'live kupitia star TV' ili kujibu madai ya madaktari.katika kipindi hicho kulikuwepo wawakilishi wa madaktari na wajumbe wa kamati ya bunge huduma za jamii.Mwinyi aliomba udhuru kwa kusema kuna mambo muhimu uanayashughulikia.
      huko bugando mkurugenzi wa hospitali anaelekea kurudia kosa lililofanywa na mkurugenzi mwenzake wa Muhimbili kwa kutishia kuwarudisha intern doctors wizarani.tukumbuke kosa hili ni moja ya chanzo cha mgomo huu unaoendelea mpaka leo.

      SIKU YA TANO
      Kiongozi wa jumuiya ya madaktari Dr Ulimboka steven atekwa na kupigwa hadi kupoteza fahamu.
      Madaktari waapa kuongeza mgomo.
      Mh pinda kutoa tamko la serikali kesho.

      SIKU YA SITA

      Afya ya dr ulimboka yaanza kuimarika,asema bado maumivu ni makali!
      Pinda akataa kutoa tamko.
      mgomo unaendelea huku kukiwa na ripoti ya madaktari bingwa wa MNH wamejiunga katika mgomo

      SIKU YA SABA
      Hali ya ulimboka si nzuri sana
      madaktari bingwa wa MNH,MOI,MUHAS,ORCI, Wametoa tamko rasmi la kujiunga kwenye mgomo.
      nawasilisha...
      Last edited by Jackbauer; 29th June 2012 at 20:18.

    2. FemaTV & Radio

    3. #41
      Kiranga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Posts : 14,130
      Rep Power : 41571
      Likes Received
      6036
      Likes Given
      1054

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Predictable as Rambo, with another clip
      Snoop Dogg - Up Jump The Boogie
      Banda lishavunjika, jogoo kaondoka. Vifaranga hangaika, kumtoa nyoka.


    4. #42
      Bitabo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2011
      Posts : 1,375
      Rep Power : 662
      Likes Received
      447
      Likes Given
      261

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Hili ni zengwe jipya. jana tu yule ''mchumi wa daraja la kwanza na mtumishi aliyetukuka wa BOT'' alisema kwenye zile trilioni 10 za matumizi ya kawaida kuna hela za madaktari ili wasigome.

      Huu ujumbe sijui kama kwenye CCM caucus wameupata.
      Kama naona jinsi CCM watakavyoumbuka huko bungeni na kwenye hili swala hakuna cha ''muongozo wa spika'' au ''taarifa kwa spika''.

      Ah Tanganyika yangu weeeeee. nchi haina mwenyewe, full fujo tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu uuuu

      FFU na nyie hamgomi hata kwa siku mbili tu??
      Nyamayao and FJM like this.
      Uovu wa siku moja, unaondoa wema wa MWAKA MZIMA

    5. #43
      Mandingo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd September 2011
      Posts : 927
      Rep Power : 572
      Likes Received
      186
      Likes Given
      52

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Mwaka huu huyu kilaza asipo jiuzuru!
      Madaktari migomo!
      Wanafunzi migomo!
      Walimu migomo!
      Wafkz wa Reli soon!
      TUCTA nawona walee!
      Huyu kweli dhaifu hebu gomeni
      bwana vasco apunguze safari kidogo.

    6. #44
      mzee wa njaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th June 2011
      Posts : 1,340
      Rep Power : 669
      Likes Received
      194
      Likes Given
      107

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Then watu wanakaa bungeni kuongea maneno ya khanga na ubishani wa kisiasa na kuacha mambo ya msingi kama haya. Sasa Mwigulu Nchemba yeye kama mjanja aje na hoja ya kuwatetea madaktari sio anajiita mchumi 1st class huku wananchi wakiteketea. Uchumi utakuwaje endapo wananchi watakuwa hawana afya njema kutokana na mgomo wa madaktari!!!

