Upepo wa Kisiasa unaashiria kwamba huko tunakokwenda hali inaweza ikawa tete kiasi cha kukosekana mtu wala taasisi yoyote ya kuirudisha kwenye hali ya kawaida.
Ushindani wa vyama hivi viwili naona kama umeingia kwenye stage ingine kabisa, kiasi kwamba hata wakati wa kujadili mambo ya msingi kabisa ya Kitaifa mambo yanabadirika na kuegemea kwenye hoja za kisiasa zaidi zenye nia ya ama kubomoa chama kingine au kujijenga.
Mfano ni mchakato wa Katiba ambao kuanzia Bungeni, ghafla ulichukua taswira ya ushindani wa kisiasa, na sasa wakati watanzania tunategemea wabunge wetu wajadiliane na hatimaye mwisho wa siku wakubaliane kwenye mambo ambayo yana maslahi kwa watanzania, ghafla pia mjadala umeamia kwenye ushindani wa hoja za kisiasa ambazo hivi sasa matusi na moja ya kiungo chake muhimu sana.
Nikikumbuka mauhaji yaliyojitokeza kwenye uchaguzi mdogo wa ulambo na arumeru mashariki, na namna Rais Kikwete a.k.a Mdhaifu anavyoendelea kushindwa kukabiliana na chagamoto za Muungano kutokea kisiwani Unguja akibuy time kwa sababu za kisiasa, naishiwa kabisa uwezo wa kuona uendelevu wa amani na utulivu katika taifa letu ndani ya kipindi kifupi kijacho.
Mimi kwa nia njema kabisa, naonelea kwamba, ili tuweze kuwa na Bunge lenye kusimamia Maslahi ya Watanzania na kuwarudisha watanzania katika hali ya kuendesha siasa za kuvumiliana kuna haja ya hivi vyama viwili vifutwe sababu naamini kwamba nguvu ya mabadiriko yanayohitajika iko mioyoni mwa watanzania ama sivyo muda si mrefu tutajikuta tunachepuka kutoka kwenye hoja ya kupigania ustawi wa jamii yetu na kuanza kupigania vyama.

Reply With Quote


Follow Us Here