    7. FJM
      #45
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,170
      Rep Power : 2568
      Likes Received
      5318
      Likes Given
      4585

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Quote By rweihimba
      Yafuatayo ni madai ya madaktari na majibu yaliyotolewa na serikali.

      Kupandisha mishahara,
      Bajeti ni finyu, kuwaongezea madaktari mishahara kutaongeza migogoro ktk secta nyingine,

      Bima ya kijani kwa watumishi wa afya
      serikali itaendelea na mazungumzo na mifuko hii, ili kuona kama wataboresha.

      Risk allowances
      serikali itatoa chanjo ya homa ya Ini(Hepatitis B) tu, nayo watapewa kwa awamu kutokana na ufinyu wa bajeti
      .

      Hardship allowances
      S
      erikali inaboresha miundombinu katika sehemu zenye maisha magumu,

      House allowances
      serikali inajenga nyumba ktk halmashauri 70 za watumishi wa umma hata madaktari wakiwemo.Hata hivyo sio madaktari wote watapata.

      Malipo ya kuitwa kazini usiku
      S
      erikali itaendelea kuliopa Tsh 25000 kwa daktari bingwa, 20000 kwa madaktari na Tsh 10000 kwa kada nyingine mpaka hapo bajeti itakaporuhusu.

      Madaktari kukopeshwa magari
      wafanyakazi wa serikali kuu wataanza mpango huo ktk bajeti ya 2011/2012.
      Hapo kwenye red kumenistua. Madaktari wanakuwa very exposed na magonjwa ya kuambukiza kwa sababu ya mazingira wanayofanya kazi, lakini serikali bado kweli inajivuta. Inakuwaje serikali 'maskini' iwe na uwezo wa kununua magari yenye thamani ya Tshs 5 trillion?

    8. #46
      Amiliki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2011
      Posts : 1,464
      Rep Power : 762
      Likes Received
      716
      Likes Given
      33

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Rais dhahifu mpaka wajanja wanautumia udhahifu wake kumwingiza mkenge kwa kumpa ushauri wa kimagumashi! Kweli cha Mjinga huliwa na mwerevu.
      Huku Magamba wakiendelea kusambaratishwa; Chadema Rahaaa!!!!! Si Rahaa!!!! WOTE: RAHAAAA!!!!!!!!!!

    9. #47
      cannulla's Avatar
      Member Array
      Join Date : 14th April 2012
      Posts : 26
      Rep Power : 363
      Likes Received
      5
      Likes Given
      22

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Quote By rweihimba
      Yafuatayo ni madai ya madaktari na majibu yaliyotolewa na serikali.

      Kupandisha mishahara,
      Bajeti ni finyu, kuwaongezea madaktari mishahara kutaongeza migogoro ktk secta nyingine,

      Bima ya kijani kwa watumishi wa afya
      serikali itaendelea na mazungumzo na mifuko hii, ili kuona kama wataboresha.

      Risk allowances
      serikali itatoa chanjo ya homa ya Ini(Hepatitis B) tu, nayo watapewa kwa awamu kutokana na ufinyu wa bajeti.

      Hardship allowances
      S
      erikali inaboresha miundombinu katika sehemu zenye maisha magumu,

      House allowances
      serikali inajenga nyumba ktk halmashauri 70 za watumishi wa umma hata madaktari wakiwemo.Hata hivyo sio madaktari wote watapata.

      Malipo ya kuitwa kazini usiku
      S
      erikali itaendelea kuliopa Tsh 25000 kwa daktari bingwa, 20000 kwa madaktari na Tsh 10000 kwa kada nyingine mpaka hapo bajeti itakaporuhusu.

      Madaktari kukopeshwa magari
      wafanyakazi wa serikali kuu wataanza mpango huo ktk bajeti ya 2011/2012.
      mlikuwa wap kuyaweka wazi toka zaman ili uma na madr wengne wajue kinachoendelea,,,,???

    10. UKI
      #48
      UKI's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Location : Mali
      Posts : 681
      Rep Power : 486
      Likes Received
      149
      Likes Given
      176

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      hii ni dalili za udhaifu wa serikali ya Jakaya Mrisho Kikwete.

    11. #49
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 484
      Rep Power : 669
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      nawaunga madaktar mkono kwa 100%..haiwezekani ikulu ikarabatiwe kila mwaka kwa mabilioni ya shilingi..2011/12-6bn,2012/13-6bn..jamani nchi yetu ni maskini alafu inatumia 12bn kukarabat ikulu within 2 yrs..?

    12. #50
      MD25's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 27th January 2012
      Location : Mugumu, Serengeti
      Posts : 1,912
      Rep Power : 0
      Likes Received
      539
      Likes Given
      66

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      TISS inabidi mumshauri vizuri huyo bosi wenye mwenye kichwa kigumu wakati legelege, ishu kama hizi mtambue kuwa kuna watu wa "human Right watch" wanahesabu na kuchukua data za idadi ya watu wanaokufa kutokana na akili za mcheza ngoma, sasa anapotoka kwenye power msishangae anapelekwa kwenye mahakama ya ICC kujibu roho za watu alizozichukua wakati wa utawala wake kutokana na uzembe na ulegelege wa kiutendaji. Kuweni makini ku-handle ishu kama hizi mtamponza bosi wenu...

    13. #51
      Ruppy karenston's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2011
      Posts : 396
      Rep Power : 482
      Likes Received
      69
      Likes Given
      26

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Madaktari simamieni maslahi yenu, kama kujitoa mmejitoa sana.
      Kama nyie wenye vipato vidogo mmevumilia, ni wakati wa serikali kuwajibika. Nitawashangaa sana watu watakaosema hamna utu,hawajui adha mnazozipata. Mimi ni mgonjwa hapa nilipo na nawahi mapema hospitali kesho ili nipate nguvu kuwasupport kwa nguvu zote!

    14. #52
      K.Msese's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 238
      Rep Power : 407
      Likes Received
      145
      Likes Given
      219

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012


      Tatizo linalo wakumba madaktari katika kudai maslahi yenu ni kuwa hampo kitu kimoja, ama kuna wenzenu wanao wazunguka katika madai yenu ili kuyadhoofisha kama ilivyo kwa mwenzenu Imani Kondo 'marcopolop'! Wengine kati yenu watagoma kwa maslahi ya wote, wengine wataendelea na kazi kwa maslahi ya wagonjwa wasioenda kutibiwa India.

      Nashauri mjiunge muwe kitu kimoja nchi nzima, then mje n maamuzi ya madaktari woote, tofauti ya hapo wengine wanagoma wengine wapo job is Ze Origino Komedy..ondoeni wanafki kati yenu.

      Kibanga Msese

    15. #53
      chitalula's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 425
      Rep Power : 518
      Likes Received
      88
      Likes Given
      40

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Safari madaktari wakigoma serikali ndipo itatutambua sisi wananchi wa hali ya chini kwani tumeshachoka na vifo vya ndugu zetu mpaka sasa, hamuwezi kutuambia tena eti madaktari wamekurupuka wakati walishawapa muda wa kutosha kushughulikia madai yao, udhaifu wenu hukohuko nyumbani kwenu

    16. #54
      jockey emmanuel's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd March 2011
      Location : namtumbo-likuyusekamaganga
      Posts : 330
      Rep Power : 479
      Likes Received
      46
      Likes Given
      71

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      dc ina-discourage tunaotaka kuwa doktaz,..honestly hata kama ni kuvumilia na kujitolea co kihivyo

    17. #55
      sweke34's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th September 2010
      Posts : 2,493
      Rep Power : 1255
      Likes Received
      734
      Likes Given
      1240

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Quote By meningitis
      bajeti ya afya badala ya kuoengezwa,inapunguzwa kana kwamba yaliyotokea ni sinema.
      Wenyewe wanakuambia kuna vipaumbele vingine...ila wenyewe wakiumwa haooo wanaenda Apolo/India...

    18. #56
      Fund's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th November 2011
      Posts : 25
      Rep Power : 383
      Likes Received
      3
      Likes Given
      21

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Kweli Mkuu,maana ,walijadiliana pasipo kuweka wazi ni yapi ambayo walikuwa wamaeyaongea,kwahiyo ni vema wakatuambia walikubliana mamabo gani na wakuu wa nchi,alafu tujue tunawaunga mkono au lah!

    19. #57
      swrc's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th June 2012
      Posts : 442
      Rep Power : 549
      Likes Received
      35
      Likes Given
      18

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Hakika muda umefika, serekali mimekuwa sirikali. Sirikali hii inaonyesha tena ni jinsi gani isivyowajali watumishi wake na wananchi wake kwa ujumla. Anzeni madaktari, waalimu tunafuatia.

    20. #58
      swrc's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th June 2012
      Posts : 442
      Rep Power : 549
      Likes Received
      35
      Likes Given
      18

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Hakika muda umefika, serekali mimekuwa sirikali. Sirikali hii inaonyesha tena ni jinsi gani isivyowajali watumishi wake na wananchi wake kwa ujumla. Anzeni madaktari, waalimu tunafuatia.

    21. #59
      Uliza_Bei's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2011
      Posts : 794
      Rep Power : 576
      Likes Received
      112
      Likes Given
      45

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Ipo haja ya watanzania kukutana Jangwani tarehe 23/06/2012 kuhoji watawala waliopo madarakani sasa ni kwaajili ya nani na maslahi ya nani....Nawalika wote. Tusipoziba ufa huu tutakuta nyumba yetu (Tanzania) imeanguka tuanze kudai uhuru mwingine baada ya miaka 50
      ukipenda asali usiogope ukali wa nyuki

    22. #60
      asungwilemwaifunga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2012
      Posts : 346
      Rep Power : 502
      Likes Received
      119
      Likes Given
      35

      Default Re: Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

      Hatujapata mapendekezo ya upande wa serikali ili tupime uzuri na ubaya wa maoni yake. Ni vigumu kutolea maamuzi kwa maoni ya upande mmoja. Ikumbukwe kuwa mgogoro ni wa pande mbili: Serikali na Madaktari. Upande wa madaktari hauwezi kuwa HAKIMU kwa shauri lake yenyewe. Madaktari hawawezi kusema kwa uhakika kuwa Serikali imekosa hiki au kile, jambo hili kwa maoni yangu haliwezi kuwa sawa.
      Madaktari wamekuwa wakisisitiza kutaka kugoma kila mara, lakini jamii na maadili ya taaluma ya udaktari yana wazuia. Hivyo kila wakipata kisingizio cha aina yoyote wanahamaki kutaka kutimiza azma yao ya kutaka kumuumiza bila huruma mlalahoi mnyonge. Hii haikubaliki hata kidogo kama malaria. Madaktari mnatuonea bure sisi wanyonge huku mkiwa tayari mlikula fedha zetu kwa kuwasomesha. Hawa mnaodhani mnawaadhibu hawapati adhabu hiyo. Lakini pia uchumi wetu bado ni mdogo, ikiwa Viongozi wanaonekana kufuja mali isivyohalali isiwe kigezo cha kudai zaidi hata ya uwezo halisi wa nchi. Hata leo hii tukimteua mwiungoni mwenu Daktari mmoja aende Ikulu hataweza kuwalipa madaktari kadri ya madai yao. Nakubaliana maslahi ya madaktari yanaweza kuboreshwa, lakini uboreshaji ni mchakato, huwezi kuboresha maslahi kwa usiku mmoja.
      Ndumbayeye likes this.

    Page 3 of 9 FirstFirst 12345 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...